Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

SEASON 1
SEHEMU YA KWANZA
MTUNZI : PATRICK.CK
Ni saa sita za usiku sasa bado jaji Elibariki chukuswa yuko sebuleni akiendelea kupitia kitabu chake cha sheria .Katika meza ndogo kulikuwa na vitabu vingine zaidi ya saba vya sheria.Aliendelea kufungua ukurasa baada ya ukurasa.Alionekana kuwa na mawazo mengi mno.Wakati akiendelea kupitia kurasa za kitabu kile mke wake akaingia pale sebuleni akiwa na kikombe cha kahawa, akakiweka mezani halafu akainama na kumbusu mumewe.

“ You need to take a rest now.Tommorow is your big day” akasema Flaviana mwanamke mwenye uzuri wa kipekee.Elibariki akakifunika kitabu chake na kumtazama mkewe ,akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kusema

“ Natamani sana nipumzike lakini sina hakika kama nitapata usingizi.”
Mke wake akamuangalia kwa makini halafu akasema
“ Kuna jambo nataka nikuulize mume wangu”
“ Uliza usihofu ”
“ Najua kesi hii ni moja kati ya kesi kubwa na ngumu kwako.Hukumu unayotarajia kuitoa kesho inasubiriwa kwa hamu kubwa sana na umma wa watanzania.Wewe ni jaji na nina imani maamuzi yako utakayoyachukua ni sahihi kabisa,lakini swali langu ni je Yule msichana ana hatia?
Swali lile lilionekana gumu sana kwa jaji Elibariki.Akainama akafikiri kidogo halafu akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kumtazama mkewe.

“ My love kesi hii ni ngumu sana na imejaa utata mwingi na ndiyo maana unaniona mpaka hivi sasa bado niko hapa.” Akasema Elibariki
Flaviana akamtazama mume wake na akagundua kwamba hakuwa tayari kumjibu swali alilouliza.Akas
imama na kusema

“ Sina wasi wasi na maamuzi utakayoyatoa kesho lakini nakuomba utoe haki kwa upande wenye haki.”
Elibariki hakumjibu kitu akabaki akimuangalia
“ Come to bed when you are done,but don’t stay till very late.You have a big day tomorrow.” Akasema Flaviana na kuelekea chumbani .Elibariki akavuta pumzi ndefu na kuchukua kitabu chake cha sheria akaendelea kukisoma.
“ Katika maisha yangu ndani ya sheria sijawahi kukutana na kesi ngumu yenye mitihani kama hii.Hata hivyo niliapa kusimamia sheria na kutenda haki kwa kila mwenye haki.

Katika maamuzi yangu ya kesho lazima nifanye kwa haki japokuwa nina hakika nitakuwa katika matatizo makubwa baada ya hukumu ya kesho lakini siwezi kupindisha sheria eti tu kwa sababu ya shinikizo toka kwa mtu au kikundi cha watu.Mungu ataniongoza na kunisimamia ili nitoe hukumu ya haki” akawaza Elibariki na kufunga vitabu vyake akaelekea chumbani kulala.tayari Flaviana mke wake amekwisha lala.Akamtazama kwa makini na kujisemea moyoni

“ Nina hakika hata wewe hautanitazama vizuri baada ya hukumu ya kesho,lakini sina namna nyingine zaidi ya kutenda haki.Utanisamehe mke wangu” akawaza Elibariki na kupanda kitandani kulala.

***********

“ Eli my love,amka kumekucha !! ..Ilikuwa ni sauti tamu na laini ya Flaviana akimuamsha mumewe.Jaji Elibariki ambaye asubuhi hii alionekana kuzama katika usingizi mzito akafumbua macho huku akiguna na kutazama saa ya ukutani.Ni saa kumi na mbili na dakika ishirini za asubuhi.
“ jana sikupata usingizi kabisa.Usiku wangu ulikuwa mrefu sana” akasema kwa sauti ya uchovu.

“ Please wake up honey.Today its going to be a very long day” akasema Flaviana.Elibariki akainuka na kuelekea katika chumba chake cha mazoezi akafanya mazoezi kidogo halafu akaelekea bafuni.Bado kichwa chake kiliendelea kuwa na mawazo mengi sana.Kisha oga akarejea chumbani na kukutana na suti nzuri aliyoandaliwa na mke wake akavaa na kujitazama katika kioo kikubwa kilichokuwamo chumbani mwao.Aliganda pale katika kioo hadi mke wake alipoingia naye akaanza kujiandaa.

“ Leo unakwenda kazini? Akauliza Jaji Elibariki.Flaviana akacheka kidogo na kusema
“ Usinichekeshe mume wangu,yaani niende kazini leo? Siwezi kufanya hivyo hata kidogo.Leo ni siku yako kubwa.Ni siku yetu kubwa.Ni siku ambayo jina lako litaingia katika vitabu vya historia kwa hukumu unayokwenda kuitoa.Vyombo vyote vya habari vitakuwepo mahakamani ,lazima na mimi niwepo nikuunge mkono pamoja na mdogo wangu Anna.” Akasema Flaviana.Elibariki hakujibu kitu akaendelea kujitazama katika kioo.

“Are you nervous my love? Akauliza Flaviana
“ No I’m not” akajibu Elibariki halafu wakaongozana kuelekea katika chumba cha chakula kwa ajili yakupata kifungua kinywa.Wakati wakiendelea na kupata kifungua kinywa simu ya Jaji Elibariki ikaita.Akaitazama ikiita akasita kuipokea.
“ Mbona hupokei hiyo simu? Akauliza Flaviana
“ Its your father.Mr President” akajibu Elibariki
“ Usiogope.Ongea naye .Si kawaida yake kupiga simu mida kama hii.Inawezekana ana jambo la maana la kukwambia” Akasema Flaviana.Elibariki akaichukua simu na kubonyeza kitufe cha kupokelea huku akiinuka na kuelekea sebuleni.

“ Hallo Mr President” akasema Jaji Elibarki
“ Hallo Jaji.Mnaendeleaje vijana wangu?
“ Tunaendelea vizuri mzee.Ninyi mnaendeleaje?
“ Tunaendelea vizuri sana”
“ Nashukuru kusikia hivyo” akasema Elibariki na kimya kifupi kikapita
“ Elibariki,today its your big day” akasema Mheshimiwa rais.
“ Najua unakwenda kutoa hukumu katika kesi ngumu inayovuta hisia za watu wengi na hasa kwa kuwa binti wa rais naye kesi hii inamuhusu kwani mchumba wake ndiye aliyeuawa.Sikufundishi kuifanya kazi yako lakini fanya maamuzi ya haki kwa namna uonavyo wewe.Pamoja na hayo kuna jambo ambalo nataka kukuomba kijana wangu” Akasema Dr Joshua Johakim rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“ Nakusikiliza mzee” akasema Jaji Elibariki kwa wasi wasi .
“ Nilikuteua kuwa jaji kwa sababu wewe ni msomi mzuri na unazifahamu sheria za nchi kwa hiyo sitaki kuingilia maamuzi yako lakini nakuomba kijana wangu,try in anyway you can to make my daughter Happy.Alimpenda sana Edson.Ni hilo tu ninalotaka kukuomba kijana wangu.Nakutakia siku njema” akasema mheshimiwa rais na kukata simu.Jaji Elibariki alibaki ameduwaa asijue afanye nini.Maneno yale ya rais ambaye ni baba mkwe wake yalimfanya ahisi kuchanganyikiwa.

“ Huu ni mtihani mgumu sana lakini Mungu atanitangulia nitatenda haki” akawaza Elibariki na kurejea mezani
“ Amekwambia nini baba? Mbona sura yako imebadilika namna hiyo? Akauliza Flaviana
“ Nothing.Just greetings” akajibu Elibariki na kuendelea kupata kifungua kinywa.Baada ya kumaliza akarejea chumbani na kujitazama tena katika kioo na kuvuta pumzi ndefu.

“ Please help me Lord.I’m in a very difficult situation” akasema Elibariki kwa sauti ndogo na mara mke wake akaingia mle chumbani
“ Its time my love.Are you ready?
“ Let’s go” akasema Elibariki ,wakatoka wakaingia garibni na kuondoka.

**********

Hakukuwa na nafasi tena ya kukaa ndani ya chumba cha mahakama kutokana na watu kujaa.Ni siku ya hukumu ya kesi ya mauaji inayomkabili mmiliki wa maduka makubwa ya mavazi ya Penny Fashion,Peniela Salimote.Kesi hii iliyovuta hisia za watu wengi na kuwafanya wafurike ili kuja kusikia hukumu ilikuwa inaonyeshwa moja kwa moja katika runinga.ILikuwa ni kesi ya kwanza kubwa kurushwa moja kwa moja katika runinga.Katika kila kona ya nchi watu walikuwa wakifuatilia matangazo ya moja kwa moja ya kesi hii ambayo hukumu yake ilikuwa inasubiriwa na watu wengi.

Ndani ya chumba cha mahakama ilikuwepo familia ya rais ikiongozwa na mke wa rais,Dr Flora Johakim ambaye alikuwa ameambatana na binti zake wawili Flaviana na Anna.Familia ya Edson Kobe kijana anayedaiwa kuuliwa na Peniela nayo ilikuwepo mahakamani hapo ili kuhakikisha kwamba haki inatendeka.Familia ya Edson na ile ya rais zilikuwa ni familia rafiki kwa muda mrefu sana.Kwa upande wa Penny hakukuwa na ndugu yake yeyote aliyefika mahakamani pale zaidi ya rafiki zake wachache.

Tayari mtuhumiwa amekwisha ingizwa mahakamani na aliyekuwa akisubiriwa ni jaji anayeisikiliza kesi ile aweze kuingia na kuisoma hukumu.Wakati wakimsubiri Jaji aingie,Jason Patrick mwanasheria anayemtetea Penny alikuwa akibadilishana mawili matatu na mteja wake .
“ Jason,kabla hukumu haijaanza ninaomba nikwambie kitu.” Akanyamaza kidogo na kuendelea.

“ Nakushukuru sana kwa kila kitu ulichonifanyia.Umenisimamia katika kesi hii kwa kila namna ulivyoweza.Najua chochote kinaweza kikatokea siku ya leo hivyo nakuomba endapo ikitokea nikakutwa na hatia na kufungwa kifungo cha maisha au kifo uhakikishe yale yote niliyokuandikia katika karatasi unayatimiza.Wewe ni zaidi ya rafiki.Wewe ni ndugu yangu pekee ninayekutambua.Ninakukabidhi kila kilicho changu endapo mambo yataenda kinyume na matarajio yetu." Akasema Penny huku machozi yakimtoka
“ Penny naomba usikate tamaa hata kidogo.Nimepambana vya kutosha kuhakikisha kwamba tunashinda kesi hii lakini kama mambo yataenda tofauti na matarajio yetu hautakuwa ni mwisho.Nitapambana hadi nihakikishe haki imepatikana.” Akasema Jason na mara jaji akaingia.

Wakati Jaji akiingia Penny akamnong’oneza Jason sikioni
“ I didn’t do it.I didn’t kill him”
“ I know Penny and I believe you” akasema Jason na mara mahakama ikaanza.”
tuendelee
 
