**~** penzi la clara **~**

**~** penzi la clara **~**

Mwanakijiji nikurudishe nyuma kidogo.
ile story iliyokwisha ya 'MSALITI'
Inavyoanza inaonekana yule mwanaume msaliti alikuwa anasimulia.
Swali langu, alisimulia akiwa kaburini au? kwani inaonyesha aliuawa kwa kisu siku aliyofumaniwa so alipataje nafasi ya kusimulia?
story zako ni Kali sana mkuu.
Hongera sana bro.

Ndibalema Ni mwanadada ndio alikuwa akisimulia...ona aliulizwa huyo dada ulikuwa unafahamu!ambaye alikuwa anafanya mapenzi na mumeo!akajibu ni mama yake mzazi..that hata mie kwa kweli nilichoka...uhh mwanakijiji we I salute.
 
Ndibalema Ni mwanadada ndio alikuwa akisimulia...ona aliulizwa huyo dada ulikuwa unafahamu!ambaye alikuwa anafanya mapenzi na mumeo!akajibu ni mama yake mzazi..that hata mie kwa kweli nilichoka...uhh mwanakijiji we I salute.

Asante mkuu,
lakini mimi nilikuwa nazungumzia kuanzia mstari wa kwanza unapoanzia
ilianza hivi,

Nilihisi kuna mtu amesimama karibu na kochi nililokuwa nimejilaza. Ni ile hisia ambapo bila kuangalia nyuma unahisi kuna mtu anakunyemelea au kuna mtu anakuangalia na unapogeuka unakuta ni kweli. Nilikuwa nimejilaza chali kwenye kochi kubwa la rangi nyeusi huku Radhiya akiwa bado amekaa juu yangu. Shanga zake zikiwa zinaning'inia na kugusa kiuno changu. Kiunoni mwake alikuwa amejifunga kanga tu, tulikuwa tumeloa jasho, miili imechoka huku usingizi ukitupitia taratibu. Ilikuwa ni mara ya pili ndani ya saa moja tulifanya mapenzi ya nguvu.

Hisia hiyo ya mtu kuwa karibu ilinishtua mimi na kabla sijafanya lolote Radhiya naye alishtuka pia. Tulipofumbua macho yetu tulipigwa na butwaa la mwaka. Mke wangu Husna, alikuwa amesimama pembeni ya kochi tulilokuwa tumejilaza. Mkononi alikuwa ameshika kisu kikubwa chenye ncha kali kilichokuwa kinameremeta. Alikuwa amekunja uso wake, huku machozi yakimtoka na midomo ikimtetemeka. Kabla sijapata nafasi ya kusema Radhiya alijiondoa kwa nguvu na kuruka pembeni huku akishikilia kanga iliyokuwa ikimning'inia. Hakufanya ajizi alinyakuwa mkoba wake uliokuwa mezani na funguo za gari lake na kukimbilia mlangoni huku akijaribu kujisitiri na kanga yake. Alitoweka
 
Ndibalema Ni mwanadada ndio alikuwa akisimulia...ona aliulizwa huyo dada ulikuwa unafahamu!ambaye alikuwa anafanya mapenzi na mumeo!akajibu ni mama yake mzazi..that hata mie kwa kweli nilichoka...uhh mwanakijiji we I salute.

Busweluuu upoooo!! duh.. siku nyingi mkuu..
 
Love at first sight. Mrembo Clara macho kodo kwa kijana PJ.Wataalamu wenegine wamapenzi wanasema lobve at first sight ni nzuri na mara nyingi hudumu.Inapendeza mwanamkena mwanaume wakipendana kabla hata ya kutongozana,hii nido penzi la kweli,sio ile eti mpaka mwanamke atongozwe ndio afikirie kumpenda na yeye mtu huyo aliyemtongoza.Sij mwisho utakuwaje,Please Mwanakijiji usiwaachanishe hawa wapendanao ikizingatiwa kuwa huyu binti kajitunza vya kutosha..Waache waoane waishi kwenye ndoa ya amani na upendo.
 
Love at first sight. Mrembo Clara macho kodo kwa kijana PJ.Wataalamu wenegine wamapenzi wanasema lobve at first sight ni nzuri na mara nyingi hudumu.Inapendeza mwanamkena mwanaume wakipendana kabla hata ya kutongozana,hii nido penzi la kweli,sio ile eti mpaka mwanamke atongozwe ndio afikirie kumpenda na yeye mtu huyo aliyemtongoza.Sij mwisho utakuwaje,Please Mwanakijiji usiwaachanishe hawa wapendanao ikizingatiwa kuwa huyu binti kajitunza vya kutosha..Waache waoane waishi kwenye ndoa ya amani na upendo.


toba yarabiiii!!!!...
 
