Peniela (Story ya kijasusi)

Peniela (Story ya kijasusi)

PENIELA SEASON 3


EPISODE 6


MTUNZI : PATRICK .CK

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Wow ! Do you mean it Kigomba? Akauliza Peniela akijifanya kushangaa
“I mean it Peniela.Nakuhakikishia nchi yoyote ile unayotaka kuishi na mimi nitakununulia jumba kubwa la kifahari na nitaishi nawe.”
“ I’m hapy to hear that.What about your family?

“ Foregt about my family.Fo you I can forget everything”

“ Ouh Dr Kigomba unanisisimua sana.This is real a big surprise for me.Before I say anything about this can you give me sometime to think about it?

“ You have all the time in the world Peniela.Think about it” akasema Dr Kigomba
“ Thank you so much Dr Kigomba.I love you” akasema Peniela na kuanza kumporomoshea mabusu mfululizo na mara ikulu kukachachamaa,taratibu Peniela akalivuta taulo alilokuwa amejifunga Dr Kigomba halafu akaupeleka mdomo wake kunako ikulu na kuanza majonjo tena.Dr Kigomba alijikuta akitoa miguno na kuongea maneno yasiyoeleweka

“ Leo nimekupata kenge we.Muda si mrefu utanifahamu mimi ni nani” akawaza Peniela huku akiendelea kumpagawisha Dr Kigomba


ENDELEA……………………..



KIla kitu walichokiongea Dr Kigomba na Dr Joshua kilisikika wazi wazi kupitia kompyuta ya Anitha iliyokuwa tayari imeunganishwa na simu ya Dr Kigomba
“ That’s why I call you a devil Anitha.Kitu ulichokifanya ni cha kipekee kabisa.Ahsante sana Anitha ,bila ya wewe haya yote yasingewezekana.” Akasema Mathew kwa furaha baada ya Dr Kigomba na Dr Joshua kumaliza maongezi na kukata simu.Jaji Elibariki naye alishindwa kujizuia akajikuta akimkumbatia Anitha

“ Hongera sana Anitha.Kitu ulichokifanya kimenishangaza .Teknolojia imekua sana siku hizi.Nilikuwa ninasikia kuhusiana na teknolojia kama hii lakini leo hii nimeshuhudia kwa macho yangu.Hongera sana” akasema
“ Ahsanteni sana ila sifa za pekee anastahili Peniela kwani bila ya yeye hakuna ambacho kingefanikiwa.Yeye ndiye aliyefanya haya yote yakawezekana .Haikuwa kazi rahisi hata kidogo kuipata simu ya Dr Kigomba na kuingiza program hii.Kuanzia sasa chochote kile ambacho atakifanya Dr Kigomba kupitia simu yake lazima tutakiona kwani program hii inaweza kurekodi kila kinachofanyika katika simu ile.Akipiga simu au kupigiwa tutasikia maongezi yote na hata kama tutakuwa mbali maongezi hayo yatarekodiwa na ukija unasikia kila kitu.Programu hii ni mpya sana na kwa mara ya kwanza imefanyiwa majaribio na shirika la ujasusi la marekani C.I.A na imeonyesha mafanikio makubwa na wameweza kuwakamata watu kadhaa waliokuwa wakishukiwa kuhusika na ugaidi.” Akasema Anitha
Wakati Anitha akiendelea kuwaelewesha akina Mathew namna mfumo ule unavyofanya kazi mara kiboksi kikatokea katika kompyuta chenye maandishi kadhaa na Anitha akatabasamu

“ Tayari Peniela amekwisha iwasha ile saa na kuanzia sasa tutafahamu kila mahala atakakokuwapo Dr Kigomba endapo atakuwa ameivaa ile saa. “ akasema Anitha na kuendelea kuwalekeza akina Mathew

“ Sasa tumewapata.Kupitia mfumo huu tutapata kila tunachokihitaji.Dr Joshua na genge lake wanaelekea mwisho wao.” Akasema Mathew

“ Katika maongezi yao,Dr Joshua anaonekana wazi hakutaka kwenda afrika ya kusini lakini anakwenda kwa ajili tu ya kuonekana na kuiridhisha familia yake.Fisadi Yule hajali mtu yeyote Yule hata wanae.Kwake yeye cha muhimu ni pesa tu.” Akasema jaji Elibariki kwa hasira
“ Pole sana jaji,najua umeumia kwa kilichompata mkeo .Tunachoweza kukifanya kwa sasa ni kumuombea Mungu amjalie nafuu ya haraka” akasema Mathew
“ Thanx” akajibu jaji Elibariki

“ Ukifuatilia maongezi ya Dr Joshua na Kigomba kuna watu wawili ambao wametajwa kama watu hatari katika kufanikisha mpango wao.Amekutaja wewe jaji pamoja na mzee Deus mkozumi.Nadhani nyote mnamfahamu huyu mzee ni rais mstaafu na ndiye aliyemuachia kiti Dr Joshua.Mpaka aingie katika orodha ya watu wanoonekana hatari kwa Dr Joshua kuufanikisha mpango wake lazima atakuwa akifahamu kuhusu anachotaka kukifanya Dr Joshua na ndiyo maana kama ukifuatilia vizuri maneno ya Dr Joshua anasema kwamba Deus aliwahi kumpigia simu na kumpa vitisho ili aachane na hicho anachotaka kukifanya .Dr Joshau anadai kwamba tayari amekwisha andaa mpango wa kumshughulikia Deus na mpango huo anategemea ukamilike mara tu atakaporejea kutoka afrika ya kusini.” Akasema Mathew na kunyamaza kidogo kisha akaendelea.

“ Kwa sasa tayari tuna mtu ambaye anaweza akatutegulia kitendawili hiki kuhusiana na hicho kitu anachotaka kukiuza Dr Joshua na washirika wake.Deus Mkozumi anaonekana kufahamu mambo mengi sana kuhusiana na jambo hili na kwa sasa ndiye hasa mtu ambaye tunamuhitaji.Swali ni je tutampata vipi? Akauliza Anitha.
“ Anitha uko sahihi kabisa.Deus Mkozumi ndiye mtu tunayemuhitaji sana kwa sasa lakini kumpata ndiyo suala gumu.Huyu ni rais mstaafu na kumfikia si jambo rahisi.Kuna mtu mmoja tu ambaye anaweza akaifanya kazi hii ya kutukutanisha na Deus.Huyu ni Peniela” akasema Mathew

“ Peniela again?! Akastuka jaji Elibariki

“ Ndiyo jaji.Deus ni mtu muhimu sana kwetu na ili mpango huu ufanikiwe hatuna budi kumpata na tutafanikiwa kumpata kama tutamtumia Peniela.” Akasema Mathew

“ Hapana Mathew.Tutafute njia nyingine lakini si kwa kumtumia tena Peniela.Kwa nini kila mara tunamuweka katika hatari? Hamuoni hatari aliyonayo sasa? Imetosha jamani.Tutafute namna nyingine ya kumpata Deus bila ya kumtumia Peniela” akasema jaji Elibariki
“ Elibariki naomba unielewe tafadhali.Deus ni mtu muhimu sana katika suala hili na ni Peniela pekee anayeweza akatufikisha kwa Deus.Unajua kwa nini Team SC41 wanamtumia katika shughuli kama hizi? Its because she’s is trained for this.She’s good at this.” akasema Mathew .Jaji Elibariki akafikiri kidogo na kusema
“ Ok ! Let us use her”
“ Thank you Eli.Kwa hiyo itabidi tuongee naye kuhusu jambo hili kesho kwa sababu kwa usiku huu yuko na Dr Kigomba na hatuwezi kumkatisha kwani hata Kigomba naye ni mtu muhimu sana kwetu.Siku ya kesho tunatarajia pia kupata taarifa toka kwa Eva kuhusiana na uchunguzi niliomuomba anisaidie kuufanya kuhusu watu waliokuwa wakiwasiliana na wale wazee wawili washirika wa Edson.Lengo ni kutaka kumfahamu mtu ambaye yuko nyuma ya mpango huu wa kuziiba karatasi zile toka ikulu.Tunahitaji sana kumfahamu mtu huyo ni nani .Kwa sasa tupumzikeni ila tujiandae kwa siku ya kesho ambayo itakuwa ni siku ndefu sana.Mambo mengi yatafanyika siku ya kesho.Anitha usisahau kuendelea kumfuatilia Kigomba na kama kuna chochote utakachokipata kinachohitaji kufanyiwa kazi haraka utaniamsha mara moja” akasema Mathew na kila mmoja akaelekea chumbani kwake kupumzika



*******

Saa kubwa ya ukutani ilionyesha ni saa sita na dakika nane za usiku.Peniela alikuwa amekilaza kichwa chake kifuani kwa Dr KIgomba ambaye alikuwa amepitiwa na usingizi mzito.Alikuwa amechoka mno kutokana na mchaka mchaka aliokimbizwa na Peniela
“ Natumai ile progaramu ya Anitha ilifanya kazi.Naomba Mungu atusaidie ili mipango yetu yote iweze kwenda kama tulivyopanga il tuweze kuisambaratisha team SC41 pamoja na kuipata hiyo package.Ndiyo maana sikutaka Josh awaonyeshe wale akina Edwin picha za Mathew kwani nina hakika lengo lao ni kutaka kumfuatilia Mathew na kumfahamu ni nani na jambo hilo linaweza likarudisha nyuma sana mpango huu wa kuimaliza team SC41.Katika jambo hili Mathew ni tegemeo langu kubwa kwa hiyo nitahakikisha ninamlinda dhidi ya hatari zote za tea……” Peniela akastuliwa toka mawazoni na mlio wa simu.Akanyosha mkono akaichukua,mpigaji alikuwa ni Josh

“ Josh anataka nini usiku hu? Akauliza Peniela na kubonyeza kitufe cha kupokelea simu
“ Hallow Josh !
“Peniela,samahani kwa kukusumbua mida hii ,niko hapa hospitali” akasema Josh

“ Nini kinaendelea hapo hospitali Josh? Madaktari wamemaliza uchunguzi wao? Wametoa ripoti gani? akauliza Peniela
“ Tayari wamemaliza uchunguzi wao na wanahitaji kukuona sasa hivi”
“ Hawajakueleza chochote?

“ Hapana hawajanieleza chochote zaidi ya kuniambia kwamba wanahitaji kukuona haraka hapa hospitali.Inavyoonekana kuna jambo la haraka sana wanataka kukueleza” akasema Josh

“ Sawa Josh ninakuja .” akajibu Peniela na kukata simu

“ Ouh Mungu wangu,nini kimetokea? Is john Ok? Is he still alive? Yawezekana amekwisha fariki ila wanaogopa kuniambia.Ngoja niwahi nikajue kinachoendelea” akawaza Peniela na kumuamsha Dr Kigomba aliyekuwa amelala fofofo
“ Dr Kigomba samahani sana nimepata dharura.Nimepigiwa simu sasa hivi natakiwa hospitali.Mjomba wangu amelazwa hospitali na hali yake si nzuri.I need to go there now” akasema Peniela

“ What? .Dr Kigomba akashangaa

“ Mbona hukuniambia kama una mgonjwa hospitali Peniela?
“ Sikuwa na wasi wasi kuhusiana na hali yake kwani tayari alikuwa katika uangalizi mkubwa wa madaktari lakini inaonekana hali yake imebadilika na ndiyo maana ninahitajika nifike mara moja”
“ I’m going with you” akasema Dr Kigomba”

“ Hapana Dr Kigomba.Endelea kupumzika nitarejea muda si mrefu.Samahani sana kwa suala hili kuingilia usiku wetu huu mzuri”

“ Usijali kuhusu hilo Peniela.Una hakika kwamba utaweza kuendesha gari mwenywe hadi hospitali?

“ Ndiyo Dr Kigomba nitaweza.Wewe endelea kupumzika,nitakufahamisha kama kuna tatizo lolote.Nyumba hii ni salama na hakuna tatizo lolote kwa hiyo kuwa na amani ” akasema Peniela
“ Peniela nilikuja hapa kwa ajili yako tu kwa hiyo kwa vile imetokea dharura hii basi na mimi ngoja niende zangu nyumbani kwani siwezi kukaa hapa ndani peke yangu.Ninaomba unijulishe hali ya mgonjwa inavyoendelea pindi ukifika hospitali na kama kuna lolote ninaloweza kulifanya kusaidia tafadhai usisite kunitaarifu.Kingine lifanyie kazi lile suala nililokwambia jana usiku ” akasema Dr Kigomba huku akivaa nguo
Dr Kigmba ndiye aliyekuwa wa kwanza kuondoka zake na dakika tano baadae Peniela akafunga nyumba yake na kuondoka kuelekea hospitali
“ Kwa hali ya John ilivyokuwa nina wasi wasi sana kama atakuwa mzima.Yawezekana amekwisha fariki .Nasikitika sana kwa kukutana na John katika siku za mwisho za uhai wake.Hata hivyo ninawashukuru Mathew na Elibariki kwa kunisaidia nikaufahamu ukweli kuhusu masha yangu toka katika kinywa cha John mwenyewe.” Akawaza Peniela akiwa njiani kuelekea hospitali
Hakukuwa na magari mengi usiku huu kwa hiyo alikuwa anakwenda kwa mwendo mkali sana.
Aliwasili hospitali na mtu wa kwanza kuonana naye alikuwa ni Josh
“ Tell me Josh ,what happened? Is he ok? Akauliza
“ Peniela sifahamu chochote kinachoendelea hapa ,madaktari wametoka katika chumba na kuagiza uitwe haraka.Wako katika ofisi ya daktari mkuu wanakusubiri” akasema Josh

“ Ok Josh.Ngoja kwanza nikaonanane nao .Ulikwenda kuifanya ile kazi niliyokuagiza?

