Pesa za Escrow ni za umma au siyo za umma vs Pesa zilizotumika kuandaa filamu ya ROYAL TOUR (sh bilioni) 7 ni za umma au siyo za umma?

Pesa za Escrow ni za umma au siyo za umma vs Pesa zilizotumika kuandaa filamu ya ROYAL TOUR (sh bilioni) 7 ni za umma au siyo za umma?

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Mjadala ulijitokeza miaka iliyopita kuhusu pesa za Escrow zilikuwa za umma au siyo za umma. Waliokuwa wanasema si za umma kimsingi walikuwa wanatetea upigaji wake na serikali isiingilie.

Waliokuwa wanasema ni za umma walikuwa wanatetea maslahi ya umma ikizingatiwa kuwa zilikuwa zinahifadhiwa benki kuu na wajanja wakafanya mchongo wa kuzipiga na kutetea kuwa hamna shida maana siyo pesa za umma.

Hali kama hiyo imeanza kujitokeza hasa baada ya dalili za awali kuonesha kuwa mradi huo wa filamu ya The Royal Tour utaingiza pesa nyingi licha ya kuvutia watalii wengi. Watu wameanza kuhoji hizo pesa zinazoingizwa na filamu hiyo ni za serikali au?

Maandalizi ya kutoa jibu hilo tayari yanaonesha dalili kuwa kuna ujanja unatumika pesa hiyo kuingia mikononi mwa wajanja!! Kiongozi mkubwa kabisa wa serikali amesema, " Zile pesa sh bilioni 7 zilizotumika kuandaa filamu hiyo hazikutoka seikalini, bali serikali iliyachangisha mashirika (bila shaka ya umma na ya binafsi) ili kupata pesa hizo".

Tujiulize maswali mawili:

1. Kwanini kauli hiyo itoke sasa wakati watu wameanza kuhoji mapato ya filamu hiyo yataishia wapi na nchi yetu itafaidikaje?.

2. Ina maana serikali ikipata mapato kwa njia ya harambee (kwa hapa harambee ya mashirika), mapato hayo hayatakuwa ya serikali?

Inajulikana kuwa serikali hupata mapato yake kwa kuchangisha kwa mfano kodi. Kodi ni mchango, tofauti yake tu ni kuwa ni mchango wa kisheria kwa hiyo si wa hiari.

Niishauri serikali yetu kuwa jambo hili halijakaa vizuri na linafukuta moto, litakuja kuiweka serikali katika hali ngumu mbele ya safari.

Nashauri serikali itangaze rasmi tangu mwanzo kuwa mapato yatakayotokana na mauzo hayo NI YA SERIKALI.

Isisubiri kuangalia upepo nukoje, itakuja imweke MAMA kwenye kona na wenzake WATAMRUKA kimamba!

Karibuni tujadili.
 
Hata km za umma nyie wanyonge haziwahusu
Mtetezi wenu amekufa km mnampenda mkazikwe naye by zito
 
Wazo kuntu. Tatizo ni kuwa hawawezi kusikiliza maana shingo zao zimeishalemaa
 
Tunampongeza Rais wetu na washauri wake kwa jambo hili kubwa na LA kihistoria ktk nchi yetu kwa Rais wetu kuwa ndiye kiongozi Mkubwa wa film hii nzuri kwa taifa

Pili, Tunaitaka serikali kutolea ufafanuzi mzuri juu ya fedha zilizowezesha uandaaji wa Film hii ya the Loyal!

Kama pesa zilizotumika kuandaa filam hiyo si za umma, na kilichoandalia ni cha kitaifa.. Huu sio wizi mpya hapa?
 
Tunampongeza Rais wetu na washauri wake kwa jambo hili kubwa na LA kihistoria ktk nchi yetu kwa Rais wetu kuwa ndiye kiongozi Mkubwa wa film hii nzuri kwa taifa

Pili, Tunaitaka serikali kutolea ufafanuzi mzuri juu ya fedha zilizowezesha uandaaji wa Film hii ya the Loyal!

Kama pesa zilizotumika kuandaa filam hiyo si za umma, na kilichoandalia ni cha kitaifa.. Huu sio wizi mpya hapa?
[emoji1784][emoji1784][emoji1784][emoji1784]
Uandishi wa hovyo hovyo pamoja na mawazo ya hovyo hovyo!!

Mfano; Loyal, filam, kilichoandalia n.k
 
Mmeambiwa pesa walichangishwa wadau mbalimbali, alafu kuna mapimbi humu yanachekelea eti anaupiga mwingi kwa sinema kuingizwa Amazon alafu serikali itapata pesa.

Hii haina tofauti na zile mvua za kutungua au jenereta za iptl.
 
I bet this will be one of the biggest scandals to happen in our country because it involves the president directly.

One day we are going to be here stoning her for misusing public money for nothing.
 
Kwa hiyo mauzo ya filamu au pesa za mtaji wa filamu?maandishi mengi sijaelewa
 
Kwa hiyo mauzo ya filamu au pesa za mtaji wa filamu?maandishi mengi sijaelewa
Ni vyote! Kama mtaji wa filamu ukidaiwa siyo wa umma yaani mtaji si wa serikali, maana yake ni kuwa msingi umeandaliwa wa kusema hata hizo pesa za mauzo ya filamu si za umma yaani si za serikali!!
Kitu kilichotisha ni kuwa anayeshupalia kuwa pesa za mtaji hazikutoka serikalini ni kiongozi wa JUU SANA! Ila anasema serikali iliyachangisha mashirika kupata mtaji!! Sasa anachokataa ni kipi? Mfano rahisi: Yusufu akichangisha pesa, zile pesa zitakazopatikana ni za Yusufu, na atazitumia kwa malengo yaliyopelekea yeye kuchangisha pesa! Hali kadhalika serikali ikichangisha pesa kwa malengo fulani, hizo pesa ni za Serikali. Huwezi kusema eti pesa hizo hazijatoka serikalini!
 