Asante kwa stori nzuri,
Tuendelee sasa
 
  • Thanks
Reactions: T11
SEASON 1
SEHEMU YA 11
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Toka nimezaliwa hata baba yangu hajawahi kunipiga kofi sembuse wewe ng’ombe ! ..Kauli ile ikampandisha hasira Elibariki na kuanza kumshushia mke wake kipigo kikali kilichomfanya apige ukelele mkubwa .Jaji Elibariki hakujali kelele zile akaendelea kumpa kipigo mkewe.Hadi anamuachia Flaviana alikuwa anavuja damu.
“ Siku nyingine usithubutu kabisa kunidharau paka wewe ..! akasema jaji Elibariki huku akitweta kwa hasira Huku akilia,Flaviana akaingia bafuni na kujifuta damu zilizotoka katika majeraha yaliyotokana na kipigo kikali
“ Eli umenipiga hadi kunitoa damu.Sasa nitakuonyesha mimi na wewe nani mwenye nguvu.I swear in heaven and earth lazima nikuonyeshe kazi na hautanisahau mpaka unaingia kaburini”akasema kwa hasira flaviana na kutoka kwa kasi akaingia katika gari lake na kuondoka kwa kasi
“ Nimechoshwa na dharau za familia hii.Yote hii ni kwa sababu baba yao ni rais .Hapana hawawezi kunitisha hata kidogo,hakuna aliye juu ya sheria.” Akasema jaji Elibariki kwa hasira.
ENDELEA…………………………
Jaji Elibariki alikaa kitandani na kuanza kutafakari maisha yaketoka alipokutanana Flaviana ,wakapendana,wakwa wachumbanabaadae wakafungandoa.Aliyatafakari maisha yake ya ndoa toka walipooana hadi leo hii
“ Sina hakika kama tuliingia katika ndoa tukiwa tumejiandaa vya kutosha.Sina hakika kama tulikuwa na mapenzi ya kweli au zilikuwa ni tama tu za ujana.Toka tumeyaanza maisha yandoa hakuna amanindani mwetu.It’s been a living hell to me.Tukiwa nje tunaonekana ni watu wenye mapenzi mazito lakini hajuna ajuaye siri yetu ya ndani.Maisha yetu yamejaa mifarakano,dharauna ugomvi.Nimechoshwa na maisha haya.Nimechoka kuwadanganya watu kwamba tunapendana kwa dhati wakati si kweli.Nadhani ni wakati muafaka sasa wa kufanya maamuzi na kila mmoja wetu akatafute furaha ya maisha yake.Siwezi kuendelea na maisha kama haya” akawaza halafu akaenda katika kabati dogo lililokuwa mle chumbani akalifunguana kutoa chupa ya mvinyo akajimiminia katika glasi akanywa na mara sura a Peny ikamjia kichwani “ Penny !!..akasema kwa sauti ndogo huku akitabaamu
“ Mwanamke kama Penny anafaa sana kuwa mke.Aba uzuri wa kipekee ambao sioniwa kumfaanisha naye na ana adabu na hata ukiongea naye utabaini wazi kwamba ni mwanamke mqwnye heshima kubwa/Jaji Elibarikiakaendelea kuwaza na mara akastuliwa namlio wa simu.Akaichukuana kutazmaa mpigaji ,alikuwa ni baba mkwe wake Dr Joshua,rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
“ Kazi imeanza” akasema kimoyo moyo na kubonyeza kitufe cha kupokelea simu
“ Hallo mzee shikamoo”
“ Marahaba mheshimiwa jaji,habari za kwenu?
“ Habari nzuri tu mzee,sijui ninyi huko”
“ Sisi wazima.Eli uko wapi?
“ Niko nyumbani mzee”
“ Ok vizuri.Nakuomba hapa ikulu sasa hivi nina maongezi nawe” akasema Dr Joshua na kukata simu
“ Flaviana amekwenda kunishitaki kwa baba yake akidhani labda nitamuogopa.Sintomuogopa mtu yeyote hata kama ni rais wan chi.Kuanzia sasa yeyote atakayenidharau kwa namna yeyote ile nitapambananaye” akawaza huku akivaa koti na kutoka kueleka ikulu kuonana na baba mkwe wake. Ilimchukua dakika zaidi ya hamsini kuwasili katikamakazi ya rais.Baada ya kama dakika kumi na tatu toka awasili ,Dr Joshua akajitokeza sebuleni.Jaji Elibariki akasimama wakasalimiana “ Mheshimiwa jaji ,hebu nieleze nini kimetokea huko kwenu na kusababisha umpige mwenzako na kumuumiza kiasi kile? Akaanzisha mazungumzo Dr Joshua.Elibariki akavuta pumzi ndefu na kisha akamsimulia rais kila kitu kilichotokea na kusababisha apandwe na hasira na kumpiga mkewe.
“ Nimekuelewa Elibariki ,lakini pamoja na yote aliyoyafanya mwenzako ulitakiwa ujizuie, hukupaswa kufikia hatua ya kumpiga mwenzako namna ile.Migongano ndani ya nyumba ni kitu cha kawaida na suluhisho lake ni kukaa mkaongea mkayamaliza na si kurushiana makonde.Wewe kama kichwa cha nyumba unahitajika uwe na busara ya hali ya juu “ akasema Dr Joshua
“ Nakuelewa mzee,lakini nilifikia maamuzi ya kumpiga kidogo mke wangu kutokana na dharau alizoniletea.Kama nilivyokueleza mzee ni muda mrefu sasa amekuwa akinidharau sana na leo hii uvumilivu ulinishinda nikaona bora nimuonye kidogo” akasema Elibariki “ Siku nyingine endapo atakuletea dharau na kiburi,wasiliana nami moja kwa moja kabla ya kuchukua maamuzi ya kumpiga.Sipendi sana kuona mwanangu yeyote akilia machozi na hasa ya kupigwa na mwanaume” akasema Dr Joshua
“Lakini mzee, Flaviana ni mke wangu na mambo yetu yanndani tunayamaliza wenyewe.Haitapendeza kila siku niwe nakupigia simu na kukwambia kwamba mwanao amenidharau.Naomba mzee utuachie mambo yetu ya ndani tuyamalize sisi wenyewe.” Akasema Elibariki
“Kuyamaliza kwa staili hii ya kutoana damu? No !.. Sitaki kabisa mwanangu aguswe tena na kutolewa damu.Usinione ninaongea nawe hapa lakini nimechukizwa mno na kitendo ulichokifanya leo cha kumpiga mwanangu.Naomba kisijirudie tena.Marufuku kumfanya mwanangu sehemu ya mazoezi” akasema Dr Joshua kwa sauti ya juu yenye amri ndani yake .Jaji Elibariki akakereka sana kwa maneno yale ya baba mkwe wake
“ Lakini mzee………….” Akataka kusema jambo ,akazuiwa na Dr Joshua
“ Hakuna cha lakini…..Nimesema sitaki mwanangu aguswe and that’s fnal.Sitaki tena mjadala.Hata akikukosea vipi sitaki umpige.Nieleze mimi mwenyewe nitaongea naye” akasema kwa ukali Dr Joshua “ lakini mzee huyu ni mke wangu na amekuwa akinifanyia mambo mengi ya dharau ambayo siwezi hata kukueleza.Unapoongea maneno kama hayo unampa nguvu ya kufanya anachokitaka kwangu kwa kuwa anajua baba yake anamtetea” akalalamika Elibariki.Dr Joshau akasimama na kumsogelea “ I’m her father and I’m warning you….” Akasema Dr Joshua.maneno yale yakamkera sana Elibariki naye akasimama. “ Yes 1 you are her father but I’m her husband !!.... akasema Elibariki kwa sauti ya juu kidogo.
“ Elibariki,tafadhali chunga sana maneno unayoongea mbele yangu.Wewe bado hauna uwezo wa kusimama na kubishana na mimi.Ukumbuke kwamba ni mimi ndiye niliye kutoa huko maporini na kukupandisha hadi hapa ulipo.kwa hiyo kuwa makini sana siku nyingine unapoongea na mimi.Nina uwezo wa kukufanya chochote kile” akafoka dr Joshua.Elibariki akamtazama kwa macho makali na kusema
“ Naomba unisikilze mzee.Nimechoshwa na wewe na wanao kila mara kunisimanga kutokana na cheo hiki.Naomba mfahamu wewe na wanao kwamba cheo hiki hukunipa wewe bali nimepewa na Jamhuri ya muungano wa Tanzania na nimepewa kwa sababu ninafaa na nina vigezo vyote vya kuwepo hapa nilipo.Kwa maana hiyo naomba muache kuanzia sasa kunisakama kuhusiana na cheo hiki.Kitu kingine mnachotakiwa kukifahamu ni kwamba ofisi hii si mali ya familia,kwa hiyo si wewe wala wanao mnaoweza mkanishinikiza nifanye kazi yangu kwa matakwa yenu.Ninaifanya kazi yangu kwa mujibu wa sheria za nchi na si kwa kumfurahisha mtu Fulani..”akasema kwa ukali na kutoka kwa hasira akimuacha Dr Joshua akishangaa.
“ Nimemueleza ukweli wake,akichukia shauri lake,nimechoshwa na dharau zao” akawaza Elibariki huku akiingia katika gari lake na kuondoka
“ Kichwa changu kimevurugwa kabisa na Yule mzee.I need someone to talk to.I need some comfort” akawaza na mara sura ya penny ikamjia
“ penny !!... I need to talk to her.pengine kichwa changu kinaweza kutulia” akapunguza mwendo wa gari akatoa simu na kuzitafuta namba za Penny ,akapiga lakini haikuwa ikipatikana.
*********
Asubuhi na mapema jaji Elibariki aliamka na kufanya mazoezi ya viungo halafu akajianda na kuondoka.Flaviana hakurejea nyumbani usiku toka alipoondoka
“ Nadhani huu utakuwa ni mwanzo wa maisha mapya.Sina hakika kama kuna suluhu yoyote itapatikana tena baina yangu na Flaviana.Ni wakati sasa wa kuanza kuitafuta upya furaha ya moyo wangu ambayo nilitegemea kuipata kwa Flaviana lakini kumbe nilikuwa najidanganya.Nimeambulia karaha badala ya raha.Toka nilipomuoa hadi hivi leo hata mtoto amekataa kunizalia kwa kisingizo cha kutokuwa tayari.Hapana imetosha sasa.Maisha haya lazima yafikie mwisho.Kwa sasa ngoja kwanza nielekeze nguvu kumtafuta muuaji wa Edsoni ili Penny aweze kuwa salama” Mara tu alipomkumbuka Penny,akatabasamu na kutoa simu yake akazitafuta namba za Penny akapiga lakini bado simu yake haikuwa ikipatikana.
“ Ameamua kuizima simu yake,inawezekana hataki usumbufu toka kwa watu.Ametoka katika matatizo makubwa na anahitaji muda wa kukaa mwenyewe atafakari maisha yake bila usumbufu toka kwa watu” akawaza Jaji Elibariki Moja kwa moja alielekea Mandarini Hotel mahala ambako hupenda sana kwenda kupata kifungua kinywa.
“ Watu wengi wananishangaa ni kwa nini mtu kama mimi,Jaji wa Mahakam kuu ninakuja kupata kifungua kinywa hotelini? Hawajui Kero nilizonazo katika ndoa yangu.lakini soon mambo yote haya yatakwisha and I’ll be happy again.” Akawaza wakati akiendelea kupata kifungua kinywa. Toka Mandarin hotel,akaelekea ofisini kwake ambako hakukaa sana akatoka akaelekea mahala alikopanga akutane na Mathew.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
PENIELA
SEASON 1
SEHEMU YA 12
ILIPOISIA SEHEMU ILIYOPITA
Mara tu alipomkumbuka Penny,akatabasamu na kutoa simu yake akazitafuta namba za Penny akapiga lakini bado simu yake haikuwa ikipatikana
“ Ameamua kuizima simu yake,inawezekana hataki usumbufu toka kwa watu.Ametoka katika matatizo makubwa na anahitaji muda wa kukaa mwenyewe atafakari maisha yake bila usumbufu toka kwa watu” akawaza Jaji Elibariki Moja kwa moja alielekea Mandarini Hotel mahala ambako hupenda sana kwenda kupata kifungua kinywa. “ Watu wengi wananishangaa ni kwa nini mtu kama mimi,Jaji wa Mahakam kuu ninakuja kupata kifungua kinywa hotelini? Hawajui Kero nilizonazo katika ndoa yangu.lakini soon mambo yote haya yatakwisha and I’ll be happy again.” Akawaza wakati akiendelea kupata kifungua kinywa. Toka Mandarin hotel,akaelekea ofisini kwake ambako hakukaa sana akatoka akaelekea mahala alikopanga akutane na Mathew.
ENDELEA……………………………..
Dakika kumi baada ya kuwasili Malaika Lounge mahala walikopanga wakutane na Mathew,Jason akawasili, wakasalimiana akavuta kiti na kuketi
“ Jason” akaanzisha mazungumzo Jaji Elibariki
“ kama nilivyokueleza simuni ,nimefikiria sana kuhusiana na jambo tunalotaka kulifanya na kuona ugumu wake .Sisi tumebobea katika masuala ya sheria na hatuna taaluma yoyote ya kufanya uchunguzi.Ni kwa sababu hii nimelazimika kumtafuta Mathew Kwanga” akanyamaza kidogo ,akamtazama Jason na kuendelea.
“ Mathew Kwanga aliwahi kufanya kazi katika idara ya ujasusi ya taifa na aliacha kazi hiyo baada ya familia yake yote kuteketezwa kwa moto.Kwa hivi sasa yeye ni mtu anayekodishwa na mataifa kazi za siri za kiuchunguzi .Ni mtu aliyebobea mno katika kazi hizi .Nina imani atatufanyia kazi nzuri “ akasema Jaji Elibariki
“Umefanya jambo la msingi sana mheshimiwa jaji.Hata mimi nilikuwa nafikiria kukushauri tufanye kitu kama hicho.Sisi peke yetu hatuwezi kulifanikisha jambo hili .Tunahitaji msaada wa mtu mwenye uzoefu wa kutosha na mambo haya.Natumai Mathew ni chaguo sahihi na atakuwa na msaada mkubwa sana kwetu” akasema Jason
“ Exactly !...Thats my point..Mathew ni mtu ambaye tumefahamiana kwa muda refu na sina shaka yoyote na uwezo wake.Ni mtu mwenye uwezo wa hali ya juu sana.By the way how’s Peniela? Akauliza Jaji Elibariki.Jason akaguna kidogo na kusema
“ Siku ya pili sasa hapatikani simuni”
“ May be she needs sometime alone. Unajua ametoka katika matatizo makubwa kwa hiyo yawezekana akahitaji kuituliza akili yake bila bughudha za watu.Let’s give her sometime” akasema Jaji Elibariki na mara Mathew akatokea.Alikuwa ni kijana nadhifu aliyevaa suti nzuri iliyompendeza
“ Hallo gentlemen…” akasema Mathew huku akipeana mikono na akina Jason
“ Mathew kutana na Jason,wakili maarufu sana hapa Tanzania.” Bila kuchelewa Jaji Elibariki akaanza kutoa utambulisho
“ Jason kutana na Mathew Kwanga.Ni rafiki yangu wa siku nyingi na mtu aliyebobea katika masuala ya kiuchunguzi”
Jason na Mathew wakashikana mikono kwa kujuana
“ Mtanisamehe sana ndugu zangu kwa kuchelewa .Nilipatwa na dharura ya ghafla” akasema Mathew
“ Usijali Mathew.Hakuna kilichoharibika.Nadhani umelifanyia kazi lile suala letu” akasema Jason
“ Ndiyo mheshimiwa Jaji.Nimejaribu kutafakari kwa kina kuhusiana na kazi mliyonipa na namna nitakavyoweza kuifanya.Naomba niwaweke wazi kwamba kazi hii si ndogo kama mnavyoifikiria. Edson alikuwa mfanyakazi katika kitengo cha habari Ikulu,huyu si mtu mdogo kama watu wanavyoweza kudhani.Ninashawishika kuamini kwamba lazima aliuawa kwa sababu maalum.Kazi yetu ni kuitafuta sababu hiyo iliyopelekea yeye kuuawa pamoja na watu waliomuua na kesi kumuangukia Peniela.Kazi hii si nyepesi lakini nawaahidi kwamba hakuna yeyote ambaye alikuwa na mkono wake katika mauaji hayo atabaki salama.Nitawatafuta katika kila pembe ya nchi hii na dunia mpaka nihakikishe nimewatia mikononi wale wote waliofanya kitendo hicho cha kinyama na mzigo wote wakamuangushia Penny.” akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Kabla hatujaendelea mbele zaidi naomba tukubaliane kwanza kitu kimoja.kazi hii ni ya gharama kubwa.Kabla sijaingiza mguu wangu katika uwanja wa mapambano nahitaji kufahamu kama mtakuwa tayari kwa gharama za shughuli hii japokuwa haitakuwa kubwa kwani ninaifanya tu kwa ajili ya ninyi ndugu zangu lakini sikuwa nataka kufanya kazi yoyote hapa nyumbani.” Akasema Mathew.Jason na Jaji Elibariki wakatazamana na Jason akasema
“ Tuko tayari Mathew.Usihofu kuhusu gharama”
“ Ok Good.Sasa tunaweza kuendelea” akasema Mathew.
“ Katika kazi hii pia nitashirikiana na watu wawili.Wa kwanza ni Anitha Monera na wa pili ni Noah Ikuso.” Akasema Mathew huku akiwapa akina Jason mafaili ya watu hao wayapitie
“ Anitha Monera ana miaka ishirini na tisa.Ni mtanzania anayeishi nchini Marekani.Huyu ninamuita ni mchawi wa kompyuta. Anaichezea kompyuta kwa kiasi cha kushangaza .Nimekuwa nikimtumia sana katika kila kazi ninayoipata na siwafichi ndugu zangu huyu amekuwa ni msaada mkubwa kwangu na ndiye amenifanya nifanikiwe katika kila kazi ninayopata” akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Noah ikuso naye ni mtanzania pia.Ana umri wa miaka thelathini na tatu .Aliwahi kufanya kazi katika idara ya usalama wa taifa .Ni kijana mahiri na hodari katika kazi.Ninao wengi ambao ninaweza kufanya nao kazi hii lakini nimewachagua hawa wawili ambao naamini wanatosha sana kuikamilisha hii kazi kwa umahiri na haraka” akasema Mathew.Jason na jaji Elibariki waliendelea kupitia mafaili ya vijana wale halafu Jason akasema
“ Kwa upande wangu sina kipingamizi chochote.Kama unawaamini vijana hawa kwamba wanaweza kazi basi unaweza kuwatumia”
“ Yah ! ninawaamini sana.Ni mahodari na hawana mchezo katika kazi.” Akasema Mathew,kikapita kimya kifupi akauliza
“ Kuna kitu kimoja bado hamjaniweka wazi.Nina hakika nitawapata watu hawa waliofanya kitendo hiki,lakini je wakipatikana nini kitafuata? Wanashughulikiwa vipi? Au mtawakabidhi katika mikono ya dola?
“ Lengo letu sisi ni kuwafichua na kuwakabidhi katika mikono ya dola.Kitu kikubwa kinachonisukuma mimi na mwenzangu tuwe tayari kugharamia jambo hili ni kuudhihirishai umma wa watanzania kwamba sikufanya maamuzi ya kukurupuka kumuachia huru Peniela.Nataka watu wawe na imani na mahakama kwamba ndicho chombo pekee chenye kutenda haki bila kujali mtu.Hatuna lengo la kulipiza kisasi,bali tukimbaini muuaji tutamfikisha katika mikono husika na sheria itachukua mkondo wake na sisi tutabaki salama.” Akasema Jaji Elibariki
“ Ok sasa nimekuelewa mheshimiwa jaji.usijali watapatikana tu.Kitu kingine ninachohitaji ni kumpata Peniela ili niweze kuongea naye mawili matatu kwani yeye ndiye aliyekutwa eneo la tukio.Nataka niyafahamu mazingira ya tukio namna yalivyokuwa.” akasema Mathew
“ Peniela leo ni siku ya pili simu yake haipatikani na sijui yuko wapi.” Akasema Jason
“ Are you sure she’s ok? Akauliza Mathew
“ Sina hakika sana kwa sababu jana nilikwenda nyumbani kwake lakini getini kulikuwa na makufuli na ilionyesha wazi kwamba hakukuwa na mtu ndani”
“ Ok Vizuri.Wakati tukimsubiri nitaanza uchunguzi wangu kwa Edson.Ninataka mnielekeze mahala alipokuwa akiishi na baada ya hapo mtaendelea na kazi zenu kama kawaida na mimi nitaendelea na kazi yangu,popote nitakapokwama na kuhitaji msaada wenu nitawaambia” akasema Mathew.Wakaendelea na kikao chao na kupeana maelekezo kadhaa halafu Jason na Mathew wakaeleekea mahala alipokuwa akiishi Edson.
“ Umeshawahi kuonana na huyo kijana Edson? Akauliza Mathew wakiwa garni
“ Hapana sijawahi kuonana naye hata mara moja”
“ Umewahi kuingia ndani mwake?
“ Ndiyo nimeingia mara moja tu wakati kesi ikiendelea.Kuna wakati iliilazimu mahakama ihamie hapa kuthibitisha madai ya upande wa mashtaka.”
“ Ok Good.” Akasema Mathew na safari ikaendelea.
Jason akaegesha gari nje ya nyumba aliyokuwa akiishi Edson
“ Ni hapa” akasema.Mathew akaitazama nyumba ile halafu akashuka na kumuomba Jason amsubiri garini.Akaelekea getini akabonyeza kengele ya getini na baada ya dakika moja mlango mdogo wa getini ukafunguliwa akatoka kijana mmoja .
“ Habari yako ndugu”
“ Habari yangu nzuri.Karibu sana.Nikusaidie nini? Akauliza Yule kijana
“ Samahani ndugu yangu.Nimemkuta Edson? Akauliza Mathew
“ Edson?!.. yule kijana akashangaa
“ Ndiyo Edson.”
“ Yawezekana umekosea nyumba.Hakuna Edson anayeishi humu ndani”
“ Yawezekana nimekosea .Ninaishi nje ya nchi na mara ya mwisho nilipokuja huku Tanzania Edson alinileta hapa mahala alipokuwa anaishi na ndiyo maana nimekuja moja kwa moja hapa.Yawezekana nimepotea nyumba lakini kumbukumbu zangu zinaniambia ni hapa hapa.” Akasema Mathew
“ Anafanya kazi wapi huyo Edson? Pengine naweza kukusaidia kumtafuta “ akasema Yule kijana
“ Edson anafanya kazi ikulu” akajibu Mathew
Yule kijana akamtazama Mathew kwa mshangao kidogo na kuuliza
“ Mara ya mwisho mliwasiliana lini ?
“ Nina zaidi ya mwaka sasa sijawasiliana naye”
“ Dah ! pole sana kaka.Kama unamuongelea huyo kijana aliyekuwa akifanya kazi ikulu ni kweli alikuwa akiishi hapa lakini inasemekena aliuawa na ndiyo maana wazazi wake wakaamua kuiuza nyumba hii”
Mathew akaonyesha mstuko mkubwa.
“ Dah sikuwa na taarifa hizo.Ahsante sana kwa taarifa hizo ndugu yangu.Nitakwenda kuwapa pole wazazi wake” akasema Mathew na kurejea garini.
“ Wazazi wa Edson wamekwisha iuza nyumba hii .Kwa maana hiyo vitu vyote vya Edson viliondolewa hapa na nina hakika vilipelekwa nyumbani kwa wazazi wake.Nahitaji kukagua vitu vyake.Nahitaji kuikagua simu aliyokuwa akiitumia na kompyuta yake kama bado vipo.“ akasema Mathew
“ Kama ni hivyo itatulazimu kwenda nyumbani kwa wazazi wake na kuonana nao na kuwaomba kupitia vitu hivyo” akasema Jason
“ Hiyo ndiyo hatua inayofuata.Unafahamu mahala wanakoishi wazazi wake?” Akasema Mathew.
“ Ndiyo ninapafahamu.Baba yake ni mtu maarufu sana hapa mjini..” akasema Jason..
“ Ok.Kama tukionana na wazazi wa Edson tukaongea nao tunaweza kupata japo sehemu ya kuanzia.” Akasema Mathew.
TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO………
 
