Peniela (Story ya kijasusi)

Duh

Hii ndiyo hadithi sasa....inanikumbusha miaka ya 80-90 wakati tukiwa na watunzi mahiri wa riwaya zinazomake sense na sio wa siku hizi wa mwendokasi

Mnaokumbuka kina Ben Mtobwa, Elvis Musiba na wengineo. huu ni mzigo mwandishi ameonyesha weledi mkubwa wa lugha, kupangilia matukio vizuri na hivyo kuwa na mantiki. Heko sana kwake

LEGE kwa niaba ya kisukari na wengine tunakushukuru kwa huu mzigo mzito usichoke kutupia
 
PENIELA SEASON 3

EPISODE 3

MTUNZI : PATRICK .CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Hallow Mathew ,uko wapi? Akauliza Anitha baada ya kupokea simu

“ Tayari nimerejea nyumbani.Wewe uko wapi? Akauliza Mathew
“ Niko njiani ninarejea nyumbani.Nimetoka kuonana na Peniela na tayari nimemkabidhi vile vifaa na jioni ya leo atakapokutana na Dr Kigomba tutaanza kupata kila taarifa toka kwa Dr Kigomba.” Akasema Anitha
“ Good job Anitha.Ninakusubiri hapa nyumbani.Kuna suala zito linalotukabili”

“ Kuna jambo jipya ? akauliza Anitha kwa wasi wasi kidogo

“ Si jipya sana lakini ni mwendelezo wa kile ambacho tumekuwa tunaendelea nacho” akasema Mathew

“ Sawa Mathew .Niko njiani ninakuja sasa hivi” akajibu Anitha na kukata simu


ENDELEA…………………


Baada ya kuachana na Anitha ,Peniela hakutaka tena kwenda sehemu yoyote ile zaidi ya nyumbani kwake.Alihisi kichwa chake kizito sana hivyo alihitaji mapumziko.Mambo mengi yalikuwa yametokea ndani ya muda mfupi.
Alifika nyumbani kwake na moja kwa moja akaelekea chumbani ,akajitupa kitandani.Kichwa kilijaa mawazo mengi sana.Picha ya kile kilichotokea chumbani kwa John bado iliendelea kuzunguka kichwani kwake na kumjaza mawazo .Sauti ya John Mwaulaya akitamka namna alivyowatoa uhai wazazi wake bado iliendelea kupenya na kusikika masikioni mwake.Machozi yakamtoka

“ Nilijitahidi nisiseme chochote kwa wakati ule kwani sikutaka watu wagundue kwamba nimeumizwa na taarifa ile lakini ukweli katika maisha yangu sijawahi kuumizwa kama nilivyoumizwa leo na taarifa ile kuhusiana na wazazi wangu.John ni binadamu mwenye roho ya kishetani kabisa.Hana hata chembe ya utu ndani yake.He killed my parents !!..Sikupata hata nafasi ya kuonja upendo wa mama yangu kipenzi.!!..akawaza Peniela na kuangua kilio .Aliumizwa mno kwa kuufahamu ukweli kuhusiana na wazazi wake.
“ Kwa mujibu wa maelezo ya John ,baba yangu alikuwa ni mtu mwenye wadhifa mkubwa serikalini na kutokana na nafasi yake kubwa aliyokuwa nayo hakutaka kuwa na kashfa yoyote ya kumpa mimba mama yangu ambaye alidhamiria kwenda kumshtaki mahakamani kwa kitendo cha kumtelekeza yeye na mtoto yaani mimi.Kwa kuogopa kashfa hiyo ,baba akaamuru John akamuue mama pamoja na mimi.The first monster was my own father.He ordered me killed.Hakuwa na huruma hata kidogo na damu yake kupotea.Natamani niione sura ya binadamu huyu ambaye hakuwa na hata chembe ya huruma kwa mtoto wake mwenyewe ambaye yeye kwake wadhifa ni muhimu zaidi kuliko hata damu yake.” Akawaza Peniela na kuendelea kulia kwa uchungu mkubwa.

“ Kwa maelekezo ya baba,John alimuua mama yangu lakini kwa mara ya kwanza katika historia ya maisha yake,John akaingiwa na moyo wa huruma na akaenda kinyume na amri aliyopewa akaamua kuniacha hai,akanichukua na kunihudumia akahakikisha ninapata huduma zote na ninaishi maisha mazuri.Kwa hili ninamshukuru sana kwani bila yeye nisingeweza kufika umri huu. Kwa upande Fulani sipaswi kumchukia au kumlaumu sana John kwani alikuwa anatekeleza amri aliyopewa na baba yangu.Mtu pekee ambaye ninapaswa kumchukia hapa ni baba.How could he be so cruel?? Akajiuliza Peniela na kuendelea kulia .Alihisi mwili wote kumuisha nguvu.

“ Tayari nimekwisha fahamu historia yangu na nimelia vya kutosha.Nimemwaga machozi mengi kumlilia mama yangu ambaye aliuawa kwa sababu yangu.Aliuawa akiwa katika harakati za kunitetea mimi.Ninachotakiwa kukifanya kwa sasa baada ya kuufahamu ukweli ni kumfahamu vyema mama yangu.Kuifahamu familia yake,kuwafahamu ndugu zake na kujua kama alikuwa na mtoto au watoto wengine.Pamoja na unyama na ukatili wake lakini nitahitaji pia kumfahamu baba yangu pia ili nijue alikuwa ni mtu wa namna gani,vile vile nifahamu kama nina ndugu zangu wengine.” Akawaza Peniela na kuchukua kitambaa akajifuta machozi
“Siku ile nilipoonana na John kwa mara ya kwanza alinikabidhi kasha na akaniambai kwamba kama akifariki nihakikishe ninayakamilisha makasha matatu na baada ya kukamilika yote ndipo nitakapoweza kufahamu mimi ni nani.Ninahisi historia yangu yote iko ndani ya makasha hayo.Inavyoelekea katika makasha hayo kuna mambo makubwa na ya msingi sana.Nitahakikisha ninayapata yote.” Peniela akastuliwa toka mawazoni na mlio wa simu .Ilikuwa ni simu ile ambayo huitumia kuwasiliana na Dr Joshua.Akainuka na kwenda kuichukua akabonyeza kitufe cha kupokelea.

“ Hallow” akasema Peniela.Zikapita sekunde kadhaa bila kujibiwa,Peniela akapatwa na wasi wasi

“ Hallow Dr Joshua” akasema tena .Safari hii akasikia mtu akivuta pumzi ndefu na kusema
“ Hallow Peniela ,unaendeleaje malaika wangu? Sauti ile ya Dr Joshua ikamshangaza kidogo Peniela kwani haikuwa ile ambayo amezoea kuisikia.
“ Dr Joshua are you ok? Akauliza Peniela

“ I’m ok Peniela.Hofu yangu ni kwako tu.You sound so strange today na ndiyo maana ulipopokea simu nilisita kidogo kuongea.Have you been crying? Akauliza Dr Josha

“ No Dr Joshua.Nimerudi sasa hivi nyumbani and I’m very tired.Vipi maendeleo ya Flaviana?

“ Pole sana kwa uchovu lakini sauti yako inaonyesha wazi kwamba ulikuwa unalia.Any way kuhusu Flaviana tayari amesafirishwa leo kwenda afrika ya kusini kwa matibabu zaidi na kwa taarifa nilizozipata muda si mrefu tayari wamefika salama na tayari ameanza kushughulikiwa japo bado hali yake si nzuri.Tuzidi kumuombea” akasema Dr Joshua
“ Pole sana Dr Joshua.Tuzidi kumuombea na Mungu atamponya.By the way aren’t you suppose to be there with your family right now? Akauliza Peniela
“ Ni kweli Peniela,natakiwa nikaungane na familia yangu sasa hivi lakini kilichonifanya nisiambatane nao ni kikao kikubwa cha wakuu wa nchi za afrika mashariki. Lakini usiku wa leo nitaondoka kwenda kuungana na familia yangu afrika ya kusini.Natamani sana kama ningeonana nawe kabla sijaondoka.Hiki ni kipindi kigumu sana kwangu and I think I need some comfort and the only person who can comfort me is you Peniela.” Akasema dr Joshua
“ Dr Joshua pole sana .Nafahamu ni wakati gani ulio nao sasa hivi lakini nasikitika kwamba sintaweza kuonana nawe kwa leo kabla hujaondoka.Nitaonana nawe utakaporejea toka afrika ya kusini ila naomba ufahamu kwamba niko pamoja nawe katika kipndi hiki kigunmu sana kwa familia yako” akasema Peniela
“ Sawa nimekuelewa Peniela.Nitaonana nawe baada ya kurejea .Tuzidi kumuombea Flaviana ili Mungu amjaklia nafuu ya haraka.Kabla hatujaagana una tatizo lolote? Kama kuna chochote kinachokusumbua na kukuumiza kichwa tafadhali naomba usisite kunieleza.” Akasema Dr Joshua
“ Ahsante sana kwa kunijali Dr Joshua ila kwa sasa sina tatizo lolote isipokuwa ni Yule mjomba wangu niliyekueleza hali yake imezidi kuwa mbaya na tayari nimempeleka katika ile hospitali na wamekwisha anza kumshughulikia”
“ Pole sana Peniela.Pole sana malaika wangu.Ulipaswa kunitaarifu mapema walau na mimi nifike nimjulie hali. “Akasema Dr Joshua
“ Usijali Dr Joshua,huna haja ya kupoteza muda wako kwa kwenda hospitali.Una mambo mengi yanayokukabili kama mkuu wa nchi .Msaada mkubwa ulionipatia wa hospitali unatosha sana.”
“ Ouh Peniela my queen usiseme hivyo.Kukusaidia wewe ni jukumu langu.Thamani yangu kwako hailinganishwi na chochote kile kwa hiyo ninajiona ni mwenye bahati sana kuwa ni sehemu ya msaada kwako.Hata hivyo nitawasiliana na daktari mkuu wa hospitali ile ili walipe uzito unaostahili suala la ugonjwa wa mjomba wako” akasema Dr Joshua
“ Nashukuru sana kwa kunijali Dr Joshua.Nakutakia safari njema na tafadhali unijulishe maendeleo ya Flaviana mara utakapowasili afrika ya kusini.”
“ Nitakutaarifu Flaviana .Ubaki salama na ninaomba nikukumbushe kwamba ninakupenda kuliko kitu chochote” akasema Dr Joshua na kumalizia kwa busu kisha akakata simu.Peniela akaitupa simu kitandani