“ Ndiyo Peniela nimekwisha ifanya”
“ Good” akasema Peniela na kutembea kwa kasi kuelekea katika ofisi ya daktari mkuu.Ndani ya chumba kile kulikuwa na madaktari watano
“ Karibu sana Peniela.” akasema Daktari mkuu
“ Ahsante sana.Poleni na kazi”

“ Ahsante sana” wakajibu kwa pamoja .Peniela akavuta kiti akaketi .
“ Nimestushwa sana na mwito wenu wa dharura.Is everything ok? Akauliza Peniela kwa wasi wasi
“ Samahani sana Peniela kwa kukupa mstuko kwa kukutaka ufike hapa haraka.Tumekuita kwa dharura usiku huu ili kukueleza kile kinachoendelea na matokeo ya uchunguzi ambao tumekuwa tukiufanya toka jana jioni. Tumefanya uchunguzi wa kina kwa mgonjwa wako .Imetuchukua muda mrefu kwa sababu tulitaka tulichimbe tatizo lake kwa undani kabisa.Katika uchuguzi wetu tumegundua kwamba ndugu yako anasumbuliwa na tatizo kubwa.Anasumbuliwa na kansa ya ubongo”

“ Ouh my God !!..akasema Peniela kwa mtuko na kuweka mikono kichwani.Daktari akaendelea
“ Hali ya John si nzuri na sisi kama madaktari bingwa tunaomba tuwe wazi kwako kwamba kwa hali ya ugonjwa wake ilipofika hatuna namna yoyote tunayoweza kufanya ili kumsaidia John.Tiba pekee ambayo ingeweza kufanyika na kumsaidia John ni upasuaji lakini mpaka kwa hatua hii tumekwisha chelewa sana.Kwa ufupi ni kwamba hakuna namna tunayoweza kumsaidia John katika kuutibu ugonjwa wake na kwa hali yake ilivyo hatakuwa na muda mrefu sana wa kuishi.”
Kauli ile ikamstua mno Peniela.Alibaki kimya kwa kama dakika mbili hivi halafu akauliza

“ John amebakiwa na muda gani?
“ Ni vigumu kusema ni lini kifo chake kitatokea lakini kuanzia sasa lazima kujiandaa kwa sababu muda wowote lolote linaweza kutokea”
“ I’m so sorry Peniela.Najua unaumia sana lakini huo ndio ukweli na hakuna lugha nyingine ya kuweza kulieleza jambo hili.Hiki ni kipindi kigumu sana kwako na kwa familaia yako lakini ninakuomba uwe jasiri.Sisi hapa hospitali tutaendelea kumpatia huduma zote hadi hapo Mungu atakapomuita” akasema Daktari.Peniela akatazama chini kwa sekunde kadhaa halafu akasema

“ Daktari kwanza kabisa ninawapeni pole sana kwa kazi kubwa na ngumu mliyoifanya.Ninawashukuru vile vile kwa kuwa wakweli.Si jambo rahisi kumweleza mtu kwamba mgonjwa wake atafariki muda si mrefu.Pamoja na hayo naomba nirudie kuwauliza tena kwa mara ya pili.Ni kweli mna hakika hakuna namna yoyote ya kuweza kumtibu John?
“ Peniela sisi sote utuonao humu ni madaktari bingwa na kama kungekuwa na namna yoyote ya kuweza kumtibu ndugu yako tusingekueleza hayo tuliyokueleza.Ni kweli hakuna namna tunayoweza kufanya kumsaidia John akapona.” Akasema Daktari mkuu Peniela akainama chini

“ Peniela kuna suala lingine” akasema daktari mkuu.Peniela akainua kichwa.
“ John is awake na he wants to see you” akasema daktari na uso wa Peniela ukajikuta ukitengeneza tabasamu

“ Thank you Lord ! akasema na kufuta machozi akainuka na kuongozana na madaktari hadi katika chumba alimolazwa .Ni kweli John alikuwa ameamka na alikuwa amelala kitandani huku kitanda chake kikiwa kimezungukwa na mitambo mingi.Peniela machozi yakamtoka
“ Stop crying my queen” akasema John kwa sauti dhaifu sana.Peniela akamsogelea pale kitandani.Madaktari wakatazamana kisha wote wakatoka na kuwaacha Peniela na John pekee mle chumbani
“Stop crying Peniela.” Akasema John.Peniela akafuta machozi na kumshika mkono
“ The’ve told you already? Akauliza John
“ Tell me what?
“ Penny suala hili si la kuficha tena na ninatumai kwamba kabla ya kuja hapa tayari wamekwisha kueleza kila kitu kuhusu mimi”

“ Ndiyo wamenieleza kila kitu” akajibu Peniela huku akiendelea kudondosha machozi
“ Usilie Peniela ,huo ndio ukweli halisi.I don’t have much time to live.I’m going to die very soon” akasema John
“ Please john don’t give up.There is must be a way out”
“ Peniela lazima sote tukubaliane na ukweli kwamba hakuna namna nyingine ya kufanya ili niweze kupona.Madaktari wamekwisha thibitisha hilo kwa hiyo hakuna haja ya kuwa na matumaini yasiyokuwepo.Mimi nimelikubali hilo na ninaomba hata wewe ulikubali hilo.Ninashukuru sana kwa jitihada zako za kuhakikisha kwamba ninapona.Pamoja na hayo kuna mambo ambayo nataka kukwambia “ akanyamaza kwa sekunde kadhaa halafu akaendelea

“ kwanza kabisa nakuomba samahani sana kwa mambo yote niliyokufanyia wewe binafsi.Sioni neno zuri ambalo ninaweza kulitumia kukuomba msamaha.Nilitoa uhai wa wazazi wako na kusababisha ukakua bila ya wazazi.Hili ni jambo ambalo linaniumiza mno.Pili nilikuingiza katika team Sc41 na kuyabadili kabisa maisha yako.Peniela nash……” John akashindwa kuendelea kuongea kwani alionekana kuanza kupumua kwa shida
“ John stop.Usiseme chochote tena” akasema Peniela

“ No Peniela.Kuna mambo ambayo lazima niyaweke sawa kabla ya pumzi zangu kukatika.Nahitaji kumuona Yule kijana aliyekuja jana pale nyumbani kwangu na kunitaka nikueleze historia yako”
“ Mathew?!!! Peniela akashangaa
“ Exactly !!..Mathew.I need to see him now.Find him” akasema John
“ John!..” Peniela akataka kusema kitu lakini John akamzuia
“ Please Peniela take the phone and call him now.Tell him to come immediately.” Akasema John
Peniela hakutaka kubishana na John akatoka nje ya chumba na kuchukua simu akampigia Mathew
Si kawaida ya Mahew kulala fofofo na ndiyo maana simu yake ilipoita akaamka mara moja na kukuta ni Peniela ndiye anayepiga.Akastuka kidogo kwani hakutegemea kabisa kama angeweza kumpigia simu usiku ule.Bila kupoteza muda akaipokea
“ Hallow Peniela” akasema Mathew

“ Mathew samahani sana kwa kukusumbua mida hii.”

“ Bla samahani Peniela.Is everything ok? Are you ok? Akauliza
“ I’m ok Mathew na wala usiwe na hofu kuhusu mimi.Jambo lililonifanya nikupigie simu usiku huu ni kwamba jana ulipoondoka nyumbani kwa John mwaulaya hali yake ilibadilika sana na ikatulazimu kumkimbiza hospitali.Baada ya uchunguzi imegundulika kwamba John ana saratani ya ubongo na kwa mujibu wa madaktari hawezi kupona.Hapa ninapoongea niko hospitali .Mathew the man is dying.Kuna mambo ambayo anataka kunieleza lakini kutokana na hali yake inamuwia ugumu lakini kuna jambo ameliomba na kulisisitiza sana.He wants to see you “
Mathew akastuka
“ Unasema ?!!...
“ Najua umestuka Mathew na hata mimi nilistuka hivyo hivyo aliponieleza lakini amesisitiza kwamba anahitaji kukuona haraka usiku huu.Inaonekana kuna kitu cha muhimu sana anataka kukueleza.Naomba uje hapa hospitali Mathew” akasema Peniela .Mathew akafikri kidogo na kusema
“ Ok Peniela ninakuja sasa hivi”
Bila kupoteza muda akamuamsha Anitha na kumfahamisha kwamba anatoka kwenda hospitali


TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
PENIELA SEASON 3


EPISODE 6


MTUNZI : PATRICK .CK

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Wow ! Do you mean it Kigomba? Akauliza Peniela akijifanya kushangaa
“I mean it Peniela.Nakuhakikishia nchi yoyote ile unayotaka kuishi na mimi nitakununulia jumba kubwa la kifahari na nitaishi nawe.”
“ I’m hapy to hear that.What about your family?

“ Foregt about my family.Fo you I can forget everything”

“ Ouh Dr Kigomba unanisisimua sana.This is real a big surprise for me.Before I say anything about this can you give me sometime to think about it?

“ You have all the time in the world Peniela.Think about it” akasema Dr Kigomba
“ Thank you so much Dr Kigomba.I love you” akasema Peniela na kuanza kumporomoshea mabusu mfululizo na mara ikulu kukachachamaa,taratibu Peniela akalivuta taulo alilokuwa amejifunga Dr Kigomba halafu akaupeleka mdomo wake kunako ikulu na kuanza majonjo tena.Dr Kigomba alijikuta akitoa miguno na kuongea maneno yasiyoeleweka

“ Leo nimekupata kenge we.Muda si mrefu utanifahamu mimi ni nani” akawaza Peniela huku akiendelea kumpagawisha Dr Kigomba


ENDELEA……………………..



KIla kitu walichokiongea Dr Kigomba na Dr Joshua kilisikika wazi wazi kupitia kompyuta ya Anitha iliyokuwa tayari imeunganishwa na simu ya Dr Kigomba
“ That’s why I call you a devil Anitha.Kitu ulichokifanya ni cha kipekee kabisa.Ahsante sana Anitha ,bila ya wewe haya yote yasingewezekana.” Akasema Mathew kwa furaha baada ya Dr Kigomba na Dr Joshua kumaliza maongezi na kukata simu.Jaji Elibariki naye alishindwa kujizuia akajikuta akimkumbatia Anitha

“ Hongera sana Anitha.Kitu ulichokifanya kimenishangaza .Teknolojia imekua sana siku hizi.Nilikuwa ninasikia kuhusiana na teknolojia kama hii lakini leo hii nimeshuhudia kwa macho yangu.Hongera sana” akasema
“ Ahsanteni sana ila sifa za pekee anastahili Peniela kwani bila ya yeye hakuna ambacho kingefanikiwa.Yeye ndiye aliyefanya haya yote yakawezekana .Haikuwa kazi rahisi hata kidogo kuipata simu ya Dr Kigomba na kuingiza program hii.Kuanzia sasa chochote kile ambacho atakifanya Dr Kigomba kupitia simu yake lazima tutakiona kwani program hii inaweza kurekodi kila kinachofanyika katika simu ile.Akipiga simu au kupigiwa tutasikia maongezi yote na hata kama tutakuwa mbali maongezi hayo yatarekodiwa na ukija unasikia kila kitu.Programu hii ni mpya sana na kwa mara ya kwanza imefanyiwa majaribio na shirika la ujasusi la marekani C.I.A na imeonyesha mafanikio makubwa na wameweza kuwakamata watu kadhaa waliokuwa wakishukiwa kuhusika na ugaidi.” Akasema Anitha
Wakati Anitha akiendelea kuwaelewesha akina Mathew namna mfumo ule unavyofanya kazi mara kiboksi kikatokea katika kompyuta chenye maandishi kadhaa na Anitha akatabasamu

“ Tayari Peniela amekwisha iwasha ile saa na kuanzia sasa tutafahamu kila mahala atakakokuwapo Dr Kigomba endapo atakuwa ameivaa ile saa. “ akasema Anitha na kuendelea kuwalekeza akina Mathew

“ Sasa tumewapata.Kupitia mfumo huu tutapata kila tunachokihitaji.Dr Joshua na genge lake wanaelekea mwisho wao.” Akasema Mathew

“ Katika maongezi yao,Dr Joshua anaonekana wazi hakutaka kwenda afrika ya kusini lakini anakwenda kwa ajili tu ya kuonekana na kuiridhisha familia yake.Fisadi Yule hajali mtu yeyote Yule hata wanae.Kwake yeye cha muhimu ni pesa tu.” Akasema jaji Elibariki kwa hasira
“ Pole sana jaji,najua umeumia kwa kilichompata mkeo .Tunachoweza kukifanya kwa sasa ni kumuombea Mungu amjalie nafuu ya haraka” akasema Mathew
“ Thanx” akajibu jaji Elibariki

“ Ukifuatilia maongezi ya Dr Joshua na Kigomba kuna watu wawili ambao wametajwa kama watu hatari katika kufanikisha mpango wao.Amekutaja wewe jaji pamoja na mzee Deus mkozumi.Nadhani nyote mnamfahamu huyu mzee ni rais mstaafu na ndiye aliyemuachia kiti Dr Joshua.Mpaka aingie katika orodha ya watu wanoonekana hatari kwa Dr Joshua kuufanikisha mpango wake lazima atakuwa akifahamu kuhusu anachotaka kukifanya Dr Joshua na ndiyo maana kama ukifuatilia vizuri maneno ya Dr Joshua anasema kwamba Deus aliwahi kumpigia simu na kumpa vitisho ili aachane na hicho anachotaka kukifanya .Dr Joshau anadai kwamba tayari amekwisha andaa mpango wa kumshughulikia Deus na mpango huo anategemea ukamilike mara tu atakaporejea kutoka afrika ya kusini.” Akasema Mathew na kunyamaza kidogo kisha akaendelea.