SEASON 1
SEHEMU YA 13
MTUNZI : PATRICK .CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Dah ! pole sana kaka.Kama unamuongelea huyo kijana aliyekuwa akifanya kazi ikulu ni kweli alikuwa akiishi hapa lakini inasemekena aliuawa na ndiyo maana wazazi wake wakaamua kuiuza nyumba hii”
Mathew akaonyesha mstuko mkubwa.
“ Dah sikuwa na taarifa hizo.Ahsante sana kwa taarifa hizo ndugu yangu.Nitakwenda kuwapa pole wazazi wake” akasema Mathew na kurejea garini.
“ Wazazi wa Edson wamekwisha iuza nyumba hii .Kwa maan hiyo vitu vyote vya Edson viliondolewa hapa na nina hakika vilipelekwa nyumbani kwa wazazi wake.Nahitaji kukagua vitu vyake.Nahitaji kuikagua simu aliyokuwa akiitumia na kompyuta yake kama bado vipo“ akasema Mathew
“ Kama ni hivyo itatulazimu kwenda nyumbani kwa wazazi wake na kuonana nao na kuwaomba kupitia vitu hivyo” akasema Jason
“ Hiyo ndiyo hatua inayofuata.Unafahamu mahala wanakoishi wazazi wake?” Akasema Mathew.
“ Ndiyo ninapafahamu.Baba yake ni mtu maarufu sana hapa mjini..” akasema Jason..
“ Ok.Tunaweza kupata japo sehemu ya kuanzia.” Akasema Mathew.
ENDELEA………………………………………………….
Jason na Mathew wakawasili katika makazi ya wazazi wa Edson.Lilikuwa ni jumba kubwa la kifahari lililozungukwa na ukuta mkubwa.
“ Wow ! inaonekana wazazi wake ni watu wenye kujiweza sana kiuchumi” akasema Mathew
“ Ndiyo.Wanamiliki biashara kadhaa kubwa kubwa hapa mjini.Ni watu wenye kujiweza sana” akasema Jason huku wakishuka na kuelekea katika geti.Mathew akabonyeza kengele ya getini na mlinzi aliyekuwa amevaa sare za kampuni binafsi ya ulinzi akafungua mlango mdogo wa geti
“ Habari zenu jamani” akawasabahi
“ Habari zetu nzuri.Habari za hapa?
“ Za hapa nzuri.Niwasaidie nini? Akauliza Yule mlinzi
“ Tuna hitaji kuonana na mzee Robinson Kobe”
“ Mzee si rahisi kumpata mida hii.Yuko katika shughuli zake.”
“ Vipi kuhusu mama? Yeye tunaweza kumpata? Akauliza Mathew
“ Hata mama naye ametoka “
“ Unaweza kutuelekeza mahala tunakoweza kumpata mama au mzee?
“ naweza kuwaelekeza ofisi ya mama ilipo lakini mzee ni mtu mwenye mizunguko mingi sana na kumpata si rahisi hata kidogo” akasema mlinzi na kuwaelekeza katika ofisi ya Bi Hellen Kobe mama wa Edson.Bila kupoteza muda Mathew na Jason wakaingia garini na kuelekea Kobe Shopping mall ambao ndiko iliko ofisi ya Bi Hellen.
Waliwasili Kobe’s shopping mall wakaegesha gari na kushuka wakaingia ndani ya jengo.Watu walikuwa wengi sana wakifanya manunuzi ndani ya jengo hili lililokuwa na biashara nyingi ndani yake
Kwa kutumia Lifti wakapanda hadi ghorofa ya tano iliko ofisi ya Bi Hellen Kobe mama wa Edson
“ Sina hakika kama Bi Hellen atakubali kuongea nasi endapo ataniona” akasema Jason
“ Kwa nini? Akauliza Mathew
“ Ananifahamu .Tumekuwa tukionana mahakamani wakati wa kesi na ananifahamu mimi ndiye wakili niliyemtetea mtuhumiwa wanayeamini kwamba ndiye alimuua mtoto wao.Lazima atakuwa na hasira nami” akasema Jason
“ Usijali Jason.Ataongea tu” akasema Mathew kwa kujiamini
Kabla ya kuingia katika ofisi ya Bi Hellen Kobe iliwalazimu waonane kwanza na katibu muhtasi wake ambaye aliwasiliana naye na kuwaruhusu waingie wakaonane naye.Wakati wakiingia ndani ya ofisi Bi Hellen,alikuwa anaongea na simu na mara tu alipokutanisha macho na Jason,mkono wa simu ukamponyoka na kuanguka mezani.Alistuka sana.
“ Ouh my gosh ! This is unbelievable !!..akasema Bi Hellen
“ You again….!!..Umeamua kunifuata hadi huku..!! akafoka Bi Hellen
Jason na Mathew hawakusema kitu wakaingia mle ofisini na kusimama mbele ya meza.
“ Shikamoo mama” akasema Mathew.Bi Hellen hakujibu kitu akainua mkono wa simu na kumpigia katibu muhtasi wake
“ Irene naomba tafadhali watoe watu hawa ofisini kwangu haraka sana.” Akasema kwa ukali Bi Hellen.Mathew akamnong’oneza kitu Jason ,akatoka mle ofisini.Bado Bi Hellen aliendelea kumuangalia Mathew kwa jicho kali hata baada ya Jason kutoka.Katibu muhtasi wa Bi Hellen akaingia mle ndani kwa ajili ya kumtoa Mathew ,huku akitabasamu Mathew akamwambia
“ Its ok Irene.Nina maongezi kidogo na mama ya muhimu sana.Naomba dakika tatu halafu nitatoka.We’re not here for trouble” Irene akamtazama Bi Hellen ambaye alimtazama Mathew usoni kwa sekunde kadhaa halafu akamfanyia ishara aketi kitini.
“ mama naomba nikusalimu tena shikamoo” akasema Mathew baada ya kuketi
“ Marahaba kijana.Una shida gani manake Yule mwenzako tayari amekwisha niharibia siku yangu.Simpendi na sitaki hata kumtia machoni”
“ Mama utanisamehe kwa kuongozana naye lakini ilinilazimu kufanya hivyo kwa sababu jambo lililonileta hapa hata yeye linamhusu vile vile” akasema Mathew
“ Ni jambo gani hilo lililowaleta? Akauliza Bi Hellen
“ Ni kuhusiana na mwanao Edson”
Bi Hellen akastuka kidogo
“ Edson?!
“ Ndiyo mama”
“ Unataka kunieleza nini kuhusu Edson?
“ Mama ,mimi naitwa Mathew ni mtu ninayefanya kazi za kiuchunguzi na kwa sasa ninafanya uchunguzi kuhusiana na kifo cha mwanao Edson” akasema Mathew
Bi Hellen akavuta pumzi ndefu ,akaweka kalamu yake mezani na kusema
“ Sikuelewi una maanisha nini unaposema unafanya uchunguzi wa kifo cha mwanangu.Tayari uchunguzi ulikwisha fanyika na muuaji akapatikana,akapandishwa kizimbani lakini kwa sababu wanazozijua wao mahakama ikamuachia huru,sasa unanishangaza unaposema kwamba unafanya uchunguzi wa kifo cha Edson” akasema Bi Hellen
“ Mama ,ninatamani sana tuongee jambo hili kwa upana wake lakini hapa si mahala pake.Naomba kama utakuwa tayari tuonane jioni ya leo nyumbani kwako ukiwa wewe na mzee na tutaongea kwa kina kuhusiana na jambo hili” akasema Mathew
“Mathew naona unanipotezea muda wangu wa kufanya kazi.Hakuna haja ya kufanya uchunguzi tena wakati kila kitu kiko wazi na muuaji alikwisha patikana lakini akaachiwa huru.Sisi tumekwisha muachia Mungu”
Mathew akamtazama Bi Hellen kwa makini na kusema
“ Mama ,mtu mnayeamini kwamba ndiye aliyemuua mwanenu siye.Peniela hakumuua Edson” akasema Mathew huku akiinuka.
“ Saa moja jioni ya leo nitakuja kuzungumza nanyi.Hakikisha mzee naye yupo ili tuzungumze sote kwa pamoja” akasema Mathew na kuondoka.Moja kwa moja akaelekea mahala walikoegesha gari ambako alimkuta Jason akimsubiri garini
“ Nilifahamu toka mwanzo Yule mama asingekubali kuongea nasi pindi akiniona.She hates me” akasema Jason
“ Usijali Jason.Jukumu letu ni kuwahakikishia kwa vitendo kwamba Penny hakumuua kijana wao.Si rahisi kukuamini kwa sasa lakini itafika wakati ambao wataamini tu. Jason nipeleke nyumbani kwa Penny” akasema Mathew.
“ Nyumbani kwa penny? Jason akashangaa kidogo
“ Yah ! nataka kwenda nyumbani kwa Penny”
“ Penny hayupo nyumbani kwake na hakuna anayeelewa yuko wapi”
“ Usijali Jason.Take me there” akasema Mathew huku akiendelea kuipekua kompyuta yake ndogo.
Baada ya Mathew kutoka mle ofisini ,Bi Hellen alimuita katibu muhtasi wake na kumuomba ampatie dawa zake kwani tayari alianza kujisikia vibaya.Maneno aliyoambiwa na Mathew yalimchanganya sana.
“ Yule kijana ni nani? Akawaza
“ Nani kamtuma afanye uchunguzi huo wakati uchunguzi wa awali ulikwisha fanyika na muuaji akapatikana? Kwa nini aliongozana na Yule wakili aliyemtetea muuaji wa mwanangu? Akawazza Bi Hellen akiwa amekiegemeza kichwa chake kitini.Hakujisikia tena kutaka kufanya kazi yoyote
“ No! hakuna mtu mwingine aliyemuua mwanangu zaidi ya Yule kahaba Peniela.Yeye ndiye aliyekutwa eneo la tukio na kuna kila ushahidi unaoonyesha kwamba ndiye aliyermuua Edson.Simuelewi huyu kijana anaposema kwamba anataka kufanya uachunguzi wakati uchunguzi ulikwisha fanyika na Mahakama ikamuachia mtuhumiwa” akaendelea kuwaza Bi Hellen na kuhisi mwili wake kuanza kutokwa na jasho jingi,akamuita dereva wake na kumuomba amrejeshe nyumbani
“ Yule kijana Mathew amenichanganya sana.Nashindwa nimuamini ama vipi.Amekitonesha kidonda changu kinachojaribu kupona” akawaza Bi Hellen akiwa garini kurejea nyumbani
*********
Jason na Mathew waliwasili nyumbani kwa Peniela.
“ Nisubiri humu humu garini” akasema Mathew huku akivaa glovu na kushuka akaenda getini,akatoa kidude Fulani toka katika koti lake na kulifungua kufuli lililofungiwa mlango mdogo wa geti akaufungua na kuingia ndani.
“ Huyu Mathew anaenda kufanya nini nyumbani kwa Penny wakati mwenyewe hayupo? Itakuaje iwapo Penny atagundua kwamba tumeingia ndani mwake wakati hayupo? Nina hakika akigundua hilo hataniamini tena na kuna hatari hata ukaribu mimi na yeye utapungua. I cant let that happen kwa sababu nina mipango mikubwa kuhusu Penny. Sijapendezwa na namna anavyoifanya kazi yake huyu jamaa” akawaza Jason akiwa garini
Ukuta ulioizunguka nyumba ya Peniela uliwekwa vipande vidogo vidogo vya chupa kwa juu.Mathew akapanda juu ya pipa tupu na kuweka kidude Fulani kati kati ya chupa zile akashuka na kuelekea katika majani mazuri yaliyooteshwa mbele ya nyumba ile ,akaufungua mkoba wake na kutoa kitu fulani mfano wa kipepeo akakibonyeza na kukirusha katikati ya majani yale.Yeyote ambaye angekiona angejua moja kwa moja yule ni kipepeo halisi. Kisha maliza kuviweka vitu vile akatoka akafunga geti na kurejea garini.
“ We can go now” akasema Mathew.Jason akavuta pumzi ndefu na kuliondoa gari maeneo yale.
*********
Katika jengo moja pembeni kidogo ya jiji la Dare s salaam,watu nane wameizunguka meza kubwa ya duara.Ni saa ya pili sasa wako katika kikao kizito.Mtu mmoja mwembamba mrefu ambaye uso wake ulikuwa umekunjana kwa hasira alikuwa akiongea kwa sauti kubwa
“Narudia kusema kwamba sitauvumilia tena uzembe kama huu mlioufanya.Haiwezekani siku ya pili leo msijue mahala aliko Penny.Amekwenda wapi? Mmempoteza vipi katika mitambo yenu wakati mlipaswa kumfuatilia saa ishirini na nne ? Naomba nirudie tena kuwaweka wazi kwamba Peniela ndiye dira yetu. Bila yeye hakuna kitu kinachoweza kufanyika.Operesheni 26B haiwezi kufanikiwa bila yeye.Kwa mwaka mzima ambao alikuwa gerezani akituhumiwa kila kitu kilisimama,na kwa sasa wakati amerejea na kila kitu kimeanza kwenda upya mnafanya tena uzembe.Ninaapa kwa mbingu na nchi kwamba sintouvuilia uzembe wa aina yoyote ile kuanzia sasa.Peniela anatakiwa afuatiliwe kwa saa ishirini na nne. Hamtakiwi kumuacha hata dakika moja.Nawaweka wazi kwamba endapo operesheni 26B itashindwa kufanikiwa kwa sababu ya uzembe tu wa watu basi tujihesabu sisi sote ni marehemu.I want to live,I don’t want to die so I cant lost my soul because of one stupid.If you mess again you’ll die first” akasema kwa ukali Yule jamaa.Watu wote walikuwa kimya wakimsikiliza na walionekana kuingiwa na woga mwingi.Kijana mmoja aliyevalia suti nyeusi na shati jekundu akakohoa kidogo na kusema
“Captain,tulijitahidi kumfuatilia Penny kwa karibu lakini kifaa ambacho huwa anatumia kwa ajili ya mawasiliano nasi kilizimwa usiku wa manane.Tulipokwenda asubuhi nyumbani kwake kufanya uchunguzi tulikutana na makufuli,Penny hakuwepo.Toka amemaliza kesi iliyokuwa ikimkabili Penny anaonekana hataki tena kushirikiana nasi.Hatoi ushirikiano wa aina yoyote.Sina hakika kama yuko tayari kuendelea na operesheni hii” akasema Yule kijana na kumfanya Captain agonge meza kwa hasira
“ Kwa nini mlienda asubuhi?? Ilitakiwa muda ule ule ambao mmeona tukio lile la kukatika kwa mawasiliano mngenitaarifu mara moja ili nijue nini cha kufanya.Uzembe wenu unatugharimu sisi sote.Narudia tena kwamba hili ni onyo la mwisho.Kuhusu Penny kutotoa ushirikiano hilo niachieni mimi.Atake asitake lazima afanye tunavyotaka sisi na si vinginevyo.” Akanyamaza kidogo halafu akaendelea
“ Leo usiku nina kikao na wakuu cha kujadili kuhusu operesheni 26B ambayo inatakiwa kuzinduliwa rasmi upya.Kabla sijaelekea kikaoni usiku wa leo nahitaji kupata taarifa kwamba tayari mmekwisha fahamu mahala alipo Penny.Kuanzia sasa nendeni tena katika vifaa vyenu,fungueni kompyuta zenu,nendeni katika satellite na mjue wapi aliko Penny.Mna kila kitu kinachotakiwa kwa hiyo ifanyeni kazi na kabla ya saa mbili usiku wa leo nataka ripoti.” Akasema kwa ukali Captain na kutoka mle katika chumba cha mikutano akaingia ofisini kwake akajifungia.Alihisi kichwa kizito kwa mawazo.
TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO……
 