‘ Hili zee halina akili nzuri hata kidogo.Laiti lingenifahamu mimi ni nani lisingethubutu kuniita mimi malaika wake.Siku inakuja na atanitambua mimi ni nani” akawaza Peniela halafu akainuka na kuelekea bafuni.
“ Imekuwa ni siku mbaya na ngumu sana kwangu.Hata hivyo namshukuru sana Mathew kwa kunisaidia kuufahamu ukweli.Bila yeye katu nisingefahamu chochote kuhusiana na wazazi twangu.Natamani hali ya John ingekuwa nzuri ili anieleze kwa kina kuhusiana na wazazi wangu.Kuna mambo mengi ambayo nahitaji kuyafahamu kutoka kwake namuomba Mungu asimchukue mapema kwani yawezekana kuna mambo mengine mengi nisiyoyafahamu kuhusu mimi” akawaza Peniela na picha ya John ikamjia
“ Pamoja na yote aliyonifanyia lakini najikuta bado nikimuonea huruma sana Yule mzee.Nadhani ni kwa sababu ya wema wake mkubwa kwangu.Toka nikiwa mdogo alihakikisha ninapata matunzo na malezi mazuri .Hakuna kitu ambacho nimewahi kupungukiwa.Ni kwa sababu yake nimesoma vizuri,nimeishi maisha mazuri.Kuwa na hasira naye kwa sasa haitanisaidia chochote.John ni mtu ambaye nimekuwa nikitamani sana kumuona toka nikiwa mdogo lakini nimepata bahati ya kukutana naye katika kipindi kama hiki akiwa mgonjwa na hajiwezi,anahitaji msaada wangu.Anyway ngoja niyaweke pembeni mambo ya John na nielekeze akili yangu katika suala kubwa lililoko mbele yangu.Jioni ya leo nina miadi na Dr Kigomba.Huyu ni mtu muhimu sana ambaye atatusaidia katika kufanikisha operesheni yetu .Ninashukuru kwa sababu tayari naye amekwisha nasa katika himaya yangu na kwa sasa nina uhakika mkubwa kwamba operesheni yetu itakwenda vizuri.Nataka tulimalize suala hili na niachane kabisa na aina hii ya maisha .Nimekuwa nikitumika kwa muda mrefu na Team SC41 kama chombo chao cha kuwatafutia taarifa na katika hilo mwili wangu umekuwa ni kama bidhaa kwa kutumiwa na wanaume ili nipate taarifa muhimu.Sitaki kuendelea na aina hii ya maisha na kitu pekee kitakachonifanya nisiendelee kuishi maisha ya namna hii ni kujiondoa kutoka team Sc41 na kuimaliza kabisa.Najua ni kazi ngumu lakini lazima nipambane hadi nihakikishe nimefanikiwa kuimaliza team Sc41.” Akawaza Peniela halafu akatoka bafuni na kupanda kitandani kujipumzisha kabla ya kuonana na Dr Kigomba jioni ya siku hiyo


********

Bado zoezi la uchunguzi wa ugonjwa unaomsumbua John Mwaulaya liliendelea.Dr Edwin na Dr Alex waliendesha uchunguzi ule wakishirikiana na madaktari bingwa wengine watatu toka katika ile hospitali.Josh na Dr Martin Desmond walikaa katika sehemu ya kupumzikia wakisubiri kupewa taarifa ya matokeo ya uchunguzi pindi utakapokamilika.
Wakiendelea na maongezi ya kawaida,mara akatokea Dr Edwin na kumuita Josh wakaenda kusimama mahala kusikokuwa na watu
“ Dr Edwin nini kinaendelea? Uchunguzi umekamilika? Akauliza Josh kwa wasi wasi.
“ Josh ni mapema mno kusema chochote kwa sasa kwani uchunguzi bado haujakamilika.Tutakapokuwa tayari tutakutaarifuni.Kwa sasa nimekuita kwa jambo moja la muhimu” akasema Edwin na kunyamaza ,akatazama huku na huko na kuhakikisha hakuna anayesikia kile wanachokiongea kisha akasema
“ Hali ya John Mwaulaya ilibadilika ghafla baada ya sisi kuondoka pale nyumbani kwake na kwa mujibu wa Martin ni kwamba kuna watu wawili walifika chumbani kwa John na kuanza kumuhoji na kumsababishia mstuko mkubwa.Je ni kweli? Akauliza Dr Edwin.Josh akainama
“ Niambie ukweli Josh kwani tayari tunafahamu kila kitu.Nataka tu unithibitishie kwamba suala hili ni la kweli.” Akasema Dr Edwin

“ Ni kweli.Kuna watu wawili walikuja kuonana naye baada ya nyie kuondoka na hapo ndipo hali ya John ilipobadilika” akajibu Josh

“ Vizuri .Unawafahamu watu hao ni akina nani? Nimeambiwa wewe ndiye uliyekuwa mlinzi wa John kwa kipindi kirefu je uliwahi kuwaona watu hawa nyumbani kwa john hata mara moja? Ni watu ambao wamekuwa wakishirikiana na John? Akauliza Dr Edwin

“ Watu wale siwafahamu vizuri ila ninamfahamu mmoja wao anaitwa Jason.Huyu niliwahi kupewa maelekezo na John ya kumfanyia mahojiano ili kufahamu mambo kadhaa kutoka kwake .Huyu mwingine aitwaye Mathew leo ndiyo nimemuona lakini wote hawa ni marafiki wa Peniela.Nadhani endapo utamuuliza Peniela anaweza akakueleza vizuri zaidi kuhusiana na huyu Mathew”
“ Ahsante Josh.Ila kwa mujibu wa Martin ni kwamba huyu Mathew aliahidi kurejea tena kwa John.Inaonekana yeye na John ni watu wanaofahamiana na nina wasi wasi lazima kuna jambo ambalo sisi hatulifahamu kuhusiana na John na Mathew.Nina wasi wasi kwamba kama mtu huyu anamfahamu sana John basi anaweza akawa anaifahamu team Sc41.Nina hitaji kumfahamu mtu huyu.Pale nyumbani kwa John kuna kamera za ulinzi naomba unipatie picha zote zilizopigwa na kamera wakati wale jamaa wakiingia.Nahitaji sana kumfahamu huyu Mathew” akasema Dr Edwin

“ Usijali Dr Edwin.Ninakwenda kushughulikia suala hilo” akajibu Josh

“ Nashukuru sana Josh” akajibu Dr Edwin na kurejea ndani.



********



Anitha alirejea nyumbani na kusalimiana na jaji Elibariki aliyekuwa amekaa sebuleni akitazama filamu.Anitha alionekana kuchoka sana.
“ Pole sana Anitha.Unaonekana umechoka sana leo” akasema jaji Elibariki
“ Ni kweli ninahisi uchovu mwingi.Nahisi nahitaji mapumziko.Mathew yuko wapi?
“ Mathew naye amejipumzisha chumbani kwake.Vipi huko utokako mambo yanakwendaje?
“ Mambo yote yamekwenda vizuri kama tulivyopanga na tayari nimempatia Peniela vile vifaa kwa hiyo tutaanza kupokea taarifa jioni ya leo pindi atakapoonana na Dr KIgomba.Kila kit………” Anitha akakatisha maongezi baada ya kusikia sauti ya Mathew

“ Hallow Anitha” akasema Mathew aliyetoka chumbani kwake alikokuwa amejipumzisha

“ Ouh Mathew .Jaji kaniambia ulikuwa umejipumsisha”

“ Ndiyo .Nilikuwa nimejipumzisha kidogo.Kichwa changu kilikuwa kizito sana.Vipi huko utokako kila kitu kimekwenda vizuri?