“ Kwa sasa tayari tuna mtu ambaye anaweza akatutegulia kitendawili hiki kuhusiana na hicho kitu anachotaka kukiuza Dr Joshua na washirika wake.Deus Mkozumi anaonekana kufahamu mambo mengi sana kuhusiana na jambo hili na kwa sasa ndiye hasa mtu ambaye tunamuhitaji.Swali ni je tutampata vipi? Akauliza Anitha.
“ Anitha uko sahihi kabisa.Deus Mkozumi ndiye mtu tunayemuhitaji sana kwa sasa lakini kumpata ndiyo suala gumu.Huyu ni rais mstaafu na kumfikia si jambo rahisi.Kuna mtu mmoja tu ambaye anaweza akaifanya kazi hii ya kutukutanisha na Deus.Huyu ni Peniela” akasema Mathew

“ Peniela again?! Akastuka jaji Elibariki

“ Ndiyo jaji.Deus ni mtu muhimu sana kwetu na ili mpango huu ufanikiwe hatuna budi kumpata na tutafanikiwa kumpata kama tutamtumia Peniela.” Akasema Mathew

“ Hapana Mathew.Tutafute njia nyingine lakini si kwa kumtumia tena Peniela.Kwa nini kila mara tunamuweka katika hatari? Hamuoni hatari aliyonayo sasa? Imetosha jamani.Tutafute namna nyingine ya kumpata Deus bila ya kumtumia Peniela” akasema jaji Elibariki
“ Elibariki naomba unielewe tafadhali.Deus ni mtu muhimu sana katika suala hili na ni Peniela pekee anayeweza akatufikisha kwa Deus.Unajua kwa nini Team SC41 wanamtumia katika shughuli kama hizi? Its because she’s is trained for this.She’s good at this.” akasema Mathew .Jaji Elibariki akafikiri kidogo na kusema
“ Ok ! Let us use her”
“ Thank you Eli.Kwa hiyo itabidi tuongee naye kuhusu jambo hili kesho kwa sababu kwa usiku huu yuko na Dr Kigomba na hatuwezi kumkatisha kwani hata Kigomba naye ni mtu muhimu sana kwetu.Siku ya kesho tunatarajia pia kupata taarifa toka kwa Eva kuhusiana na uchunguzi niliomuomba anisaidie kuufanya kuhusu watu waliokuwa wakiwasiliana na wale wazee wawili washirika wa Edson.Lengo ni kutaka kumfahamu mtu ambaye yuko nyuma ya mpango huu wa kuziiba karatasi zile toka ikulu.Tunahitaji sana kumfahamu mtu huyo ni nani .Kwa sasa tupumzikeni ila tujiandae kwa siku ya kesho ambayo itakuwa ni siku ndefu sana.Mambo mengi yatafanyika siku ya kesho.Anitha usisahau kuendelea kumfuatilia Kigomba na kama kuna chochote utakachokipata kinachohitaji kufanyiwa kazi haraka utaniamsha mara moja” akasema Mathew na kila mmoja akaelekea chumbani kwake kupumzika



*******

Saa kubwa ya ukutani ilionyesha ni saa sita na dakika nane za usiku.Peniela alikuwa amekilaza kichwa chake kifuani kwa Dr KIgomba ambaye alikuwa amepitiwa na usingizi mzito.Alikuwa amechoka mno kutokana na mchaka mchaka aliokimbizwa na Peniela
“ Natumai ile progaramu ya Anitha ilifanya kazi.Naomba Mungu atusaidie ili mipango yetu yote iweze kwenda kama tulivyopanga il tuweze kuisambaratisha team SC41 pamoja na kuipata hiyo package.Ndiyo maana sikutaka Josh awaonyeshe wale akina Edwin picha za Mathew kwani nina hakika lengo lao ni kutaka kumfuatilia Mathew na kumfahamu ni nani na jambo hilo linaweza likarudisha nyuma sana mpango huu wa kuimaliza team SC41.Katika jambo hili Mathew ni tegemeo langu kubwa kwa hiyo nitahakikisha ninamlinda dhidi ya hatari zote za tea……” Peniela akastuliwa toka mawazoni na mlio wa simu.Akanyosha mkono akaichukua,mpigaji alikuwa ni Josh

“ Josh anataka nini usiku hu? Akauliza Peniela na kubonyeza kitufe cha kupokelea simu
“ Hallow Josh !
“Peniela,samahani kwa kukusumbua mida hii ,niko hapa hospitali” akasema Josh

“ Nini kinaendelea hapo hospitali Josh? Madaktari wamemaliza uchunguzi wao? Wametoa ripoti gani? akauliza Peniela
“ Tayari wamemaliza uchunguzi wao na wanahitaji kukuona sasa hivi”
“ Hawajakueleza chochote?

“ Hapana hawajanieleza chochote zaidi ya kuniambia kwamba wanahitaji kukuona haraka hapa hospitali.Inavyoonekana kuna jambo la haraka sana wanataka kukueleza” akasema Josh

“ Sawa Josh ninakuja .” akajibu Peniela na kukata simu

“ Ouh Mungu wangu,nini kimetokea? Is john Ok? Is he still alive? Yawezekana amekwisha fariki ila wanaogopa kuniambia.Ngoja niwahi nikajue kinachoendelea” akawaza Peniela na kumuamsha Dr Kigomba aliyekuwa amelala fofofo
“ Dr Kigomba samahani sana nimepata dharura.Nimepigiwa simu sasa hivi natakiwa hospitali.Mjomba wangu amelazwa hospitali na hali yake si nzuri.I need to go there now” akasema Peniela

“ What? .Dr Kigomba akashangaa

“ Mbona hukuniambia kama una mgonjwa hospitali Peniela?
“ Sikuwa na wasi wasi kuhusiana na hali yake kwani tayari alikuwa katika uangalizi mkubwa wa madaktari lakini inaonekana hali yake imebadilika na ndiyo maana ninahitajika nifike mara moja”
“ I’m going with you” akasema Dr Kigomba”

“ Hapana Dr Kigomba.Endelea kupumzika nitarejea muda si mrefu.Samahani sana kwa suala hili kuingilia usiku wetu huu mzuri”

“ Usijali kuhusu hilo Peniela.Una hakika kwamba utaweza kuendesha gari mwenywe hadi hospitali?

“ Ndiyo Dr Kigomba nitaweza.Wewe endelea kupumzika,nitakufahamisha kama kuna tatizo lolote.Nyumba hii ni salama na hakuna tatizo lolote kwa hiyo kuwa na amani ” akasema Peniela
“ Peniela nilikuja hapa kwa ajili yako tu kwa hiyo kwa vile imetokea dharura hii basi na mimi ngoja niende zangu nyumbani kwani siwezi kukaa hapa ndani peke yangu.Ninaomba unijulishe hali ya mgonjwa inavyoendelea pindi ukifika hospitali na kama kuna lolote ninaloweza kulifanya kusaidia tafadhai usisite kunitaarifu.Kingine lifanyie kazi lile suala nililokwambia jana usiku ” akasema Dr Kigomba huku akivaa nguo
Dr Kigmba ndiye aliyekuwa wa kwanza kuondoka zake na dakika tano baadae Peniela akafunga nyumba yake na kuondoka kuelekea hospitali
“ Kwa hali ya John ilivyokuwa nina wasi wasi sana kama atakuwa mzima.Yawezekana amekwisha fariki .Nasikitika sana kwa kukutana na John katika siku za mwisho za uhai wake.Hata hivyo ninawashukuru Mathew na Elibariki kwa kunisaidia nikaufahamu ukweli kuhusu masha yangu toka katika kinywa cha John mwenyewe.” Akawaza Peniela akiwa njiani kuelekea hospitali
Hakukuwa na magari mengi usiku huu kwa hiyo alikuwa anakwenda kwa mwendo mkali sana.
Aliwasili hospitali na mtu wa kwanza kuonana naye alikuwa ni Josh
“ Tell me Josh ,what happened? Is he ok? Akauliza
“ Peniela sifahamu chochote kinachoendelea hapa ,madaktari wametoka katika chumba na kuagiza uitwe haraka.Wako katika ofisi ya daktari mkuu wanakusubiri” akasema Josh

“ Ok Josh.Ngoja kwanza nikaonanane nao .Ulikwenda kuifanya ile kazi niliyokuagiza?

“ Ndiyo Peniela nimekwisha ifanya”
“ Good” akasema Peniela na kutembea kwa kasi kuelekea katika ofisi ya daktari mkuu.Ndani ya chumba kile kulikuwa na madaktari watano
“ Karibu sana Peniela.” akasema Daktari mkuu
“ Ahsante sana.Poleni na kazi”

“ Ahsante sana” wakajibu kwa pamoja .Peniela akavuta kiti akaketi .
“ Nimestushwa sana na mwito wenu wa dharura.Is everything ok? Akauliza Peniela kwa wasi wasi
“ Samahani sana Peniela kwa kukupa mstuko kwa kukutaka ufike hapa haraka.Tumekuita kwa dharura usiku huu ili kukueleza kile kinachoendelea na matokeo ya uchunguzi ambao tumekuwa tukiufanya toka jana jioni. Tumefanya uchunguzi wa kina kwa mgonjwa wako .Imetuchukua muda mrefu kwa sababu tulitaka tulichimbe tatizo lake kwa undani kabisa.Katika uchuguzi wetu tumegundua kwamba ndugu yako anasumbuliwa na tatizo kubwa.Anasumbuliwa na kansa ya ubongo”

“ Ouh my God !!..akasema Peniela kwa mtuko na kuweka mikono kichwani.Daktari akaendelea
“ Hali ya John si nzuri na sisi kama madaktari bingwa tunaomba tuwe wazi kwako kwamba kwa hali ya ugonjwa wake ilipofika hatuna namna yoyote tunayoweza kufanya ili kumsaidia John.Tiba pekee ambayo ingeweza kufanyika na kumsaidia John ni upasuaji lakini mpaka kwa hatua hii tumekwisha chelewa sana.Kwa ufupi ni kwamba hakuna namna tunayoweza kumsaidia John katika kuutibu ugonjwa wake na kwa hali yake ilivyo hatakuwa na muda mrefu sana wa kuishi.”
Kauli ile ikamstua mno Peniela.Alibaki kimya kwa kama dakika mbili hivi halafu akauliza

“ John amebakiwa na muda gani?
“ Ni vigumu kusema ni lini kifo chake kitatokea lakini kuanzia sasa lazima kujiandaa kwa sababu muda wowote lolote linaweza kutokea”
“ I’m so sorry Peniela.Najua unaumia sana lakini huo ndio ukweli na hakuna lugha nyingine ya kuweza kulieleza jambo hili.Hiki ni kipindi kigumu sana kwako na kwa familaia yako lakini ninakuomba uwe jasiri.Sisi hapa hospitali tutaendelea kumpatia huduma zote hadi hapo Mungu atakapomuita” akasema Daktari.Peniela akatazama chini kwa sekunde kadhaa halafu akasema

“ Daktari kwanza kabisa ninawapeni pole sana kwa kazi kubwa na ngumu mliyoifanya.Ninawashukuru vile vile kwa kuwa wakweli.Si jambo rahisi kumweleza mtu kwamba mgonjwa wake atafariki muda si mrefu.Pamoja na hayo naomba nirudie kuwauliza tena kwa mara ya pili.Ni kweli mna hakika hakuna namna yoyote ya kuweza kumtibu John?
“ Peniela sisi sote utuonao humu ni madaktari bingwa na kama kungekuwa na namna yoyote ya kuweza kumtibu ndugu yako tusingekueleza hayo tuliyokueleza.Ni kweli hakuna namna tunayoweza kufanya kumsaidia John akapona.” Akasema Daktari mkuu Peniela akainama chini

“ Peniela kuna suala lingine” akasema daktari mkuu.Peniela akainua kichwa.
“ John is awake na he wants to see you” akasema daktari na uso wa Peniela ukajikuta ukitengeneza tabasamu

“ Thank you Lord ! akasema na kufuta machozi akainuka na kuongozana na madaktari hadi katika chumba alimolazwa .Ni kweli John alikuwa ameamka na alikuwa amelala kitandani huku kitanda chake kikiwa kimezungukwa na mitambo mingi.Peniela machozi yakamtoka
“ Stop crying my queen” akasema John kwa sauti dhaifu sana.Peniela akamsogelea pale kitandani.Madaktari wakatazamana kisha wote wakatoka na kuwaacha Peniela na John pekee mle chumbani
“Stop crying Peniela.” Akasema John.Peniela akafuta machozi na kumshika mkono
“ The’ve told you already? Akauliza John
“ Tell me what?
“ Penny suala hili si la kuficha tena na ninatumai kwamba kabla ya kuja hapa tayari wamekwisha kueleza kila kitu kuhusu mimi”

“ Ndiyo wamenieleza kila kitu” akajibu Peniela huku akiendelea kudondosha machozi
“ Usilie Peniela ,huo ndio ukweli halisi.I don’t have much time to live.I’m going to die very soon” akasema John
“ Please john don’t give up.There is must be a way out”
“ Peniela lazima sote tukubaliane na ukweli kwamba hakuna namna nyingine ya kufanya ili niweze kupona.Madaktari wamekwisha thibitisha hilo kwa hiyo hakuna haja ya kuwa na matumaini yasiyokuwepo.Mimi nimelikubali hilo na ninaomba hata wewe ulikubali hilo.Ninashukuru sana kwa jitihada zako za kuhakikisha kwamba ninapona.Pamoja na hayo kuna mambo ambayo nataka kukwambia “ akanyamaza kwa sekunde kadhaa halafu akaendelea

“ kwanza kabisa nakuomba samahani sana kwa mambo yote niliyokufanyia wewe binafsi.Sioni neno zuri ambalo ninaweza kulitumia kukuomba msamaha.Nilitoa uhai wa wazazi wako na kusababisha ukakua bila ya wazazi.Hili ni jambo ambalo linaniumiza mno.Pili nilikuingiza katika team Sc41 na kuyabadili kabisa maisha yako.Peniela nash……” John akashindwa kuendelea kuongea kwani alionekana kuanza kupumua kwa shida
“ John stop.Usiseme chochote tena” akasema Peniela

“ No Peniela.Kuna mambo ambayo lazima niyaweke sawa kabla ya pumzi zangu kukatika.Nahitaji kumuona Yule kijana aliyekuja jana pale nyumbani kwangu na kunitaka nikueleze historia yako”
“ Mathew?!!! Peniela akashangaa
“ Exactly !!..Mathew.I need to see him now.Find him” akasema John
“ John!..” Peniela akataka kusema kitu lakini John akamzuia
“ Please Peniela take the phone and call him now.Tell him to come immediately.” Akasema John
Peniela hakutaka kubishana na John akatoka nje ya chumba na kuchukua simu akampigia Mathew
Si kawaida ya Mahew kulala fofofo na ndiyo maana simu yake ilipoita akaamka mara moja na kukuta ni Peniela ndiye anayepiga.Akastuka kidogo kwani hakutegemea kabisa kama angeweza kumpigia simu usiku ule.Bila kupoteza muda akaipokea
“ Hallow Peniela” akasema Mathew

“ Mathew samahani sana kwa kukusumbua mida hii.”