SEASON 1
SEHEMU YA 14
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Kwa nini mlienda asubuhi?? Ilitakiwa muda ule ule ambao mmeona tukio lile la kukatika kwa mawasiliano mngenitaarifu mara moja ili nijue nini cha kufanya.Uzembe wenu unatugharimu sisi sote.Narudia tena kwamba hili ni onyo la mwisho.Kuhusu Penny kutotoa ushirikiano hilo niachieni mimi.Atake asitake lazima afanye tunavyotaka sisi na si vinginevyo.” Akanyamaza kidogo halafu akaendelea
“ Leo usiku nina kikao na wakuu cha kujadili kuhusu operesheni 26B ambayo inatakiwa kuzinduliwa rasmi upya.Kabla sijaelekea kikaoni usiku wa leo nahitaji kupata taarifa kwamba tayari mmekwisha fahamu mahala alipo Penny.Kuanzia sasa nendeni tena katika vifaa vyenu,fungueni kompyuta zenu,nendeni katika satellite na mjue wapi aliko Penny.Mna kila kitu kinachotakiwa kwa hiyo ifanyeni kazi na kabla ya saa mbili usiku wa leo nataka ripoti.” Akasema kwa ukali Captain na kutoka mle katika chumba cha mikutano akaingia ofisini kwake akajifungia.Alihisi kichwa kizito kwa mawazo.
ENDELEA…………………………………
Saa moja kasoro dakika nane za jioni,Mathew alisimamisha gari nje ya nyumba ya Bwana na Bi Robinson Kobe wazazi wa Edson.Jioni hii alikuwa ameambatana pia na wakili Jason.Geti lilifunguliwa wakaingia ndani
“ Mathew una hakika watakubali kuongea nasi wakiniona nimeongozana nawe? Akauliza Jason kwa wasi wasi
“ Usijali Jason.Wataongea nasi tu” akasema Mathew huku akibonyeza kengele ya mlango wa sebuleni ambao ulifunguliwa na mwanadada mmoja mwembamba mrefu.Aliwakaribisha sebuleni na kuwahudumiwa vinywaji na baada ya dakika kama tatu hivi wazazi wa Edson wakatokea.Bi Hellen alikuwa anatembea kwa uchovu na ilionekana wazi kwamba hali yake haikuwa nzuri.Hii ilitokana na mstuko alioupata mchana baada ya kuongea na Mathew na kumkumbusha kuhusiana na kifo cha mwanae Edson .Jason na Mathew wakasimama na kuwasalimu wazee wale kwa heshima .Bado Bi Hellen aliendelea kumuangalia Jason kwa macho makali sana .Ilionyesha wazi kwamba hakupendezwa na uwepo wake pale
“ Karibuni vijana” akasema mzee Robinson Kobe
“Nimeambiwa kwamba mna jambo mnataka kuzungumza nasi”
“ Ndiyo mzee.Tulionana na mama mchana na tukaomba tukutane na kuonana nanyi.Tuna jambo tunataka kuzungumza nanyi wazee wetu” akasema Mathew
“ Ni kuhusu nini? Akauliza mzee Robinson
“ Ni kuhusu mwanetu Edson”
“ Kuna jambo gani kumuhusu Edson? Kesi yake imekwisha malizika na mtuhumiwa akaachiwa huru.Huyo mwenzako anafahamu kila kitu kwani yeye ndiye aliyekuwa akimtetea mtuhumiwa” akasema mzee Robinson
“ Nalifahamu hilo mzee” akasema Mathew na kunyamaza kidogo kisha akaendelea
“ Wazee wangu naomba kwanza nijitambulishe kwenu kwa sababu huyu mwenzangu tayari mnamfahamu.Mimi naitwa Mathew Kwanga.Kazi yangu ni mchunguzi wa kimataifa.Ninapokea na kufanya kazi mbali mbali za kiuchunguzi toka sehemu mbali mbali duniani” akanyamaza kidogo na kuendelea
“ Nilifuatwa na ndugu zangu hawa wawili.Jason na mwingine ambaye tulitakiwa kuwa naye hapa lakini amepata udhuru .Yeye ni Jaji Elibariki ambaye alikuwa akiisikiliza kesi ya mauaji ya Edson.” Akasema Mathew.Wazazi wa Edson wakatazamana baada ya jina la Jaji Elibariki kutajwa
“ Ndugu zangu hawa “ akaendelea Mathew
“ Waliniomba niwasaidie kufanya uchunguzi kuhusiana na kifo chenye utata cha kijana wenu Edson na kumfahamu nani muuaji”
Kabla hajaendelea mzee Robinson akaingilia kati
“ Kijana Uchunguzi ulikwisha fanyika na mtuhumiwa akapatikana japokuwa mahakama kwa sababu wanazozijua wao wakamuachia huru. Sioni haja ya kufanya tena uchunguzi kwa sababu jambo hili sisi tumekwisha muachia Mungu kwani yeye pekee ndiye mwenye kutenda haki.Duniani hapa hakuna haki” akasema mzee Robinson akionekana kukata tamaa
Jason aliyekuwa kimya toka wamefika akakohoa kidogo na kusema
“ Mzee naomba na mimi niongee kidogo” akasema huku akitazamana na mzee Robinson.Akaendelea
“ Naomba niwafahamishe wazee wangu kwamba Peniela siye muuaji wa Edson?
Kauli ile ilimfanya mzee Robinson amtazame kwa jicho kali na kusema
“ Kijana ,nafahamu kwamba wewe ni mwanasheria mahiri kabisa na umeifanya kazi yako vyema ya kuishawishi mahakama ikakubali kumuachia huru mteja wako.Najua hata siku moja hutakubali kwamba mteja wako alimuua mwanetu.Yote hii ni kwa sababu anakulipa pesa nyingi.Pesa inaweza kufanya jambo lolote hata kupindisha sheria na wenye hatia wakaachiwa huru.Ndiyo maana hapo awali nilisema kwamba haki inapatikana mbinguni tu.Huku duniani hakuna haki.” Akasema mzee Robnson
“Hapana mzee.Si hivyo unavyofikiri.Sheria na Mahakama vimewekwa ili kutoa haki.Mahakama haiko kwa ajili ya kupindisha sheria na kulipendelea kundi fulani la watu kwa sababu ya pesa zao au nafasi zao.Peniela aliachiwa huru baada ya mahakama kuridhika kwamba hakuwa na hatia.Hakutenda kosa.Hakumuua Edson.Baada ya kesi kumalizika na Peniela kuachiwa huru ,Jaji Elibariki ambaye ndiye aliyetoa hukumu ile alinifuata na kunieleza nia yake ya kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na kifo cha Edson.Aliamua kufanya hivyo kutokana na sintofahamu nyingi alizozigundua katika mwenendo mzima wa kesi ile.” Jason akanyamaza kidogo na kusema
“ Kumekuwa na maneno mengi na hisia tofauti kuhusiana na hukumu ile kwa hiyo tunataka tufanye uchunguzi wa kina tuufahamu ukweli.Tumfahamu muuaji wa edson na kumfikisha sehemu husika apate adhabu stahili.Kwa kuwa sisi ni wanasheria na hatuna taaluma ya kiuchunguzi tumeamua kutumia gharama zetu kumkodisha huyu ndugu yetu Mathew aweze kuifanya kazi hiyo.Yeye amebobea katika masuala haya ya kiuchunguzi,amekwisha fanya kazi katika idara mbali mbali nyeti za kiusalama hapa nchini kabla ya kuamua kufanya kazi zake binafsi.Kabla ya kuanza kufanya uchunguzi wake Mathew ameona ni bora aje azungumze nanyi mambo kadhaa. “ akasema Jason.Kimya kikatawala pale sebuleni.Mzee Robinson aliinama akatafakari huku akikuna kichwa chake.Baada ya dakika mbili akainua kichwa na kusema
“Natamani niamini maneno uliyoniambia kijana wangu lakini nafsi yangu inakataa kabisa. Sidhani kama kuna kitu cha kunishawishi niamnini kwamba Penny siye aliyemua mwanangu” akasema mzee Robinson
“ Mzee wangu sina kitu cha kukushawishi kwa sasa lakini naomba unipe muda kidogo tu na nitakuwa na cha kukukushawishi uamini hivyo.Ninachohitaji toka kwenu sasa ni ushirikiano tu” akasema Mathew.Mzee Robinson akainama akafikiri na kusema
“ Unahitaji nini toka kwetu?
“ Mzee,mimi ni mzoefu katika masuala haya .Nimekwisha fanya chunguzi mbali mbali za vifo vyenye utata kama hiki cha mwanao.Mara nyingi kinapotokea kifo kama hiki kunakuwa na sababu Fulani nyuma yake.Sitaki kuongea sana lakini ninachotaka kukisema ni kwamba tutaifahamu sababu hiyo na kwa nini Edson aliuawa.Sahauni uchunguzi uliopita na tushirikiane katika uchunguzi huu tunaotaka kuufanya. Kitu cha kwanza ninachotaka kukifahamu toka kwenu japo kwa ufupi tu ni kuhusiana na mwanenu Edson alikuwa ni mtu wa namna gani?
Mzee Robinson akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Edson alikuwa ni mtoto pekee wa kiume kati ya watoto wanne tulionao.Kimakuzi Edson tumemlea katika maadili mazuri.Alikuwa ni kijana mtaratibu sana na asiye na makuu.Alipohitimu shahada yake ya mawasiliano nchini marekani alirudi nchini na akapata kazi katika kampuni moja ya simu na baadae akapata kazi ikulu katika kitengo cha mawasiliano ambako alifanya kazi hadi mauti yalipomkuta.Kitabia Edson hakuwa na tabia ambayo naweza kusema kwamba ni mbaya,hakuwa mnywaji wa pombe ,wala mtumiaji wa kilevi chochote kile.Muda mwingi aliutumia kwa kusoma na kufanya kazi zake.Alipoanza kazi ikulu alianzisha mahusiano na kimapenzi na Anna binti wa rais.Urafiki wao ulianza toka wakiwa wadogo kwa sababu familia zetu mbili ni familia rafiki kwa muda mrefu sana.Baada ya kuingia katika mahusiano na Anna,tuliamua kumpatia moja ya nyumba zetu aishi ili aweze kuwa huru.Edson na Anna walipendana sana na sote tulikuwa na matarajio makubwa kwamba siku moja familia zetu mbili zingeweza kuunganishwa na hawa vijana lakini ghafla tukasikia kwamba wamefarakana na tayari Edson alikuwa katika mahusiano na msichana mwingine aitwaye Peniela.Hatukutaka kuingilia mambo yake ya kimahusiano tukamuacha aendelee na Peniela hadi pale mauti yalipomkuta.Kwa ufupi hivyo ndivyo ninavyoweza kumuelezea mwanangu Edson japokuwa kuna mambo mengi sana ambayo naweza kuyaeleza. Kuhusiana naye” akasema mzee Robinson
“ I see….He was a nice guy..” akasema Mathew
“ Yah ! ..” akajibu mzee Robinson
“ Siku chache kabla ya kifo chake ulifanikiwa kuonana naye? Alikuwa katika hali gani? Kuna kitu chochote ambacho hakikuwa cha kawaida kwa namna ulivyomuona? Akauliza Mathew.Mzee Robinson akafikiri kidogo na kusema
“ Nilionana naye wiki mbili kabla ya kifo chake.Alikuja ofisini kwangu tukaongea kidogo akaondoka.Alikuwa katika hali ya kawaida kabisa.Ninachokumbuka ni siku tatu kabla ya kifo chake alimpigia simu mama yake usiku na kuongea naye.Alikuwa anamsalimu tu.Hakuwa na kawaida ya kupiga simu usiku lakini hakusema kama ana tatizo lolote ” akasema mzee Robinson
“ Nilifika katika nyumba aliyokuwa akiishi Edson nikaambiwa kwamba umeiuza” akasema Mathew
“ Ndiyo niliamua kuiuza ile nyumba. Sikutaka kuendelea kuimiliki ile nyumba baada ya mwanangu kuuliwa ndani yake” akasema mzee Robinson
“ Vifaa vyake mmevihifadhi wapi? Akauliza Mathew
“ Tuna nyumba ndogo iko huko nyuma ndiko tumevihifadhi”
“ Nitahitaji kuvipitia baadhi ya vitu vyake kama vitabu vya kumbu kumbu ili tuonne kama kuna kumbu kumbu yoyote isiyo ya kawaida ambayo anaweza kuwa aliiweka vitabuni ,vile vile kompyuta yake pamoja na simu” akasema Mathew
“ Edson alikuwa na vitabu vingi sana kwani alikuwa msomaji mzuri.Nadhani tunaweza kuchukua siku kadhaa kuvipitia vyote kuchambua kimoja kimoja.Kuhusu kompyuta zake ni kwamba hazikuwahi kuonekana na hatujui ni nani aliyezichukua.Simu yake pia haikuwahi kuonekana.Hatuelewi ni kwa nini vitu hivi vilitoweka katika mazingira yenye utata mkubwa. Akasema mzee Robinson
“ Baba Eddy..! akaita Bi Hellen
“ Kuna kitu nimekikumbuka.Katika mojawapo ya chungu cha maua kilichokuwa chumbani kwake siku tunahamisha vyombo vyake ilianguka laini ya simu ambayo nimeihifadhi ndani.Nadhani inaweza ikawa ni ile laini ya simu ambayo aliitumia aliponipigia simu mara ya mwisho kwa sababu hakutumia namba zake ninazozifahamu.” akasema Bi Hellen
“ Ok,nitaomba unipatie laini hiyo ya simu ili tuifanyie uchunguzi.Inaweza ikawa na jambo la muhimu kwetu” akasema Mathew na Bi Hellen akainuka akaelekea chumbani kuchukua laini ile ya simu
“ Bado sijapata jibu ni kwa nini muuaji aliondoka na kompyuta na simu wakati Edson alikuwa na kiasi cha shilingi milioni ishirini ndani.” Akasema mzee Robinson
“ Shida yao haikuwa pesa.Kuna kitu walichokuwa wakikitafuta ambacho ni zaidi ya pesa” akasema Mathew
“ Kwa mbali hata mimi ninaanza kupata picha kwamba mauaji ya kijana wangu ni tofauti kabisa na tunavyofikiri.Yawezekana kuna mtu au kitundi cha watu waliofanya mauaji yale na si Yule msichana aliyekuwa akituhumiwa” akasema mzee Robinson.Mathew na Jason wakatazamana.
“ Ahsante sana mzee kwa kuliona hilo.Jukumu letu sasa ni kubaini mtu huyo au kikundi cha watu waliotekeleza mauaji hayo “ akasema Mathew .Bi Helen akarejea na kumpatia ile laini ya simu aliyoikuta katika vifaa vya Edson
“ Wazee wangu nashukuru kwa kutusikiliza .Mimi na wenzangu tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha kwamba tunaufahamu ukweli.Nitakuwa nikiwapa taarifa za mara kwa mara kuhusiana na uchunguzi wetu unavyoendelea .Ninachoomba suala hili liwe ni la siri na asifahamu mtu mwingine yeyote kwamba kuna uchunguzi unaendelea .” akasema Mathew
“ Msijali vijana wangu,muda wowote mnakaribishwa.Hapa ni nyumbani kwenu na milango iko wazi muda wote.Chochote mnachokihitaji msisite kutueleza tuwasaidie.” Akasema mzee Robinson
“ Tunashukuru sana wazee wetu.Sisi tutajitahidi kwa kila tuwezavyo kuhakikisha tumelichimba suala hili hadi katika mzizi wake na tuufahamu ukweli.Endapo kuna chochote kile mnaachoona kinaweza kutusaidia katika uchunguzi wetu msisite kututaarifu” akasema Mathew. Wakaagana na kuondoka.
“ Tayari kuna mwanga umeanza kuonekana,” akasema Mathew
“ kuna sababu iliyowafanya watu watu waliofanya mauaji ya Edson waondoke na kompyuta zake na simu.Kuna kitu gani walikuwa wanakificha? Kwa kuwa Edson alikuwa katika masuala ya mawasiliano inawezekana kuna jambo alikuwa analifahamu ambalo hakupaswa kulifahamu na kusababaisha kifo chake.Tutajua tu ni jambo gani hilo” akasema Mathew.Jason akaitika kwa kichwa alikuwa kimya sana .Mawazo yake yote yalikuwa kwa Peniela.Alijiuliza maswali mengi mahala aliko na kwa nini ameizima siku yake
“ Baba Eddy !.. akaita Bi Hellen baada ya Mathew na Jason kuondoka
“ Niliwadharau wale vijana lakini wamenifumbua macho na kwa sasa hata mimi nimeanza kuamini kwamba kuna watu walimuua mwanangu kwa sababu maalum ingawa itanichukua muda mrefu kuamini kwamba Yule msichana Peniela hakuhusika na kifo cha Edson” akasema bi Hellen.Mzee Robinson akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Peniela hakumuua Edson” akageuka na kujifunika shuka akalala mke wake akabaki akimshangaa
*********
Jason alimfikisha Mathew nyumbani kwake na kisha akaendelea na safari ya kuelekea kwake.Mathew akaingia ndani mwake na kitu cha kwanza alichokifanya ni kuelekea katika chumba chake kikubwa kilichokuwa na runinga kubwa nane zilizotundikwa ukutani.Akaziwasha runinga zote na zikaanza kuonyesha picha zikaanza kuonekana.
“ wow ! my birds are working” akasema na kukaa kitini akaanza kufuatilia picha zile zilizokuwa zikionekana katika runinga.Runinga namba sita ilikuwa ikionyesha makazi ya Peniela.Vifaa vile mithili ya vipepeo Mathew alivyoviweka katika nyumba ya Peniela mchana vilikuwa ni kamera ambazo zilikuwa zikionyesha kila kilichokuwa kikiendelea katika makazi yale.Alizipeleka mbele picha zile na hakukuonekana mtu yeyote akiingia katika makazi yale hadi ilipotimu saa mbili na dakika ishirini na mbili.Geti dogo lilifunguliwa na watu wawili wakaingia kwa kunyata huku wakiwa na bastora mikononi.
“ Who are these people? Akajiuliza Mathew huku akiisogelea karibu runinga yake.
TUKUTANE TENA SEHEMU IJAYO……
 
SEASON 1
SEHEMU YA 15
ILIPISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Jason alimfikisha Mathew nyumbani kwake na kisha akaendelea na safari ya kuelekea kwake.Mathew akaingia ndani mwake na kitu cha kwanza alichokifanya ni kuelekea katika chumba chake kikubwa kilichokuwa na runinga kubwa nane zilizotundikwa ukuitani.Akaziwasha runinga zote na zikaanza kuonyesha picha zikaanza kuonekana.
“ wow ! my birds are working” akasema na kukaa kitini akaanza kufuatilia picha zile zilizokuwa zikionekana katika runinga.Runinga namba sita ilikuwa ikionyesha makazi ya Peniela.Vifaa vile mithili ya vipepeo Mathew alivyoviweka katika nyumba ya Peniela vilikuwa ni kamera ambazo zilikuwa zikionyesha kila kilichokuwa kikiendelea katika makazi yale.Alizipeleka mbele picha zile na hakukuonekana mtu yeyote akiingia katika makazi yale hadi ilipotuimu saa mbili na dakika ishirni na mbili.Geti dogo lilifunguliwa na watu wawili wakaingia kwa kunyata huku akiwa na bastora mikononi.
“ Who are these people? Akajiuliza Mathew huku akiisogelea karibu runinga yake.
ENDELEA………………………………
Watu wale wawili walikuwa makini sana wakiangaza huku na huko halafu wakaweka kitu Fulani kidogo katika mlango wa kuingilia sebuleni kwa Penny.
“ Wanaweka nini pale? Akajiuliza Mathew na kuikuza picha ili aone kitu kile kilichokuwa kimewekwa pale mlangoni.
“ Kamera !..” akasema kwa sauti ndogo
“ Wameweka kamera .Kwa nini wameweka kamera mlangoni? These people looks so professional” akawaza Mathew.
Baada ya kuweka kamera ile mlangoni kwa Peniela,kwa kutumia vifaa maalum wakafungua mlango wakaingia ndani.Mathew hakuweza kuona kilichokuwa kinaendelea ndani kwa sababu hakuwa ametega kamera yoyote ndani ya nyumba ya Penny.Baada ya kama dakika kumi hivi watu wale wakatoka na kuondoka na kuzidi kumchanganya Mathew
“ Watu wale ni akina nani? Wamefuata nini kwa Peniela? Akaendelea kujiuliza Mathew.Akarudisha tena picha nyuma na kuwatazama vizuri watu wale
“ Watu hawa ni akina nani ? kwa nini wameweka kamera mlangoni kwa Penny.Mle ndani waliingia kufanya nini? Akawaza huku akiendelea kuwatazama wale wale jamaa katika runinga.
“ Hapa kuna jambo ambalo si la kawaida.Watu hawa wamekuja wakiwa na bastora mkononi na tena wanaonekana ni watu makini na wazoefu.Mhh! suala hili si dogo kama ninavyolifikiri.Tayari nimepata sehemu ya pili ya kufanyia uchuguzi .Natakiwa kuwafahamu watu hawa ni akaina nani, na nini lengo la kuja kwa Peniela wakati mwenyewe hayupo.” Akawaza Mathew na kuprint zile picha za wale jamaa.
“Bado sipati jibu watu wale ni akina nani na kwa nini wameweka kamera nyumbani kwa Penny.Nadhani lengo lao ni kufuatilia kila kinachoendela pale. Inaonekana kuna watu ambao wanafuatilia nyendo za Penny na walifahamu fika kwamba kwa muda huu hayupo nyumbani ndiyo maana wakaingia na kufanya walichotaka kukifanya.Watu hawa lazima niwafahamu na nini lengo lao kwa Penny.Ninaanza kuwa na wasi wasi sana kuhusiana na maisha ya Penny.Inaonekana yuko katika hatari kubwa.Kuna watu wanaomfuatilia ambao sijui lengo lao ni nini .Penny yuko wapi? Kwa mujibu wa Jason ni kwamba siku ya pili leo Penny hajulikani yuko wapi .Kesho nitaanzia kazi kwa Penny.Lazima nifahamu yuko wapi ” Akawaza Mathew na kuondolewa katika mawazo na simu iliyoita.Zilikuwa ni namba ngeni katika simu yake
“ Hallow ! akasema
“ Hallow kaka,kuna mtu anahitaji kuongea nawe.” Ikasema sauti ya upande wa pili.Baada ya sekunde kadhaa akasikia sauti tamu ambayo aliitambua mara moja
“ Hallo Mathew” ikasema sauti ile
“ Anitha ! akasema Mathew
“ Niko hapa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere”
“ Ouh gosh ! Kwa nini hukuniambia utaingia muda gani ili nije nikupokee?
“ Hapana sikutaka kukusumbua Mathew.Hapa ni nyumbani.Nisubiri hapo hapo nyumbani nitachukua taksi” akasema Anitha na kukata simu
“ The hacker is here…” akasema Mathew kwa sauti ndogo huku akitabasamu.
“ Bado Noah.yeye aliniambia anakuja kesho.Kazi imeiva” akawaza Mathew huku akiendelea kuziangalia picha mbali mbali zilizokuwa zinapita katika runinga zilizokuwamo mle ndani.
**********
Penny alijiangalia katika kioo kikubwa ,kugeuka nyuma akajitazama na kutabasamu
“ Siku zote huwa sina wasi wasi na uzuri wangu” akasema Penny kwa sauti ndogo huku akiikoleza rangi ya mdomo.Akachukua kichupa kidogo cha uturi na kudondoshea matone machache shingoni.
“ Leo lazima Dr Joshua atapagawa na mimi.Ni muda mrefu sana hajakutana nami.Nitampa vitu adimu ambavyo vitampagawisha na kumchanganya .Huu ni wakati wa kutumia kila aina ya ujuzi nilionao ili niweze kuimaliza kazi” akawaza Penny huku akichukua mkoba wake mdogo na kufungua mlango.Nje ya mlango wake alisimama kijana mmoja aliyevalia nadhifu.
“ Uko tayari? Akauliza Yule kijana
“ Ndiyo niko tayari.Tunaweza kwenda” akasema penny na kuongozana na Yule kijana mpaka katika gari moja la kifahari akafunguliwa mlango na kuingia kisha wakaondoka.
“ Najua Jason na Jaji Eklibariki watakuwa wamenitafuta sana baada ya kutoniona kwa siku ya pili leo.Natamani niwataarifu kwamba niko salama lakini naogopa kwani Kareem alinionya nisimpigie simu mtu yeyote na kumfahamisha kwamba niko Arusha.” Akawaza Penny akiwa garini
“ Sijui wamefikia wapi ule mpango wao wa kumtafuta muuaji wa Edson.Nikirudi nitawashauri waachane na jambo hili kwani lina mkanganyiko mkubwa na ni hatari kwa usalama wao.Sitaki yeyote kati yao apatwe na tatizo lolote.Hawa ni watu wangu wa muhimu sana bila wao hivi sasa ningekuwa ninakula maharage ya jela. ” Akaendelea kuwaza na mara picha ya Jason ikamjia kichwani .
Saa tatu na dakika arobaini wakawasili Meru view hotel,moja kati ya hoteli kubwa sana afrika mashariki na kati.Ni katika hoteli hii ndipo alipofikia rais wa jamhuri ya mungano wa Tanzania Dr Joshua tayari kabisa kwa ajili ya kuongoza kikao cha wakuu wa nchi za afrika msahariki kinachotarajiwa kufanyika jijini Arusha kwa muda wa siku tatu.Ulinzi ulikuwa mkali sana kuizuguka hoteli hii na kila gari lililoingia hapa ililazimika kukaguliwa na askari.Gari alilopanda Penny halikukaguliwa likapita moja kwa moja hadi katika maegesho ya viongozi wakuu mlango ukafunguliwa na Penny akashuka.
“ Wow ! what a beautiful place” akawaza Penny huku akitabasamu akiifurahia mandhari ile ya kupendeza ya hoteli ile kubwa.Yule kijana ambaye hakuwa muongeaji alimuongoza Penny hadi katika mlango wa nyuma wakaingia ndani ya hoteli na kwa kutumia lifti wakapanda hadi ghorofa ya sita wakashuka na kulifuata varanda refu.Hakukuwa na mtu anayeranda randa katika ghorofa hii zaidi ya walinzi wa rais ambao walikuwa makini na kila aliyeonekana eneo hili. Hakuna kati yao aliyethubutu kumuuliza chochote Penny kwani alikuwa ameongozana na mmoja wa walinzi wa rais.Moja kwa moja akampeleka Penny hadi katika chumba cha rais akagonga mlango ukafunguliwa na Kareem mlinzi wa rais.
“ Penny karibu ndani” akasema Kareem huku akimshika mkono na kumuelekeza aketi sofani.Kilikuwa ni chumba kikubwa na kizuri mno.Kwa muda wa sekunde kadhaa Kareem aliendelea kuchezea simu yake halafu akainua kichwa na kusema
“ Unatumia kinywaji gani Penny?
“ Nipatie mvinyo tafadhali” akasema Penny.Kareem akamletea chupa ya mvinyo na kumuwekea mezani
“ Mheshimiwa rais bado yuko katika kikao.Utaendelea kumsubiri” akasema Kareem na kuendelea kuchezea simu yake kubwa
“ How’ve u been Kareem? Maisha yako yanakwendaje? Akaamua kuanzisha maongezi Penny baada ya kuona Kareem amekuwa kimya sana na ilionyesha hakutaka maongezi
“ I’m ok Penny.I’m doing fine.Samahani kama umeboreka lakini niko kazini.Tuna marais karibu watano watahudhuria mkutano mkubwa wa marais wa afrika mashariki kuanzia kesho kwa hiyo yatubidi tuwe macho sana katika ulinzi ndiyo maana unaniona nimekuwa kimya sana nafuatili akila kinachoendelea hapa hotelini”
“ Usijali Kareem.Ninaelewa” akasema Penny na kuelekeza macho yake runingani akitazama muziki
“ Kareem ! akaita Penny baada ya muda
“ Unasemaje Penny? Akauliza Kareem
“ Nitakuwepo hapa Arusha kwa muda gani?
“ As long as present wants” akajibu Kareem, kwa ufupi
“ No Kareem.I need to go back to Dar as soon as possible.” Akasema Penny
Kareem hakumsemesha kitu akaendelea na kazi zake
Saa sita na dakina nane mlango wa chumba cha rais ukafunguliwa na Dr Joshua rais wa jamhuri ya muungano akaingia
“ Where is she? Akamuuliza Kareem ambaye alimfanyia ishara kwamba tayari yuko chumbani
“ Thank you Kareem.Thank you so much.From now I need a privacy.No calls no any disturbance” akasema Dr Joshua
“ Ok Mr President” akajibu Kareem kwa adabu.Dr Joshua akakinyonga kitasa cha mlango na kuingia chumbani kwake.Ilimlazimu avue miwani yake ili ajiridhishe kwamba alichokuwa akikiona kitandani binadamu wa kawaida na si malaika .Kiumbe kilichokuwa kimejilaza katika kitanda kilichotandikwa mashuka mazuri meupe kilikuwa na uzuri usio wa kawaida.
“ Penny ! akaita
“ Dr Joshua ! akasema Penny kwa sauti ndogo.Dr Joshua akafunga mlango na kumuendea Penny akamkumbatia kwa nguvu
“ Welcome back my angel” akasema Dr Joshua .Penny hakutaka kupoteza muda akammwagia mzee Yule mabusu mfululizo na kumchanganya. Dr Joshua akajikuta akianza kuhema kwa nguvu.Taratibu akatoa ulimi na kuuingiza kinywani kwa Dr Joshua ambaye alianza kutoa miguno.Penny akamvua koti taratibu huku akiendelea kumfanyia manjonjo yaliyozidi kumpagawisha Dr Joshua. Taratibu akalegeza tai na kuitoa halafu akaanza kufungua vifungo vya shati .Alikichezea kifua cha mzee yule kwa ufundi mkubwa halafu akaufungua mkanda wa suruali yake ikaanguka chini akabakiwa na nguo ya ndani,Penny akaivuta taratibu nguo ile ya ndani akaishusha hadi magotini halafu akapiga magoti na kuanza kufanya utundu maeneo ya ikulu.Dr Joshua hakuwa akijiweza tena.Penny akamsukuma akangukia kitandani halafu akafungua zipu ya gauni lake likaanguka chini.Dr Joshua mate yakamtoka alipoushuhudia mwili mwororo wa kimalaika wa msichana aliyesimama mbele yake.Taratibu akaivua nguo yake ya ndani na kupanda kitandani na kuendeleza utundu.Dr Joshua alibaki akilalama kwa raha alizokuwa akipewa.Baada ya dakika kumi na tano tayari walikuwa wakiogelea katika ulimwengu wenye raha isiyoelezeka.
*******
“ Ouh Peniela..nakosa neno la kusema kwa raha ulizonipa.I missed you .I missed this….” Akasema Dr Joshua akiwa hoi baada ya kumaliza mzunguko mmoja.Penny akajiinua na kumsogelea akambusu na kukilaza kichwa chake kifuani
“ I missed you too Dr Joshua..Umri umekwenda lakini bado una nguvu kama kijana wa miaka kumi na nane.You make me so happy” akasema Penny
“ Muda wote uliokaa gerezani ukikabiliwa na kesi nilikosa raha na amani.Kwa sasa najiona kijana tena.You are amazing my angel” akasema Dr Joshua huku akizichezea nywele za Penny
“ Don’t lie to me Dr Joshua.Kama ningekuwa na umuhimu kwako usingekubali kuniona nikiteseka gerezani mwaka mzima kwa kosa ambalo sikulitenda na zaidi ya yote ulishinikiza nifungwe kifungo kirefu gerezani.You didn’t stand by my side.Pamoja na mateso yote na hata kunusurika kwenda maisha gerezani lakini sikufumbua mdomo wangu na kuongea lolote kuhusiana na kifo cha Edson.Ninajua wewe ndiye uliyeamuru watu wako wamuue Edson kwa sababu unazozijua mwenyewe lakini kwa kuwa ninakupenda Dr Joshua mpaka leo hii hakuna mtu anayefahamu chochote” akasema Penny na machozi yakamtoka alipomkumbuka Edson.Dr Joshua akamfuta machozi na kusema
“ Tafadhali usilie Penny.Usilie malaika wangu.Kuna mambo mengi ambayo yametokea kitu cha kwanza ninachokihitaji toka kwako ni msamaha wako.Ni kweli nilikuacha ukaingia katika matatizo makubwa na sikusimama pamoja nawe.Penny please forgive me my angel.We have so many to talk” akasema Dr Joshua.Penny akainua kichwa akamtazama na kusema
“ Nimekwisha kusamehe Dr Joshua na ndiyo maana niko hapa.Umesema tuna mambo mengi ya kuongea hata mimi nina mengi ya kuuliza lakini kwanza nataka unieleze kwa nini Edson aliuawa? Akauliza Penny.Dr Joshua akachukua kitambaa na kujifuta jasho,akainuka na kwenda mezani akajimiminia mvinyo na kupiga funda kubwa.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………
 