Shukran mkuu,hadithi ni nzuri mno. Nadhani itatupa funzo jema kadiri inavyoendelea. Kila la heri mkuu.
 
MM shukrani, una hadithi nzuri mno. Hivi iile ya kumbatio la mwenye makosa mboa sijamalizia? nimesoma chapters 4 tu mwenzio...napatwa wazimu kabisaa na hadithi zako.


SEHEMU YA KWANZA:

Tangu utotoni nilijuwa kuwa nimejaliwa uzuri wa maumbile na sura. Nikiwa mtoto wa kike wa pekee na wa mwisho wa Mzee Erasto Malyamkono (mtaani alijulikana kama Mzee Mswahili) nilikuwa nimedekezwa nikadekeka. Kaka zangu walikuwa wakinichunga utadhani mboni ya jicho vile, na hakuna kitu nilichotamani ambacho sikukipata. Nilijitahidi kuitunza heshima yangu na heshima ya familia hususan maswala ya wanaume. Nilimaliza kidato cha nne kule Bwiru Mwanza na baadaye kujiunga na shule ya Masista wa Damu Takatifu kule Kifungilo Lushoto. Hadi naanza kidato cha tano nilikuwa bado bikira.

Kabla ya hapo vijana wengi kule mtaani maeneo ya Isamilo walikuwa wakinitaka na kunifukuzia. Nawakumbuka kina Maiko, John, Almasi na Mugisha (alikuwa na umbo kubwa na kakichwa kidogo, utadhani hana shingo) wa pale magorofa ya Benki jinsi walivyokuwa wakinisarandia. Nilikuwa mcheshi na sikuwa na maringo yoyote. Yangu yalikuwa ni maneno na ahadi kem kem, lakini kuwavulia chupi la!! Nilikula vi pesa vyao vya sangara n(a kujinoma kwa tuzawadi twao.) Mademu wengi pale mtaani walinichukia sana, na hawakuficha wivu wao. Wengi waliokuwa wakinitaka walikuwa ni watoto wa wakubwa (miongoni mwao walikuwemo mtoto wa Jaji maarufu na mwingine alikuwa ni mtoto wa RPC). Namkumbuka mhindi mmoja ambaye naye alikuwa akinifukuzia ile mbaya. Nilijiona mimi ni malkia wa mbingu nikiitetemesha nchi kila nipitapo.

Ilikuwa ni huko Lushoto ndiko nilikopata kwa mara ya kwanza kuonja joto la mapenzi. Ilikuwa ni likizo ya pili ndipo nilipokutana na Petro J Shekitondo (Alipenda kuitwa PJ). Basi letu lilisimama pale Mombo kwa ajili ya kujipatia chakula kabla ya kuendelea na safari yetu hadi Moshi. Yeye alikuwa ni mfanyakazi katika Hoteli ya Usambara, mojawapo ya hoteli mashuhuri pale Mombo. Nilikuwa nimekaa kwenye meza moja na marafiki zangu wawili; Sakina Mwanakibili (mtoto wa Mbunge) na Grace Chambi (mtoto wa Katibu wa Wizara, ambaye boyfriend wake alikuwa Mbunge mmoja).

Tukiwa tunapeana gumzo, tulikatishwa mazungumzo yetu na kijana mrefu, aliyevalia suruali ya jeans na T-Shirt yenye maandishi ya “Daytona Beach” Kifuani. Alikuwa ni mtanashati na sote watatu tulijikuta tukipoteza mtiririko wa mawazo kwa sekunde.

“Habari zenu” Alitusalimia kwa sauti nzito yenye upole
“Powa” Tulimjibu kwa pamoja huku tukijifanya hatumjali “Mko tayari kuagiza chochote” Alituuliza tena akituangalia kwa kutupokeza.
“Tupe dakika chache” Nilisema kwa niaba ya wenzangu, ambao waliafiki kwani muda wote huo tulikuwa tukipiga gumzo wala hatukuaangalia ile menu ubaoni.
“Clara” Grace aliniita
“Nini” Nilimjibu
“Mbona unamuangalia kaka wa watu utadhani unataka kummeza!” Aliniambia
“Hamna kitu, nilikuwa mbali tu” Nilimjibu, laiti wangejua ni umbali gani nilikuwa!!
“aha!” Walihamaki wote wawili kana kwamba hawakuamini maneno yangu. Aliporudi tena alijitambulisha kwetu kwa jina na kuchukua oda zetu.