Au ndio utaratibu wa kila mbuzi kula kulingana na urefu wa kamba yake?? Au ndio utaratibu wa KUJIPIMIA?
Kama kila mbuzi akila kulingana na urefu wa kamba yake, wote tumeshuhudia kamba ya mbuzi fulani ni ndeeeeefuuuu hadi marekani!! Si atavimbiwa mbuzi huyu!!!! Amejipimia kupita kiasi!!!! chonde chonde, huu utaratibu wa kujipimia HAPANA!!! Kila mtu apimiwe!!. Na kamba za mbuzi wengine ni ndefu sana zinafika mpaka kwenye mashamba ya watu wengine!! HAPANA!!
Ni vyote! Kama mtaji wa filamu ukidaiwa siyo wa umma yaani mtaji si wa serikali, maana yake ni kuwa msingi umeandaliwa wa kusema hata hizo pesa za mauzo ya filamu si za umma yaani si za serikali!!
Kitu kilichotisha ni kuwa anayeshupalia kuwa pesa za mtaji hazikutoka serikalini ni kiongozi wa JUU SANA! Ila anasema serikali iliyachangisha mashirika kupata mtaji!! Sasa anachokataa ni kipi? Mfano rahisi: Yusufu akichangisha pesa, zile pesa zitakazopatikana ni za Yusufu, na atazitumia kwa malengo yaliyopelekea yeye kuchangisha pesa! Hali kadhalika serikali ikichangisha pesa kwa malengo fulani, hizo pesa ni za Serikali. Huwezi kusema eti pesa hizo hazijatoka serikalini!
 
Wala haiwezi kuchukuliwa kuwa kiongozi wa serikali aliyeitisha huo mchango kwa ajili mtaji wa kuandaa filamu hiyo ya ROYAL TOUR kuwa alifanya hivyo kwa niaba yake yeye mwenyewe kama mtu binafsi! HAPANA. Maadili nya utumishi wa umma hayakubaliani na hilo. Ndiyo maana mtumishi wa umma haruhusiwi kupokea zawadi kwa huduma afanyayo kama mtumishi wa umma. Na kama akikubali kuipokea zawadi hiyo inakuwa ni mali ya umma. Ataiwasilisha ofisini kwa mkuu wake, ni mali ya umma hiyo. Tuko macho, hatutakubali kupigwa changa la macho hapa!
Ila tuwe wakweli, UBUNIFU HUU WA MAMA NI WA KUPONGEZWA SANA. Ila asikubali watu wampotoshe halafu mbele ya safari waje KUMRUKA!!
 
Kuna maswali kadhaa yanahitaji ufafanuzi wa kina toka serikalini:
1. Fedha iliyotumika ilikuwa ya umma au siyo ya umma? Hili ni swali la msingi.
2. Kama fedha iliyotumika siyo ya umma, yalichangishwa makampuni, mgawanyo wa mapato ya mauzo ukoje? Serikali (umma) inapata nini?
3. Kwa filamu kutumia rais wa nchi km mwigizaji mkuu (starring) mapato anayolipwa huyo rais ni personal au ni ya umma? Kwenye nchi za wenzetu chochote anachopewa rais akiwa madarakani, hata kama ni zawadi, huwa ni mali ya umma!
 
Kuna maswali kadhaa yanahitaji ufafanuzi wa kina toka serikalini:
1. Fedha iliyotumika ilikuwa ya umma au siyo ya umma? Hili ni swali la msingi.
2. Kama fedha iliyotumika siyo ya umma, yalichangishwa makampuni, mgawanyo wa mapato ya mauzo ukoje? Serikali (umma) inapata nini?
3. Kwa filamu kutumia rais wa nchi km mwigizaji mkuu (starring) mapato anayolipwa huyo rais ni personal au ni ya umma? Kwenye nchi za wenzetu chochote anachopewa rais akiwa madarakani, hata kama ni zawadi, huwa ni mali ya umma!
1. Ni ya umma kwa sababu inaenda kufanya mradi utakaoongeza mapato serikalini kupitia utalii na hata mauzo ya filamu yenyewe yataongeza kipato serikalini, ambayo ni mali ya umma.
2. Makampuni yalichangia kihisani tu kwa ajili ya kuisaidia serikali ambayo inafanya kazi kwa ajili ya umma, mgawanyo wa mapato ni kama mapato mengine ya serikali yanavyogawanywa.
3. Mshahara anaolipwa Rais ni personal au ni wa umma? Rais anapewa allowance kulingana na kazi aliyoifanya kwenye hiyo project ya Royal Tour na hizo pesa ni zake na na zitatumwa kwenye account yake binafsi. Hata kwenye hizo nchi za wenzenu nafikiri iko hivyo hivyo.
 
Wenyewe wanapita hapa kimya kimya huko wakisema "inaelakea kitumbua keshaingia mchanga hapa, tumekwama wapi?"
Niwaambie tu mtakwama sanas, watanzania wako macho!! Tambueni jinai haiozi!!
 
Wenyewe wanapita hapa kimya kimya huko wakisema "inaelakea kitumbua keshaingia mchanga hapa, tumekwama wapi?"
Niwaambie tu mtakwama sanas, watanzania wako macho!! Tambueni jinai haiozi!!
 
Wabongo tatizo lao ni kutanguliza maslahi binafsi mbele bila kujali athari kwa taifa.
 
Back
Top Bottom