Pesa za REA zianze kupelekwa kwenye gesi ya kupikia ili vijijini nao waanze kutumia gesi badala ya kuni na mkaa

Pesa za REA zianze kupelekwa kwenye gesi ya kupikia ili vijijini nao waanze kutumia gesi badala ya kuni na mkaa

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
Pesa za REA zianze kupelekwa kwenye gesi ya kupikia ili vijijini nao waanze kutumia gesi badala ya kuni na mkaa.

Inawezekanaje? PESA za REA zielekezwe kwenye ruzuku ya gesi.

Takwimu zinasema umeme umeenda nchi nzima vijiji kibao vijiji vichache tu vimesalia kupata umeme

Pesa za REA sasa zipelekwe kwenye gesi ya kupikia.
 
Mimi ni pro-government kwa 100%, ila Kuna baadhi ya sehemu tuache tu kwanza.

Gesj hii mnayozungumzia kumbuka tunaiagiza nje, hatuizalishi hapa nyumbani

Pili, kwa wwatu wa vijijini Cha kwanza ni maisha yao kubadilika alafu ndio tuje na gesi.
Vinginevyo tutakua tunampigia mbuzi gitaa

Ni sawa na kwenda kufungua yard ya magari vijijini ili kuwahamasisha watumie magari badala ya baiskeli.
 
Mimi na wewe ni pro government, Ila kwenye hili mimi naona Kuna sehemu halipo sawa.

Njoo hapa tufanye mjadala, uniambie kwa nn unaunga mkono hili
Anyway mimi sio huyo uliyemuuliza kwa hiyo vijiji vyote vikifikiwa na miradi ya REA hizo pesa za REA tunachangia kila tukinunua mafuta au gesi au umeme unataka ziende wapi kulipa posho na mishahara ya wafanyakazi wa Tanesco au? Au unataka zifutwe once vijiji vyote vikipata umeme ,mission accomplished no need of any other Rural project? Tozo zifutwe?
 
Pesa za REA zianze kupelekwa kwenye gesi ya kupikia ili vijijini nao waanze kutumia gesi badala ya kuni na mkaa.

Inawezekanaje? PESA za REA zielekezwe kwenye ruzuku ya gesi.

Takwimu zinasema umeme umeenda nchi nzima vijiji kibao vijiji vichache tu vimesalia kupata umeme

Pesa za REA sasa zipelekwe kwenye gesi ya kupikia.
Unaposema vijijini unaapajua lakini? unajua vipato vyao? mtu anunute mtungi mdogo wa 35,000 wakati chakula cha kukipika kwenye hiyo gesi ni mtihani? Hizo pesa wanataka kuzipiga tu na si vinginevyo
 
Anyway mimi sio huyo uliyemuuliza kwa hiyo vijiji vyote vikifikiwa na miradi ya REA hizo pesa za REA tunachangia kila tukinunua mafuta au gesi au umeme unataka ziende wapi kulipa posho na mishahara ya wafanyakazi wa Tanesco au? Au unataka zifutwe once vijiji vyote vikipata umeme ,mission accomplished no need of any other Rural project? Tozo zifutwe?
Na sasa tuanze kupaza sauti wapunguze ile asilimia tatu wabakishe asilimia moja tu. Kwa kweli wanatuonea sana.
 
Mimi ni pro-government kwa 100%, ila Kuna baadhi ya sehemu tuache tu kwanza.

Gesj hii mnayozungumzia kumbuka tunaiagiza nje, hatuizalishi hapa nyumbani

Pili, kwa wwatu wa vijijini Cha kwanza ni maisha yao kubadilika alafu ndio tuje na gesi.
Vinginevyo tutakua tunampigia mbuzi gitaa

Ni sawa na kwenda kufungua yard ya magari vijijini ili kuwahamasisha watumie magari badala ya baiskeli.
Maisha kubadilika ni pamoja na huduma bora na nafuu za nishati.
Umeme, gas.
Pia maji salama
 
Mimi na wewe ni pro government, Ila kwenye hili mimi naona Kuna sehemu halipo sawa.

Njoo hapa tufanye mjadala, uniambie kwa nn unaunga mkono hili
Nipe hoja zako kwa nini unapinga hili then na mimi nikupe hoja zangu kwa nini naliunga mkono?
 