“ Bla samahani Peniela.Is everything ok? Are you ok? Akauliza
“ I’m ok Mathew na wala usiwe na hofu kuhusu mimi.Jambo lililonifanya nikupigie simu usiku huu ni kwamba jana ulipoondoka nyumbani kwa John mwaulaya hali yake ilibadilika sana na ikatulazimu kumkimbiza hospitali.Baada ya uchunguzi imegundulika kwamba John ana saratani ya ubongo na kwa mujibu wa madaktari hawezi kupona.Hapa ninapoongea niko hospitali .Mathew the man is dying.Kuna mambo ambayo anataka kunieleza lakini kutokana na hali yake inamuwia ugumu lakini kuna jambo ameliomba na kulisisitiza sana.He wants to see you “
Mathew akastuka
“ Unasema ?!!...
“ Najua umestuka Mathew na hata mimi nilistuka hivyo hivyo aliponieleza lakini amesisitiza kwamba anahitaji kukuona haraka usiku huu.Inaonekana kuna kitu cha muhimu sana anataka kukueleza.Naomba uje hapa hospitali Mathew” akasema Peniela .Mathew akafikri kidogo na kusema
“ Ok Peniela ninakuja sasa hivi”
Bila kupoteza muda akamuamsha Anitha na kumfahamisha kwamba anatoka kwenda hospitali


TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
 
PENIELA SEASON 3

EPISODE 7


MTUNZI : PATRICK.CK


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ I’m ok Mathew na wala usiwe na hofu kuhusu mimi.Jambo lililonifanya nikupigie simu usiku huu ni kwamba jana ulipoondoka nyumbani kwa John mwaulaya hali yake ilibadilika sana na ikatulazimu kumkimbiza hospitali.Baada ya uchunguzi imegundulika kwamba John ana saratani ya ubongo na kwa mujibu wa madaktari hawezi kupona.Hapa ninapoongea niko hospitali .Mathew the man is dying.Kuna mambo ambayo anataka kunieleza lakini kutokana na hali yake inamuwia ugumu lakini kuna jambo ameliomba na kulisisitiza sana.He wants to see you “
Mathew akastuka
“ Unasema ?!!...
“ Najua umestuka Mathew na hata mimi nilistuka hivyo hivyo aliponieleza lakini amesisitiza kwamba anahitaji kukuona haraka usiku huu.Inaonekana kuna kitu cha muhimu sana anataka kukueleza.Naomba uje hapa hospitali Mathew” akasema Peniela .Mathew akafikri kidogo na kusema

“ Ok Peniela ninakuja sasa hivi”
Bila kupoteza muda akamuamsha Anitha na kumfahamisha kwamba anatoka kwenda hospitali


ENDELEA………………………..


Peniela alipomaliza kuwasiliana na Mathew akarejea chumbani kwa John
“ Thank you Peniela.Come sit here” akasema John.Peniela akaenda kuketi katika kitanda .John akamtazama kwa sekunde kadhaa kisha akasema

“ Peniela kuna mambo mengi ambayo ningependa nikueleze ila kutokana na hali yangu ilivyo kuna mambo machache ambayo nitakueleza ” akanyamaza na baada ya muda akaendelea

“ Ninatamani kama ningekuwa na muda mrefu wa kuishi ili niweze kuyabadili maisha yako ambayo kwa kiasi kikuwa nimechangia mimi kuyaharibu kwa kukuingiza katika team SC41.Ninalitambua kosa langu na nina nia ya dhati ya kuyabadili maisha yako na kuyafanya bora zaidi .Kuna mambo mawili au matatu ambayo nataka uyafanye” akanyamza na baada ya muda akaendelea

“ Kitu cha kwanza kukifanya nitakapokuwa nimekufa ni kufuata maelekezo niliyokupa kuhusu kuhakikisha umeyapata yale makasha matatu.Wafuate watu niliokuelekeza na utayaunganisha makasha yote.Yakikamilika yote utafahamu mambo mengi hususan jistoria yako japokuwa tayari umeifahamu lakini bado unatakiwa kuifahau kiundani zaidi.” John akanyamaza na kufumba macho kana kwamba kuna kitu anakikumbuka halafu akafumbua macho na kusema

“ Kitu cha pili ninachotaka ukifanye ni kujitahidi kwa kila uwezavyo kuikamilisha operesheni ile inayoendelea na hakikisha kwa kila namna ile package inapatikana na ukishaipata hakikisha haitui katika mikono ya mtu yeyote Yule zaidi yako”

“ Hata team SC41? Akauliza Peniela

“ Especially team SC41” akajibu John
“ Kwani package hiyo ina kitu gani ndani yake John? Akauliza Peniela

“ Siwezi kukwambia kwa sasa lakini ina umuhimu mkubwa sana.Ukiipata keep it somewhere safe ambako haitaweza kufikiwa na mtu yeyote zaidi yako”
Kabla John hajaendelea ,simu ya Peniela ikaita alikuwa ni Mathew
“ Halow Mathew”

“ Peniela ninakaribia kufika hapo hospitali.Uko sehemu gani kwa sababu hospitali hiyo ina majengo mengi”
“ Mathew utanikuta getini ninakusubiri”akasema Peniela na kutoka mle chumbani kwenda kumsubiri Mathew.


********

Mathew aliwasili hospitali na kumkuta Peniela getini akimsubiri
“ Samahani sana Mathew kwa kukusumbua usiku huu” akasema Peniela

“ Bila samahani Peniela.John anaendeleaje?
“ Bado hali yake si nzuri japokuwa anaweza kuongea .Bado anasisitiza kutaka kukuona”

“ This is weird Peniela.Mimi na John Mwaulaya ni maadui wakubwa na yeye analifaamu hilo.Kitu gani basi anachotaka kunieleza? Akauliza Mathew

“ Sifahamu chochote Mathew.Nadhani tusiendelee kupoteza muda twende ukaonane naye kwani kadiri dakika zinavyokwenda ndivyo anavyozidi kudhoofika.Lakini kabla hatujakwenda huko kunajambo ninataka nikuweke wazi.Usijitambulishe kwa mtu yeyote Yule.Kuna madaktari wawili wa team Sc41 wako hapa na wanahitaji kukufahamu.Nimemwelekeza Josh akafute picha zako zote katika kamera za kule nyumbani kwa John.Watu hawa ni wabaya na wanaweza wakavuruga mipango yetu yote” akasema Peniela
“ Ahsante sana Peniela kwa kunitahadharisha mapema.Wamenifahamuje?
“ Walimuhoji Martn Yule daktari ambaye amekuwa akimuuguza John kwa muda mrefu na kutaka kufahamu sababu ya hali ya John kubadilika ghafla naye akawaambia ukweli kwamba hali yake ilibadilika kutokana na vitisho ulivyompa na ndiyo maana wakataka wakufahamu wewe ni nani kwani wana wasi wasi kwamba unaweza ukafahamu mambo mengi kuhusiana na Team SC41 kitu ambacho hawakitaki”

“ Sawa Peniela.Twende tukamuone John” akasema Mathew na Peniela akamuongoza hadi chumbani kwa John.Mara tu Mathew alipomuona John,picha ya moto mkubwa ukiiteketeza nyumba yake pamoja na familia yake ikamjia kichwani

“ I hope when you die you’ll go straight to hell you devil.” Akawaza Mathew huku akimtazama John kwa macho makali

“ John,mtu uliyekuwa unamuhitaji huyu hapa amefika” akasema Peniela.Mathew na John wakatazamana kwa sekunde kadhaa

“ Ahsante sana Mathew kwa kuja” akasema John
“ What do you want from me? Akauliza Mathew kwa sauti ya ukali.John akamtazama Peniela na kusema
“ Peniela naomba utupishe nina maongezi muhimu sana na Mathew”
Peniela akaonyesha wasi wasi Fulani na hasa baada ya kuona namna Mathew alivyokuwa amebadilika
“ Its ok Peniela.Give us a room” akasema Mathew na Peniela akatoka japo kwa shingo upande.Alitamani sana kusikia kile ambacho John na Mathew wanakiongea
“ What is he doing in there? Akauliza Josh kwa wasi wasi huku akimtazama Mathew kupitia kioo kidogo kilichokuwa mlangoni
“ Relax Josh.John mwenyewe ndiye aliyetaka kuonana naye” akasema Peniela
“ What ?! John ametaka kuonana na Mathew? Josh akashangaa

“ Ndiyo” akajibu Peniela

“ Kwa nini?
“ hata mimi sifahamu “ akajibu Peniela
“ Bado sijamsahau Yule jamaa namna alivyoingia chumbani kwa John na bila kujali hali yake ya afya akamfanyia vitisho na kupelekea hali ya John kubadilika.Sina amani kabisa nikimuona Mathew karibu na John” akasema Josh
Kupitia kioo kilichokuwa katika mlango Mathew na John mwaulaya walionekana kuongea kwa kuelewana kana kwamba ni watu wanaofahamiana sana.
“ Kwa nini John ametaka kuonana na Mathew? Kwa mujibu wa Mathew ni kwamba John akishirikiana na team SC41 waliiteketeza familia yake.Mathew bado ana hasira kubwa na John na inanishangaza sana kwa John kutaka kuonana na adui yake” akawaza Peniela halafu akageuka na kuungana na Josh kuwaangalia Mathew na John mwaulaya wakiongea
“ What are they talking about? Akajiuliza Peniela

“ Natamani nifahamu wanachokiongea.Natamani pia nipate walau dakika chache za kuongea na John mwaulaya ili anipe ufafanuzi kuhusiana na wazazi wangu.Walizikwa wapi na vile vile nataka kufahamu kama anawafahamu ndugu zangu .Kitu kingine ambacho ninataka kukifahamu ni kuhusu John mwenyewe.Katokea wapi.Familia yake iko wapi.Ndugu zake wako wapi? Nahitaji kuyafahamu haya kwa sababu John hana maisha marefu na kila mtu ananiangalia mimi wakijua ndiye ninayefahamu kila kitu kuhusu John Mwaulaya.” Akawaza Peniela
Maongezi kati ya John Mwaulaya na Mathew yalichukua zaidi ya dakika hamsini.Hakuna aliyesikia walichokiongea.Walionekana kuongea kwa kuelewana sana na kuna nyakati Mathew alionekana kuandika mambo Fulani aliyoelekezwa na John katika kijitabu kidogo
Baadae Mathew akaonekana akimshika mkono John Mwaulaya wakaagana kisha akatoka mle chumbani na kuwakuta Peniela na Josh mlangoni

“ Thank you Peniela.I have to go now” akasema Mathew na Peniela akamsindikiza
“ John anasemaje? Alikuitia nini? Akauliza Peniela

“ Nothing important.It was just a normal talk” akajibu Mathew

“ Normal talk? Peniela akashangaa

“ Ndiyo Peniela.It was just a normal talk.John alitaka tumalize tofauti zetu mimi na yeye.Thats all” akasema Mathew Peniela akasimama na kumtazama Mathew

“ Mathew hainingii akilini hata kidogo eti John akuite na atake kumaliza tofauti zenu.Alisema nikuite kwa sababu kuna jambo ambalo hakutoka mimi nilijue.Mathew me and you we’re team now so in order to win this war we have to trust each other.I told you everything I know and you must do the same.Tell me the truth” akasema Peniela .Mathew akamtazama kwa sekunde kadhaa halafu akasema
“ Ni kweli kuna mambo amenieleza ambayo hakutaka kumweleza mtu mwingine yeyote .Ni mambo mazito ambayo sintaweza kukwambia kwa sasa hadi hapo tutakapokuwa tmeipata package toka kwa Dr Joshua na kundi lake.Kwa hiyo kwa sasa inabidi tuelekeze nguvu zetu nyingi katika kuhakikisha kwamba package hiyo inapatikana.” Akasema Mathew na kumshika mkono Peniela
“ Peniela the man is dying so if there is anything that you want to know from him,this is the time” akasema Mathew
“ Ni kweli Mathew,kuna mambo mengi ambayo nahitaji kuyafahamu toka kwa John lakini kila nikimuona katika hali ile ninashindwa kumuuliza chochote najikuta nikilia.Japokuwa kuna mambo mengi ambayo amenifanyia lakini kwa hali aliyonayo sasa namuonea huruma sana” akasema Peniela

“ John hana maisha marefu.Go get what you want from him.Nitakupigia simu asubuhi “ akasema Mathew na kuingia katika gari lake akaondoka.Baada ya Mathew kuondoka,Peniela akarejea chumba cha John

“ Peniela come close “ akasema John
“ Peniela kuna mambo kadhaa ambayo nataka nikueleze lakini kubwa ni kwamba baada ya mimi kufariki Mathew ndiye atakayebaki ngao yako.Nimempa maelekezo yote na amenihakikishia kwamba atafanya yale yote niliyomuelekeza”