“ Huko kila kitu kimekwenda vizuri.Tayari nimempatia Peniela vile vifaa na jioni ya leo tutaanza kupokea taarifa toka kwa Dr Kigomba.Vipi huko ulikokwenda ulifanikiwa? Uliniogopesha kidogo uliposema kuna jambo zito” akasema Anitha
“ Nilikokwenda kuna mafanikio.Elibariki alikuwa sahihi kuhusiana na asili ya Peniela.Tumefahamu kila kitu kuhusiana na Peniela.” Akasema Mathew kisha akamsimulia Anitha kila kitu kilichotokea na alichokigundua
“ Ouh Mungu wangu.Nimestushwa sana na taarifa hiyo.Huyu John mwaulaya ni shetani kabisa.Nimesikia taarifa zake za kikatili lakini sikuwahi kuhisi kama anaweza akawa mkatili kiasi hiki.Lakini mbona nilipoonana na Peniela hakuonyesha dalili zozote za kama kuna jambo zito lilimtokea.Alikuwa katika hali ya kawaida kabisa” akasema Anitha

“ Peniela is a strong woman.Hata kama kuna jambo linamsumbua huwa si rahisi kuonyesha kwa nje but I know she’s deeply hurt” akasema jaji Elibariki

“ Namuonea huruma sana Peniela” akasema Anitha
“ Anyway tuachane na masuala hayo ya peniela,kwa sasa kuna suala lingine kubwa limejitokeza.Yash amerejesha majibu ya zile karatasi “

“ Real ?!!...Amegundua nini? Akauliza Anitha
“ Anitha its something very serious” akasema Mathew na kuwafanyia ishara Elibariki na Anitha wamfuate ofisini.
“ Yash kwa kushirikiana na jopo la wanasayansi wamegundua kwamba kilichoandikwa katika karatasi zile ni kanuni za kutengeneza kirusi ambacho kinatajwa kuwa hatari sana na ambacho kinaweza kutumika kufanya maangamizi makubwa .” Akasema Mathew
“ Ouh my God !..Anitha akastuka sana.
Mathew akaendelea kumueleza kwa undani kuhusiana na kile alichokiandika Yash.
“ Sasa picha imeanza kuja” akasema Anitha baada ya Mathew kumaliza kumpa maelezo
“ Ni kweli ,lakini kuna maswali ambayo lazima tujiulize na tuyatafutie majibu.Kwanza tunatakiwa kumfahamu aliyeandika kanuni zile ni nani? Yuko wapi ? Karatasi zile zimefikaje katika ikulu yetu? Kitu kingine ambacho tunatakiwa tukitafutie majibu ni kwamba kama karatasi zile zilikuwa ikulu basi kutokana na unyeti wake ni lazima zilikuwa zimehifadhiwa mahala pa siri kubwa na ambapo si rahisi kwa mtu kama Edson kuweza kuzifikia na kuziiba.Edson alikuwa ni mfanyakazi wa kawaida katika idara ya habari ikulu na asingeweza kabisa kujua mahala nyaraka nyeti kama hizi zilikohifadhiwa kwa hiyo basi nashawishika kuamini kwamba lazima kuna watu au mtu ambaye alifanikisha kwa Edson kuweza kuzipata kirahisi.Nahisi Edson alitumiwa tu ili kuweza kuzipata kirahisi nyaraka zile.Na kama hisia zangu ni kweli basi lazima mtu huyo ndiye atakayekuwa kinara wa mpango huu wote.Kingine kikubwa ambacho tunatakiwa tukifahamu ni kama kirusi hicho kimekwisha tengenezwa ama bado na kama tayari kiko wapi? Kama bado hakijatengenezwa ni kufuta kabisa mpango wowote wa kukitengeneza kwa kuhakikisha tunalichimba jambo hili hadi mzizi wake na kuwapata wahusika.Guys we’re going into something very dangerous so we need to get prepared for this.This is a victory or death.Siwaogopeshi lakini hiyo ndiyo hali halisi na ninapenda niwe muwazi kwenu.” Akasema Mathew
“ Binafsi hufurahi sana ninapofanya kazi pamoja nawe Mathew.Una akili kubwa ya kuchambua mambo.Ni kweli tunalazimika kutafuta majibu ya maswali hayo uliyoyaorodhesha.Katika jambo ulilolisema mwishoni kuhusiana na mtu ambaye anaweza akawa nyuma ya mpango huu nakubaliana nawe kabisa.Si rahisi kwa akina Edson peke yao kulifanikisha jambo kubwa kama hili.Kufanikiwa kuiba nyaraka ikulu si jambo dogo lazima ni mpango mkubwa uliobuniwa na watu makini na ambao walifahamu mahala nyaraka hizo zilipo.”akasema Anitha

“ We need to find out who is behind this.Tukimpata huyo anaweza akatusaidia sana katika kupata majibu ya baadhi ya maswali yetu” akasema Mathew
“ Jamani kwa mtazamo wangu mimi nadhani mtu ambaye yuko nyuma ya jambo hili lazima atakuwa ndani ya ikulu.Si rahisi kwa mtu wa nje akafahamu kuhusu uwepo wa karatasi muhimu kama hizi na mahala ziliko.Nina wasi wasi sana na Dr Joshua mwenyewe au wasaidizi wake.” Akasema jaji Elibariki

“ Hapana .Sina hakika kama Dr Joshua anaweza akahusika katika jambo hili.Yule ni mtu mkubwa na hawezi kufanya jambo kubwa na la hatari na watu wadogo kama akina Edson.Nina wasi wasi na wasaidizi wake.Lakini tusiseme chochote kwa sasa hadi hapo tutakapofanya uchunguzi wa kina wa jambo hili.Nadhani sehemu nzuri ya kuanzia uchunguzi wetu ni kwa wale wazee wawili waliokuwa katika mtandao mmoja na Edson.Mzee Kitwana na mzee Matiku” Akasema Mathew

“ Lakini Mathew wazee hawa,Kitwana na Matiku wamekwisha fariki kitambo,unadhani tutafanikiwa kupata taarifa zozote za kuweza kutusaidia kupata ufumbuzi wa jambo hili kutoka kwao? Wazo langu mimi ni kwamba ,kwa kuwa tayari tunamfahamu mtu ambaye alikuwa akihitaji kuzinunua karatasi hizo ni kwa nini basi tusimfanyie uchunguzi yeye na kufahamu kwanza alikuwa akiwasiliana na akina nani hapa nchini na pia tunaweza kujua alikuwa na lengo gani na zile karatasi? Akasema Anitha

“ Anitha wazo lako ni zuri sana na hapo kabla nilijadiliana na Elibariki kuhusiana na kumfanyia uchunguzi wa kina huyu mtu anayetajwa kuzitaka karatasi hizo.Tutalifanya hilo lakini kabla ya kulifanya hilo nadhani ingekuwa vizuri kama tungewafanyia uchunguzi hawa wazee wawili tukizipitia taarifa zao za mawasiliano ya mwisho ili tuweze kuwafahamu watu ambao walikuwa wakiwasiliana nao mara kwa mara na katika hao tunaweza tukampata kinara wao.Katika hili Eva atatusaidia sana.Kama nilivyowahi kuwaambia kwamba Eva anafanya kazi katika idara ya usalama wa taifa kwa hiyo ana taarifa nyingi sana na katika hili hatashindwa kutusaidia.” Akasema Mathew

“ Are you sure she will help us? Nakumbuka mara ya mwisho alipoondoka hapa alikuwa na hasira mno na baada ya Yule msichana Sabina kufariki sina hakika kama bado atakuwa tayari kutusaidia” akasema Anitha
“ Believe me Anitha,she will help us” akasema Mathew

“ Nitakwenda kuonana naye sasa hivi.Wewe utabaki hapa ukisubiri taarifa toka kwa Peniela.Sintakawia sana.Endapo kuna jambo lolote kubwa litajitokeza utanitaarifu” akasema Mathew na kuingia chumbani kwake akajiandaa na kuondoka kuelekea kwa Eva.


TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
PENIELA SEASON 3

EPISODE 4

MTUNZI : PATRICK.CK

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA


“ Anitha wazo lako ni zuri sana na hapo kabla nilijadiliana na Elibariki kuhusiana na kumfanyia uchunguzi wa kina huyu mtu anayetajwa kuzitaka karatasi hizo.Tutalifanya hilo lakini kabla ya kulifanya hilo nadhani ingekuwa vizuri kama tungewafanyia uchunguzi hawa wazee wawili tukizipitia taarifa zao za mawasiliano ya mwisho ili tuweze kuwafahamu watu ambao walikuwa wakiwasiliana nao mara kwa mara na katika hao tunaweza tukampata kinara wao.Katika hili Eva atatusaidia sana.Kama nilivyowahi kuwaambia kwamba Eva anafanya kazi katika idara ya usalama wa taifa kwa hiyo ana taarifa nyingi sana na katika hili hatashindwa kutusaidia.” Akasema Mathew

“ Are you sure she will help us? Nakumbuka mara ya mwisho alipoondoka hapa alikuwa na hasira mno na baada ya Yule msichana Sabina kufariki sina hakika kama bado atakuwa tayari kutusaidia” akasema Anitha
“ Believe me Anitha,she will help us” akasema Mathew
“ Nitakwenda kuonana naye sasa hivi.Wewe utabaki hapa ukisubiri taarifa toka kwa Peniela.Sintakawia sana.Endapo kuna jambo lolote kubwa litajitokeza utanitaarifu” akasema Mathew na kuingia chumbani kwake akajiandaa na kuondoka kuelekea kwa Eva.


ENDELEA……………………

Tayari kiza kimekwisha anza kutanda angani wakati Mathew alipowasili katika baa inayomilikiwa na mwanadada Eva.Alishuka garini na kuingia ndani ya baa hii maarufu sana mahala ambako vigogo wengi wa serikali na matajiri hupendelea kwenda kupumzika na kupata vinywaji.Wakati akielekea katika ofisi ya Eva iliyoko juu kabisa mwa baa hii maarufu ,mara akamuona Eva akiwa amekaa katika meza moja na baadhi ya wazee Fulani walioonekana kuwa na nyadhifa kubwa kubwa.

“ Kama kawaida yake huwa haachi kukaa na vigogo na wengi huvutiwa na uzuri na uchangamfu wake.Hii ni njia inayomsaidia sana Eva kuweza kupata kila aina ya taarifa anayoitaka” akawaza Mathew halafu akaelekea kaunta akaagiza kinywaji halafu akamuita muhudumu mmoja wa kiume aliyekuwa amevalia nadhifu ,suti nyeusi na tai nyekundu akamuelekeza aende akamuite Eva na baada ya dakika mbili Eva akatokea.Akastuka sana alipokutanisha macho na Mathew aliyekuwa akitabasamu kwa m bali.Eva akageuka na kuanza kupiga hatua akiondoka , Mathew akamfuata
“ Samahani Eva kwa kukuvamia mida hii.I need to talk to you” akasema Mathew .Eva akamtazama kwa hasira halafu akageuka na kutembea kwa kasi kuelekea ofisini kwake .Mathew akamfuata .Walipoingia katika ofisi ya Eva ,akamtazama Mathew kwa macho makali na kusema

“ Sikutegemea kabisa kama unaweza ukaleta sura yako hapa.Mathew you are a monster” akasema Eva kwa ukali
“ Calm down Eva..!!” akasema Mathew na kuzidi kumpandisha Eva hasira

“ Calm down? Do you think its easy? No ! Mathew I wont calm down.What you did to that girl is unforgivable.You killed her.You are a monster” akasema Eva huku midomo yake ikimtetemeka kwa hasira
“ Eva please listen to me.!!” Akasema Mathew kwa sauti ya upole
“ No Mathew.I don’t want to hear anything from you.Please get out of my office now !!..akasema Eva kwa ukali
“ Eva please..I need your help” akasema Mathew
“ I’m not going to help you ever again.You are a monster” akasema Eva.
“ Stop calling me a monster.!! Akasema Mathew kwa ukali kidogo

“ Iwe mwanzo na mwisho kunilaumu kwa kifo cha msichana Yule.Sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya vile nilivyofanya .Eva wewe unafahamu namna kazi zetu zilivyo.Kuna nyakati tunalazimika kufanya maamuzi magumu sana ili kupata kitu muhimu tunachokitafuta.Kwa hiyo tusiendelee kulaumiana kwa kilichotokea.Sabina alikuwa na taarifa muhimu sana ambazo ilikuwa lazima tuzipate na kwa taarifa zile tulizozipata toka kwake tumeokoa maisha ya mamilioni ya watu waliokuwa hatarini.Kwa hiyo Eva nakuomba sana usahau yale yote yaliyopita na unisaidie.Nahitaji sana msaada wako.Siku zote umekuwa ni kimbilio langu kila pale ninapokuwa na tatizo.Please Eva..” akaomba Mathew.Eva akamtazama Mathew kwa macho yake makali halafu akakaa mezani na kushusha pumzi
“ What do you need? Akauliza Eva.Mathew akavuta kiti akaketi na kumweleza kitu anachohitaji Eva amsaidie.Eva akainama akafikiri na kusema

“ Ok nitakusaidia japokuwa uliniumiza sana kwa kitendo ulichomfanyia Sabina”

“ Ahsante sana Eva” akasema Mathew halafu ukimya mfupi ukatanda

“ Nina mahusiano ya karibu na wakuu wa polisi kwa hiyo haitakuwa kazi ngumu kupata taarifa hizo unazozitaka.Mpaka kesho asubuhi nina uhakika nitakuwa nimepata kitu na nitakufahamisha” akasema Eva.
“ Eva nakushukuru sana sana kwa kukubali kunisaidia.This is very important to me” akasema Mathew na kumfanya Eva atabasamu
“ Mathew sijui unatumia dawa gani kwa sababu dakika kumi zilizopita ulikuwa ni mtu ambaye ninakuchukua kuliko wote lakini baada ya kukupa nafasi nimejikuta nikisahau yote yaliyotokea na nimekubali tena kukusaidia.Anyway tusahau yaliyopita na tuangalie yajayo.By the way unaendeleaje na chunguzi zako? Akauliza Eva.
“Eva nakushukuru sana kwa kusahau yaliyotokea na kukubali kunisaidia tena.Kuhusu chunguzi zangu zinaendelea vizuri” akasema Mathew.Eva akamtazama kidogo halafu akasema

“ Mathew unachunguza jambo gani? Can you tell me? Akauliza Eva
“ Ni mapema sana kukueleza chochote kwa sasa lakini its something very important and dangerous” akasema Mathew.Wakatazamana kwa sekunde kadhaa kisha Mathew akasema
“ Eva naona nisiendelee kuchukua muda wako mwingi nitawasiliana nawe kesho asubuhi ili kupata taarifa za kile ambacho utakuwa umekipata”

“ Ok Mathew nitajitahidi” akasema Eva.Mathew akaufungua mlango na kutoka akamuacha Eva bado amekaa juu ya meza akitafakari.





******


Anitha akiwa ofisini nyumbani kwa Mathew akiendelea na kazi zake,mara simu iliyokuwa mezani ikaita akaipokea

“ Hallow !..akasema Anitha

“ Hallow habari yako” ikajibu sauti ya mwanadada upande wa pili
“ Habari yangu nzuri.Naongea na nani? Akauliza Anitha

“ Naitwa Anna mtoto wa rais wa Tanzania ,napiga simu kutokea afrika ya kusini”

“ Ouh Anna.Nafurahi kukufahamu.Nikusaidie nini?
“ Nahitaji kuongea na jaji Elibariki.Aliwahi kuwasiliana na dada yangu Flaviana ambaye ni mke wake kupitia namba hii na ndiyo maana nimepiga ili niongee naye.Kama yuko karibu tafadhali naomba unipe niongee naye.It’s very important” akasema Anna

“ Ok Anna,naomba usubiri kidogo.” Akasema Anitha na kutoka mle ofisini akaelekea sebuleni alikokuwako jaji Elibariki
“ Jaji Elibariki samahani kwa kukusumbua kuna dada mmoja amepiga simu akitokea afrika ya kusini anaitwa Anna amejitambulisha kama mtoto wa rais”
Jaji Elibariki akastuka sana baada ya kusikia taarifa ile
“ Anna !!. amepataje namba za Mathew? Amejuaje kama niko hapa?

“ Relax jaji .Kumbuka ulitumia simu ile kumpigia mkeo Flaviana” akasema Anitha
“ Sawa nimekumbuka.Anasemaje Anna? Anataka nini?

“ Hajanieleza anataka nini ila bado yuko kwenye laini ya simu anakusubiri.Go talk to her” akasema Anitha.Jaji Elibariki akainuka na kwa kasi akaelekea katika ofisi ya Mathew akachukua simu

“ Hallow Anna“ akasema
“ Hallow Elibariki” akasema Anna.Jaji Elibariki akashusha pumzi na kusema
“ Anna how are you?

“ I’m ok Eli.How are you?
“ I’m fine too” akajibu Elibariki halafu kikapita kimya kifupi
“ uhhm Elibariki nafahamu utakuwa umestuka sana kwa mimi kukupigia simu mida hii hasa kutokana na kutokuwa na maelewano mazuri baina yetu kwa kipindi kirefu...” akasema Anna .
“ Ni kweli Anna nimestuka kidogo kwani ni kitu ambacho sikuwahi kukitegemea.Ok !Tusahau yaliyopita.Niambie hali ya Flaviana anaendeleaje?