Anyway mimi sio huyo uliyemuuliza kwa hiyo vijiji vyote vikifikiwa na miradi ya REA hizo pesa za REA tunachangia kila tukinunua mafuta au gesi au umeme unataka ziende wapi kulipa posho na mishahara ya wafanyakazi wa Tanesco au? Au unataka zifutwe once vijiji vyote vikipata umeme ,mission accomplished no need of any other Rural project? Tozo zifutwe?
Hata wewe ni sawa, upo tayari tufanye mjadala na hili?
Makato ya REA ni kweli yanasaidia kupeleka miundombinu ya umeme vijijini, japo hayatoshi moja kwa moja. Kumbuka hapa ni kupeleka miundombinu tu sio kuchangia gharama za matumizi yao ya umeme.

Matumizi yao ya umeme hatuyachangii, ndio maana unaona hawawezi kumudu kutumia umeme kupikia badala ya kuni

Kumbuka huu umeme tunazalisha wenyewe hapahapa, lakini bado hawawezi kumudu kuutumia kupikia.

Vipi wataweza gesi ambayo tunainunua kutoka nje ya nchi? Kumbuka tena kuwa unachonunua kutoka nje ya nchi huna control nacho

Mwisho kabisa REA tunaichangia 3% tu ambayo kwa mujibu ya mapato ya Tanesco kutokana na matumizi ni around bil 40 kwa mwaka.
Bil 40 utawezw kusaidia matumizi gani ya gesi vijijini? Achilia mbali tu mjini

Nakaribisha mjadala
 
Unaposema vijijini unaapajua lakini? unajua vipato vyao? mtu anunute mtungi mdogo wa 35,000 wakati chakula cha kukipika kwenye hiyo gesi ni mtihani? Hizo pesa wanataka kuzipiga tu na si vinginevyo
Kuna watu nahisi kama kichwani zimeruka kidogo. Chakula tu cha kupika hata kwenye kuni tu hawana uhakika nacho.
Leo ndio aje kuweza kununua gesi kila inapoisha
 
Maisha kubadilika ni pamoja na huduma bora na nafuu za nishati.
Umeme, gas.
Pia maji salama
Gesi ni nishati nafuu??
Maji? Unajua watanzania nusu yetu hatupati maji ya bomba? Na haya maji ni ambayo tunaweza kuyavuta mtoni au ziwani au kuchimba visima, lakini bado watu wameshindwa.

Karibu kwenye mjadala, lakini huku ukiwa unafahamu nusu ya watanzania ni maskini wa kutupwa kwa mujibu wa benki ya dunia. Watu ambao hawana uhakika hata wa chakula Cha kupikia kwenye hizo kuni, leo wataweza gesi?

Karibu kwa mjadala
 
Nipe hoja zako kwa nini unapinga hili then na mimi nikupe hoja zangu kwa nini naliunga mkono?
Sipingi kwa maana isije kufanyika kabisa hapana, napinga kwa sababu ya muda huu tuliopo

Tuendelee kufanya miradi mingi ya kukuza uchumi wa wananchi, alafu tuje kwenye hili la nishati ya gesi na umeme kwa matumizi ya kupikia.

Watanzania nusu ni maskini sana kwa mujibu wa data za bank ya dunia, hapa wanazungumzia wale ambao hawawezi hata kupata milo.mitatu kwa siku. Hawa wananchi asilimia kubwa wanaishi vijijini, ikiwa kupata mlo tu wa uhakika ni shida, leo wataweza kutumia gas ambayo watainunua ili kupikia ikiwa kuni anaziokota bure?

Ukiachana hao wa vijijini, sisi tu ambao tuna ajira na tupo mijini lakini gas imetushinda kutumia kupikia, tunatumia mkaa na gas ili kuifanya gas iweze hata kufikisha mwezi.
 
Sipingi kwa maana isije kufanyika kabisa hapana, napinga kwa sababu ya muda huu tuliopo

Tuendelee kufanya miradi mingi ya kukuza uchumi wa wananchi, alafu tuje kwenye hili la nishati ya gesi na umeme kwa matumizi ya kupikia.