“ John umeongea nini na Mathew? What did you tell him? Akauliza Peniela

“ Kuna mambo ambayo nimemweleza aliyotakiwa kuyafahamu yeye pekee.Kitu kingine ni kwamba mwanzo nilikueleza kuhusu kwamba ukifanikiwa kuipata ile package uiweke mahala ambako hakuna anayeweza kuifikia lakini kwa sasa ninakuomba ukifanikiwa kuipata salama mkabidhi Mathew.Nimekwisha mpa maelekezo yote. Yeye ndiye atakaye kusaidia hata kukutoa ndani ya Team Sc41.” akasema John Mwaulaya.Peniela alisikia uchungu mwingi na kujikuta akitoa machozi
“ John you’ve been like my father so it hurt me a lot that I cant do anything to save you”
“Peniela ahsante sana kwa maneno yako mazito.Ninakupenda sana Peniela na siku zote nimekupenda kama mwananngu.Naamini toka ndani kabisa mwa moyo wako utanisamehe kwa yale yote mabaya niliyokufanya .” akasema John
“ John pamoja na yote uliyonitendea ambayo unayaita mabaya nakuhakikishia kwamba toka ndani ya moyo wangu nimekusamehe.Umenifanyia mambo mengi mazuri na siwezi kuusahau wema wako kwangu.Toka nikiwa mdogo ulihakikisha ninaishi maisha mazuri na ninapata kila ninachokihitaji..Ahsante sana John” akasema Peniela.Kikapita kimya kidogo Peniela akauliza

“ John where is your family?
John akamtazama Peniela kwa makini na kusema
“ Hakuna anayefahamu historia yangu wala aliyewahi kuniuliza chochote kuhusu historia yangu.Wewe umekuwa ni kwanza kutaka kunifahamu na kwa kuwa ninakupenda nitakeuelza ukweli kuhusu mimi.” John akanyamza halafu akaendelea.
“ I don’t have a family.I grew up without a family.Siwafahamu wazazi wangu wala ndugu zangu.Nmelelewa katika kituo cha watoto wa mitaani.Nikiwa na umri wa miaka kumi na moja niliondoka katika nyumba ya malezi na kujiunga na kundi la watoto wa mitaani na huko ndiko nilikoanza kujifunza mambo mengi mabaya.Siku moja tukiwa bondeni tukicheza kamari ghafla akatokea mzee mmoja tuliyemfahamu kama mzee Mgomba.Huyu alikuwa ni mwanajeshi na tulimuogopa sana.Wote tukatimua mbio lakini akatusihi tusikimbie kwani hakuwa na tatizo lolote na sisi.Wenzangu wote walitokomea bondeni isipokuwa mimi.Mzee Mgomba akanipa kazi ya kumtafuta mbwa wake aliyepotea.Aliahidi kunilipa fedha nyingi endapo ningefanikiwa kumpata mbwa wake.Sikuwa muoga nikamtafuta Yule mbwa na baada ya siku mbili nikafankiwa kumpata,alikuwa ameibiwa.Mzee Mgomba alifurahi sana na akanipatia shilingi laki mbili.Pamoja na fedha alizonipa lakini aliniuliza mahala nikaoishi nikamueleza historia yangu akasikitika sana akaomba nikubali kubadilika ili anisaidie.Alinipatia kazi ya kuhudumia mbwa wake wawili .Niliifanya kazi hiyo kwa ustadi mkubwa na kumfurahisha sana na akamua kunipeleka shule moja nzuri ya gharama ambako nilianza kusoma.Mzee Yule alinipenda kama mwanae” John akanyamaza kidogo ,akaendelea

“ Nilisoma kwa bidii sana na nikawa mmoja wa wanafunzi hodari kila mwaka.Nilifaulu na kuendelea na elimu ya sekondari .kidato cha nne nikafaulu pia nikaendelea na kidato cha tano na sita.Baada ya hapo nikajiunga na jeshi la wananchi na baadae nikachaguliwa kuingia katika mafunzo ya urubani wa ndege za vita.Nilipelekwa nchini Marekani kwa mafunzo zaidi na hapo ndipo nilipojiunga na Team SC41” akasema John na kuvuta pumzi ndefu kwa taabu

“ John basi imetosha.Usiongee tena” akasema Peniela
“ Peniela acha niongee.Historia yangu ni ndefu lakini mbaya sana.Imejaa mambo machafu na jambo pekee ambalo kwangu mimi ninaliona ni zuri ni kitendo cha kukataa kukutoa uhai kama nilivyoelekezwa na baba yako.Nadhani ni hicho pekee kizuri nilichokifanya katika maisha yangu lakini historia yangu imejaa uchafu wa kila namna na haifai hata kuisikiliza.Nimetoa roho za watu wengi na kwa sasa ninasikia watu niliowaua wakinililia.” Akasema John na kumshika Peniela mkono

“ Peniela wewe ndiye ndugu yangu pekee ninayekufahamu kwa sasa na hata kama nikifa ni wewe ndiye mwenye uamuzi na kila kitu kuhusiana na mazishi yangu.Narudia tena kukukumbusha kwamba baada ya mimi kufariki hakikisha unafuata maelekezo yote niliyokupa” akasema John.Peniela hakusema kitu akabaki anamtazama John kwa huzuni kubwa.Baada ya muda John akasema
“ Ninasikia sauti za watu niliowakatikli maisha yao wananililia na kuniuliza kwa nini niliwakatili haki yao ya kuishi? Katika dakika zangu za mwisho ninadiriki kusema kwamba ninahitaji msamaha wa Mungu.Japokuwa sijawahi kujiunga na dini yoyote ile lakini naamini kwamba kuna Mungu na anaweza akanisamehe.Peniela naomba unitafutie padre nahitaji kutubu makosa yangu na kumuomba Mungu msamaha.I can feel death and I can feel the fire.I can feel hell.I don’t want to go to hell.Please Peniela go now! Akasisitiza John na hali yake ikaanza kubadilika.Peniela akatoka na kwenda kuwaita madaktari ambao walifika haraka
“ Josh natakiwa kumtafuta Padre.John anahitaji padre na sijui nitampataje kwa sababu toka nilipoondoka nyumbani kwa bi Bernadetha sijwahi kushiriki ibada yoyote ile.” Akasema Peniela

“ Tutafanya nini sasa Peniela? Akauliza Josh
“ Kuna kitu nimekumbuka.Twende tukamuone mtu Fulani yeye ndiye aayeweza kutusaidia katika hili” akasema Peniela na bila kumuaga mtu yeyote wakaingia garini na kuondoka
“ John amekiona kifo chake na ndiyo maana anataka kutubu dhambi zake .Do you think God will forgive him? Akauliza Peniela
“ I don’t know Peniela” akajibu Josh.Safari ikaendelea hadi walipofika nje ya nyumba Fulani iliyokuwa na geti kubwa na walinzi wawili

“ Hapa ni wapi? akauliza Josh huku akiufungua mlango na kutaka kushuka
“ Usishuke Josh.Kuna walinzi wakali sana hapa na unaweza ukajeruhiwa” akasema Peniela na kuchukua simu akazitafuta namba Fulani akapiga.Simu ikaita bila kupokelewa,akapiga tena ikaita bila kupokelewa
“ C’mon mom pick up the phone” akasema na kupiga kwa mara ya tatu.

“ Hallow Peniela! Ikasema sauti ya upande wa pili baada ya kupokea simu.Peniela akaitambua sauti ile akatabasamu
“ mama Bernadetha shikamoo”

“ marahaba Peniela,Habari za siku nyingi? Unaendeleaje wewe mtoto? Kulikoni usiku huu? Akauliza bi Bernadetha

“ Mama nina tatizo na niko hapa nje kwako”

“ Uko hapo nje?

“ Ndiyo mama nahitaji sana msaada wako.”

“ Ok nakuja” akajibu bi Bernadetha

“ Hapa ndipo nilipolelewa “ Penielea akamwambia Josh na mara geti likafunguliwa akatokea bi Bernadetha akiwa ameongozana na walinzi wawili.Peniela akashuka garini na kwenda kukumbatiana naye halafu wakaelekea ndani.
“ Habari za siku nyingi Peniela? Pole sana kwa matatizo .Kwa nini umepata matatizo bila ya kunitaarifu” akauliza bi Bernadetha

“ Mama utanisamehe sana .Nitakuja siku nyingine na nitakueleza kila kitu lakini kwa sasa kuna jambo moja kubwa lililonileta” akasema Peniela na kumsimuliza Bernadetha kila kitu kuhusiana na John Mwaulaya.
“ Kwa hiyo mama nimekuja kuomba msaada wako.Nafahamu wewe uko karibu sana na hawa viongozi wa dini na unaweza knisaidia kumpata mmoja” akasema Peniela
Kwa msaada wa bi Bernadetha walifanikiwa kumpata padre ambaye waliongozana naye hadi hospitali.Baada ya kuwasili hospitali watu wote wakatolewa mle ndani ya chumba cha John akabaki yeye na Padre tu.
Padre alitumia zaidi ya dakika hamsini ndani ya chumba cha John.Walionekana kuongea na baadae akamuombea na kumpaka mafuta usoni baadae Padre akatoka.
“ Ndugu zangu kama nyote mnavyofahamu kwamba kutokana na ugonjwa wake ndugu yetu hatakuwa na maisha marefu sana kwa hiyo basi nimempatia huduma ya mwisho kabla ya mwenyezi Mungu kumuita.John Mwaulaya amekubali kwa hiari yake kubatizwa na amekuwa mpya tena . John ametubu dhambi zake zote na kwa mamlaka niliyopewa na kanisa nimemuondolea dhabi zake. Amepokea komunyo takatifu na Yesu yuko ndani yake.Kwa sasa hata kama akiitwa na Mungu dakika yoyote tuna hakika atakuwa sehemu salama.Kitu cha msingi ni kuzidi kumuombea ili hata atakapoondoka katika maisha haya aweze kupokelewa Mbinguni” akasema Padre na kuwabariki wote kisha Peniela akamrudisha nyumbani kwake.



TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
PENIELA SEASON 3

EPISODE 8

MTUNZI : PATRICK.CK

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

Padre alitumia zaidi ya dakika hamsini ndani ya chumba cha John.Walionekana kuongea na baadae akamuombea na kumpaka mafuta usoni baadae Padre akatoka.

“ Ndugu zangu kama nyote mnavyofahamu kwamba kutokana na ugonjwa wake ndugu yetu hatakuwa na maisha marefu sana kwa hiyo basi nimempatia huduma ya mwisho kabla ya mwenyezi Mungu kumuita.John Mwaulaya amekubali kwa hiari yake kubatizwa na amekuwa mpya tena . John ametubu dhambi zake zote na kwa mamlaka niliyopewa na kanisa nimemuondolea dhabi zake. Amepokea komunyo takatifu na Yesu yuko ndani yake.Kwa sasa hata kama akiitwa na Mungu dakika yoyote tuna hakika atakuwa sehemu salama.Kitu cha msingi ni kuzidi kumuombea ili hata atakapoondoka katika maisha haya aweze kupokelewa Mbinguni” akasema Padre na kuwabariki wote kisha Peniela akamrudisha nyumbani kwake.


ENDELEA…………………

Mlio wa simu ulimstua Mathew toka usingizini .Haraka haraka akaichukua simu yake na kutazama mpigaji.Alikuwa ni Eva

“ Hallow Eva? Akasema Mathew
“ Mathew habari za asubuhi? Bado umelala?
“ Ahsante sana kwa kuniamsha Eva.Nilikuwa katika usingizi mzito sana.Kuna habari gani? Akauliza Mathew
“ Mathew nimekupigia kukupa taarifa kuhusiana na ile kazi uliyoniomba nikufanyie.Kuna kitu cha ajabu ambacho kimetokea na kunishangaza sana.Hakuna taarifa zinazoonyesha mawasiliano ya simu ya wale wazee kwa muda wa miezi sita ya mwisho kabla hawajauawa.Taarifa hizo zimefutwa kabisa katika kumbu kumbu kwa hiyo ni vigumu kufahamu walikuwa wakiwasiliana na akina nani kabla hawajafariki.Hii imenishangaza sana Mathew.” Akasema Eva.Mathew akakaa kimya kidogo na kusema
“ Thank you Eva.
“Kuna chochote kingine nikusaidie? Akauliza Eva
“ No thank you Eva.Nikihitaji msaada tena nitakujulisha.Ila nashukuru sana kwa msaada huu mkubwa” akasema Mathew na kukata simu.
“ Kwa miezi sita hakuna taarifa za mawasiliano ya simu za wazee wale.Ni wazi taarifa hizi zimeondolewa makusudi kabisa na lengo hapa ni kumficha Yule mtu ambaye alikuwa nyuma yao.Watu hawa wako makini sana kwani walifahamu fika uchunguzi ungefanyika na yangefuatiliwa mawasiliano kati ya wazee wale na mtu huyo angefahamika na ndiyo maana wakawahi kufuta kabisa kumbu kumbu zote za mawasiliano .Lakini hata hivyo kuna njia nyingine ya kuweza kumfahamu mtu huyo ni nani.Ngoja turudi sasa katika lile wazo la Anitha la kumchunguza Habib ambaye anatajwa kutaka kununua karatasi zile.Nina hakika kupitia yeye basi tunaweza kugundua jambo Fulani.Nina rafiki yangu katika shirika la ujasusi la C.I.A yeye anaweza akanisaidia sana katika jambo hili kwani C.I.A wamejipenyeza karibu kila kona ya dunia na ni rahisi sana kumfuatilia mtu yeyote Yule” akawaza Mathew na kutoka mle chumbani.Tayari Anitha alikwisha amka kitambo na alikuwa jikoni akiandaa mlo wa asubuhi.Mida hiyo ilipata saa moja na dakika kumi na saba za asubuhi
“ Hallow Anitha” akasema Mathew huku akifungua kabati na kutoa chupa ya mvinyo akamimina kidogo katika glasi akagugumia yote.Anitha akamtazama na kusema
“ Is something bothering you? I know you.Ukinywa mvinyo kama hivyo lazima kuna jambo linalokusumbua.” Akasema Anitha
“ nataka kuchangamsha mwili tu ,naona umechoka sana” akajibu Mathew.Anitha akaacha shughuli aliyokuwa akiifanya akamtazama Mathew na kusema
“ Ulionana na John jana? Anaendeleaje? Alikuitia jambo gani? .
Mathew akaongeza tena mvinyo katika glasi akanywa na kusema
“ Nothing important.Hali yake si nzuri na kwa mujibu wa uchunguzi wa madaktari john anasumbuliwa na saratani ya ubongo kwa hiyo hakuna tegemeo la kupona.Aliniita na kuniomba msamaha kwa kitendo kile cha kuiteketeza familia yangu vile vile akanitaka nimlinde Peniela na kuhakikisha anakuwa salama siku zote.Thats all” akasema Mathew na kunywa funda lingine la mvinyo.
“ Anything from Kigomba? Akauliza Mathew