“ To be honest She’s not good.Tumemuhamishia huku afrika ya kusini kwa matibabu zaidi lakini bado hali yake si nzuri.Madaktari wanajitahidi kila wawezavyo kuhakikisha anakuwa salama.We need to pray for her” akasema Anna.Zikapita sekunde kadhaa za ukimya

“ Dah ! masikini Flaviana” akasema jaji Elibariki kwa sauti ndogo na kukawa kimya tena.Baada ya sekunde kadhaa za ukimya Elibariki akasema
“ Anna nakushukuru sana kwa kunipa taarifa za maendeleo ya Flaviana .Kwa hivi sasa mimi niko mafichoni na sielewi chochote kinachoendelea huko nje kwani siwezi kutoka ninasakwa kila kona.” akasema jaji Elibariki

“ Elibariki ninalifahamu hilo na ndiyo maana nimekupigia ili kukupa taarifa za mkeo.Pamoja na hayo kuna jambo ambalo nataka tuongee.Ni kuhusiana na kilichotokea usiku ule ulipokwenda kuonana na Flaviana .Kuna mambo ambayo nataka kuyafahamu kutokak wako.What real happened that night? Who shot Flaviana? Nimejiuliza maswali mengi sana kuhusiana na suala hili na kile kinachosemwa lakini inaniwia ugumu kukubaliana na kile ambacho kinasemwa na upande mmoja na nikaona ni bora endapo nitasikia na kwako ili niweze kuufahamu ukweli halisi.Elibariki siku si nyingi nimempoteza mama yangu katika mazingira ya kutatanisha.Nimebakiwa na dada yangu ambaye nampenda sana lakini kwa sasa naye anapigania maisha yake.Please Elibariki tell me the truth what real happened that night? Akasema Anna.Jaji Elibariki akavuta pumzi ndefu kisha akasema
“ Do you believe on what they say? Do you believe I shot my wife?
Anna akavuta pumzi ndefu ndefu na kusema
“ Nafahamu wewe na Flaviana ndoa yenu ilitawaliwa na migogoro mingi na ya mara kwa mara isiyokwisha lakini pamoja na hayo ,toka ndani kabisa ya moyo wangu ninaamini kwamba wewe si muuaji na hukufanya kitendo kile.lakini ni nani basi aliyefanya kitendo kile cha kikatili?”

“ Ahsante sana Anna kwa kulitambua hilo.Ahsante kwa kutoamini kile kinachosemwa juu yangu.Nitakueleza ukweli” akasema Elibariki na kukaa kimya kidogo halafu akasema
“ Anna kuna jambo zito linaloendelea hivi sasa na ili uweze kupata picha halisi nitaanzia alipofariki Dr Flora” akasema Elibariki

“ Mazingira ya kifo cha Dr Flora yalimpa shaka sana Flaviana na hasa baada ya kutolewa amri ya kutoufanyia uchunguzi mwili wa Dr Flora ili kubaini sababu ya kifo chake.Flaviana alikuwa mtu wa kwanza kutilia shaka jambo lile na kwa hiyo akaniita na kuniomba nimsaidie kufanya uchunguzi wa siri kubaini ukweli wa kilichosababisha kifo cha Dr Flora.Kwa mapenzi makubwa niliyonayo kwa mke wangu nilikubali kufanya kazi ile ya hatari kubwa.Ninafahamiana na watu wengi kwa hiyo walinisaidia na tukafanikiwa kuufahamu ukweli.Anna I swear in heaven and earth taarifa ile niliyoileta ilikuwa ya kweli kabisa na uchunguzi ulifanywa na madaktari bingwa wawili.Katika harakati za kuutafuta ukweli tulimpoteza daktari mkuu wa hospitali ile ya jeshi.Anna ninakueleza haya yote ili uweze kupata picha halisi ya nini kilitokea na kinaendelea.” Jaji Elibariki akanyamaza kidogo na kumeza mate kisha akaendelea
“ Anna nafahamu bado itakuwa vigumu sana kwako kuamini lakini ukweli ni kwamba Dr Flora aliuawa ,tena na watu toka ndani ya ikulu.Amri ya kutoufanyia uchunguzi mwili wa Dr Flora ilitolewa na Dr Kigomba ambaye ni mtu wa karibu sana na rais. Hebu jiulize kulikuwa na sababu gani ya kutoufanyia uchunguzi mwili wa mke wa rais ili kujiridhisha na kilichosababisha kifo chake? Halafu jiulize tena Dr Kigomba ambaye ni katibu wa rais alipata wapi nguvu ya kuweza kuzuia madaktari wasiufanyie uchunguzi mwili wa Dr Flora? Kwa picha ya haraka haraka unaweza kuona kwamba kuna jambo lililokuwa linafichwa.Kitu cha kushangaza zaidi ni kwamba Dr Joshua aliitupilia mbali taarifa yangu ile ya uchunguzi na kuiita ni ya kihuni na badala yake ikatolewa taarifa nyingine ikidaiwa ni ya uchunguzi uliofanywa na madaktari bingwa na mkaaminishwa kwamba ndiyo matokeo ya kweli ya uchunguzi wa kile kilichomuua Dr Flora.Kama unakumbuka baada ya kikao kile nilikasirika na kuondoka zangu.Baadae Flaviana akanipigia simu na kuniomba nirejee pale nyumbani kuna jambo anataka tuongee.Nilirejea nyumbani kuonana naye na suala alilotaka kunieleza ni kuachana na masuala yale ya kuhusu ripoti ya kifo cha Dr Flora.Alitambua kwamba nilikuwa nimekasirishwa sana na kitendo cha baba yake kuidharau taarifa yangu na kuiita ya kihuni.Alinitaka niachane na mambo hayo na maisha yaendelee kwani Dr Flora amekwisha fariki na hatarejea tena.Mimi kama jaji na ambaye siku zote kazi yangu ni kuhakikisha haki inatendeka sikukubaliana naye na hivyo tukashindwa kuelewana nikaondoka zangu.Nikiwa barabarani usiku ule baada ya kuachana na Flaviana ndipo likatokea shambulio lile ambao nilinusurika kwa namna ya ajabu kabisa” akasema jaji Elibariki akanyamaza kidogo halafu akaendelea.
“ Nikiwa mafichoni kwa kuogopa kuuawa niliwasiliana na Flaviana na kumjulisha kwamba niko salama na vile vile nilimuomba afanye kila awezalo ili aipate ripoti ile ya madaktari na aniletee.Nilimuelekeza sehemu ya kukutana na mara tu alipofika likatokea shambulio la kustukiza ambalo lilifanywa na watu ambao siwafahamu na Flaviana akajeruhiwa .Inaonekana kuna watu waliokuwa wakimfuatilia nyuma na walifahamu kabisa kwamba anakuja kuonana nami.Mlengwa katika shambulio lile nilikuwa mimi na si Flaviana ila alijeruhiwa wakati wa jitihada za kumkinga asishambuliwe .Pamoja na Flaviana kujeruhiwa lakini nilifanikiwa kuipata taarifa ya uchunguzi aliyokuwa ananiletea.Baada ya kuifanyia kazi tumegundua kwamba taarifa ile haikuwa ya kweli.Madkatari bingwa walioorodheshwa katika ripoti ile kwamba ndio walioufanyia uchunguzi mwili wa Dr Flora hawapo katika orodha ya madaktari bingwa kutoka hospitali kuu ya taifa na hata katika orodha ya madaktari wa hapa nchini.Kwa maana hiyo taarifa ile ambayo Dr Joshua aliwaaminisha kwamba ndiyo sahihi haikuwa ya kweli hata kidogo.Hapo unapata tena picha nyingine kwamba bado nguvu kubwa inaendelea kutumika kuhakikisha kwamba chanzo cha kifo cha Dr Flora hakijulikani.Ukweli halisi ni kwamba Dr Flora aliuawa kama nilivyowaeleza.Kwa sasa mimi na watu wangu tunaendelea kuchunguza nini sababu ya kifo chake kwa hiyo Anna huo ndio ukweli wote wa nini kilitokea. I didn’t shoot my wife” akasema jaji Elibariki.Ukimya ukatanda.Kila mmoja akasikika akivuta pumzi ndefu .Baada ya sekunde kadhaa Anna akasema

“ Elibariki nashukuru sana kwa maelezo yako and I believe you.Ahsante sana kwa kunithibitishia kwamba hisia zangu zilikuwa sahihi.Kifo cha mama hata mimi kilinipa mashaka sana namna kilivyotokea.Pole sana kwa masahibu yote yaliyokukuta.Nina hakika waliomuua mama ndio hao wanaokuwinda wakuue kwa sababu tayari unaufahamu ukweli.I wish tungekuamini toka mwanzo……” akasema anna na kudondosha machozi

“ Anna najua unaumia sana lakini huu si wakati wa kuendelea kudondosha machozi.Huu ni wakati wa kusimama imara na kupambana na wale wote walioamua Dr Flora na kumjeruhi Flaviana dada yako.Bado hatujachelewa bado nafasi tunayo.” Akasema Elibariki na kukawa kimya tena.Baada ya sekunde kadhaa Anna akasema
“ Elibariki I want to ask you one thing and please be honest with me.Tell me the truth even if its going to hurt me badly” akasema Anna

“ What do you want to know Anna?
“ Baba yangu anahusika katika jambo hili? Tafadhali niambie ukweli Elibariki”
Jaji Elibariki akabaki kimya kwa muda akitafakari
“ Elibariki are you there?