Watanzania nusu ni maskini sana kwa mujibu wa data za bank ya dunia, hapa wanazungumzia wale ambao hawawezi hata kupata milo.mitatu kwa siku. Hawa wananchi asilimia kubwa wanaishi vijijini, ikiwa kupata mlo tu wa uhakika ni shida, leo wataweza kutumia gas ambayo watainunua ili kupikia ikiwa kuni anaziokota bure?

Ukiachana hao wa vijijini, sisi tu ambao tuna ajira na tupo mijini lakini gas imetushinda kutumia kupikia, tunatumia mkaa na gas ili kuifanya gas iweze hata kufikisha mwezi.
Hapana wakati ni sasa

Hata hiyo miradi ya Gesi itakuza uchumi

Kwa mujibu wa TPDC kwa gesi inayochimbwa tu Songosongo na Mnazi Bay haitumiki ipasavyo! Na mbaya zaidi nishati ya kuni inaiweka nchi kwenye hatari kubwa zaidi ya kugeuka jangwa!

Ukitembea maeneo mengi ya Tanzania kama ni mtu mwenye uelewa wa mambo utagundua hii nchi miaka si mingi sana tutaanza kuzalisha chakula pungufu na kukosa hata mvua za kujaza mabwawa yetu ya umeme kwa ukataji wa miti wa kutisha unaoendelea kwa sababu ya matumizi ya kuni na mkaa
 
Hapana wakati ni sasa

Hata hiyo miradi ya Gesi itakuza uchumi

Kwa mujibu wa TPDC kwa gesi inayochimbwa tu Songosongo na Mnazi Bay haitumiki ipasavyo! Na mbaya zaidi nishati ya kuni inaiweka nchi kwenye hatari kubwa zaidi ya kugeuka jangwa!

Ukitembea maeneo mengi ya Tanzania kama ni mtu mwenye uelewa wa mambo utagundua hii nchi miaka si mingi sana tutaanza kuzalisha chakula pungufu na kukosa hata mvua za kujaza mabwawa yetu ya umeme kwa ukataji wa miti wa kutisha unaoendelea kwa sababu ya matumizi ya kuni na mkaa
Wengi hili suala la gesi hamjalijua vizuri. Tanzania tunazlisha CNG, hatuzalishi LPG(hii mitungi ya kupikia).
CNG kuigeuza kuwa LPG ni ngumu na gharama na ni hatuwezi kabisa.
Option iliyopo ni kutumia mabomba kupitisha hii CNG ili iweze kutumika direct. Mradi wa kujenga mabomba kwa nchi nzima hadi vijijini ni gharama na ni ngumu sana, nadhani unakumbuka mradi wa bomba la gesi mtwara tulitumia tril 2.4 na zilikua za mkopo ambao hadi leo haujaisha. Hii CNG yenyewe ni kitendawili maana sio yetu tunainunua kutoka kwa hao wawekezaji

Hapo ni kutoka mtwara kuja dar, vipi kutoka mtwara kwenda Bukoba, kigoma, mwanza, katavi, Tabora, geita n.k tena mabomba yafike kila Kijiji. Ni trillions ngapi hizo zitakua?? Na pia hata hii CNG yenyewe nayo tunainunua kutoka kwa wawekezaji

Ndio maana tunanunua hii LPG(mitungi) kutoka nje, na hasara yake ni Kama unavyoona kwenye mafuta, ni ngumu kucontrol bei na upatikanaji. Ambapo watu wataendelea bado kutumia mbadala kwa kuwa ni rahisi na unapatikana(mkaa na kuni).

Unasema miti inaisha? Ni kweli inaisha, Ila kwenye hili kwanza ningeishauri serikali kusitisha tena biashara ya magogo maana imeanza tena na yanasafirishwa nje ya nchi.

Lakini kwa watu wa vijijini kwa umaskini huu uliopo, na hayo niliyokueleza unafikiri watakuwa na laki 1 kila mwezi ili kutumia gesi? Ikiwa tu chakula ni shida kukipata? Wafanyakazi hawa tu wa serikali wenye mishahara huo ubavu hawana
 
Kuna watu nahisi kama kichwani zimeruka kidogo. Chakula tu cha kupika hata kwenye kuni tu hawana uhakika nacho.
Leo ndio aje kuweza kununua gesi kila inapoisha
Mkuu labda mtungi ukiwaishia

Watajaziwa bure....

Ova
 
Back
Top Bottom