“ hakukuwa na simu ya maana aliyopiga tena zaidi ya kuwapigia simu waanwake wawili na akamuahidi mmoja wao kwamba anakwenda kulala kwake.Vile vile alimpiga simu mke wake na kumweleza kwamba hataweza kurejea nyumbani usiku ule kutokana na kuwa na kikao kizito.Kigomba anaonekana ni mpenda wanawake sana.”akasema Anitha

“ Usimweleze jaji Elibariki chochote kuhusiana na simu hizo za Kigomba alizowapigia wanawake wengine,si unajua anavyompenda peniela.By the way Eva amenipigia simu muda si mrefu na amenipa taarifa kuhusiana na kazi ile niliyomuomba anisaidie kuifanya.Hakuna kumbu kumbu zozote za mawasiliano za wazee wale kwa miezi sita kabla ya kufariki kwao.Zimefutwa kwa makusudi kabisa kwa ajili ya kumficha huyo ambaye walikuwa wakiwasiliana naye.Kwa sababu hiyo basi tunarejea katika lile wazo lako la kumchunguza Habib ambaye anatajwa kutaka kuzinunua karatasi zile.”akasema Mathew

“ Nina rafiki yangu mmoja anafanya kazi katika idara ya ujasusi ya marekani C.I.A.Nina hakika anaweza akatusaidia katika suala hili.” Akasema Mathew halafu akaongozana na Anitha hadi ofisini na kumpigia simu huyo rafiki yake afanyaye kazi katika shirika la ujasusi la marekani.Baada ya sekunde kadhaa mwanadada mmoja akaonekana katika luninga kubwa iliyokuwa ukutani.
“ hallow Mathew” akasema mwanadada Yule mwenye asili ya afrika

“ hallow Kerry.habari za siku ?
“ habari nzuri sana .habari za Tanzania?
“ Tanzania kwema.Samahani kwa kukusumbua Kerry,ninashida naomba unisaidie”
“ Bila samahani Mathew.Nikusaide nini?

“ Kuna mtu mmoja ambaye ninahitaji unisaie kumchunguza.Anaitwa Habib soud ni raia wa Saudi Arabia.Ninataka kufahamu kama ana mawasiliano na mtu yeyote kutoka Tanzania.Kuna jambo ninalichunguza na yeye amejitokeza katika picha .Najua ni kinyume na taratibu zenu za kazi lakini naomba unisaidie Kerry,Ni muhimu sana kwangu” akasema Mathew..Kerry akaonekana kufikiri kidogo kisha akasema
“ sawa Mathew nitakusaidia.Nisubiri dakika mbili.”akasema Kerry na kukata simu
“ Unapofanya kazi kama hizi kuna ulazima wa kuwa na marafiki wengi toka katika mashirika mbali mbali ya kijasusi na kipelelezi duniani ili unapohitaji taarifa Fulani basi inakuwa rahisi sana kuipata.Mimi nina marafiki karibu katika mashirika mengi makubwa ya ujasusi duniani.C.I.A,KGB,MOSSAD,MSS la china,BND ujerumani,MOIS Iran,na mengine mengi” Akasema Mathew na mara Kerry akarejea hewani
“ Mathew huyu Habib Soud ni mtu ambaye amekuwa katika orodha ya watu wanaochunguzwa na C.I.A kwa kufadhili vikundi vya kigaidi.Habib ana utajiri mkubwa sana na inasemakana anautumia utajiri huo katika kufadhili ugaidi.Baba yake alikuwa ni mfadhili wa siri wa Alqaeda na aliuawa na vikosi vya Marekani .” akasema Kerry na kusogeza tena taarifa nyingine katika tablet yake.

“ C.I.A tumekuwa tukimfuatilia pia mawasiliano yake .kwa upande wa Tanzania taarifa zinaonyesha kwamba amekuwa na mawasiliano ya mara na mtu mmoja anaitwa Rosemary Mkozumi.Huyu aliwahi kuwa mke wa rais wa Tanzania na ana taasisi yake inayojishughulisha na miradi mbalimbali ya kuwawezesha akina mama kiuchumi .Kupitia taasisi hii amekuwa akipata wadhili toka sehemu mbali mbali duniani na mmojawapo wa wafadhili wa taasisi hii ni Habib.Amekuwa akitoa pesa nyingi kama misaada kwa taasisi hii kwa dhumuni la kuwawezesha wanawake kiuchumi.Habib anafanya hivi ili kuificha ile dhana kwamba anafadhili makundi ya kigaidi.Mathew hizo ndizo taarifa ninazoweza kukupa kwa sasa kuhusiana na habib.Sisi bado tunaendelea kumchunguza na kama kuna lolote ambalo unaona linaweza likatusaidia katika kupata ushahidi wa kutosha kuhusu Habib kujihusisha na makundi ya ugaidi basi naomba unitaarifu mara moja na endapo utahitaji tena msaada wowote mimi niko tayari kukusaidia muda wowote.” Akasema Kerry

“ Kerry nakushukuru sana kwa msaada wako huo mkubwa.Endapo nitapata jambo lolote la kumuhusu Habib katika uchunguzi wangu nitakutaarifu mara moja” akasema mathew na kuagana na Kerry akata simu.Muda huo huo jaji Elibariki akaingia mle ofisini

“ Kuna taarifa yoyote mpya imepatikana? Akauliza jaji Elbarki
“ Ndiyo jaji.Kuna taarifa tumezipata .Kwanza ni kutoka kwa Eva.hakuweza kupata taarifa zozote za mawasiliano za mzee Mustapha na Ktwana.Inaoenaka zimefutwa kabisa kwa makusudi.Tumewasiliana na trafikiyangu mmoja aanayefanya kazi katika shirika la ujasusi la marekani na ametutaarifu kwamba mtu ambaye alitajwa kutaka kuzinunua karatasi zile zilizoibwa ikulu Habib soud amekuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na Rosemary Mkozumi mke wa rais mstaafu Deus Mkozumi.Amekwenda mbali zaidi na kusema kwamba Habib amekuwa akiifadhili taasisi inayoongozwa na bi Rosemary kwa kuimwagia mabilioni ya fedha .” Mathew akanyamaza kidogo kisha akaendelea
“ Jana tumemsikia Dr Joshua akimtaja adui yake namba moja katika mpango wa kuiuza package ni Deus mkozumi.Leo tena tunasikia kwamba mke wa Deus mkozumi anapokea mamilioni ya fedha toka kwa mtu anayedaiwa kuufadhili ugaidi.Hapa kuna picha inajengeka.Ninapata picha kwamba package hiyo anayotaka kuiuza Dr Joshua ilikuwepo hata wakati wa uongozi wa Deus na anaifahamu fika na ndiyo maana amekuwa kinyume na mpango wa Dr Joshua wa kutaka kuiuza.Pili nina hakika kabisa kwamba hata hizo karatasi zilizoibwa zilikuwepo ikulu wakati wa uongozi wa Deus na nina hakika kabisa kwamba Rosemary kwa kuwa naye alikuwepo ikulu wakati huo alifahamu uwepo wa karatasi hizo.Ninaweza kutamka bila wasi wasi kwamba Rosemary ndiye aliyekuwa nyuma ya mpango wa kuziuza karatasi zile.Kumbu kumbu za mawasiliano za mzee Kitwana na mzee Mustapha zimefutwa kwa sababu ya kumficha ili asijulikane kama alikuwa akiwasiliana nao.” Akasema Mathew akawaangalia akina Anitha na kusema
“ kama Habib anashukiwa kuufadhili ugaidi basi ni wazi alihitaji sana karatasi zile ili kuweza kuzitumia kanuni zilizomo ndani yake katika kutengeneza kirusi hicho hatari ili kitumike katika mashambulio ya kigaidi.Hii ni sababu pekee ambayo ilimfanya Habib kutaka kuzinunua karatasi zile kwa mabilioni ya fedha.Mnaona namna picha inavyojengeka? Akauliza Mathew

“ Nakubaliana nawe kabisa Mathew.Maelezo uliyoyatoa yanatoa taswira ya wazi ya namna Rosemary Mkozumi alivyohusika katika uibwaji wa karatasi zile ikulu.Kwa mantiki hiyo basi Rosemary naye atakuwa ni mtu wa muhimu sana kwetu .Kuna mambo mengi ambayo tutahitaji kuyafahamu kutoka kwake.” Akasema Anitha

“ Jamani kuna jambo na mimi naomba niliseme.” Akasema jaji Elibariki
“ Ninamfahamu huyu Rosemary Mkozumi .Alikuwa ni mke wa rais mstaafu Deus Mkozumi lakini baada ya Deus kumaliza awamu yake ya pili ya uongozi walitengana.Hakuna sababu iliyowekwa wazi kuhusiana na kutengena kwao.Rosemary anamiliki jumba kubwa la kifahari ufukweni mwa bahari na vile vile anamiliki pia biashara nyingine nyingi kubwa kubwa.Ni mwanamke tajiri na mpaka sasa haijawekwa wazi utajiri wake ameupataje.Ninaweza kukubaliana na maneno ya mathew kwamba Rosemary aliingiwa na tamaa ya pesa na akaamua kusuka mpango wa kuziuza karatasi zile. Edson alitumiwa tu katika kuziiba lakini maelekezo yote yalitoka kwa Rosemary.” Akasema jaji Elibariki na mara ikasikika kengele ya getini.
“ Ngoja nikaangalie nani anagonga” akasema Mathew na kutoka

“ Is Mathew ok? Akauliza jaji Elibariki baada ya Mathew kutoka.Aligundua kwamba Mathew hakuwa sawa.
“ There is must be something bothering him.Jana usiku alipigiwa simu na peniela kwamba john Mwaulaya anamuhitaji.Aliondoka na kwenda hospitali kuonana na John.Nimemuuliza ni kitu gani John alichomuitia lakini bado hajanipa jibu la kweli.Amekuwa akificha ficha.Ninamfahamu Mathew ,kuna jambo aliambiwa na John” Akasema Anitha

“ Umesema alikwenda kuonana na John mwaulaya? Jaji Elibariki akashangaa
“ ndiyo alikwenda kuonana naye jana usiku na….” kabla Anitha hajaendelea akaingia Mathew akiwa ameongozana na peniela.Jaji Elibariki na peniela walipoonana wakajikuta wakikumbatiana kwa nguvu na kupeana mabusu

“ Are you ok my love?akauliza jaji Elibariki

“ I’m ok Elibariki.What about you,are you ok?

“ I’m ok peniela” akasema jaji Elibariki .Anitha na Mathew wakatazamana wakatabasamu

“ karibu sana peniela” akasema Mathew
“ Ahsante sana Mathew.mambo yanakwendaje hapa?
“ mambo yanakwenda vizuri .Anaendeleaje John? Akauliza Mathew
“ Bado hali yake si nzuri.Jana ulipoondoka hali ilizidi kuwa mbaya akaomba tumtafutie padre.Tulifanikiwa kumpata Padre kwa usiku ule na akampatia huduma ya kiroho kumuandaa kwa lolote linaloweza kutokea.Nimeondoka kule saa kumi na moja alfajiri bado hali yake haikuwa nzuri.Nimewapigia tena simu madaktari kabla sijaja huku na wakaniambia kwamba kwa sasa hali yake imezidi kuwa mbaya .Anything can happen at anytime.” Akasema peniela na chumba kikawa kimya.Mathew akauvunja ukimya

“ Tuko pamoja Peniela katika wakati huu mgumu” jaji Elibariki na Anitha wakamuhakikishia peniela kwamba wako pamoja naye pia

“ Ahsanteni sana kwa ushirikiano wenu.Nimepita hapa ili kufahamu ni kitu gani kinachoendelea kwani toka jana hatukuwasiliana.Vipi ule mpango wetu ulifanikiwa? Akauliza Peniela

“ Ulifanya kazi kubwa sana jana na kila kitu kimeenda vizuri kama tulivyopanga Tayari tunaweza kufuatilia kila kinachofanyika katika simu ya Dr Kigomba.Mfano jana tumeweza kusikia maongezi yote aliyoongea na Dr Joshua akiwa afrika ya kusini.Vile vile tunaweza kufahamu kila mahala aliko Dr Kigomba endapo atakuwa ameivaa ile saa” akasema Anitha na kumuelekeza Peniela namna program ile inavyofanya kazi.Akayafungua maongezi ya simu kati ya Dr Kigomba na Dr Joshua na wote kwa pamoja wakayasikia.
“kumbe Yule mzee ni mtu katili sana.Amekwenda afrika ya kusni shingo upande.Kwake yeye fedha ni muhimu sana kuliko uhai wa binadamu tena mtoto wake mwenyewe” akasema peniela kwa hasira

“ kwa mujibu wa maongezi yao inaonekana wanajiandaa kuifanya biashara hii haraka iwezekanavyo.Alimuachia Dr Kigomba jukumu la kuhakiki kama fedha tayari imekwisha ingia katika akaunti zao za siri nje ya nchi na mara tu wakihakikisha kwamba fedha yote imelipwa basi wataikabidhi hiyo package.Mtu wa muhimu na wa kuchunga sana hapa ni Dr Kigomba kwani ndiye atakayefanya makabidhiano kwa niaba ya Dr Joshua Kwa vile tayari tuna uwezo wa kumfuatilia Dr Kigomba .Peniela unatakiwa ukae karibu sana na Dr Kigomba.Ongeza ukaribu pia na Kaptain Amos ambaye mko naye team SC41 na yuko timu moja na akina Kigomba .Katika team SC41 mmejipanga vipi katika kuichukua hiyo Package? Akauliza Mathew
“ Jana walikuja watu watano kutoka makao makuu ya team SC41 Marekani na dhumuni lao kubwa ni kuja kusimamia suala hilo la uchukuaji wa hiyo Package na kuondoka nayo.Leo kutakuwa na kikao cha watu wote wa team SC41 kwa ajili ya kuweka mikakati ya mwisho kuhusiana na package hiyo.Team SC41 wamejipanga kikamilifu kuhakikisha wanaipata package hiyo na katika operesheni hiyo wanatutegemea sana sisi wawili mimi na captain Amos.
"
“ Mpaka sasa hivi hujafanikiwa kufahamu kilichomo ndani ya hiyo Package? Akauliza Anitha

“ Hapana bado.Mpaka sasa hakuna ajuaye ndani ya hipo package kuna nini.Nmejaribu kuwadadisi wale jamaa waliotoka Marekani lakini hawako tayari kuweka wazi.”
“ Ok vizuri.Basi utaendelea kutufahamisha mipango yote ya team SC41 kuhusiana na package hiyo Kitu cha muhimu sana kuzingatia jihadhari wasije wakagundua kwamba unashirikiana nasi” akasema Mathew
“ Ninalifahamu hilo na niko makini sana katika kuhakikisha kwamba hawagundui lolote.Hata nijapo huku huwa ninatumia mbinu za hali ya juu sana. Ili nisiweze ku…..” Peniela akastushwa na mlio wa simu yake.Akaitazama ikiita akaogopa kuipokea.