“ I’m here Anna” akajibu
“ Anna kwa kuwa umeomba nikueleze ukweli hata kama utakuumiza basi nitakueleza.Katika uchunguzi tulioufanya tumegundua kwamba baba yako anafahamu kinachoendelea kwani amekuwa sehemu ya kuhakikisha kwamba ukweli haujulikani.Ninasema bila kuogopa kwamba baba yako kuna kitu anakifahamu kuhusiana na kifo cha Dr Flora ingawa bado hatuna ushahidi wa moja kwa moja wa kumuhusisha na jambo hili lakini nakuhakikishia kwamba tutaupata” akasema Elibariki
Huku akisikika kulia kwa kwikwi Anna akasema

“ Ahsante sana Elibariki kwa kunieleza ukweli.Kwa asilimia kubwa nakubaliana na hicho ulichokisema.Hata mimi na Flaviana tumewahi kujiuliza sana kuhusu hilo na kwa sasa nimefahamu ukweli.Elibariki naomba kama kuna chochote ambacho ninaweza kukifanya ili kufanikisha kupatikana kwa ushahidi wa kumuhusisha baba na jambo hili usisite kuniambia.Niko tayari kutoa kila aina ya ushirikiano katika jambo hili”.akasema Anna
“ Anna hili si jambo rahisi hata kidogo.Ni jambo zito na la hatari.Naomba nikuweke wazi huyu ni mkuu wa nchi na kuupata ushahidi wa kuweza kumtia hatiani si kitu rahisi kukifanya.Zaidi ya yote huyu ni baba yako mzazi kwa hiyo ukiingia katika jambo hili kwanza wewe mwenyewe utajiweka katika hatari kubwa na pili damu ni nzito kuliko maji.Utaumia sana pale utakapoona baba yako mzazi akipandishwa mahakamani lakini kama umeamua kwa moyo mmoja kuitafuta haki basi ninashukuru sana.Nakuhakikishia mimi na wenzangu tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba tunapata kila aina ya ushahidi.Kuna mambo mengine mengi ambayo ningeweza kukueleza lakini sintoweza kukueleza simuni.Kama ikitokea bahati nikaonana nawe nitakueleza mambo mengi” akasema jaji Elibariki

“ Elibariki hakuna anayeweza kujua namna nilivyoumizwa kwa kifo cha mama.Pili kila ninapomuona Flaviana akipigania uhai wake ninapatwa na hasira sana na niko tayari kwa lolote lile katika kuhakikisha kwamba yeyote aliyehusika katika kusababisha kifo cha mama au katika kumshambulia dada yangu Flaviana anakamatwa.Hata kama ni baba yangu kama anahusika , niko tayari kushirikiana nanyi kuhakikisha anakamatwa na kufikishwa mbele ya haki.Kwa hili sintakuwa na huruma hata kidogo” akasema Anna

“ Ahsante sana Anna.Ahsante sana kwa kunielewa na ahsante kwa kuniahidi ushirikiano mkubwa.Naomba nikukumbushe kwamba haya ni mapambano na tunaopambana nao ni watu wenye uwezo na nguvu kwa hiyo naomba asifahamu mtu yeyote Yule kama mimi na wewe tuna mawasiliano.Kuwasiliana nami kwa sasa ni jambo la hatari kubwa kwako.Kingine ninachokiomba naomba uwe ukinipa taarifa za maendeleo ya Flaviana kwa kutumia namba hii ya simu uliyotumia leo.Nakukumbuisha tena uwe makini sana unapowasiliana name,asifahamu mtu mwingine yeyote na hata siku moja usije ukatumia simu yako ya mkononi kwani nina wasi wasi simu zenu zitakuwa zinafuatiliwa ”

“ Usijali Eli.Kuanzia sasa nitakuwa makini sana na nitachukua tahadhari kubwa kwa kila nitakachokifanya” akasema Anna halafu akasita kidogo na kusema

“ Elibariki I’m sorry for everything I did or say to you in the past.I’m real very sorry.Eli I have to go now naona kuna muuguzi ananiita.Nitakutafuta tena kesho” akasema Anna na kukata simu


TUKUTANE SEHEMU IJAYO……
 
PENIELA SEASON 3


EPISODE 5

MTUNZI 😛ATRICK.CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Ahsante sana Anna.Ahsante sana kwa kunielewa na ahsante kwa kuniahidi ushirikiano mkubwa.Naomba nikukumbushe kwamba haya ni mapambano na tunaopambana nao ni watu wenye uwezo na nguvu kwa hiyo naomba asifahamu mtu yeyote Yule kama mimi na wewe tuna mawasiliano.Kuwasiliana nami kwa sasa ni jambo la hatari kubwa kwako.Kingine ninachokiomba naomba uwe ukinipa taarifa za maendeleo ya Flaviana kwa kutumia namba hii ya simu uliyotumia leo.Nakukumbuisha tena uwe makini sana unapowasiliana name,asifahamu mtu mwingine yeyote na hata siku moja usije ukatumia simu yako ya mkononi kwani nina wasi wasi simu zenu zitakuwa zinafuatiliwa ”

“ Usijali Eli.Kuanzia sasa nitakuwa makini sana na nitachukua tahadhari kubwa kwa kila nitakachokifanya” akasema Anna halafu akasita kidogo na kusema

“ Elibariki I’m sorry for everything I did or say to you in the past.I’m real very sorry.Eli I have to go now naona kuna muuguzi ananiita.Nitakutafuta tena kesho” akasema Anna na kukata simu



ENDELEA…………………………..


Ni mlio wa simu uliomstua Peniela toka usingizini.Alikuwa amelala muda mrefu toka aliporejea kutoka hospitali.Kwa uchovu akajiinua pale kitandani akanyoosha mkono na kuchukua simu.Josh ndiye aliyekuwa akipiga
“ Hallow Josh habari ya huko? Akauliza Peniela

“ Hallow Peniela.Sauti yako inaonyesha ulikuwa umelala.Samahani sana kwa kukusumbua”

“ Bila samahani Josh.Nini kinaendelea hapo? Kuna taarifa zozote madaktari wametoa?
“ Hapana Peniela.Mpaka muda huu hawajasema chochote lakini kuna jambo nataka kukwambia”
“ Jambo gani Josh? Akauliza Peniela.

“Martin amewaeleza wale madaktari kilichotokea na kusababisha hali ya John kubadilika” akasema Josh
“ He told them?
“ Yes he did.Dr Edwin alinifuata na kunieleza kila kitu na kwa sasa wanahitaji kumfahamu Mathew ni nani na ana historia gani na John Mwaulaya.Ameagiza nimpelekee picha za kutoka katika kamera ili aweze kumuona Mathew.Nimeona nisifanye hivyo bila ya kukutaarifu kwanza wewe” akasema Josh
“ You did great Josh.Ninashukuru kwamba hukufanya hivyo alivyotaka Edwin and please don’t do it” akasema Peniela

“ Peniela who is this guy Mathew? Akauliza Josh

“ Josh you don’t need to know him for now.Unachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kwamba Dr Edwin hazipati hizo picha.Nenda nyumbani sasa hivi na ufute kumbukumbu zote.Hatakiwi kabisa kumfahamu Mathew.Umenielewa Josh?
“ Nimekuelewa Peniela.Ninakwenda kufanya hivyo sasa hivi” akajibu Josh na kukata simu
Peniela aliendelea kukaa kitandani akiwa na mawazo mengi
“ Watu wale hawatakiwi kabisa kumfahamu Mathew kwani wakimjua kiundani inaweza kuwa mbaya kwa usalama wake na hivyo kupelekea hata mipango yetu isiende vizuri.I wont let that happen.Nimedhamiria kuifuta team SC41 na lazima nifanye hivyo” akawaza Peniela
“ Ouh ! Kumbe leo nina miadi na Dr Kigomba.Ngoja nijiandae kwani mida tuliyokubaliana inakaribia”
Peniela akainuka na kuanza kujiandaa kwa ajili ya kukutana na Dr Kigomba jioni hiyo
Hadi inagonga saa mbili kamili za usiku ,tayari Peniela alikwishamaliza maandalizi tayari kwa kukutana na Dr Kigomba