SEASON 1
SEHEMU YA 16
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Tafadhali usilie Penny.Usilie malaika wangu.Kuna mambo mengi ambayo yametokea kitu cha kwanza ninachokihitaji toka kwako ni msamaha wako.Ni kweli nilikuacha ukaingia katika matatizo makubwa na sikusimama pamoja nawe.Penny please forgive me my angel.We have so many to talk” akasema Dr Joshua.Penny akainua kichwa akamtazama na kusema
“ Nimekwisha kusamehe Dr Joshua na ndiyo maana niko hapa.Umesema tuna mambo mengi ya kuongea hata mimi nina mengi ya kuuliza lakini kwanza nataka unieleze kwa nini Edson aliuawa? Akauliza Penny.Dr Joshua akachukua kitambaa na kujifuta jasho,akainuka na kwenda mezani akajimiminia mvinyo na kupiga funda kubwa.
ENDELEA………………………………….
“ Kwa nini unataka kufahamu Penny? Akauliza Dr Joshua
“ Edson was my friend and my lover so I need to know why you ordered him killed” akasema Penny
“ He was your lover ! akasema Dr Joshua kwa sauti ya juu.Penny hakujibu kitu akakaa kimya
“ You cheated on me !
“ I loved him..He was such a gentleman” akasema Penny na Dr Joshua akakaa kimya akazunguka chumbani halafu akasema
“ Unataka kuufahamu ukweli?
“ Ndiyo nahitaji kuufahamu ukweli “ akasema Penny.Dr Joshua akamsogelea akamshika mkono na kusema
“ Ni wivu ndio ulionifanya nitoe maamuzi yale.Ninakupenda mno Peniela na nilipogundua kwamba unanisaliti kwa kutembea na Yule kijana nilikasirika sana.Penny wewe ni wangu peke yangu na sitaki unichanganye na mtu yeyote hususani hawa vijana wadogo.Kijana Yule hakuwa na kitu chochote cha kukupatia .Nilikuahidi kukupa kila fahari ya dunia hii lakini bado ukanisaliti.Penny I’m a powerful man in the country so I can do anything when I’m angry.Nakupa uhuru nieleze kitu chochote na kila unachokitaka nitakupatia lakini ubaki kuwa wangu peke yangu na usije ukanichanganya na mtu mwingine.” Akasema Dr Joshua
Penny akafuta machozi na kumtazama Dr Joshua kwa macho makali
“ Hukutakiwa kufanya vile.Hutakiwi kuwa na wivu na mimi,wewe ni mtu mwenye familia yako.You cant control me.You cant give me all that I want.You cant be there all the time when I need you.I’m a human Dr Joshua and I have needs” akasema penny kwa sauti ya juu
“ Penny mara ngapi nikwambie kwamba wewe ni kila kitu kwangu? Unataka niende katika luninga na kuutangazia ulimwengu kwamba ninakupenda? Niko tayari kufanya hivyo kama hiyo itakufanya uufungue moyo wako na kuniruhusu niingie ndani.Nipe nafasi ya kukuonyesha ni namna gani ninakupenda Penny.Forget that I’m married and I have a family.Not all marriages are real.Some are in papers. Kama ukinipa nafasi ndani ya moyo wako ,nitakuweka katika nafasi ya juu kuliko wanawake wote wa nchi hii.You’ll be the first lady.So why cant we skip the past and talk about our bright future? Akasema Dr Joshua Penny akamuangalia na kusema
“ Najaribu kukubaliana nawe lakini bado moyo wangu na maswali mengi ambayo yanahitaji majibu sahihi Dr Joshua.”
“ Just one question Penny.One question only” akasema Dr Joshua
“ Kwa nini kesi ile ya mauaji ya Edson iliniangukia mimi na ukakubali kuniona nikinusurika kuangamia wakati ukijua kabisa kwamba sikutenda kosa? Kwa nini hukufanya lolote kunisaidia kama kweli unanipenda?
“ Hayo ni maswali mawili Penny.Nitajibu swali moja tu” akasema Dr Joshua ,akanywa funda moja la mvinyo na kusema
“ I was angry” akasema na kunyamaza
“ I was angry for what you did to me and I wanted to destroy you.Nilitaka ufutike kabisa katika dunia hii,nilidhani kwamba ile ilikuwa ni njia muafaka ya kuweza kukusahau,but I was wrong.Penny naomba uelewe kwamba tayari umeniingia katika kila mshipa wa mwili wangu na siwezi kukutoa tena.Ninaomba utambue kwamba nilipata wakati mgumu sana kwa maamuzi yale na hilo ndilo jambo ambalo nitaendelea kulijutia hadi siku ninaingia kaburini.Tafadhali naomba utafute ndani ya moyo wako unisamehe na tuendelee na mapenzi yetu kama zamani.Nilifanya kosa kutaka kukupoteza mara ya kwanza safari hii sitaki tena kurudia kosa .Please lets not talk about the past .Lets not ruin our lovely night.Lets open new chapter in our book.” Akasema Dr Joshua kwa sauti ya kubembeleza,akamvuta Penny na kumkumbatia akambusu
“ Nimekwisha kusamehe Dr Joshua kwa sababu ninakupenda na ndiyo maana niko hapa ila tafadhali nakuomba usifanye tena jambo kama lile.Kama kuna tatizo kati yetu tafadhali naomba uniadhibu mimi na si watu wengine wasiokuwa na hatia.Please don’t hurt people that I love”
“ Siwezi kufanya hivyo tena kama utanihakikishia kwamba hautakuwa na mahusiano na mtu mwingine zaidi yangu. Niambie chochote kile nitakupatia Penny.I have power ,money and everything to make you live like a queen”
‘ Dr Joshua I’m still young and you are getting old.You have a family,you have a wife on bed,you have huge responsibilities and you cant be there all the time that I need you……………..” Penny hakumaliza sentensi yake Dr Joshua akamkatisha
“ I’ll be there ! Anytime you need me just call me and I’ll be there.Kwako sintakuwa na neno la hapana.Niambie chochote unachokitaka nitakutimizia” akasema Dr Joshua na kumfanya Penny atabasamu
“ This is the moment I’ve been waiting .Tayari ameingia mwenyewe katika nyavu na kilichobaki sasa ni kumvua tu.Ni wakati wangu sasa kumaliza kazi yangu” akawaza Penny
“ Dr Joshua kabla ya yote kuna jambo ambalo nataka nikuombe”akasema penny
“ Omba chochote Peniela.Kila kitu katika nchi hii kipo chini yangu” akasema Dr Joshua
“ Ninao watu wangu wawili ambao ni zaidi ya marafiki.Niko nao karibu sana watu hawa.Naomba kwa namna yoyote ile watu hawa wasije wakadhurika.Wana mchango mkubwa sana katika maisha yangu.Can you give me your word that you wont hurt them?” akasema Penny.Dr Joshua akatabasamu na kusema
“ I give you my word Penny.Who are they?
“ Wakili wangu Jason pamoja na Jaji Elibariki”
Dr Joshua akastuka kidogo baada ya kusikia jina la jaji Elibariki likitajwa
“ Usihofu Penny.Jaji Elibariki ni mwanangu.Amemuoa binti yangu. Ni kijana makini na mchapakazi na ndiyo maana nikamchagua kuwa jaji wa mahakama kuu.Nafahamu wewe na yeye ni marafiki na baada tu ya kumalizika kwa kesi mlikutana kwa chakula cha usiku.Nadhani ulikwenda kumshukuru kwa kukuachia huru” akasema Dr Joshua huku akicheka
“ Kwa hiyo umeweka watu wa kunifuatilia maisha yangu? Akauliza Penny
“ Ni kwa sababu ya usalama wako Penny.
“ Tafadhali naomba uwaondoe watu wako wasiendelee kunichunguza.I can defend myself.Siku nikigundua kwamba bado watu wako wanaendelea kunfuatilia it’ll be the end of us”
“ Ok Penny nitawaondoa kama ndivyo unavyotaka lakini ukumbuke kwamba wewe ni mke mtarajiwa wa rais kwa hiyo unahitaji ulinzi.Sema kingine unachokitaka” Penny akatabasamu na kusema
“ Kwa sasa kingine ninachokihitaji ni hiki” akasema na kulivuta taulo alilojifunga Dr Joshua na kumsukuma kitandani halafu akaanza tena kumfanyia utundu na baada ya dakika kadhaa wakaingia tena katika mzunguko mwingine.Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwa Dr Joshua.
***********
Kengele ya mlangoni ililia kuashiria kwamba kuna mtu mlangoni.Mathew akainuka na kwenda kuufungua.
“ Anitha the devil ..!! akasema kwa furaha Mathew baada ya kuufungua mlango na kukutana na Anitha
“ Welcome my dear.Welcome home” akasema Mathew huku akikumbatiana na Anitha
“ Thank you so much Mathew.” Akasema Anitha
“ Ungenitaarifu muda ambao utatua ili nije nikupokee “ akasema Mathew
“ Usijali Mathew,hapa ni nyumbani na hauna haja ya kupoteza muda wa kufanya mambo mengine kwa kuja kunipokea.Npe habari kazi inaendeleaje? Akauliza huku akifungua friji na kutoa chupa ya mvinyo akajimiminia katika glasi.
“ Hautaki hata kupumzika Anitha? Pumzika kwanza halafu mambo ya kazi yatafuata baadae” akasema Mathew na kumfanya Anitha acheke kidogo
“ Mathew you know me,I work like a devil. Nimekuja kikazi kwa hiyo tufanye kazi na mambo mengine yatafuata baadae” akasema Anitha.Mathew akatasamu na kusema
“ Kazi tayari imeanza na mpaka sasa hakuna hatua kubwa iliyopigwa japo kuna mwangaza kidogo tayari nimeupata” akasema Mathew.Anitha akageuza kichwa na kumtazama Mathew akasema
“ Nilipata kazi ya pesa nyingi nchini Brazil ambayo nilitakiwa nikaifanye wiki hii lakini nimelazimika kuweka pembeni kwanza ile kazi na kuja kuimaliza kwanza kazi uliyoniitia. Nipe taarifa za kina kuhusiana na kazi hii” akasema Anitha huku akiifungua mizigo yake na kutoa zana zake za kazi
“ Ahsante sana Anitha kwa kuahirisha mambo yako mengine na kuja kuungana nami.Hata mimi pia nimelazimika ksimamisha baadhi ya shughuli zangu kwa ajili ya shughuli hii. Si kazi yenye malipo makubwa lakini ni muhimu sana kwa rafiki zangu” akasema Mathew
“ Kuna kijana mmoja aitwaye Edson,ambaye alikuwa mfanyakzi wa kitengo cha mawasiliano ikulu,aliuawa na watu wasiofahamika na kesi hiyo kumuangukia msichana mmoja aitwaye Peniela . Jaji Elibariki ambaye alikuwa akiisikiliza kesi ile aligundua kwamba msichana Yule aliyekuwa akituhumiwa hakutenda kosa hivyo akalazimika kumuachia huru.Baada ya kesi kumalizika alishawishika kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na kesi ile kutokana na sintofahamu kadhaa alizozigundua wakati wa usikilizwaji wa kesi.Aliungana na wakili Jason aliyekuwa anamtetea mtuhumiwa na kwa pamoja wakaamua kunipa kazi hii kutokana na kwamba wao hawana taaluma ya uchunguzi.Kwa hiyo naomba ufahamu kwamba tunaifanya kazi hii kuitafuta haki na vile vile kuwasaidia rafiki zetu” akasema Mathew
“ Kesi hii inafanana na ile ya Justine Abangiza wa Rwanda” akasema Anitha huku akiunganisha vifaa vyake
“ Yah ! zinashabihiana sana ingawa hii ya Edson ina utofauti kidogo” akasema Mathew
“ Nimeongea na wazazi wake jioni ya leo .Nilitaka tu kufahamu mtoto wao alikuwa ni mtu wa namna gani.Kabla ya hapo mchana wa leo nilikwenda nyumbani kwa Peniela,msichana aliyetuhumiwa kumuua Edson, na kutega kamera mbili ,niliporudi nimekutana na picha hizi” akasema Mathew na kumuonyesha Anitha zile picha za wale watu walionaswa katika kamera nyumbani kwa Penny
“ They look so professional “ akasema Anitha
“ Yah ! Wanaonekana wazoefu sana .Ninachojiuliza ni kwa nini wametega kamera mlangoni kwa Penny?
“ Jibu ni jepesi Mathew,Wanataka kuangalia kila kinachoendelea nyumbani kwa Penny.Cha kujiuliza ni kwa nini wanataka kutazama kila kinachoendelea nyumbani kwa Penny?Kwa nini Peniela anachunguzwa? Au watu hawa yawezekana wakawa ni walinzi binafsi wa Peniela? Akauliza Anitha
“ Sina hakika kama watu wale ni walinzi wa Peniela kutokana na namna walivyoingia.Wanaonekana wazi kufahamu kwamba muda ule Peniela hakuwepo nyumbami ndiyo maana waliingia kwa kunyata na kuweka ile kamera nadhani kwa lengo la kutaka kufahamu mienendo ya Penny.Tunachotakiwa kufahamu watu hawa ni akina nani na nini lengo lao la kumchunguza Penny.Tayari tuna sehemu nzuri sana ya kuanzia uchunguzi wetu.Sehemu nyingine ya kufanyia uchunguzi ni katika laini ya simu ya Edson. Wauaji waliondoka na simu na pamoja na kompyuta zake zote.Inaonekana wazi kwamba kuna kitu kilichokuwa kinafichwa na ndiyo maana wauaji wale hawakuwa na shida na pesa na wakaondoka na vitu hivyo tu.Wakati wa kuhamisha vifaa vyake,ilipatikana laini ya simu ikiwa imefichwa katika chungu cha maua.Sielewi ni kwa nini aliificha laini hii ya simu lakini nina imani hakutaka ionekane kwa sababu maalum.Inaweza ikawa na msaada kwetu.Tunatakiwa tuichunguze laini hii pia” akasema Mathew.Anitha hakujibu kitu aliendelea na kazi yake ya kuunganisha mitambo yake. Nusu saa baadae alimaliza kuunganisha mitambo yake akaiwasha na kujaribu
“ Everything is in position.We can start our job now” akasema Anitha
 
