Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi (kwamba Katiba Mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi) siyo msimamo wa Kanisa Katoliki

Amlisema sana Jakaya kumbe ni mnafiki mkubwa na ni shetani
 
Pengo yuko sahihi hata uingereza kipaumbele chao sio katiba na hawajawahi kuwa na katiba na hawatarijii kuwa na katiba. kipaumbele ni kero halisia za raia wake kutatuliwa. Askofu pengo yuko sahihi asilimia 100
Huwezi kuifananisha Tz na UK katika mambo kama hayo nasidhan kama kuna kitu cha kujifananisha
 
Mkuu ni 70 ukiwa na nguvu basi 80 mambo ya agano la kale yamefanyiwa review na ujio wa Bwana Yesu

Huko kwenye agano la kale kuna walio ishi miaka 900 je unafikiria inawezekana kwa sasa hivi kuishi miaka 900?
Huo mstari ni Mungu mwenyewe aliifanya hiyo review.
Sidhan kama Yesu alilizungumzia hili.
 
Msitukane mzee wetu kwa uzwazwa wenu. Hakuna alichokosea hapo na kaeleza utaratibu unaotumika kutoa msimamo wa kanisa kama hutaki anzisha lako utoe msimamo.
 
Pengo ni mtu wa heshima na anajua mipaka yake ya madaraka. Usilazimisha aingie kwenye siasa kama unavyotaka wewe.
Watu wana matatizo ya akili mkuu yani anachofikiri yeye kwa kuwaza kula ugali na maharage anataka na watu wenye akili na heshima zao wafuate mihemko yao.
 
Hamjamuelewa Pengo. Kasisitiza kuwa kuna utaratibu wa kanisa kuhusu kutoa matamko ya kisiasa. Sasa wapinga kila kitu wanakuja na mipash yao. Kwani pengo kasosea wapi? kwani Pengo kasema hataki katiba mpya?
Hata na sisi tunamkumbusha akae kimya, utaratibu hausemi kuwa yeye ndio msemaji. Mbona unawashwawashwa wewe?
 
BAK katumia maneno yapi mabaya? Huyo Pengo ashavimbiwa vya kunyonga sasa hivi anatupumilia tu hewa chafu

Halafu huyo ni mwanadamu kama wewe kuwa Kadrinali hakumfanyi awe malaika hivyo akiongea ujinga atakosolewa tu

Jibu hoja zangu pasipo kusimjibia BAK.

Hakuna neno lolote nimeandika kuwa Pengo ni malaika.

Uwe tu makini unapojibu hoja.
 
Kashawekwa mfukoni huyo! Lazima aangalie namna ya kuendelea kuficha madhambi yake kama ile ishu ya mgao wa Mkombozi benki..
 
Alishaulizwa amekula maharagwe ya wapi huyu Mzee?
 
Kanisa Katoliki linafanya kazi katika mitizamo miwili ya kisiasa ambapo ndani kuna karibu taratibu zote za kiserikali, wapo makatibu wa idara mbalimbali ikiwemo elimu, afaya, chakula n.k, pia mtizamo mwingine ni wa kidini kama unavyojulikana.
kwa hiyo swali linajijibu katika mitizamo hiyo miwili.
 
Pengo ni MNAFIKI sana ,Niwemugizi alitoa maoni yake binafsi wakati wa kongamano lile,kwani kuna sehemu ilinukuliwa ikisema yale ni maoni ya Kanisa Katoliki? Tuache unafiki nimekosa uvumilivu na Baba kadinal Pengo
Pengo alisisitiza hilo wakati akitoa ufafanuzi juu ya sintofahamu iliyojitokeza miongoni mwa Watanzania na waumini wa kanisa hilo kutokana na kauli ya Askofu Niwemugizi.
ulielewa hapo katika bluu??
 
Kwani lazima Pengo afuate Sera za upinzani ndo mwone anafaa, Shem on you! CHADEMA
Hata nami nawashangaa povu jingi kwa vile hafungamani na sera zao, pumbavu kabisa kumfanya mtu aache kufikiri anavyotaka kwa vile tu eti watu flani wanafikiri katika mtizamo mmoja.
 
Sema kwa mtazamo wako. usitake kufanya mtizamo wako uwe msimamo wa wengi. lazima ukubali kuishi kwa kukubaliana pasipo kukubaliana!
 
Mtazamo wa Watanzania wengi hata Viongozi wastaafu ambao wamemkoromea huyo dikteta uchwara na hawa ni MACCM wala si wa upizani. Mwinyi, Butiku, Warioba, Kinana na hata Kikwete wiki chache zilizopita kabla ya shambulizi la Lissu alimkoromea kwamba wapinzani si maadui wa Serikali, lakini cha kushangaza huyo askofu uchwara yeye haoni maovu yanayotendwa na huyo dhalimu.

Tia akili kichwani badala ya kukurupuka eti ni msimamo wangu!

sema kwa mtazamo wako. usitake kufanya mtizamo wako uwe msimamo wa wengi. lazima ukubali kuishi kwa kukubaliana pasipo kukubaliana!
 
Nadhani haya pia ni mawazo binafsi ya mzee wetu,
naye katumia uhuru wake wa kutoa maoni
ila kwa kuwa ndiye kiongozi mkuu wa kanisa hilo
hapa nchini basi mawazo yake ndo msimamo wa kanisa,

Mimi binafsi ninamwelewa askofu Niwemugizi
hapingani na serikali bali anashauri ili yanayofanyika
sasa hivi yawe endelevu ni lazima yawe na msingi
wa kisheria,yaani yalindwe kwa kuwekwa kwenye katiba.

Nasema hayo kwa sababu,nchi hii Mwalimu Nyerere aliiacha
ina viwanda vingi,kwa kuwa havikulindwa kikatiba
waliokuja nyuma yake wakavipiga mnada na kuviuza kwa bei
chee.Aliacha nchi hii ikiwa na madini kwa kudhani kwamba
tusomeshe wataalam wetu ndo yachimbwe,leo tunashuhudia
yanavyosombwa kwa kasi ya ajabu bila huruma.Sababu ya kukosa ulinzi kikatiba.

Moyo wa rais Magufuri unaumizwa na yaliyofanyika
lakini kama atatawala kikatiba miaka 10
bila aliyoyafanya kuyalinda kikatiba,nayo yatauzwa
mbele ya macho yake,kama vile NBC ilivyouzwa
macho ya mwalimu yakishuhudia,alipiga kelele
lakini alikuwa tayari nje ya mfumo.

Naunga mkono hoja ya kuwa na katiba
itakayofanya mambo anayoyafanya rais Magufuli
yawe endelevu kwa mabnufaa ya watanzania.
 
Pengo ni janga kwa Wakatoliki wa taifa hili... Anna Abdhalah ni janga kwa maendeleo ya WanaKusini..
Jibuni hoja na sio kumtukana mtoa hoja...na ataendelea kuwa janga kwa vilaza na waropokaji
 
Kanisa katoliki litawatolea statement wanyonge wote wanaonyanyasika na wote wanaodhurika kinyume na matakwa ya Mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…