“Mbona hupokei simu? Akauliza Mathew
‘ Its Josh.Yuko kule hospitali” akasema Peniela kwa wasi wasi
“ Pokea ufahamu anataka kukwambia nini.Yawezekana ana jambo la muhmu sana la kukwambia”akasema jaji Elibariki .Peniela akabonyeza kitufe cha kupokelea na kuweka simu sikioni

“ hallow Josh ” akasema.Zikapita sekunde kadhaa bila ya Josh kuongea kitu
“ Josh are you there? Akauliza peniela
“ Peniela where are you? Akauliza Josh
“ Josh kuna nini?
“ Naomba uje mara moja hapa hospitali” akasema Josh na kukata simu.Peniela akapatwa na wasiwasi mwingi

“ Is everything ok peniela? Akauliza Mathew
“ Josh ananitaka nifike haraka hospitali .Sijui kuna nini.I’m so scared.”akasema Mathew

“ Usiogope peniela .Yawezekana kuna jambo la msingi analokuitia..I’ll take you there.” Akasema Mathew

“ No thank Mathew I can manage” akasema peniela

“ Peniela uko katika mstuko na ni hatari sana kuendesha gari ukiwa katika hali hiyo.Naomba usiweke ubishi katika hilo.Nitakupeleka hospitali.Anitha endelea kumfuatilia Dr Kigomba na kama kuna jambo lolote la dharura utanitaarifu mara moja” akasema Mathew na kuingia chumbani kwake akavaa kisha akaongozana na Peniela akamuendesha kuelekea hospitali.
“ Anitha ninakubaliana nawe kwamba mathew leo hayuko sawa sawa.Kuna jambo linalomsumbua kichwa chake.” Akasema jaji Elibariki.

“ Ninavyofahamu mimi,Mathew na John Mwaulaya ni maadui wakubwa.Ni John mwaulaya aliyeiteketeza familia ya Mathew.Siku zote Mathew alikuwa akitafuta nafasi ya kulipiza kisasi kwa John Mwaulaya na ndiyo maana aliponiambia kwamba John amemuita hospitali nilistuka sana .Lakini tumuache kwanza atulie na atatueleza “akasema Anitha
Mathew na Peniela wakawasili hospitali.Safari yao haikuwa na maongezi mengi kwani Peniela alionekana kuzama katika mawazo na Mathew hakutaka kumsumbua

“ Mathew ahsante sana .Ulikuwa sahihi.Nisingeweza kuendesha gari kwa hali hii.Miguu inanitetemeka ” akasema Peniela huku akifungau mlango na kushuka wakaelekea katika jengo alikolazwa john.Mtu wa kwanza kuonana naye alikuwa ni Josh.Macho yake yalionekana kuwa mekundu .Peniela akazidi kujawa na wasi wasi.Josh alipomuona akamfuata na kumkumbatia

“ Peniela I’m sorry.He’s gone.John is gone”akasema Josh.Peniela akaishiwa nguvu na kuzirai.Haraka haraka akachukuliwa na kupelekwa kupatiwa huduma ya kwanza .Wakati Peniela akiendelea kupatiwa huduma ya kwanza simu ya Mathew ikaita.Alikuwa ni Anitha

“ hallow anitha.Nilikuwa katika harakati za kukupigia simu kukufahamisha mambo ya huku .Kuna habari gani hapo? Akaulzia Mathew
“ Dr Joshua amempigia simu Dr Kigomba muda si mrefu.Flaviana is gone.She’s dead.” Akasema peniela .Ilimchukua Mathew zaidi ya dakika moja kutamka lolote

“ How’s Elibariki?
“ ameishiwa nguvu.Nimempeleka chumbani kupumzika.”akasema Anitha

“ Ok Endelea kumpa uangalizi wa karbu sana.Huku nako mambo si mazuri.John is gone too” akasema Mathew



TUKUTANE SEHEMUJAYO…
 
PENIELA SEASON 3


SEHEMU YA 9


ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

“ Peniela I’m sorry.He’s gone.John is gone”akasema Josh.Peniela akaishiwa nguvu na kuzirai.Haraka haraka akachukuliwa na kupelekwa kupatiwa huduma ya kwanza .Wakati Peniela akiendelea kupatiwa huduma ya kwanza simu ya Mathew ikaita.Alikuwa ni Anitha

“ hallow anitha.Nilikuwa katika harakati za kukupigia simu kukufahamisha mambo ya huku .Kuna habari gani hapo? Akaulzia Mathew
“ Dr Joshua amempigia simu Dr Kigomba muda si mrefu.Flaviana is gone.She’s dead.” Akasema peniela .Ilimchukua Mathew zaidi ya dakika moja kutamka lolote
“ How’s Elibariki?
“ ameishiwa nguvu.Nimempeleka chumbani kupumzika.”akasema Anitha

“ Ok Endelea kumpa uangalizi wa karbu sana.Huku nako mambo si mazuri.John is gone too” akasema Mathew



ENDELEA………………..



Kimya kikatawala halafu Mathew akasema
“ Anitha ,Jaji Elibariki na Penile ni watu wa muhimu sana .Kutokana na matatizo yaliyowakuta kwa pamoja kwa wote kuondokewa na watu wao wa muhimu inaweza kuwachukua muda ili waje kukaa sawa tena.Kutokana na suala zito linalotukabili hatuna huo muda wa kusubiri.Tunawategemea sana wao na hasa peniela kwa hiyo pamoja na uchungu walio nao lazima kila kitu kiende kama kilivyopangwa.Kwa maana hiyo jitahidi kwa kadiri uwezavyo kumtuliza jaji Elibariki ili aweze kurejea katika mstari na mimi hapa ninajitahidi nionane na peniela pindi akizinduka na niweze kumuweka sawa arejee katika mstari ili kifo cha John mwaulaya kisiathiri mipango yetu” akasema Mathew
“ Sawa nimekuelewa Mathew,lakini kwa namna Elibariki alivyostuka sina hakika kama anaweza akareja katika mstari hivi karibuni.Hata hvyo nitajitahidi kumuweka sawa.”
Wakati Mathew akionge ana Peniela ghafla kukatokea jambo Fulani lililomstua kidogo Mathew
“ Anitha nitakupigia simu baadae kidogo..” akasema Mathew na kukata simu.Macho aliyaelekeza katika kundi la watu zaidi ya kumi waliowasili pale hospitali.

“ Team SC41” akaongea mwenyewe kwa sauti ndogo.
“ Tayari wamekwisha pata taarifa za kufariki kwa kiongozi wao.hapa sintoweza tena kuipata nafasi ya kuongea na Peniela.” Akawaza Mathew na kumuona Josh amesimama mlangoni akamuita kwa ishara.
“ hallow Mathew” akasema Josh
“ Nikumbushe jna lako” Akauliza Mathew

“ naitwa josh”
“ Ok Josh.Ninahitaji sana kuongea na Peniela kuna jambo la muhimu nataka kumwambia lakini kutokana na mkanganyiko uliopo sintoweza kuonana naye kwa sasa .Ninakuachia maagizo pindi akizinduka mwambie kabla ya kufanya jambo lolote awasiliane kwanza na mimi” akasema Mathew

“ Sawa Mathew nitamweleza” akasema Josh na Mathew akaondoka zake.Gari alilolitumia kuja hospitali lilikuwa la peniela kwa hiyo ikamlazimu kuchukua taksi kurejea nyumbani.Wakati akielekea katika kituo cha taksi akachukua simu na kumpigia Eva
“ hallow Mathew” akasema Eva

“ Eva Uko wapi mida hii?

“ Kwa sasa ninajianda kutoka nyumbani kuelekea mizungukoni.Unahitaji kuniona?

“ Ndiyo Eva,.Nina shida nahitaji kukuona kama hutajali”
“ sawa Mathew.basi nenda kanisubiri pale ofisini kwangu,nakuja tuonane hapo.” Akasema Eva.mathew akakodisha taksi iliyompeleka hadi katika baa ya Eva ambako aliagiza supu ya kuku na kuanza kunywa akimsubiri Eva
“ Ninashindwa kupata jibu kwa nini mtu kama Rosemary Mkozumi ajihusishe katika jambo la hatari kama lile la kumuuzia nyaraka nyeti mtu ambaye ana mafungamano na vikundi vya ugaidi.? Je haelewi kilichomo ndani ya karatasi zile au ni tamaa tu ya fedha? Nitakula naye sahani moja lazima nihakikishe nimemtia mikononi na kuufahamu ukweli na atanieleza ukweli kwa nini anataka kufanya jambo la hatari kama lile.Ninaanza kupatwa na hisia kwamba yawezekana hata huyu mama naye akawa na mafungamano na vikundi vya ugaidi.Nitahakikisha nimeuchimba mtandao wake wote na hakuna atakayesalimika” akawaza Mathew na mara mawazo yake yakakatishwa baada ya kuliona gari la Eva
Eva mwandada mwenye nywele ndefu nyeusi zenye kung’aa akashuka toka ndani ya gari lake na kuanza kutembea kwa mwendo wake wa madaha kuelekea ofisini kwake.Mathew akainuka na kumfuata

“ karibu sana Mathew” Eva akamkaribisha Mathew ofisini kwake

“ Ahsante sana Eva”
“ sikuwa na ratiba ya kuja hapa asubuhi hii lakini imenilazimu kuja kwa ajili yako.Una tatizo gani Mathew?
“ Eva ahsante sana kwa kuahirisha shughuli zako na kuja kunisikia shida yangu.Nimekuja kuomba msaada wako tena.Kuna mtu ninahitaji kumpata ili nimuhoji anaitwa Rosemary Mkozumi”
Eva akastuka na kumtazama kwa sekunde kadhaa akasema

“ Rosemary mkozumi? Akauliza Eva kwa mshangao kidogo

“ Ndiyo”akajibu Mathw .Eva akashusha pumzi
“ Amefanya nini Rosemary?