SEHEMU YA 17
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Tunachotakiwa kufahamu watu hawa ni akina nani na nini lengo lao la kumchunguza Penny.Tayari tuna sehemu nzuri sana ya kuanzia uchunguzi wetu.Sehemu nyingine ya kufanyia uchunguzi ni katika laini ya simu ya Edson. Wauaji waliondoka na simu na pamoja na kompyuta zake zote.Inaonekana wazi kwamba kuna kitu kilichokuwa kinafichwa na ndiyo maana wauaji wale hawakuwa na shida na pesa na wakaondoka na vitu hivyo tu.Wakati wa kuhamisha vifaa vyake,ilipatikana laini ya simu ikiwa imefichwa katika chungu cha maua.Sielewi ni kwa nini aliificha laini hii ya simu lakini nina imani hakutaka ionekane kwa sababu maalum.Inaweza ikawa na msaada kwetu.Tunatakiwa tuichunguze laini hii pia” akasema Mathew.Anitha hakujibu kitu aliendelea na kazi yake ya kuunganisha mitambo yake. Nusu saa baadae alimaliza kuunganisha mitambo yake akaiwasha na kujaribu
“ Everything is in position.We can start our job now” akasema Anitha
ENDELEA…………………………..
“ Kazi ya kwanza ambayo tunaweza kuifanya usiku wa leo ni kuichunguza laini hii ya simu ili tufahamu Edson alikuwa akiwasiliana na akina nani kwa siri.Tukiwafahamu watu ambao aliwasiliana nao kwa siri kuna jambo tunaweza tukalipata toka kwao.Nina hakika lazima kuna sababu iliyomfanya Edson akaificha laini hii isionekane na mtu yeyote” akasema Mathew na kumpa Anitha ile laini ya simu akaipachika katika kifaa fulani kidogo mithili ya mkebe na kuanza kuibonyeza kompyuta yake.Baada ya sekunde kadhaa Anitha akaguna
“ Vipi mbona unaguna Anitha? akauliza Mathew
“ Laini hii ya simu imewekewa uzio.” Akasema Anitha
“ Una maana gani unaposema uzio?
“ Nina maana kwamba mtumiaji aliiwekea program maalum ambayo inaiwezesha laini hii ya simu kutumika katika simu yake tu .Inaonekana huyu jamaa alikuwa ana ufahamu mkubwa sana wa kompyuta”
“ Unaweza kuiondoa hiyo program? Akauliza Mathew
“ Ndiyo.Ninaweza kuiondoa.Hivi ni vitu vidogo sana kwangu” akasema Anitha huku akiendelea kucheza na kompyuta yake.Baada ya dakika saba akaegemea kiti na kuvuta pumzi ndefu
“ Tayari”
“ Congraturations” akasema Mathew lakini mara Anitha akaguna tena
“ This is strange !..Anitha akashangaa
“ Nini Anitha?
“ Inaonekana Edson alitumia laini hii ya simu kuwasiliana na watu wawili pekee.”
“ watu wawili ?! Mathew naye akashangaa
“ Ndiyo.Ameitumia kwa watu wawili tu”
“ Unaweza ukatafuta ni akina nani hao?
Anitha akaendelea kubonyeza kompyuta yake na baada ya dakika nne akasema
“ Kwa mujibu wa taarifa toka kampuni ya simu ya Tanphone namba hizo ni za Hellen Francis Kobe na nyingine ni ya Brigita samini.Inaonyesha Edson na Brigita wamekuwa wakiwasiliana mara kwa mara na hata siku moja kabla ya kifo chake Edson aliongea na Brigita kupitia laini hii.” Akasema Anitha
“ Hellen francis Kobe ni mama yake mzazi Edson na alinieleza kwamba kuna siku mwanae alimpigia simu kwa kutumia namba ngeni nadhani ni hii.Huyu Brigita simfahamu ni nani.Inawezekana alikuwa ni mtu muhimu sana kwa Edson na ndiyo maana akawa akitumia laini ya pekee kuwasiliana naye.” Akasema Mathew na kuziandika namba zile za Brigita katika simu yake akajaribu kupiga lakini hazikuwa zikipatikana.
“ Inawezekana mawasiliano ya watu hawa wawili yalikuwa ni ya siri mno.Inawezekana hata huyu Brigita hii akawa na laini ya ya siri ambayo huitumia kuwasiliana na Edson” akasema Mathew na kuzitafuta namba za simu za mzee Robinson Kobe na kumpigia
“ Hallo Mathew” akasema mzee Roinson baada ya kupokea simu
“ Samahani mzee wangu kwa kukupigia simu mida hii” akasema Mathew
“ Bila samahani Mathew.Kuna kitu chochote ninachoweza kukusaidia?
“ Ndiyo mzee.Ninataka kujua kama unamfahamu mtu anayeitwa Brigita Samini”
Kimya cha sekunde kadhaa kikapita halafu mzee Robinson akasema
“ Ninamfahamu Brigita.Edson aliwahi kunitambulisha kwake kwamba ni marafiki wakubwa.Brigita anafanya kazi katika hoteli ya kitalii ya Potina palace.”
“ Ok ahsante sana mzee” akasema Mathew na kukata simu
“ Brigita na Edson ni marafiki wakubwa kwa mujibu wa mzee Robinson.” Mathew akamwambia Anitha
“ Kama walikuwa na urafiki mkubwa kwa nini basi wawasiliane kwa siri? Akauliza Anitha
“ Hicho ndicho tunachotakiwa kukifahamu. Haiingii akilini kama watu ni marafiki wakubwa halafu wawasiliane kwa siri.Lazima kuna sababu iliyowafanya wawe na mawasiliano ya siri ” akasema Mathew na kuchukua kitabu chenye namba za simu za makampuni mbali mbali akaitafuta Potina palace hoteli anayofanya kazi Brigita.Akaipata na kuchukua namba zao za simu akapiga.
“ Karibu Potina palace nikusaidie nini? Ikasema sauti nzuri ya mwanadada baada ya kupokea simu
“ Namtafuta dada mmoja anaitwa Bigita Samini ni mfanyakazi wa hapo hotelini kwenu” akasema Mathew
“ Wewe ni ndugu yake?
“ Hapana mimi ni rafiki yake “
“ Samahani ndugu yangu Brigita hatunaye tena hapa hotelini.Alikwisha fariki dunia.”
“ Amefariki dunia?
“ Ndiyo alifariki dunia “
“ Alifariki lini na nini kilimuua?
“ Alilipukiwa na gesi na kufariki yeye na familia yake yote yapata mwaka sasa” akasema Yule dada na kumtajia Mathew tarehe ambayo Brigita alifariki dunia.Mathew akashukuru na kukata simu.
“ Vipi wanasemaje? Akauliza Anitha
“ Mambo yanazidi kuibuka.Brigita alifariki dunia wiki moja tu baada ya Edson kufariki dunia.Alilipukiwa na gesi na wakafariki yeye na familia yake yote ” akasema Mathew na kimya kikapita
“ Walikuwa wakiwasiliana kwa siri na hata vifo vyao vimetokea kwa kufuatana.Mathew kuna kitu hapa si bure.Kama walikuwa ni marafiki kuna jambo lazima watakuwa wakilifahamu kwa pamoja au wakilificha na ndiyo maana hata mawasiliano yao yalikuwa ya siri kubwa na hawakutaka mtu mwingine yeyote Yule afahamu kama walikuwa wakiwasiliana.Siri hiyo waliyokuwa wakiificha ndiyo iliyowagharimu maisha yao.” Akasema Anitha
“ Anitha inatosha kwa leo.Tupumzike na kesho tuanze kazi rasmi.Tutaanza kazi kwa kutafuta taarifa za Brigita Samini .Anaonekana ni mtu muhimu sana katika suala hili” akasema Mathew.Anitha akamtazama na kutabasamu halafu akazima kompyuta zake
“ Uko sahihi Mathew.Leo imekuwa ni siku ndefu sana.Tupumzike ili kesho tuanze kazi “ akasema Anitha
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
SEASON 1
SEHEMU YA 18
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Walikuwa wakiwasiliana kwa siri na hata vifo vyao vimetokea kwa kufuatana.Mathew kuna kitu hapa si bure.Kama walikuwa ni marafiki kuna jambo lazima watakuwa wakilifahamu kwa pamoja au wakilificha na ndiyo maana hata mawasiliano yao yalikuwa ya siri kubwa na hawakutaka mtu mwingine yeyote Yule afahamu kama walikuwa wakiwasiliana.Siri hiyo waliyokuwa wakiificha ndiyo iliyowagharimu maisha yao.” Akasema Anitha
“ Anitha inatosha kwa leo.Tupumzike na kesho tuanze kazi rasmi.Tutaanza kazi kwa kutafuta taarifa za Brigita Samini .Anaonekana ni mtu muhimu sana katika suala hili” akasema Mathew.Anitha akamtazama na kutabasamu halafu akazima kompyuta zake
“ Uko sahihi Mathew.Leo imekuwa ni siku ndefu sana.Tupumzike ili kesho tuanze kazi “ akasema Anitha
ENDELEA…………………………..
Kumekucha Dar es salaam,saa tatu za asubuhi Iliwakuta Mathew na Anitha nje ya hoteli ya kitalii ya Potina Palace.Waliegesha gari na kushuka wakaingia hotelini na moja kwa moja wakaelekea mapokezi ambako walimkuta mwanadada mmoja mrembo wakajitambulisha kama rafiki wa Brigita Samini aliyekuwa akifanya kazi pale hotelini.Yule mwanadada wa mapokezi akashangaa kidogo na kuuliza
“ Hamkuwa na mawasiliano naye au ndugu zake?
“ Sisi tunaishi Marekani na kwa muda msrefu kidogo hatukuwa tumewasiliana naye.Mara ya mwisho tulipowasiliana naye alituelekeza kwamba anafanya kazi hapa.” Akasema Mathew
“ Poleni sana ndugu zangu.Brigita hatuko naye tena,alifariki dunia yapata mwaka mmoja sasa umepita” akasema yule dada ambaye kitambulisho cha kazi alichokivaa kilionyesha anaita Stella manana .Mathew na Anitha wakaonyesha mstuko ili kumfanya Yule dada asiwe na wasi wasi wowote kuhusu wao.
“ Nini ilikuwa sababu ya kifo chake? Akauliza Anitha
“ Mtungi wa gesi ulilipuka na kusababisha nyumba yao iteketee kwa moto.Hakuna hata mtu mmoja aliyetoka hai.Ilikuwa ni ajali mbaya sana.Brigita alikuwa ni meneja wetu na mtu mwenye roho nzuri sana na kila mtu hapa alimpenda “
Kikapita kimya cha sekunde kadhaa Mathew akauliza
“ Kuna mtu yeyote ambaye alikuwa ni mtu wake wa karibu sana ili aweze kutuelekeza kwa ndugu zake tukawape pole? Akauliza Mathew
“ Brigita alikuwa na marafiki wengi na kila mtu alikuwa ni rafiki yake lakini kuna mmoja ambaye alikuwa ni rafiki yake mkubwa anaitwa Subira.Kwa sasa hayupo hapa hotelini anasomea shahada ya hoteli pale Ikandala University.Kama mnahitaji taarifa za kina kuhusiana na Brigita mtafuteni huyo Subira kwani ni yeye anayewafahamu hadi ndugu zake “ akasema Yule dada na kuwapatia namba za simu za Subira wakaagana Mathew na Anitha wakarejea katika gari lao.
“Mpigie simu Subira tufahamu yuko wapi” akasema Mathew.Anitha akaziandika zile namba katika simu yake na kupiga.Simu ikaita na kukatika,akapiga tena ikaita lakini haikupokelewa
“ Simu yake inaita tu lakini haipokelewi” akasema Anitha
“ Jaribu tena kumpigia.Isipopokelewa tutamfuata pale pale chuoni kwao” akasema Mathew ,Anitha akapiga tena na safari hi ikapokelewa
“ Hallow !..Ikasema sauti ya mwanadada upande wa pili
“ Hallow naongea na nani? Akasema Anitha
“ Unaongea na Subira Abdul.Wewe ni nani mwenzangu?
“ Ninaitwa Anitha”
“ Nikusaidie nini Anitha? Akauliza Subira ambaye alikuwa na sauti ya upole
“ Subira ninahitaji kukuona.Nina maongezi nawe kidogo” akasema Anitha
“ Una maongezi na mimi? Subira akashangaa
“ Ndiyo Subira.Nahitaji sana kukuona”
“ Ni maongezi kuhusu nini? Halafu mbona sikufahamu?
“ Usihofu Subira.Hata mimi sikufahamu nimepewa namba zako za simu pale Potina Palace ulipokuwa ukifanyakazi kabla ya kuanza kusoma.”
“ Ok Unataka tuongee jambo gani?
“ Mimi ni rafiki wa siku nyingi wa Brigita Samini ambaye nimeelezwa kwamba wewe ulikuwa na ukaribu naye mkubwa .Ninaishi Marekani kwa sasa na nimekuja kwa mapumziko mafupi.Nimeenda kumtembelea Brigita mahala nilikomuacha akifanya kazi kipindi cha kama mwaka mmoja uliopita nikaambiwa kwamba alifariki dunia katika ajali ya moto.Nimestuka sana .Ninataka kufahamu mengi kuhusiana na kifo hicho na hata kuwafahamu ndugu zake ili nikatoe pole.Nimeelekezwa kwako kwamba unaweza ukanisaidia kwa hilo Subira” akasema Anitha
“ Kwa sasa uko wapi? Subira akauliza
“ Kwa sasa ninaondoka hapa Potina Palace.wewe uko wapi?
“ Mimi niko chuoni hapa Ikandala University.Ninamalizia kipindi cha mwisho .Unaweza ukaja kunisubiri hapa chuoni nimalize kipindi?
“ Usijali Subira ninakuja” akasema Anitha na kukata simu
“ Yuko chuoni anamalizia kipindi,anasema tumfuate tukamsubiri” Anitha akamwambia Mathew
Wakiwa njiani, kuelekea chuoni,Mathew akawasiliana na Jason kutaka kujua kama Penny amekwisha rejea lakini mpaka muda huo Jason hakuwa na taarifa zozote za kumuhusu Penny
“ Penny atakuwa amekwenda wapi? Mpaka leo hajaonekana na hajulikani yuko wapi” akasema Mathew
“ Unahisi anaweza kuwa amepatwa na tatizo? Akauliza Anitha
“ Sina hakika sana lakini hata kama hajapatwa na tatizo bado hayuko salama.Bado nawafikiria watu wale walioingia ndani ya nyumba yake jana na kuweka kamera za siri ni akina nani na wana lengo gani kwa Penny.Nashawishika kutaka kumfahamu vizuri zaidi Penny.” Akasema Mathew
“ Have you met her? Akauliza Anitha huku akiendelea kucheza na kompyuta yake
“ No I haven’t” akajibu Mathew
Waliendelea na safari hadi walipofika Ikandala University,Anitha akamtumia Ujumbe Subira kumfahamisha kwamba tayari wamekwisha fika wako nje wanamsubiri.Baada ya dakika ishirini Subira akatoka.Hakuwa akimfahamu Anitha hivyo ikamlazimu kumpigia simu ,Anitha akamuelekeza mahala walipo akawafuata
“ Habari yako Subira” akasema Anitha.Subira alionyesha hofu kidogo alipogundua kwamba Anitha hakuwa peke yake bali alikuwa na Mathew
“ Habari yangu nzuri.habari zenu?
“ Habari zetu nzuri.Pole na masomo”
“ Ahsante” akajibu Subira
“ Subira huyu hapa ni mwenzangu anaitwa Mathew kwa hiyo naomba usiwe na hofu.” Anitha akafanya utambulisho kwani alimuona Subira akiingiwa na uoga.
“ Subira hatutaki kuchukua muda wako mwingi kwani najua una shughuli nyingi za kufanya.Tunaweza kupata sehemu hapa karibu tukakaa na kuongea japo kwa dakika chache? Akauliza Anitha
“ Kuna hoteli pale karibu tunaweza kwenda kukaa tukaongea” akajibu Subira halafu wakaongozana kuelekea katika hoteli iliyokuwa kandoni mwa chuo.
“ Subira kama tulivyoongea simuni,mimi ni rafiki wa siku nyingi wa Brigita.Kwa sasa ninaishi Marekani na nimerudi nchini kwa mapumziko mafupi.Ni muda umepita sijawasiliana naye na mara ya mwisho kuwasiliana naye alinielekeza mahala anapofanyia kazi nikamwambia kwamba nikija Tanzania nitamtembelea.Nimefika kumtembelea mahala alikonielekeza anafanya kazi nikakutana na taarifa hizi za kustusha za kifo chake.Nimeumia sana.Hebu nieleze japo kwa undani kidogo nini kilitokea na kusababisha kifo chake? Akauliza Anitha.
Subira akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Brigita alikuwa ni rafiki yangu mkubwa na tulikuwa tunaelewana mno.Usiku wa siku alipofariki tulipanga twende taarabu mashauzi Classic lakini baadae alibadili maamuzi na kuniambia kwamba hangekwenda tena Mashauzi kwani alipigiwa simu na babu kwamba wanatakiwa waonane jioni ya siku ile.Safari yetu ikawa imeishia hapo,hatukutoka tena hadi nilipopata taarifa za kifo chake asubuhi.Kwa kweli hata mimi niliumia mno na hadi leo hi bado ninaendelea kuumia.Nilimpenda sana Brigita.Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa inasemekana kwamba mtungi wa gesi ulilipuka na kusababisha maafa yale” akasema Subira
“ Pole sana Subira” akasema Anitha
“ Nimekwisha poa” akajibu subira
“ Umesema kwamba mlipanga muende mashauzi Classic lakini mkaahirisha aliposema kwamba alipigiwa simu akaonane na babu.Huyu babu ni nani?
Subira akatabasamu kidogo na kusema
“ Brigita alikuwa na mahusiano na mzee mmoja hivi ambaye ndiye aliyemjengea nyumba,akamnunulia gari na ndiye aliyekuwa akimuhudumia kwa kila kitu.Mzee Matiku alifariki dunia wiki mbili tu baada ya Brigita kufariki kwa kujipiga risasi ya kichwa.Inasemekana kifo cha Brigita kilimuumiza sana na ndiyo maana akaamua kujimaliza kwa risasi. ”
“ Dah ! akasema Anitha
“ Nakumbuka Brigita aliwahi kuwa na mahusiano na kijana mmoja hivi anaitwa Edson.Aliwahi kunitumia picha wakiwa naye.Gosh he was very handsome,je waliachana hadi akaamua kuingia katika mahusiano na huyo mzee? Akauliza Anitha
“ Edson ninamfahamu lakini naye alikwisha fariki dunia.Aliuliwa na mpenzi wake.Ninachokifahamu mimi,Brigita na Edson walikuwa wanakutana kwa siri.Hakuwa akimpenda mzee Matiku na alikuwa naye kwa ajili ya pesa zake tu lakini moyo wake ulikuwa kwa Edson.Mzee Matiku alikuwa na wivu uliopitiliza na aliwahi kumwambia Brigita kwamba siku akimkuta na mwanaume mwingine basi huo ungekuwa ni mwisho wake.Brigita alimuogopa sana mzee Yule hivyo akawa akiwasiliana na Edson kwa siri.Mzee Edson alikuwa akimfuatilia sana hadi alimuwekea kifaa maalum katika simu yake cha kuchunguza watu aliokuwa akiwasiliana nao.Hakutaka kabisa amuone na mwanaume yeyote zaidi yake.Brigita alianza kuchoshwa na mahusiano yake na Yule mzee na kila siku alikuwa akiniambia kwamba siku moja lazima atakuja kumkimbia .Aliniambia kwamba kuna biashara wanataka kuifanya na Edson na endapo ikifanikiwa basi watapata pesa nyingi na kisha atamkimbia mzee yule na kuhama kabisa nchi.Hakuwahi kuniambia ni biashara gani walitegemea kuifanya na Edson.Siku moja aliniambia kwamba kuna kitu amekichukua toka kwa mzee Matiku ambacho endapo angegundua basi kingemletea shida sana.Hakuniambia ni kitu gani hadi alipofariki.” Akasema Subira
