Kigoma haikuwahi kuwa sehemu ya Burundi, Kigoma ilipaswa kuwa nchi kamili kama ilivyo Rwanda na Burundi. Kigoma Ina eneo lake linalotambulika, Ina watu ambao ni waha wenye mila zao na tamaduni zao zinazotofautiana kidogo sana na Rwanda na Burundi.
Kigoma ni moja ya mikoa au majimbo yaliyoshirikishwa kikamilifu kuunda Jamuhuri ya Tanganyika. Kukubali kwa Kigoma kuachana na Utawala wake wa kichifu "Mwami" na kukubaliana na Nyerere kuunda Tanganyika na kuuzika ukabila ndio ulioiponza Kigoma ambayo hadi leo watu wake wanatengwa na kubaguliwa ndani ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Watu wasiojua historia ya taifa hili ndio wanaoeneza propaganda za kipuuzi kuwa Kigoma irudi Burundi, kwa bahati mbaya sana watu wa aina hiyo ndio walioajiriwa Serikalini "Uhamiaji" na wanaendeleza ubaguzi unaoweza kuligawa taifa.
Inashangaza sana, Rais wetu ana nasaba na waarabu lakini hakuna anaepaaza sauti kuhoji uhalali wake kuwa Rais, lakini muha wa Kigoma kuonekana kwenye eneo lake ndani ya Afrika ni kosa linalostahili kifo ? Hii dhambi ya kubaguana ndani ya JMT itakuja kupata majibu siku za usoni kama haya yanayotokea sasa kule Gaza, kati ya waisrael na wapalestina.