“ Amejitokeza katikati ya jambo ninalolichunguza kwa hiyo basi ninahitaji kumfanyia uchunguzi naye pia.Kuna mambo ninayohuitaji kuyafahamukutoka kwake na kubwa ni kwamba ninataka kupata kumbu kumbu za mawasiliano kati yake na mtu mmoja raia wa Saudi Arabia anaitwa Habib soud”
Eva akamtazama Mathew kwa sekunde kadhaa na kusema

“ Mathew you are playing with fire my friend.Kwa sisi tunaomfahamu Rosemary Mkozumi tunaelewa kwamba huyu ni mwanamke hatari sana.Huyu aliwahi kuwa make wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania .Huyu ni mwanamke mwenye sura mbili.Katika jamii anafahamika sana kama mtetezi hodari wa haki za wanawake na amekwisha pewa tuzo nyingi kutokana na kuwa na mchango mkubwa katika kuchochea maendeleo ya wanawake nchini.Hii ni taswira nzuri sana aliyojijengea katika jamii.Upande wa pili wa Rosemary ambao wengi hawaufahamu ,ni mwanamke katili na hatari.Ana mtandao wake mkuwa wa watu hatari ambao wako tayari kufanya jambo lolote lile la hatari muda wowote.kwa sasa ninasikia tetesi kwamba ana mpango wa kutaka kugombea urais baada ya Dr Joshua kumaliza muda wake na kutokana na mtandao mkubwa alio nao kuna uhakika mkubwa akaweza kushinda uchaguzi.” Eva akanyamaza na kuendelea
“ Rosemary anatajwa kuwa na utajiri mkubwa sana na anatajwa kama mmoja wa watu matajiri wakubwa sana hapa nchini.Ninamfahamu vizuri mama huyu na ndiyo maana uliponiambia kwamba unataka kumchunguza nilistuka sana.She’s powerfull and very dangerous woman na kama unataka kumchunguza basi inakubidi ujiandae sana kwa lolote”akasema Eva
“ Eva ahsante sana kwa kunitahadharisha mapema kuhusiana na Rosemary na hata hivyo nilikwisha jiandaa toka awali kukabiliana naye kwa hiyo usihofu”akasema Mathew.Eva akabaki anamtazama bila kusema chochote

“ Eva are you going to help me or not?akauliza Mathew

“ Mathew sina sababu ya kukataa kukusaidia lakini ninajaribu kutafakari ombi lako ninashindwa kupata jawabu nitawezaje kufanya kazi hiyo.Rosemay kama nilivyosema ni mtu mwenye mtandao mkuwa na hata ndani ya idara ya usalama wa taifa ana watu wake wanaomsaidia katika mambo yake na ndiyo maana huwa ni vigumu sana kumchunguza huyu mama.” Akasema Eva

“ Ok sawa nimekuelewa Eva.basi nitakuomba kitu kimoja.Nisaidie niweze kuingia ndani ya nyumba yake ili nikafanye uchunguzi mimi mwenyewe.Kazi yako ni kunifanyia uchunguzi ni namna gani nitakavyoweza kuingia ndani ya nyumba ya Rosemary.” Akasema Mathew.Eva bado aliendelea kumtazama Mathew kwa makini

“Are you sure you want to do this Mathew” akauliza Eva

“ Eva katika dunia hii ninayemuogopa ni Mungu peke yake .Please find out how I will get in there “akasema Mathew
“ok Mathew nitajitahidi”akasema Eva

“ Ahsante sana Eva,nakutegemea sana” akasema Mathew na kuagana na Eva akaondoka



********

Baada ya kuondoka ofisini kwa Eva,Mathew akarejea nyumbani kwake

“ Elibariki yuko wapi? Akamuuliza Anitha

“ Yuko chumbani .” akajibu Anitha.Moja kwa moja Mathew akaelekea chumbani kwa jaji Elibariki akagoga mlango na sauti ya Elibariki toka ndani ikamruhusu aingie ndani.Jaji Elibariki alikuwa amekaa kitandani ,alionekana kuzama katika mawazo mengi sana.
“ Pole sana Elibariki.Jambo hili ni zito na limetustua sote”akasema Mathew

“ Ahsante sana Mathew” akajibu jaji Elibariki na kukaa kimya kidogo halafu akasema
" Mimi na Flaviana ndoa yetu ilikuwa na misuko suko mingi sana na kuna nyakati niliamini kwamba hakuwa mwanamke ambaye Mungi alonipangia niwe naye.Nilivumilia misukosuko yote kwa sababu nilikuwa nampenda sana.Nimeumizwa sana na kifo chake.Mathew siwezi kuongea sana lakini ninataka nikuombe jambo moja kwamba fanya kila uwezavyo na uhakikishe kwamba yeyote aliyehusika katika tukio hili anapatikana na analipa uovu wake.Can you promise me that? Akauliza jaji Elibariki
“ yes Elibariki.I promise you .Yeyote ambaye ana mkono wake katika kusababsha kifo cha Flaviana hatasalimika.Nitafanya kazi usiku na mchana na nitahakikisha wote wanatiwa nguvuni na kukutana na mkono wa sheria.kazi hii si rahisi na ninahitaji sana msaada wa watu wanaonizunguka.Anitha,wewe na Peniela ndiyo watu wangu wa karibu .Sote tumeumizwa sana na tukio hili lakini pamoja na uchungu wote tulio nao we have to focus what is ahead us.Mbele yetu kuna suala kubwa na zito.Tunatakiwa tuipate package muhimu sana na vile vile kuwatafuta na kuwapata wote waliosababisha kifo cha Flaviana ,kwa hiyo basi nitakuomba usimame imara na tupambane sote kwa pamoja” akasema Mathew

“ Mathew I’m deeply hurt .Siwezi kuelezea ni kwa kiasi gani nimeumizwa na jambo hili.Kibaya zaidi nikwamba siwezi hata kwenda kumuaga mke wangu katika safari yake ya mwisho.Siwezi kuhudhuria mazishi yake.Hii inaniumiza sana Mathew.Ninachoomba mniache kwa kwanza hadi hapo akili yangu itakapotulia lakini kwa sasa siwezi kufanya jambo lolote” akasema jaji Elibariki

“ Elibariki I know you are deeply hurt so do we all.Flaviana is gone and we need to pay back what they did to her.The only way to pay back is to stand up and fight.kwa hatua inayofuata sote lazima tuingie katika mapambano.So I need you to stop everything and get ready to fight” akasema Mathew na kumpiga piga jaji Elibariki mgongoni halafu akatoka na kuelekea ofisini ambako alimkuta Anitha

“Anitha naomba nisikie maongezi ya Dr Joshua na Kigomba aliyomtaarifu kuhusu kifo cha Flaviana”akasema Mathew.Anitha akafungua faili anakohifadhi maongezi yote ya Dr Kigomba yakaanza kusikikika
“ hallow Mr President” Ikaanza kusikika sauti ya Dr Kigomba
“ hallow Kigomba ,habari za huko?

“ habari za huku nzuri .Vipi huko,Flaviana anaendeleaje ?“ akauliza Dr Kigomba halafu kukawa kimya na baada ya muda ikasikika sauti ya Dr Joshua
“They tried all they could but they didn’t succeed .She passed away few minutes ago.”akasema Dr Joshua kwa masikitiko halafu kukawa na ukimya
“I’m so sorry Mr President for your loss” akasema Dr Kigomba halafu kukawa kimya tena.
“ Niliwasiliana na Hussein jana usiku na akaniambia kwamba tayari fedha imekwisha ingia yote katika akaunti.Ulifanya uhakiki? Akauliza Dr Joshua

“ Ndiyo Mr President.Nimewasiliana na benki leo asubuhi na wamenitumia barua pepe na kunihakikishia kwamba pesa yote imeingia .Katika akaunti ya kwanza kuna shilingi Trilioni tatu na bilioni mia nne na akaunti ya pili ina shilingi trilioni mbili na bilioni mia saba.Katika kiasi tulichokuwa tumekubaliana tayari wamekilipa chote kwa hiyo kilichobaki ni sisi kuwakabidhi mzigo wao”

“ sawa Kigomba.Nitawasiliana na hussen li tupange namna ya kuwakabidhi mzigo wao.Nimechoshwa na mambo yanayoendelea kutokea kila uchao.Biashara hii tayari imeingia mkosi .Mpaka sasa nimepoteza mke na mtoto ndani ya kipindi kifupi na wote wamepotea ili biashara hii iweze kufanikiwa.Imetosha sasa .Nataka tulimalize suala hili ili maisha yakaendelee.Vipi kuhusu jaji Elibariki kuna taarifa zozote kuhusiana na mahala alipo? Kuna chochote ulikigundua kwa Peniela? Akauliza Dr Joshua

“ Mpaka sasa bado sijafanikiwa kupata taarifa zozote za mahala aliko jaji Elibariki au hata kitu cha kuweza kumuunganisha na Peniela.Ninahisi chanzo kilichotokea taarifa kwamba jaji Elibariki amejificha kwa Peniela hakikuwa chanzo cha uhakika.” akajibu Dr Kigomba
“ Dr Kigomba.Tutaongea zaidi nitakaporejea kwani tunatarajia jioni ya leo kuwasili na mwili wa marehemu.Hatuna sababu ya kuendelea kukaa huku .Kwa hiyo anza kuandaa shughuli za msiba” akasema DrJoshua.
“ sawa mheshimiwa raisi ninaanza sasa hivi kushughulikia suala hilo.Kwa mara nyingine tena napenda kuchukua nafasi hii kukupa pole sana wewe na familia yako kwa msiba huu mkubwa”

“ Ahsante sana ninashukuru.Nitawasiliana nawe tena baadae kidogo kukupa taarifa zaidi.” Akasema Dr Joshua na kukata simu

“ Huyu mzee ana roho ya kishetani kabisa.Hana uchungu wowote na kifo cha mwanae anachowaza yeye ni pesa tu” akasema Anitha
“ Kamwe hatakuweza kufanikiwa katika mipango yake.kwa mujibu wa maelekezo aliyompa Dr kigomba inaonekana wanakaribia kufika mwisho wa biashara yao kwani tayari fedha zimekwisha ingizwa katika akaunti zao za siri walizozifungua nje ya nchi.Ni fedha nyingi sana ambazo wamelipwa.Ninajiuliza ni kitu gani hiki ambacho kinaweza kugharimu fedha nyingi kiasi hiki? Halafu katika maongezi yao kuna mtu ametajwa kwa jina moja tu la Hussein.Inaonekana huyu ndiye mnunuzi mkuu wa Package hiyo.Tungeweza kumfahamu huyo mtu ni nani ingeweza kuturahisishia kujua kile kilichomo ndani ya hiyo Package” akasema mathew

“ Sehemu pekee ya kuweza kumfahamu huyu Hussein ni nani ni kwa kuipata simu ya Dr Joshua na anayeweza kuifanya kazi hiyo ni Peniela pekee” akasema Mathew

“ Kwa tukio hili lililompata unadhani anaweza kuifanya kazi hii kwa ufanisi? Ulifanikiwa kuzungumza naye? Akauliza Anitha

“ Sikufanikiwa kuongea naye kama nilivyotaka kwani watu wa team SC41 waliwasil ghafla .hata hivyo nitajitahidi nionane naye ili nimpe hali halisi .Ninam……………….” Mathew akanyamaza baada ya simu yake kuita.Mpigaji alikuwa ni Eva

“ Hallow Eva” akasema Mathew
“ Mathew unaweza kuja hapa ofisini kwangu mara moja? Kuna jambo nataka tujadili kuhusiana na lile suala uliloniomba nikusadie” akasema Eva
“ Tayari kuna jambo umelipata?
“ Ndiyo Mathew.Tukutane ofisini kwangu” akasema Eva na kukata simu

“ Nilipotoka hospitali niilikwenda kuonana na Eva na nikamuomba anisaidie kutafuta namna ya kuweza kuingia ndani ya nyumba ya Rosemary Mkozumi .Mama huyu lazima tumfanyie uchunguzi tubaini kama ni kweli yeye ndiye kinara wa kutaka kuuza karatasi zile kwa mtu anayesaidikiwa kufadhili ugaidi.Nilipata pia maelezo mengine toka kwa Eva kwamba mama huyu ni hatari sana na ana mtandao mkubwa wa watu hatari unaojishughulisha na mambo mengi maovu.Tunaposhughulikia suala hili ni lazima tuuchimbe kwa undani mtandao huu hadi mzizi wake na wote wanaohusika tuwatie nguvuni.” Akasema Mathew
“ Nina hakika kwa simu hii ya Eva kuna jambo la msingi sana ambalo ameligundua.Ngoja nikaonane naye.Wewe endelea kumfuatilia Dr Kigomba na kama kuna jambo lolote la dharura utanitaarifu mara moja” akasema Mathew na kuondoka kuelekea kwa Eva

“ Wakati Elibariki akinikabidhi kazi hii sikutegemea kama ingeweza kuwa kubwa kiasi hiki.Kila uchao linaibuka jambo jipya na kulifanya suala hili kuzidi kuwa kubwa .Tayari maisha ya watu kadhaa yamekwisha potea kwa sababu ya suala hili na maisha ya mamilioni wengine yapo hatarini endapo kirusi kile kitatua katika mikono isiyo salama.” Akawaza Mathew wakati akielekea ofisini kwa Eva
“ Sikutegemea kama siku moja mimi na John Mwaulaya tunaweza kuongea kama marafiki kutokana na kitendo alichonifanyia.Nilikuwa na hasira kali juu yake na kwa miaka mingi nilikuwa ninaisubiri siku ya kulipiza kisasi lakini imekuwa tofauti na nilivyotegemea.Nimefanikiwa kuonana tena na John na katika dakika zangu za mwisho nimejikuta nikishindwa kutekeleza mpango wangu wa kulipiza kisasi.Hali yake nilivyoiona jana ilikuwa mbaya na mimi mwenyewe nikamuonea huruma .Alikiri kosa lake na nikakubali kumsamehe.John alinieleza mambo makubwa na mazito sana na ninapaswa kumshukuru sana kwa kunichagua mimi niyafahamu mambo yale.Amekufa na siri nyingi kubwa kubwa na laiti kama ningepata muda wa kutosha wa kuongea naye angeweza kunieleza mambo mengi makubwa zaidi lakini ninashukuru hata kwa hili alilonieleza.Kitu kingine kizuri ni kwamba katika dakika za mwisho za uhai wake alipata huduma ya kiroho na kama maandiko yanavyosema hata kama tukiwa na dhambi nyingi kiasi gani tukifanya toba ya dhati Mungu hutuondolea dhambi zote na kutufanya wapya tena.Mungu amrehemu na ampe pumziko la milele” akawaza Mathew wakati akikaribia sana kufika katika baa ya Eva


JOHN MWAULAYA ALIMWELEZA NiNI MATHEW? KWA NINI JAMBO ALILOAMBIWA LIMEBAKI KUWA SIRI YAKE? ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII……
 
LEGE tushushie nyingine
haina shida najitahidi kadri ya uwezo wangu kufidia na mkwazo nilio wakwaza mchana kwa kuwabania uhondo.

lkn naamini speed yangu sio mbaya sana wakuu sema ndio hivyo kwa kuwa story tamu na nzuri ndio maana ikiisha watamani utumiwe ujue mwishowake.
 
John jamaan kapumzike kwa amani umeshamehewa dhambi zako eli pole sana kwa kumpoteza mkeo alaf mathew kwa nn anawaficha wenzie alichoongea na john
 
haina shida najitahidi kadri ya uwezo wangu kufidia na mkwazo nilio wakwaza mchana kwa kuwabania uhondo.

lkn naamini speed yangu sio mbaya sana wakuu sema ndio hivyo kwa kuwa story tamu na nzuri ndio maana ikiisha watamani utumiwe ujue mwishowake.
Shukran kwa uungwana wako LEGE
 
Back
Top Bottom