“ Now I’m ready.Ngoja nimsubiri huyu kibwengo ambaye naye kama walivyo wengine amechanganyikiwa na mimi” akawaza Peniela akiwa ameketi sofani.Usiku huu alikuwa amevaa gauni refu jeupe lenye kuonyesha dhahiri kila kitu cha ndani
“ kwa nini Dr Edwin anataka kumfahamu Mathew? Kuna kitu gani amekihis…” Peniela akastuliwa mawazoni na mlio wa kengele ya getini iliyoashiria kuna mtu
“ Nadhani atakuwa ni Dr Kigomba kwani sina miadi na mtu mwingine jioni hii” akawaza Peniela na kuinuka akatoka akaelekea getini akalifungua na kukutana na Dr Kigomba,Peniela akamfuata akamkumbatia na kumwagia mabusu mfululizo

“ Nilikuwa na wasi wasi sana pengine huwezi kuja akasema Peniela akiwa amemshika mkono Dr Kigomba akimuongoza kuingia ndani
“ Siwezi kusahau miadi hii ya muhimu.Hata kama baba yangu angefariki leo hii nisingeshindwa kuja kwako.” Akasema Dr Kigomba huku akimtazama Peniela kwa makini
“ What ! Mbona unanitazama namna hiyo? Akauliza Peniela
“ Peniela you are beautiful.Uzuri wako sijui niufananishe na nini.Ninapokuona ninakuona ni kama malaika uliyeshushwa toka juu.You are amazing.Ninakosa neno zuri la kukusifia Peniela” akasema Dr Kigomba na kumfanyia Peniela atoe tabasamu zito akamkumbatia Dr Kigomba na kumpiga mabusu mfululizo.
Dr Kigomba akashindwa kuvumilia na akajikuta maeneo yake nyeti yakichachamaa.Peniela alifanya makusudi kuupeleka mkono wake maeneo nyeti ya Dr Kigomba.Hakutaka kupoteza muda akaendelea kuyachezea na kumfanya Dr Kigomba azidi kuchanganyikiwa zaidi.Peniela akazidisha manjonjo na Dr Kigomba akashindwa kuhimili manjonjo ya Peniela wakajikuta wakijitupa katika zuria na kuanza mambo.Peniela akampeleka Dr Kigomba barabara na kumfanya aweweseke na kuongea maneno kama chizi

“ Leo utaongea mambo yote paka mkubwa we ! akawaza Peniela huku akiendelea kumpagawisha Dr Kigomba
Dakika kumi na tano za mzunguko mmoja zilimfanya Dr Kigomba abaki hoi akihema mfululizo huku jashio jingi likimtirirka

“ Peniela umeichanganya akili yangu mno.Sijawahi kuchanganywa na mwanamke kiasi hiki.Peniel……” akasema Dr igomba huku akihema kwa nguvu.Peniela akamzuia asiendelee kuongea kwa kumuwekea kidole mdomoni

“ Shhhh..!!!
“ Don’t say anything yet.I still have so much suprises for you tonight.Huu ulikuwa ni utangulizi tu” akasema Peniela akamshika mkono Dr Kigomba wakaelekea katika bafu la chumbani kwake na kuingia katika jaccuzi wakaanza kuoga huku wakipata na mvinyo.Baada ya muda Peniela akasema
“ I need some ice” akasema na kumuomba Dr Kigomba amsubiri kwa muda wakati akienda kuchukua vipande vya barafu.Alipotoka bafuni akachukua simu yake na kwa haraka akaelekea sebuleni ambako Dr Kigomba alivua nguo zake na kwa haraka akapekua katika koti la Dr Kigomba na kuipata simu yake.Haraka haraka bila ya kupoteza muda akampigia simu Anitha.Baada ya sekunde kadhaa Anitha akaipokea
“ Hallow Peniela” akasema Anitha baada ya kuipokea simu
“ Anitha tayari ninayo simu ya Dr Kigomba.Tell me what to do? Akasema Peniela
“ Ok Good.Utafuata maelekezo nitakayokupa.Tafadhali jaribu kwenda kwa haraka na kwa umakini mkubwa “ akasema Anitha.
Anitha akaanza kumpa maelekezo ya namna ya kufanya na baada ya kama dakika tatu tayari kila kitu kikakamilika

“ Sasa kila kitu tayari.Good job Peniela.Sasa rudisha kila kitu namna kilivyokuwa ili asiweze kustuka.Kwa sasa tayari tunaweza kuona kila atakachokifanya katika simu yake.Jitahidi pia umvishe na ile saa ili tumalize kila kitu” akasema Anitha

“ Sawa Anitha .Ngoja niwahi ili asije akastuka” akasema Peniela na kukata simu akaelekea jikoni akachukua vipande vya barafu na kurejea tena chumbani
“ Sorry I’m late Dr Kigomba” akasema Peniela na kuingia tena katika jaccuzi
“ welcome back my angel” akasema Dr Kigomba.Peniela akanywa funda moja la mvinyo

“ Peniela wewe ni kiumbe wa kipekee kabisa kuwahi kukutana naye.Toka nilipokutana nawe haujapita hata sekunde moja ambayo sijakuwaza.Ndani ya kipindi kifupi tu umeniingia katika kila mshipa wa mwili wangu.Peniela sijui umeniwekea nini kiasi cha kunichanganya namna hii.I want to be with you forever.I want to……”
Dr Kigomba akaongea maneno mfululizo.Peniela akamkatisha
“ Dr Kigomba bado tuna muda mwingi tutaongea mambo hayo yote lakini kwa usiku wa leo kuna jambo moja tu ambalo tunatakiwa kulifanya” akasema Peniela na kumsogelea Dr Kigomba akaanza kumchezea nyeti zake ambazo zilifura kwa hasira.Peniela hakutaka kupoteza muda akaanzisha tena mtanange mwingine humo humo ndani ya maji
Mambo ambayo Peniela alimfanyia Dr Kigomba yalimpagawisha mno.Alibaki akiweweseka na kuongea maneno yasiyoeleweka.Baada ya kumaliza mzunguko wa pili walitoka ndani ya maji na kukaa kitandani Peniela akaenda jikoni na kuleta nyama za huku na kuweka mezani wakaendelea kula huku wakinywa mvinyo.Chumba kilitawaliwa na vicheko na maongezi ya kimahaba.Mara Dr Kigomba akastuka na kusema

“ Peniela nimesahau simu yangu sebuleni .Naomba nikaichukue kwani nahisi nitakuwa nimetafutwa sana mpaka sasa” akasema Dr Kigomba
“ Relax Kigomba.Ngoja nikakuchukulie” akasema Peniela akatoka hadi sebuleni na kuzichukua nguo za Dr Kigomba na moja kwa moja Dr Kigomba akachukua simu yake .Peniela kiroho kikamdunda baada ya kuona sura ya Dr Kigomba imebadilika ghafla na kukunja ndita

“ Ouh My God ! Amegundua kama simu yake imechezewa? Akajiuliza Peniela
“ Dr Kigomba mbona umestuka ghafla? Is everything ok? Akaulizia Peniela

“ I missed an important call from Mr President.Naomba dakika mbili ni jaribu kumpigia” akasema Dr Kigomba huku akijifunga taulo na kutoka mle chumbani akaelekea sebuleni huku simu yake ikiwa sikioni akimpigia rais.
Wakati Dr Kigomba akimpigia Dr Joshua simu ,nyumbani kwa Mathew kompyuta ya Anitha ilionyesha ishara kwamba Dr Kigomba alikuwa akipiga simu.Tayari simu ya Dr Kigoba ilikwisha unganishwa katika kompyuta ya Anitha kwa hiyo kila kitu atakachokifanya katika simu yake kilionekana katika kompyuta ya Anitha .Haraka haraka akawaita Mathew na jaji Elibariki ambao walifika haraka sana ili kusikia simu nje ya kwanza kupigwa na Dr Kigomba toka walipoiunganisha simu yake.Simu iliita kwa mara ya kwanza bila kupokelewa,akapiga tena safari hii ikapokelewa.
“ Hallow Dr Kigomba” akasema Dr Joshua

