Peter Kibatala Wakili wa CHADEMA, Mungu akubariki sana

Peter Kibatala Wakili wa CHADEMA, Mungu akubariki sana

Memento

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2021
Posts
4,423
Reaction score
9,986
Tumezoea kuona watu wakitoa sifa nyingi mtu anapokufa, lakini ninaomba sifa nizitoe mtu akiwa hai.

Mara nyingi nimeona wakili Kibatala akipanda mahakamani kwenye kesi za viongozi wa chadema, analipwa au halipwi hio sijui na hainihusu.

Lakini kitendo tu cha kukubali kusimamia kesi za upinzani kwenye nchi kama hii ambayo inaendeshwa kibabe ni kitendo Cha kishujaa sana.

Angeweza tu kuwa wakili wa serikali au wakili wa kujitegemea na mambo yakaenda, ila Hilo amelikataa.

Yote tisa, kumi ni tukio la leo kisutu ambalo limeniacha mdomo wazi baada ya kumuona wakili Kibatala akitoka mahakamani na kwa mbele akaona gari ya polisi imembeba mmoja wa watu waliokamatwa kwa kubeba mabango.

Kibatala aliifata ile gari ya polisi bila woga na kumuambia yule mtu kuwa asiwe na wasiwasi, wapo pamoja na atamuwekea dhamana. Hivyo atulie atahakikisha anatoka kwa dhamana kwani kubena bango sio kosa.

Ipo hivi, kutokana na kuwa busy siku ya jana na leo, wakili Kibatala angeweza kupita tu kimya bila kumfuataa yule mtu na maisha yakaendelea.

Fikiria tu Kibatala hamfahamu huyo Mtu, na wala huyo Mtu hana uwezo wa kumlipa Kibatala Ila Kibatala ameamua tu kumsaidia bure kabisa.

Ni watu wachache Sana wenye huu moyo.

Kwa kitendo hiki Cha Kibatala ninaomba mnaokuwa nae karibu mtieni moyo sana kwa anayofanya, ni Mtu wa muhimu Sana.

Mtieni moyo Kibatala, mtieni moyo jamani

Screenshot_20210805-153153_1.jpg
 
Ndege zanunuliwa kwa kodi za wananchi na huku hospitali hazina dawa, watoto wetu wanasomea chini bila sakafu na wengine chini ya miti.Kwa maana hiyo,hedge sio kipaumbele cha walipa kodi wengi.
Ndege badala ya hedge
 
Tumezoea kuona watu wakitoa sifa nyingi mtu anapokufa, lakini ninaomba sifa nizitoe mtu akiwa hai.

jamani
Una ushahidi gani kuwa atamsaidia bure? Asikudanganye mtu Kibatala ni miongoni mwa wanufaika wakubwa wa SACCOS ya Mbowe. Kila kesi analipwa kiasi kikubwa sana. Kumfuata huyo unayemsema ni yeye kukimbilia mteja ili apate kazi.

Ni sawa tu na wamachinga wanavyokimbilia wateja barabarani. Na yeye amekimbilia mteja. Jiongeze mzee, watu wanapiga pesa kupitia matatizo yako.
 
Una ushahidi gani kuwa atamsaidia bure? Asikudanganye mtu Kibatala ni miongoni mwa wanufaika wakubwa wa SACCOS ya Mbowe. Kila kesi analipwa kiasi kikubwa sana. Kumfuata huyo unayemsema ni yeye kukimbilia mteja ili apate kazi. Ni sawa tu na wamachinga wanavyokimbilia wateja barabarani. Na yeye amekimbilia mteja. Jiongeze mzee, watu wanapiga pesa kupitia matatizo yako.
Ni mtazamo wako,ila ulioegemea upande usio wa kupenda haki.
 
Ndege zanunuliwa kwa kodi za wananchi na huku hospitali hazina dawa, watoto wetu wanasomea chini bila sakafu na wengine chini ya miti.Kwa maana hiyo,hedge sio kipaumbele cha walipa kodi wengi.
Ugaidi ni kipaumbele cha walipa kodi?
 
Una ushahidi gani kuwa atamsaidia bure? Asikudanganye mtu Kibatala ni miongoni mwa wanufaika wakubwa wa SACCOS ya Mbowe. Kila kesi analipwa kiasi kikubwa sana. Kumfuata huyo unayemsema ni yeye kukimbilia mteja ili apate kazi. Ni sawa tu na wamachinga wanavyokimbilia wateja barabarani. Na yeye amekimbilia mteja. Jiongeze mzee, watu wanapiga pesa kupitia matatizo yako.
Ni sahihi ila ana ziada ya ubinadamu kuliko pesa.Mawakili wengine husikia huyo mchovu
 
Una ushahidi gani kuwa atamsaidia bure? Asikudanganye mtu Kibatala ni miongoni mwa wanufaika wakubwa wa SACCOS ya Mbowe. Kila kesi analipwa kiasi kikubwa sana. Kumfuata huyo unayemsema ni yeye kukimbilia mteja ili apate kazi. Ni sawa tu na wamachinga wanavyokimbilia wateja barabarani. Na yeye amekimbilia mteja. Jiongeze mzee, watu wanapiga pesa kupitia matatizo yako.
Hata kama analipwa si haki yake? Sasa ulitaka huyo mwananchi asitetewe?
 
Tumezoea kuona watu wakitoa sifa nyingi mtu anapokufa, lakini ninaomba sifa nizitoe mtu akiwa hai.

Mara nyingi nimeona wakili Kibatala akipanda mahakamani kwenye kesi za viongozi wa chadema, analipwa au halipwi hio sijui na hainihusu.

Lakini kitendo tu cha kukubali kusimamia kesi za upinzani kwenye nchi kama hii ambayo inaendeshwa kibabe ni kitendo Cha kishujaa sana.

Angeweza tu kuwa wakili wa serikali au wakili wa kujitegemea na mambo yakaenda, ila Hilo amelikataa.

Yote tisa, kumi ni tukio la leo kisutu ambalo limeniacha mdomo wazi baada ya kumuona wakili Kibatala akitoka mahakamani na kwa mbele akaona gari ya polisi imembeba mmoja wa watu waliokamatwa kwa kubeba mabango.

Kibatala aliifata ile gari ya polisi bila woga na kumuambia yule mtu kuwa asiwe na wasiwasi, wapo pamoja na atamuwekea dhamana. Hivyo atulie atahakikisha anatoka kwa dhamana kwani kubena bango sio kosa.

Ipo hivi, kutokana na kuwa busy siku ya jana na leo, wakili Kibatala angeweza kupita tu kimya bila kumfuataa yule mtu na maisha yakaendelea.

Fikiria tu Kibatala hamfahamu huyo Mtu, na wala huyo Mtu hana uwezo wa kumlipa Kibatala Ila Kibatala ameamua tu kumsaidia bure kabisa.

Ni watu wachache Sana wenye huu moyo.

Kwa kitendo hiki Cha Kibatala ninaomba mnaokuwa nae karibu mtieni moyo sana kwa anayofanya, ni Mtu wa muhimu Sana.

Mtieni moyo Kibatala, mtieni moyo jamani


Mathayo 5 kwa ujumla wake ina

“...Heri yenu nyinyi watu wakiwatukana, wakiwadhulumu na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa ajili yangu. Furahini na kushangilia maana tuzo lenu ni kubwa mbinguni. ..."

Yamhusu sana mtumishi wa Mungu kama bwana Peter Kibatala.
 
Back
Top Bottom