Tulikula kwa haraka haraka kwani tulianza kusikia honi ya basi letu ikianza kulia. Kama kawaida tuliangalia alipokaa dereva na demu mmoja wakila, hatukuwa na haraka. Tulipomaliza kula tulijiandaa kuondoka. Kabla hata hatujafika nje tukasikia mtu akituita.
“Samahani kina dada” Alikuwa ni PJ Shekitondo.
“Nini tena” Tulimuuliza tukishangaa labda tumesahau kitu.
“Dada wewe” akinionyesha mimi, “naomba nikuulize kitu” alisema. Tukasogea chemba. Akaja karibu yangu kiasi cha kusikia joto la mwili wake na akasogea kuninong’oneza jambo.
“Tangu uingie hapa hotelini macho yangu yalikuwa kwako, natamani tufahamiane” Aliniambia na sauti kakamavu ilivunja vunja kila vizuio nilivyokuwa navyo. Sikuamini kuwa mwanamme anaweza kunigusa kihisia namna hiyo.
“Mbona basi letu liko karibu kuondoka” Nilimjibu kwa aibu na kudengua kidogo
“Si unasoma Kifungilo” Alinijibu kumbe alishajua mimi ni Mwanafunzi.
“Umejuaje? Kwani tuna alama kwenye paji?” Nilimjibu kwa aibu.
“Nimeshawahi kukuona mlipokuja Mazinde Juu kwa debate” Alinijibu. Dereva wa basi alitoka nje na kuelekea kwenye basi. Nikajua nilazime niamue haraka.
“Sikiliza John” Nilimwambia, “Ninarudi tena shuleni mwezi ujao katikati, labda tuwasiliane wakati huo au vipi?” Nilimwambia.
“Poa tu” Alinijibu.

Alichukua kipande cha karatasi na kuandika namba yake ya simu na kuniambia kuwa siku nikiwa njiani kurudi nimpigie ili tukutane. Nilimwahidi kuwa nitampigia simu wakati nikirudi toka likizo. Nilikimbilia kupanda basi. Rafiki zangu waliniangalia kwa mshangao jinsi uso wangu ulivyong’ara kwa aibu na soni. Wakataka niwasimulie yaliyotokea. Nilisubiri kwa hamu siku ya kurudi toka likizo.

Itaendelea.... (hakikisha unarudi kusoma posti hii ya kwanza kwa mwendelezo)...
 
duh.. hii hadithi kwa kweli sitoweza kuiendeleza kwani itawaoffend baadhi ya watu.. hasa wenye misimamo mikali ya mapenzi; sorry guys.
 
duh.. hii hadithi kwa kweli sitoweza kuiendeleza kwani itawaoffend baadhi ya watu.. hasa wenye misimamo mikali ya mapenzi; sorry guys.

Duu,utakuwa hujatundea haki.Umetuonjesha utamu halafu utuachie njiani,sio fair kabisa..Tutakubaliana na hali,kwani maisha si ndio yalivyo?tupo tayari kwa vyoyote ulivyotunga.Tuendelezee hadithi hii tafadhali..
 
Jamani Mwanakijiji na hadithi zako hongera sana kazi nzuri..natamani siku moja uniazime kichwa chako

hhahha unataka kukocopy hadithi zote kwenye hard disk yako au flash? au uzisome hadithi zote....
 
duh.. hii hadithi kwa kweli sitoweza kuiendeleza kwani itawaoffend baadhi ya watu.. hasa wenye misimamo mikali ya mapenzi; sorry guys.

Lol Mwanakijiji vibaya hivyo mhhh umetupokonya tonge mdomoni:redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces::redfaces:
 
thijui ni "kiherehere" gani kilinifanya niitafute hii hadithi mweh.. maana.. hadi mwenyewe nimeona aibu.. maskini Da' Bupe!
 
duh.. hii hadithi kwa kweli sitoweza kuiendeleza kwani itawaoffend baadhi ya watu.. hasa wenye misimamo mikali ya mapenzi; sorry guys.
unabeep halafu ukipigiwa unakata lol

halafu mwanakijiji kuna shairi nimeliweka jaribu kupitia
 
Hivi wewe Mwanakijiji ukoje na wewe babu... ..nini maana ya hadithi ? hebu tuwekeee ubaoni kila mtu ana msimamo wake mkali kimapenzi hakuna anayetania ,
kwa nini unapokonya tinge mdomonijamani ?????????
 
Hivi wewe Mwanakijiji ukoje na wewe babu... ..nini maana ya hadithi ? hebu tuwekeee ubaoni kila mtu ana msimamo wake mkali kimapenzi hakuna anayetania ,
kwa nini unapokonya tonge mdomonijamani ?????????
 
Back
Top Bottom