“ Halow Mr President .Samahani nilikuwa mbali na simu mbali pale uliponipigia”
“ Dr Kigomba hutakiwi kuacha simu.Wewe ni mtu muhimu sana unatakiwa muda wote uwe na simu.hata kama unakwenda chooni hakikisha unakwenda na simu yako.” Akasema Dr Joshua kwa sauti iliyoonyesha amri Fulani ndani yake
“ Sawa nimekuelewa mzee.” Akajibu Dr Kigomba
“ Bye the way nilikupigia kukutaarifu kwamba muda si mrefu nitaondoka kuelekea afrika ya kusini kufuatilia hali ya Flaviana.Nisipoenda familia yangu haitanielewa kabisa.Hata hivyo sintokaa sana.Kesho jioni nitarejea.Nitakaporejea sitaki kuendelea kupoteza muda nataka tumalize muda nataka tumalize biashara yetu haraka iwezekanavyo kwani tayari kumeanza kujitokeza vizingiti vingi.Kila uchao mambo mapya yamekuwa yakiibuka.Tayari tumekwisha kuwa na maadui yupo huyu Deus Mkozumi na yupo huyu shetani Elibariki.Mzee Deus yeye anafahamu kila kitu kuhusiana na kinachoendelea kwani aliambiwa na Flora na amewahi kunitolea vitisho kwamba nisiendelee na biashara hii.Tayari nimekwisha anza mpango wa kumshughulikia huyu mzee .Nategemea nitakaporejea toka afrika ya kusini nitahakikisha mzee huyu anashughulikiwa ipasavyo na kufumbwa kabisa mdomo wake.Huyu ana sumu kali sana.Kwa upande wako endelea kushughulika na suala la Elibariki.Kama taarifa zile za kwamba Elibariki alikuwa amejificha nyumbani kwa Peniela ni za kweli basi itakuwa rahisi sana kwetu kuweza kumpata kwa hiyo endelea kumchunguza Peniela.Jambo la mwisho nimeongea na Omar amedai kwamba kila kitu kipo tayari na kuanzia kesho wataanza kuingiza fedha katika akaunti.Baada ya zoezi hilo kukamilika tutawapatia mzigo wao .Kigomba gari ziko tayari zinanisubiri kunipeleka uwanja wa ndege tutaongea zaidi nikifika afrika ya kusini “

“ Sawa mheshmiwa rais .Nitayafanyia kazi hayo yote uliyoniagiza.Nakutakia safari njema” akasema Dr Kigomba na kukata simu

“ Dah sasa mambo yameiva.Tayari nimeanza kusikia harufu ya mabilioni ya fedha.Si muda mrefu sana toka sasa nitakuwa bilionea na sintaishi tena katika nchi hii .Nitakwenda kuishi mbali kabisa na hapa nikitumia mabilioni yangu” akawaza Dr Kigomba huku akitabasamu ,mara akakumbuka kitu
“ Peniela anaweza kweli kuwa na mahusiano na jaji Elibariki? Hapana .Taarifa hizo hazikuwa za kweli.Sijaona dalili zozote za kuonyesha Peniela ana mahusiano na jaji Elibariki.Lakini hata kama ningegundua ana mahusiano na Elibariki katu nisingemweleza chochote Dr Joshua .Penzi la kigoli huyu limenikolea na kuniingiza katika kila mshipa wa mwili wangu.Sielewi binti huyu anatumia uchawi au nini hadi akanichanganya kiasi hiki” akawaza Dr Kigomba na kurejea chumbani kwa Peniela
“ Sorry I’m late my queen.Nilikuwa na maongezi kidogo na mheshimiwa rais.Unajua mimi ni mtu wa karibu sana na mheshimiwa rais kwa hiyo kuna maagizo alikuwa ananipa.Usiku huu anaondoka kueleka afrika ya kusini ambako mwanae Flaviana amepelekwa kwa matibabu zaidi” akasema Dr Kigomba
“ Nilisikia kuhusu shambulio alilofanyiwa binti yake vipi anaendeleaje? Akauliza Peniela kana kwamba hafahamu chochote kilichotokea kuhusiana na Flaviana
“ Hali yake bado si nzuri hata kidogo na ndiyo maana akamuhamishia afrika ya kusini kwa matibabu zaidi”
“ Lakini ni nani aliyefanya kitendo hicho cha kikatili? Tayari amekwisha kamatwa? Akauliza Peniela

“ Taarifa za awali zinaonyesha aliyefanya kitendo hicho ni mume wake,jaji Elibariki ambaye ni jaji wa mahakama kuu”

“ Jaji Elibariki?Peniela akashangaa

“ Ndiyo.Do you know him? Akauliza Dr Kigomba
“ Ndiyo namfahamu .Ni jaji ambaye alisikiliza kesi yangu na akanitolea hukumu.NImestuka kwa sababu kwa kumtazama ni mtu mpole sana na huwezi kudhani kwamba anaweza akafanya jambo kama hilo”

“ Peniela dunia ya sasa imebadilika sana.Binadamu wa sasa ni wazuri usoni lakini moyoni ni wakatili kuzidi wanyama pori.Ni vigumu sana kuamini kama Elibariki alidhamiria kumuua mke wake wa ndoa.Kwa hivi sasa anasakwa kila mahali na atapatikana tu muda si mrefu.Anyway tuachane na hayo tusije tukauharibu usiku wetu bure.” Akasema Dr Kigomba na kumsogelea Peniela akambusu

“ I love you Peniela and tonight I have a surprise for you” akasema Dr Kigomba
“ Wow ! I like suprises.I have a surprise for you too.Kwa hiyo nani aanze ? akauliza Peniela huku akitabasamu
“ Ladies first” akasema Dr Kigomba
Peniela akaenda katika kabati lake kubwa la nguo akalifungua na kuta kiboksi kidogo kilichofungwa uzuri na kimetiwa nakshi za kupendeza.Akampatia Dr Kigomba

“ Open it ! akasema Peniela.Taratibu Dr Kigomba akaanza kukifungua kile kibokisi huku akitabasamu na ndani ya kiboksi kile akakutana na kiboksi kingine kidogo.Akakishika na kumtazama Peniela
“ Open it ! akasema Peniela.Dr Kigomba akakifungua na kupatwa na mshangao kwa alichokikuta ndani
“ wow ! akasema Dr Kigomba na kuitoa saa nzuri sana ya dhahabu akaishika mkononi ,akamtazama halafu akamkumbatia Peniela kwa nguvu
“ thank you Peniela.Thank you so much” akasema Dr Kigomba.Peniela akaichukua ile saa ,akaishika mkononi
“ Dr Kigomba from now on you’ll wear this watch.Kila utakapoitazama saa hii itakukumbusha kuhusu mimi.Sitaki unisahau hata sekunde moja.” Akasema Peniela huku akimvalisha Dr Kigomba ile saa mkononi halafu akabonyeza kidude kimoja wapo kati ya vitatu vilivyokuwapo

“ Clock starts now “ akasema Peniela .Dr kigomba ambaye alionekana kuchanganyikiwa kwa penzi alilopewa na Peniela akambusu mfululizo
“ Peniela saa hii uliyonipa hautabanduka mkononi.Nitaivaa kila siku na kila nitakapoivaa itanikumbusha sura ya malaika mwenye uzuri wa kipekee.Ahsante sana Peniela.Ninakupenda sana”
“ nafurahi kusikia hivyo Dr Kigomba.Sasa ni zamu yako.Suprise me” akasema Peniela
Dr Kigomba akamshika mkono na kumtazama usoni kwa makini halafu akasema

“ Kipindi cha pili cha uongozi wa Dr Joshua kinaelekea ukingoni na kwa mujibu wa katiba hatagombea tena .Wengi wa tuliohudumu katika kipindi chake hatutarejea tena katika ulingo wa siasa na mimi nikiwa mmoja wao.Ninataka nipumzike siasa na niishi maisha ya kawaida.Nimepanga baada ya kumaliza utumishi wangu nitaondoka hapa nchini na kwenda kuishi nje ya nchi.Nina nyumba uingereza,Norway,Canada,Marekani n.k.Ninakupa ofa ya kuchagua nchi yoyote ile ambayo ungependa kwenda kuishi na mimi nitakununulia jumba kubwa la kifahari na utaishi kama malkia” akasema Dr Kigomba
“ Wow ! Do you mean it Kigomba? Akauliza Peniela akijifanya kushangaa
“I mean it Peniela.Nakuhakikishia nchi yoyote ile unayotaka kuishi na mimi nitakununulia jumba kubwa la kifahari na nitaishi nawe.”

“ I’m hapy to hear that.What about your family?

“ Foregt about my family.Fo you I can forget everything”

“ Ouh Dr Kigomba unanisisimua sana.This is real a big surprise for me.Before I say anything about this can you give me sometime to think about it?
“ You have all the time in the world Peniela.Think about it” akasema Dr Kigomba
“ Thank you so much Dr Kigomba.I love you” akasema Peniela na kuanza kumporomoshea mabusu mfululizo na mara ikulu kukachachamaa,taratibu Peniela akalivuta taulo alilokuwa amejifunga Dr Kigomba halafu akaupeleka mdomo wake kunako ikulu na kuanza majonjo tena.Dr Kigomba alijikuta akitoa miguno na kuongea maneno yasiyoeleweka

“ Leo nimekupata kenge we.Muda si mrefu utanifahamu mimi ni nani” akawaza Peniela huku akiendelea kumpagawisha Dr Kigomba


TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………………………
 
Dah hivi wanawake kama Peniela wapo bongo....
 
I guess hiyo package inayotafutwa na CS41 ndo itakuwa ni ile formula ya ile virus.
Na tayari vile virusi vimeshatengenezwa ndo Dr. Joshua anataka kuviuza sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…