“ Huyo mzee Matiku alikuwa anafanya kazi gani? Alikuwa na familia?
“ Mzee Matiku ni mfanyabiashara,ndiye mwenye ile hoteli niliyokuwa nikifanya kazi na ndiyo maana Brigita alikuwa na kazi nzuri sana pale.Watu wanasema kwamba ni mwanajeshi mstaafu.Wanasema kwamba aliwahi kuwa mlinzi wa rais miaka ya nyuma sana.Kwa upande wa familia mzee Matiku hakuwa na familia” akasema Subira.
“ Subira nashukuru sana kwa kunipa mwanga kuhusiana na kifo cha rafiki yangu Brigita.Kwa sasa kuna mahala ninatakiwa kwenda ila nitakutafuta mwishoni mwa wiki tukae tuongee na unieleze mambo mengi kuhusiana na Brigita na pia unitambulishe kwa ndugu zake unaowafahamu ili niweze kuwapa pole.Ahsante sana kwa muda wako na tutaonana tena” akasema Anitha huku akifungua pochi yake na kumpatia Subira kiasi cha dola hamsini za Marekani halafu wakasimama na kuondoka
“mambo mapya yanazidi kuibuka kila siku.Kwa sasa tuna mtu mwingine ameongezeka katika uchunguzi wetu,babu Matiku.” Akasema Mathew wakiwa garini wakiondoka maeneo ya chuo
“ Brigita alikuwa na mahusiano na mzee Matiku na wakati huo huo akawa na mahusiano ya siri na Edson.Walikuwa wakiwasiliana kwa siri ili mzee Yule asigundue na ndiyo maana laini ile ya simu ya Edson iliwekewa uzio ili mtu mwingine asiweze kugundua walichokuwa wakikiongea.Kwa mujibu wa Subira siku chache kabla ya kifo chake Brigita alimweleza kwamba kuna kitu alikichukua toka kwa mzee Matiku je ni kitu gani hicho? Ni biashara gani aliyokuwa akiifanya na Edson ambayo ingewapatia pesa nyingi kiasi cha kumfanya Brigita afikirie hatan kukimbia na kuhama nchi? Akauliza Mathew
“ Majibu ya maswali haya yanakuwa magumu kupatikana kwa sababu wahusika wote ambao wangeweza kutupatia majibu wamekwisha fariki.Tumerudi katika sifuri .Lakini kuna muunganiko wa kifo cha Edson,Brigita na mzee Matiku.Sababu ya vifo vyao ni moja.Ninahisi hicho kitu Brigita alichokichukua toka kwa mzee Matiku alimshirikisha pia Edson na inawezekana ndiyo iliyosababisha vifo vyao.Je ni kitu gani hicho? Ni biashara gani walitaka kuifanya? Mzee matiku ni nani? Nadhani ili tupate mwangaza tunatakiwa tumfahamu pia huyu mzee ni nani ,vyanzo vyake vya mapato n.k.Yawezekana akawa ni mtu aliyekuwa akijishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya..” akasema Mathew lakini akastuliwa na Anitha
“Mathew…!!” Anitha akaita
“ Kamera kipepeo nyumbani kwa Penny imetoa mlio.Kuna watu wanaingia nyumbani kwa Penny” akasema Anitha.Mathew akasogeza gari pembeni na kusimama akawatazama watu wale waliokuwa wakiinga kwa Penny kupitia kompyuta ya Anitha
“ Ni sura zile zile za jana.Who are these people? Wanatafuta nini kwa penny?
“ We need to find out” akasema Mathew huku akiwashuhudia watu wale wakiufungua mlango wa Penny na kuingia ndani
“ Twende nyumbani kwa Penny.Leo lazima tuwafahamu” akasema Mathew na kuwasha gari wakaelekea nyumbani kwa Penny
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
SEASON 1
SEHEMU YA 19
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Majibu ya maswali haya yanakuwa magumu kupatikana kwa sababu wahusika wote ambao wangeweza kutupatia majibu wamekwisha fariki.Tumerudi katika sifuri .Lakini kuna muunganiko wa kifo cha Edson,Brigita na mzee Matiku.Sababu ya vifo vyao ni moja.Ninahisi hicho kitu Brigita alichokichukua toka kwa mzee Matiku alimshirikisha pia Edson na inawezekana ndiyo iliyosababisha vifo vyao.Je ni kitu gani hicho? Ni biashara gani walitaka kuifanya? Mzee matiku ni nani? Nadhani ili tupate mwangaza tunatakiwa tumfahamu pia huyu mzee ni nani ,vyanzo vyake vya mapato n.k.Yawezekana akawa ni mtu aliyekuwa akijishughulisha na biashara ya madawa ya kulevya..” akasema Mathew lakini akastuliwa na Anitha
“Mathew…!!” Anitha akaita
“ Kamera kipepeo nyumbani kwa Penny imetoa mlio.Kuna watu wanaingia nyumbani kwa Penny” akasema Anitha.Mathew akasogeza gari pembeni na kusimama akawatazama watu wale waliokuwa wakiinga kwa Penny kupitia kompyuta ya Anitha
“ Ni sura zile zile za jana.Who are these people? Wanatafuta nini kwa penny?
“ We need to find out” akasema Mathew huku akiwashuhudia watu wale wakiufungua mlango wa Penny na kuingia ndani
“ Twende nyumbani kwa Penny.Leo lazima tuwafahamu” akasema Mathew na kuwasha gari wakaelekea nyumbani kwa Penny
ENDELEA…………………….
“ Wanafungua mlango wa sebuleni ,wanaingia ndani” akasema Anitha aliyekuwa akiwatazama wale jamaa kupitia kompyuta iliyounganishwa na kamera zilizoko nyumbani kwa Peniela
“ Kwa bahati mbaya hakuna kamera yoyote niliyoweka ndani ya nyumba ya Penny kwa hiyo hatuwezi kujua wanakwenda kutafuta kitu gani mle ndani lakini leo lazima tupate majibu watu hawa ni akina nani na wanatafuta nini kwa Penny” akasema Mathew ambaye alikuwa makini sana katika usukani
Waliwasili katika mtaa anaoishi Penny wakasimamisha gari nyumba ya tatu toka nyumba ya Penny.
“ We’re here.Nyumba ya Penny ni ile yenye bati jekundu.Ngoja tuendelee kuwasubiri wale jamaa watoke” Mathew akamuonyesha Anitha nyumba ya Penny
“ Wow ! Nyumba nzuri sana.Anafanya kazi gani Penny? Akauliza Anitha
“ Penny ni mfanya biashara.Ana maduka makubwa ya urembo na mavazi” akajibu Mathew
Waliendelea kukaa ndani ya gari wakiikodolea macho kompyuta na mara mlango wa mbele wa nyumba ya Penny ukafunguliwa
“ Wanatoka” akasema Anitha
“ Ok Get ready” akasema Mathew huku akiwasha gari
Wale jamaa walitoka wakafunga geti na kuingia katika gari lao wakaondoka.Mathew na Anitha wakawafuata
Toka nyumbani kwa Penny ,walielekea hadi katika duka moja la kuuza vyakula mmoja wao akashuka na kuingia ndani ya duka lile na baada ya muda mfupi akatoka akiwa na mfuko mkononi ,wakaendelea na safari yao bila kujua kama walikuwa wakifuatiliwa na akina Mathew
Saa sita na dakika nane wakawasili Miseko hospital,moja kati ya hospitali kubwa nchini.
“ Wamefuata nini hapa hospitali? Akauliza Mathew
“ Lazima kuna kitu wamekifuata hapa.Tuendelee kuwafuatilia.Ninaingia katika mfumo wa kompyuta wa hapa hospitali ili niweze kuwafuatilia kupitia kamera za ulinzi zilizoko hapa hospitali “ akasema Anitha
Wale jamaa wakashuka garini na kuangaza huku na huko halafu wakaanza kutembea kwa kasi kuelekea kusini mwa hospitali kuliko na wodi za kulipia na zile wa watu maarufu
“ Wanaonekana kuelekea sehemu ziliko wodi za watu maarufu.Anitha wewe utabaki ndani ya gari mimi nitawafuatilia nione wanakwenda kufanya nini kule katika wodi.Endelea kuwafuatilia kupitia kamera “ akasema Mathew huku akiweka sikioni kifaa cha mawasiliano kati yake na Anitha.Akakijaribu na kuona kinafanya kazi ,akashuka garini
“ I’m in now.I can access every thing.Ninawaona wale jamaa kwa kupitia kamera 4g ambayo imeelekezwa kusini” Anitha akamtaarifu Mathew aliyekuwa akitembea kwa kasi kuwafuata wale jamaa ambao hawakuwa na wazo kwamba wanafuatiliwa
“ Good Job Anitha,keep an eye on them” akasema Mathew. Ukubwa wa hospitali hii ulichangia kuwepo kwa idadi kubwa ya watu.Karibu magonjwa yote yalikuwa yakitibiwa hapa hivyo hospitali hii ilikuwa ikipokea mamia ya wagonjwa kila siku toka katika sehemu mbali mbali za nchi na hata nchi za jirani
“ Mathew nimebadilisha kamera na sasa natumia kamera 6 C” Anitha akamtaarifu Mathew
“ Ok Anitha.Endelea kuwafuatilia.Hata mimi bado sijawapoteza.Niko nao sambamba” akasema Mathew
Wale jamaa walinyooka na kuingia katika jengo lililokuwa na kibao VIP Private 2.
“ Wanaingia VIP Private 2” Mathew akamwambia Anitha
“ Ok nimekwisha waona.Itabidi ufanye haraka ili usiwapoteze kwa sababu mle ndani ninaiona kamera moja tu inayofanya kazi .Kamera nyingine zote inaonekana hazifanyi kazi.” akasema Anitha.Mathew akaongeza mwendo na kuacha umbali mfupi baina yake na wale jamaa.Watu wale hawakutaka kutumia lifti ,wakapanda ngazi kwa miguu hadi ghorofa ya nne ambayo ilionekana kuwa kimya sana.Wale jamaa wakasimama nje ya mlango mmoja wakagonga na baada ya sekunde kadhaa mlango ukafunguliwa wakaingia ndani. Mathew aliyekuwa akitembea kwa uangalifu mkubwa ili wale jamaa wasije wakastuka kwamba anawafuatilia akatazama pande zote hakuona mtu,akaukaribia mlango ule na kusoma namba zilizobandikwa juu.
“ Anitha wameingia chumba namba PV2 – 78.Angalia katika orodha ya wagonjwa tufahamu ni nani aliyelazwa katika chumba hiki” akasema Mathew.Baada ya kama dakika moja Anitha akasema
“Katika chumba hicho amelazwa mgonjwa mmoja anaitwa John Mwaulaya Albert,anasumbuliwa na tatizo la kupoteza fahamu mara kwa mara”
Mathew akastuka sana aliposikia jina lile la John Mwaulaya Albert
“ Anitha umesema John Mwaulaya Albert? akauliza Mathew
“ Ndiyo.Do you know him? Akauliza Anitha.Mathew hakujibu kitu .Alionekana wazi kupatwa na mstuko
“ Mathew say something.Do you know him? Akauliza tena Anitha
“ Subiri kidogo Anitha” akasema Mathew halafu akaukaribia ule mlango na kujaribu kutega sikio ili asikie kinachoongelewa ndani lakini hakusikia chochote.Alionekana kuchanganyikiwa ghafla
********
Gari mbili nyeusi ziliwasili katika eneo la kuegeshea magari katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Kilimanjaro .Watu wanne waliovalia suti nyeusi wakashuka wawili toka katika kila gari.Mlango wa kati wa gari lililotangulia ukafunguliwa na mwanadada mmoja mwenye uzuri wa kimalaika akashuka.Alikuwa amevalia koti kubwa la kujikinga na baridi.Toka katika gari la pili,mabegi matatu yakashushwa na kuanza kukokotwa kuelekea ndani ya uwanja wa ndege kulikokuwa na ndege maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya mwanadada huyu mwenye uzuri usio na kifani.Baada ya hatua kama tano hivi ,simu ya mmoja wa wale vijana ikaita akaipokea na kisha akampatia Yule mwanadada waliyekuwa wameongozna naye
“ Madam Penny mheshimiwa rais anataka kuongea nawe.” Akasema Yule jamaa .Penny akaichukua ile simu na kuiweka sikioni
“ hallo” akaita
“ Hallo my angel.Tayari umeshafika uwanja wa ndege? I’ve missed you already” akasema Dr Joshua rais wa jamhuri ya mungano wa Tanzania
“ I’ve missed you too Dr Joshua,hivi sasa ndio tumewasili uwanjani tunaelekea ndegeni”
“ Penny ,hakuna sababu ya msingi iliyonifanya nikupigie simu .I just…I ..Just want to talk to you,to hear your voice and tell you how much I do miss you.Peniela thank you so much for everything.” Akasema Dr Joshua
Peny akatabasamu na kusema
“ Thank you too Dr Joshua for everything.You know how to treat a woman.You made me so happy.” Akasema Penny
“ Nafurahi kusikia hivyo Penny lakini bado sijakufanyia kitu chochote kikubwa cha kuweza kunishukuru.Thi
s is just the beginning Penny.I’ll make you a Tanzanian queen.From now you are going to live like a queen” akasema Dr Joshua
“ Ahsante sana Dr Joshua.” Akasema Penny
“ Ok Penny.Najua nikiwa Dar es salaam nafasi yangu ya kuonana nawe itakuwa ndogo sana kutokana na kazi lakini nitajitahidi kadiri inavyowezekana kuonana nawe mara kwa mara ndiyo maana nimekuhamishia katika nyumba ambayo itakuwa rahisi kwangu mimi kufika mara kwa mara.Nisikucheleweshe Penny tutaongea mengi tutakapoonana Dar es salaam Jioni ya leo nitakuwa mgeni wako na kukupa habari njema ” akasema Dr Joshua
“ Ouh Dr Joshua ,you are so sweet.See you later” akasema Penny na kukata simu
“ Nimemchanganya sana huyu mzee kiasi kwamba hafikirii kitu chochote kingine zaidi yangu.Hahaha…the old man is deadly in love with me..Now that I can control him the way I want ,its time to finish my job.Kuna nyakati namuonea huruma sana huyu mzee kwa namna alivyokufa akaoza kwangu na kuwa tayari kufanya jambo lolote lile kwa ajili yangu,lakini sina namna nyingine ya kufanya zaidi ya kufanya kile ninachotakiwa kukifanya.” Akawaza Penny akiongozwa na walinzi wale wa rais kuelekea katika ndege maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya kumrejesha Dar es salaam.Aliingia ndani ya ndege na kukaa,akafumba macho na kukumbuka mambo yote yaliyotokea jijini Arusha
“ Dr Joshua amejitahidi kufanya kila alichoweza ili kunifanya niwe na furaha. Nilivaa uhusika vizuri sana na kumfanya aamini kwamba nimefurahi na ninampenda.Yule mzee ananipenda sana na yuko tayari kufanya kitu chochote kunifanya niwe na furaha.Amenipatia jumba jipya pembeni ya bahari ili iwe rahisi kwake kufika katika muda wowote anaoutaka.Pamoja na yote haya anayoyafanya kwangu lakini si mtu wa saizi yangu.I don’t love him at all na toka ndani ya moyo wangu nina kisasi naye kikubwa sana kwa kumuua Edson kijana niliyempenda kwa moyo wangu wote.Ngoja niendelee kuuvaa uhusika hadi hapo mambo yangu yatakapotimia ndipo atakapogundua kwamba mimi si malaika kama anavyodhani” Akawaza Penny akiwa angani akielekea Dare s salaam
********
Baada tu ya kumaliza kuongea na Penny simuni,Dr Joshua akiwa amejifungia chumbani kwake akazitafuta namba Fulani katika simu yake na kutaka kubonyeza kitufe cha kupigia lakini akasita.Akaenda dirishani akatazama nje na kuzama katika mawazi kwa muda wa dakika kadhaa halafu akasema kwa sauti ndogo
“ let me do it”
Akabonyeza kitufe cha kupigia na kuiweka simu sikioni.Baada ya muda smu ikapokelewa
“ Captain Amos” akasema Dr Joshua
“ Hallo mheshimiwa “ akasema Captain Amos
“ Mgonja anaendeleaje?
“ Hali yake iko hivyo hivyo.Bado si nzuri .”
“ Ok Captain.Do it” akasema Dr Joshua.Kimya cha sekunde kadhaa kikapita Captain Amos akasema
“ Are you sure Mr President?
“ yes I’m sure.Do it. And Captain Amos,Thank you so much for this” akasema Dr Joshua na kukata simu.
Captain Amos aliyekuwa ni daktari wa familia ya rais akaegemea ukuta akawaza kwa dakika kadhaa halafu akachukua mkoba wake na kuelekea katika chumba cha mke wa rais,akagonga mlango ukafunguliwa na msaidizi wa mke wa rais
“ Muda wa matibabu sasa” akasema Captain amos na Yule msaidizi wa mke wa rais akatoka.
Captain Amos akachukua kichupa kidogo chenye dawa toka katika mkoba wake akainyonya dawa ile katika bomba la sindano na kumchoma mke wa rais
“ I’m sorry for this madam first lady” akasema Captain Amos na kutoka mle chumbani
********
Kwa muda wa dakika tatu Mathew aliendelea kusimama nje ya mlango wa kile chumba walichoingia wale jamaa.Alitamani ajue kilichokuwa kinaendelea mle ndani
“ Mathew talk to me” Anitha akasema
“ Anitha una hakika umesoma vizuri jina la mtu aliyemo ndani ya chumba hiki? Akauliza Mathew
“Chumba PV 2 – 78 amelazwa mgonjwa anayeitwa John Mwaulaya Albert.Kwani vipi Mathew.Unamfaha
mu mtu huyo?
Mathew akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Yah ! Ninamfahamu.Kama ni kweli aliyemo ndani ya chumba hiki ni John Mwaulaya basi mambo si rahisi kama tunavyofikiri” akasema Mathew kwa sauti ndogo huku akiwa makini akiangalia kila upande kuhakikisha usalama wake kwani alikwisha anza kuhisi hatari eneo lile
“ Mathew who is this guy John Mwaulaya ? Akauliza Anitha
“ Anitha tutaongea baadae.Eneo hili si salama hata kidogo.Please stay in the car and don’t get out” akasema Mathew
“ Mathew whats going on? Akauliza Anitha.Mathew hakujibu kitu .Kuna watu wawili walikuwa wakija kwa kasi.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
SEASON 1
SEHEMU YA 20
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Anitha una hakika umesoma vizuri jina la mtu aliyemo ndani ya chumba hiki? Akauliza Mathew
“Chumba PV 2 – 78 amelazwa mgonjwa anayeitwa John Mwaulaya Albert.Kwani vipi Mathew.Unamfaha
mu mtu huyo?
Mathew akavuta pumzi ndefu na kusema
“ Yah ! Ninamfahamu.Kama ni kweli aliyemo ndani ya chumba hiki ni John Mwaulaya basi mambo si rahisi kama tunavyofikiri” akasema Mathew kwa sauti ndogo huku akiwa makini akiangalia kila upande kuhakikisha usalama wake kwani alikwisha anza kuhisi hatari eneo lile
“ Mathew who is this guy John Mwaulaya ? Akauliza Anitha
“ Anitha tutaongea baadae.Eneo hili si salama hata kidogo.Please stay in the car and don’t get out” akasema Mathew
“ Mathew whats going on? Akauliza Anitha.Mathew hakujibu kitu .Kuna watu wawili walikuwa wakija kwa kasi.
ENDELEA………………………………..
Mathew alihisi wale jamaa wanamfuata ikamlazimu kuingia katika choo kilichokuwa chumba cha tatu kutoka kile chumba.Wale jamaa wawili waliouwa wakija kwa kasi wakaingia nao katika kile chumba alicholazwa John Mwaulaya.
“ Lazima nipate uhakika kama ni kweli mtu aliyelazwa mle ndani ni John Mwaulaya.Kama kweli ni yeye basi tutakuwa tumeingia katika hatari kubwa.” Akawaza Mathew akiwa amejificha chooni huku macho yake akiwa ameyaelekeza katika kile chumba cha John akitaka kufahamu kila kilichokuwa kikiendelea.
“ Mathew !.akaita Anitha
“ Hallow Anitha” akasema Mathew kwa kunong’ona
“ Say something.Whats going on over there? Akauliza Anitha
“ Anitha endelea kukaa ndani ya gari,bado ninaendelea kuwafuatilia hawa jamaa” akasema Mathew
“ Mathew mbona hutaki kunieleza nini kinachoendelea huko juu?
“ Anitha,nitakueleza lakini si sasa.” Akasema Mathew
Baada ya dakika kama thelathini hivi ,mlango wa kile chumba ukafunguliwa na jamaa wanne wakatoka wakiwa wameongozana na daktari mmoja wa kizungu
“ Anitha,wametoka watu wanne ndani ya kile chumba wameongozana na daktari mmoja wa kizungu.Nadhani wanashuka chini” Mathew akamtaarifu Anitha
“ Ok nitawaona katika kamera watakapofika chini” akasema Anitha
“ Tunamuhitaji Yule daktari wa kizungu.” Akaelekeza Mathew
“ Nimekusoma Mathew” akajibu Anitha
Mathew akatoka mle chooni alimokuwa amejibanza na kutembea kwa kasi akishuka chini kuwawahi wale jamaa.
“ Mathew tayari nimewaona wale jamaa katika kamera.Wako wanne na daktari mmoja wa kizungu.Wale jamaa wameagana na Yule dakatari ambaye kwa sasa anaongea na daktari mwenzake.Namuona Yule daktari ana kitambulisho katika koti lake .Ngoja nimvute karibu nifahamu jina lake” akasema Anitha
“ Ok Anitha.Achana na wale jamaa.Elekeza macho kwa daktari.Mimi niko ghorofa ya pili ninashuka ” akasema Mathew
Baada ya sekunde kadhaa Anitha akasema
“ I’ve got him !”
“ Anaitwa Michael Rodriguerz “
“ Good Job Anitha “ akajibu Mathew tayari akiwa ghorofa ya kwanza
Bado Dr Michael aliendelea kuongea na daktari mwenzake.Mathew akawapita halafu akaenda kusimama nje katika maua
“ Anitha niko hapa nje nikimsubiri atoke” akasema Mathew
“ Mathew , Dr James anatoka nje ya jengo anaelekea upande wa mashariki nadhani ndiko iliko ofisi yake” akasema Anitha
“ Ok Anitha nimekwisha muona,ninamfuatilia” akasema Mathew na kuanza kutembea taratibu akimfuata Dr Michael
“ Mathew nimetafuta kwa haraka haraka taarifa za Dr Michael ni kwamba ana umri wa miaka 53,ni mzaliwa wa Mexico,amesoma nchini Marekani ,Mexico na Urusi.Ni baba wa watoto watatu,Peter,Michael jr na Celine .Mke wake anaitwa Michelle Donalds mzaliwa wa Texas marekani.Dr Michael ni daktari bingwa wa mishipa ya fahamu” akasema Anitha
“ Thank you Anitha.Dr Michael sasa anaingia katika jengo lenye ofisi.Sintoweza tena kuingia mle ndani kwa sababu kuna kibao hapa kinachoonyesha kwamba huruhusiwi kuingia ndani kama si muhusika.Endele
a kumfuatilia kupitia kamera” akasema Mathew na kuanza kurudi mahala walikoegesha gari
“ John Mwaulaya !..” akawaza Mathew na mwili wote ukamsisimka
“ Bado siamini kama kweli ni yeye ndiye aliyelazwa ndani ya chumba kile hadi nitakapomtia machoni ndipo nitaamini” akawaza Mathew huku akitembea kwa kasi .Mara Anitha akaumuita
“ Mathew ,Dr Joshua ametoka,anaelekea katika eneo la kuegesha magari ya madaktari,anaingia katika gari lenye namba BV36P44.Umefika wapi ? akauliza Anitha
“ Tayari nimekwisha fika Anitha” akasema Mathew wakati akilikaribia gari lao.Alitembea kwa haraka akaufungua mlango na kuingia ndani
“ Ameelekea wapi? Akauliza Mathew huku akiwasha gari
“ Ameelekea geti la Mashariki”
“ Ok twende tuondoke tutamuwahi hapo bara bara kuu.” Akasema Mathew na kuwasha gari wakaondoka
Walisimama kwa dakika tatu kusubiri nafasi ya kuingia barabara kuu na mara Anitha akaliona gari la Dr Michael akamuonyesha Mathew
“ Ok.Nimemuona” akasema Mathew na kuingia barabarani akiacha magari matatu kati yao na Dr Michael
“ Hatupaswi kumpoteza.Tunamuhitaji sana” akasema Mathew
“ Mathew whats going on? Who is John mwaulaya? Nimejaribu kutafuta taarifa zake lakini hakuna mahala nimeweza kupata.Who is he? Akauliza Anitha
“ Tutaongea baadae Anitha lakini kwa sasa tuelekeze macho yetu kwa Dr Michael tusije tukampoteza.” akasema Mathew
“ Mathew tunaifanya kazi hii pamoja,na ili tufanikiwe tafadhali naomba uwe muwazi kwangu katika kila jambo ili tusaidiane mawazo nini cha kufanya” akasema Anitha
“ Usihofu Anitha.Kuna mambo mengi sana ambayo unahitaji kuyafahamu lakini kwa sasa tuyaweke pembeni na tuhakikishe hatumpotezi Michael” akasema Mathew.Anitha hakuuliza kitu tena wakaendelea na safari yao ya kumfuatilia Dr Michael.
Baada ya kutoka hospitali,Dr Michael alikwenda moja kwa moja Tanganyika Internationa school akaegesha gari na baada ya dakika kama tatu hivi ,mwanadada mmoja akatokea akiwa amemshika mkono mtoto mdogo .Dr Michael akamkumbatia Yule mtoto na kuwafungulia mlango wakaingia garini halafu wakaondoka.
“ Yule mtoto anaitwa Michael jr.Ni mtoto wa pili wa Dr Michael na Yule mwanadada aliyeongozana nao nadhani ni mtumishi wao” akasema Anitha
Waliendelea kumfuatilia Dr Michael bila ya yeye kufahamu kama anafuatiliwa.Toka pale shuleni Dr Michael hakupita sehemu nyingine ,alielekea moja kwa moja nyumbani kwake.Alipofika kwake alipiga honi akafunguliwa geti na kuingia ndani kisha geti likafungwa
“ Whats next ? akauliza Anitha
“ Najaribu kutafakari nini cha kufanya” akasema Mathew na mara mlango mdogo wa geti ukafunguliwa na Yule mwanadada aliyekuwa ameongozana na Dr Michael toka shuleni akatoka.
“ Yule dada anatoka.Amebeba mkoba wake inaonekana kama vile anaondoka” akasema Anitha
“ Go get her.We can use her .Tunahtaji kumpata Yule mtoto wa Dr Michael na itakuwa rahisi kama tukimtumia yeye” akasema Mathew.Anitha akashuka garini na kutembea kwa haraka akamfuata Yule dada ambaye alikuwa akitembea taratibu huku akiongea na simu.Mara tu alipomaliza kuongea na simu Anitha akamsalimu
“ Habari yako dada”
“ Habari yangu nzuri.Habari yako? Akasema Yule dada ambaye alikuwa na sauti laini ya upole
“ Naitwa Anitha,mwenzangu unaitwa nani? Akasema Anitha hukuakitabasamu
“ Naitwa Lydie Masawe” akasema
“ Nafurahi kukufahmu Lydie.Unaelekea wapi hivi sasa?
“ Naelekea nyumbani lakini nitapita kwanza saluni kurekebisha nywele na kucha”
“ Sawa Lydie,nadhani ni mara ya kwanza mimi na wewe kuonana”
“ Ndiyo ni mara ya kwanza dada Anitha.Sina kumbu kumbu kama tumewahi kuonana” akasema Lydie
“ Ok Lydie.Kama hutajali nina maongezi nawe kidogo kuhusu kazi.Sijui unaweza kuwa na nafasi sasa hivi? Au kama unaelekea uko saluni,nina usafiri wangu tunaweza tukaongozana na tukapata wasaa wa kuzungumza” akasema Anitha.Lydie hakuwa na wasi wasi wakaelekea mahala akina Mathew walikoegesha gari
“ Lydie huyu ni dereva angu anaitwa Mathew” Anitha akafanya utambulisho mfupi baada ya kuingia garini
“ Mathew tupeleke Zulphat beauty salon” akaelekeza Anitha.
Ndani ya gari walikuwa wakiongea mambo mbali mbali yahusuyo urembo kwa ujumla hadi walipowasili Zulphat beauty salon moja kati ya saluni kubwa za akina mama jijini Dar.Lydie alitengenezwa kwa gharama za Anitha kwani saluni hii ni moja kati ya saluni zenye gharama kubwa.Baada ya hapo wakaelekea Ibona hotel kwa ajili ya maongezi
“ Lydie nimekuleta hapa ili tuweze kuongea kwa utulivu na nafasi” akasema Anitha wakiwa katika bustani tulivu
“ Nakusikilza dada Anitha”
“ Lydie umeolewa? Akauliza Anitha ili kutaka kumfahamu vizuri
“ Hapana bado ila nina mtoto mmoja”
“ Hongera.Mwanao yuko wapi? Akauliza Anitha
“ Yuko kwa babu yake huko Moshi”
“ Kwa nini usimchukue ukaishi naye?
“ Natamani sana kufanya hivyo lakini hali ngumu ya maisha inanilazimu nimuache kwa babu zake”
“ Sawa nimekuelewa Lydie.Sasa dada yangu bila kupoteza wakati nimekufuata nina kazi moja ambayo nahitaji unifanyie.Endapo utakubali basi unaweza ukapata pesa ambayo itakusaidia sana katika kuondokana na maisha haya duni na ukaanzisha biashara zako mwenyewe na hutafanya tena kazi kwa mtu na utakuwa na uwezo wa kuishi na mwanao na kumpatia elimu bora ” akasema Anitha
“ Nitashukuru sana dada Anitha kama utanipatia kazi ambayo itaniwezesha niweze kupata mtaji wa kujiajiri mwenyewe.Niambie ni kazi gani unataka nikufanyie? Una mtoto wa kulea?”
“ Hapana sina mtoto bado Lydie lakini kuna kazi nyingine ndogo tu tena ya masaa machache.Kwanza nieleze pale kwa Dr Michael unafanya kazi gani?
“ Kazi yangu ni kumlea Michael Jr.Asubuhi kumuandaa na kumpeleka shule ambako huwa nikishinda huko hadi saa nane mchana.Dereva huja kutuchukua na kuturudisha nyumbani.Saa tisa kamili ndiyo mwisho wangu wa kazi na hurejea nyumbani” akasema Lydie
“ Ok Lydie sasa ni hivi,kuna taarifa muhimu sana tunayoihitaji toka kwa Dr Michael na ambayo hawezi kutupatia hivi hivi,kwa hiyo tunahitaji kutumia njia mbadala kuipata taarifa hiyo.Nahitaji kumtumia mtoto wake Michael kumtisha kidogo ili aweze kunipatia taarifa hiyo” akasema Anitha na kumtazama Lydie
“ Wewe ni polisi? Akauliza Lydie kwa wasi wasi
“ Hapana,mimi si polisi lakini kazi zangu zinafanana kidogo na za polisi.” akajibu Anitha
“ Kwa hiyo unataka kumtumiaje Michael Jr?
“ Nitamtumia kama chambo ili niweze kuipata taarifa ninayoitaka toka kwa Dr Michael.Najua anampenda sana mwanae hivyo akisikia kwamba mtoto wake yuko mikononi mwangu lazima atatoa taarifa hiyo ninayoitaka” akasema Aitha.Lydie akaonekana kuogopa sana
“ Dada Anitha naona siwezi kuifanya hiyo kazi.Ni kazi ya hatari sana na inaweza kunisababishia matatizo.Hilo ni kosa kubwa na endapo nikishikwa na polisi nitaweza hata kufungwa kwa kosa la utekaji na mwanangu akabaki akiteseka.Utanisamehe dada yangu sintoweza”
Anitha akatabasamu kidogo na kusema
“ Usiogope Lydie.Suala hili haliwezi kwenda polisi kwa sababu mimi ninafanya kazi kwa niaba ya polisi kwa hiyo hata kama likifika kwao wananifahamu kwamba niko kazini na lengo langu si kumuumiza mtoto huyo wala Dr Michael,bali ni kupata taarifa hiyo muhimu sana kwa usalama wa taifa.”
“ Pamoja na hayo dada Anitha bado naona sintoweza.Sijawahi kufanya kazi kama hiyo hata mara moja,zaidi ya yote familia ile wananipenda na kunihudumia vizuri ,siwezi kuwafanyia kitendo kama hicho” akasema Lydie.Anitha akamtazama kwa sekunde kadhaa na kumuuliza
“ Lydie unatoka katika mkoa wa Kilimanjaro,si ndiyo?
“ Ndiyo”
“ Ninawafahamu watu wa Kilimanjaro hususani wanawake ni watafutaji wazuri wa pesa.Ni wapambanaji wa kweli katika kutafuta maisha.Wanaitafuta pesa bila kuchoka na hawaogopi changamoto zilizoko mbele yao na hiyo ndiyo siri ya wao kufanikiwa sana.Tunawaona wengi hapa Dar es salaama namna walivyofanikiwa ,namna walivyochangamka kuitafuta pesa,hawakuja hapa mjini kutazama maghorofa au kuza sura zao nzuri,bali wamekuja kutafuta pesa.Ninakupa fursa ya kujikwamua kiuchumi naomba usiipuuze.Please Lydie wake up.This is your chance.Vaa uhusika wa mwanamke wa kichaga asiye ogopa changamoto na ukubali kuifanya kazi hii ndogo lakini yenye maslahi manono.Niambie unahitaji kiasi gani nikupatie? Akauliza Anitha.Lydie akainama akafikiri
“ Ok ngoja nikutajie .Mimi nitakupa Tsh Milioni saba ili uweze kunifanyia kazi hiyo” akasema Anitha na mara Lydie akainua kichwa
“ Kiasi hicho kiko tayari?
“ Ndiyo kipo tayari.Uko tayari kuifanya kazi hii?
“ Kama mtanilipa kiasi hicho cha pesa mimi niko tayari lakini kwa sharti moja tu kwamba mnipatie kwanza kabla sijawafanyia kazi hiyo kwa sababu ninaweza nikahatarisha usalama wangu halafu msinilipe chochote nikawa nimeharibu kazi yangu na maisha yangu”
“ Usihofu kuhusu pesa hata sasa hivi unaweza ukapewa mradi tu ukubali kuifanya hiyo kazi” akasema Anitha
“ Mimi niko tayari kuifanya.Si umesema suala hili haliwezi kufika polisi?
“ Ndiyo haliwezi kufika polisi”
“ Ok nielekeze unataka nifanye nini?
“ Asubuhi utampeleka Michael Jr shule kama kawaida.Saa tano za asubuhi tutakuja na gari na utawaambia waalimu kwamba umepigiwa simu uwahi kurejea nyumbani.Utatukabidhi mtoto na tutakukabidhi mzigo wako na utapotea na huo utakuwa ni mwisho wako kufanya kazi pale kwa Dr Michael.Sisi tutakaa na Yule mtoto kwa masaa machache na Dr Michael atakapotupatia taarifa yetu basi tutampatia mtoto wake.Nakuhakikishia tena kwamba hatuna lengo la kumdhuru mtoto wala mtu yeyote” akasema Anitha.Wakakubaliana na Lydie halafu wakaagana
“ Amekubali japo haikuwa rahisi kumshawishi.Imenilazimu kumtajia dau kubwa ndipo akakubali.Tutamlipa Tsh Milioni saba.” Akasema Anitha baada ya kuachana na Lydie na yeye kurejea garini alikomuacha Mathew
“ Good.Una hakika hawezi kutusumbua au kutuletea matatizo? Akauliza Mathew
“ She wont.She needs money.” Akajibu Anitha
“ Ok Good.Noah amenipigia simu tayari amekwisha wasili.Timu imekamilika” akasema Mathew
“ Wow that’s great.So whats next?
“ Kwa sasa tunatakiwa kuwasiliana na Elibariki ili tumfahamishe kuhusiana na pesa hii ili watupatie au kama hawana basi tutatumia za kwangu na wataturejeshea.Hatuwezi kukwama kwa sababu ya pesa” akasema Mathew
*********
Eugenia Conrad,msaidizi wa Dr Flora Johakim mke wa rais,alitoka mbio ndani ya chumba cha Dr Flora huku akipiga kelele. Walinzi walimkamata na kumuuliza kulikoni kupiga kelele zile
“ Mama Flora !!....Mama Flor……………!!!” hakumaliza sentensi yake akaanguka na kupoteza fahamu.Koplo Winifrida mlinzi wa Dr Flora akakimbia hadi chumbani kuangalia kuna nini,na ghafla akahisi miguu inamuisha nguvu.Dr Flora Johakim mke wa rais alikuwa amelala kitandani huku damu zikimtoka mdomoni na puani.Akajikaza na kukisogelea kitanda na kuita
“ Dr Flora.!!,Dr Flora !!....
Dr Flora hakutikisa hata ukope.Haraka haraka Winifrida akakimbilia katika simu akampigia Captain Amos daktari wa familia ya rais ambaye alifika mara moja na vipimo akampima na kuamuru liitwe gari la wagonjwa haraka.Gari la wagonjwa likafika Dr Flora akapakiwa na kukimbizwa katika hospitali ya jeshi.Pale akapimwa na kukutwa tayari amekwisha fariki.Baada ya kuthibitishwa kwamba amefariki dunia Captain Amos akampigia simu Dr Joshua
“ Hallow Captain” akasema Dr Joshua
“ Mr President its done.She’s dead”
“ Thank you Captain Amos.Niko njiani narejea Dar es salaam” akasema Dr Joshua na kukata simu.Captain Amos alibaki amesimama ameegemea mti.Alikuwa na mawazo mengi sana.
“ I’ve killed the first lady…Please forgive me lord” akawaza Captain Amos
TUKUTANE SEHEMU IJAYO………………
 
Back
Top Bottom