Petition: Susia Azam TV, susia CECAFA challenge cup

Ha ha ha, madhira wanayopata hayafai ndo maana mataifa mengi yanalaani maana hata ile ya wahamiaji haramu ulaya wengine walikuwa na watetezi tena wazungu
 
ukitaka ujue inferiority complex ya watu weusi ni kupitia comments za hapa,kina nyerere walivyowasusia south africa hadi wakatengwa kwenye michezo walikuwa wajinga sio?
Yaani unashindwa kutofautisha kati ya ilivyokuwa South Africa na ilivyo Libya?!

South Africa ulikuwa ni mfumo rasmi wa serikali!

Kinyume chake, kinachotokea Libya ni matunda ya taifa kuparaganyika kutokana na vita!

Mataifa mengi yakitoka vitani yanipitia kipindi cha mpito na kugeuka kuwa magenge ya wahalifu wa aina mbalimbali!

Sote sisi tumeshuhudia Somalia ikigeuka kuwa makazi ya magenge ya magaidi na maharamia wateka meli! Iraq na Afghanistan tumezishuhudia zikigeuka kuwa makazi ya magenge ya kigaidi na wauza mihadarati! Hata vita kwenye Ukanda wa Maziwa Makuu uliacha magenge ya wauza silaha ambazo zilitapakaa hadi Tanzania!

Kwa staili ile ile; Libya nayo ikageuka kuwa pepo ya magenge ya wahalifu wanaofanya human trafficking to Europe!!

Ni hawa human traffickers ndio wanaoendesha hizo biashara haramu za kuuza watu!

Sasa unadhani hiyo mifano unayotoa inasadifu na kilichopo Libya?!
 
KWA JIBU LA UBALOZI WA LIBYA TANZANIA HAPO JANA,BADO UTAKUWA NA HII HOJA YAKO?HALAFU KAMA HAWA WATU NI CONTROVERSIAL KULIKUWA NA HAJA GANI YA CECAFA KUWAITA,AZAM TV KAMA MAIN SPONSOR HAWAWEZI KUWAAMBIA KWAMBA A LOT OF PEOPLE ARE UNEASY WITH LIBYA PRESENCE?
 
Taarifa ya Balozi wa Libya ina sehemu mbili... kwanza, wameelezea wanachofahamu wao kuhusu ile minada na sehemu yao ya pili wakasema ikiwa yanayosemwa itathibitika, wahusika watachukuliwa sheria kwa mujibu wa sheria za Libya!

But all in all, yote hayo hayafuti hoja yangu kwamba mifano unayotoa kulinganisha Libya vs Israel or Libya vs South Africa (ya Makaburu) ni mifano isiyoendana! Kilichhopo Libya ni kusambaa kwa magenge ya uhalifu yaliyotokana na nchi hiyo kuwa vitani!

Kama ni ukandamizaji, ukandamizaji huo kwa Israel unafanywa au ulikuwa unafanywa na serikali na sio magenge ya kihalifu! Kama ni ukandamizaji, uonevu, ubaguzi n.k wakati wa Afrika ya Kusini ya Makaburu; hayo hayakuwa yakifanywa na magenge ya kihalifu bali na serikali!

Libya, haipo hivyo! Serikali yenyewe bado haipo stable. Magenge ya wahalifu yamejaa kila kona ya Tripoli kiasi kwamba hata the so called government hadi leo haijisikii salama!

CNN, ambao ndio watu wa mwanzo kuiweka taarifa ya biashara ya utumwa waliandika
But a recent clampdown by the Libyan coastguard means fewer boats are making it out to sea, leaving the smugglers with a backlog of would-be passengers on their hands.

So the smugglers become masters, the migrants and refugees become slaves.
Hapo unaona ni shughuli inayofanywa na magenge ya kihalifu!!! Lakini kwanini Magenge ya kihalifu yanaachwa yatambe kiasi hicho?

Serikali ya Uingereza ikitoa ripoti kwa raia wake kiasi cha wiki mbili tu zilizopita hivi ndivyo wanasema: Hapo unaambiwa uwepo wa wanamgambo waliojihami kwa silaha kila mahali! I hope unafahamu kwamba wanamgambo huwa hawawajibiki kwa serikali lakini hiyo inaonesha ni namna gani serikali yenyewe isivyo na full control over Libya!!!

Uingereza wanaendelea: Hivi nchi kama hiyo utasema serikali ina control?!

Kila pahala kuna magenge ya wahalifu wenye silaha! Sasa unadhani ni sahihi kuiadhibu Libya kwa mambo yanayotokea nchini mwao wakati hata wao wenyewe hawana control nayo?!

That's one but two; hivi unaamini kabisa hayo magenge ya kihalifu yana time na siasa za CECAFA?! Unaamini hayo magenge yatapata athari yoyote?!

Kwanini tugeukie kwenye unproductive solutions wakati solutions inaonekana kabisa ipo vidoleni mwetu! Mosi, serikali zetu kujenga nchi zao ili vijane wasiwe wanajiripua kupitia safari za hatari namna hii na pili, ambayo ni very immediate solution, serikali zenye raia wake kule ifanye hima kuwarudisha kwa sababu wapo stranded between the crossfire!
 
watawachukuliaje hataua kwa sheria za libya kama serikali haipo incharge ya nchi? sasa swali langu ni kwanini Cecafa waialike Libya??issue hii ni controversial kweli imeshindikana kuwaleta Angola au Togo au Guinea hata gambia? why Libya???
 
watawachukuliaje hataua kwa sheria za libya kama serikali haipo incharge ya nchi?
Kumbe ulitarajia aseme nini?!
sasa swali langu ni kwanini Cecafa waialike Libya??issue hii ni controversial kweli imeshindikana kuwaleta Angola au Togo au Guinea hata gambia? why Libya???
Watu wanaamini soka inaleta mahasimu pamoja! Soka inaweza kutumika kuponya vidonda vya uhasama. Soka na michezo kwa ujumla ni alama ya umoja bila kujali rangi, dini wala jinsia!!

Na ni kutokana na ukweli huo ndio maana, pamoja na minyukano ya CCM na upinzani, inafika wakati wabunge wa pande mbili wanasakata soka! Pamoja na minyukano ya kidini nchini mwetu, lakini sio ajabu kusikia kuna mechi kati ya masheikh na mapadri!

Hiyo ndiyo soka!!

Si ajabu hata kidogo kuona team ya Libya, kuanzia wachezaji hadi viongozi; miongoni mwao si ajabu ni pro-government na miongoni mwao si ajabu ni wafuasi wa Waasi na Magaidi!! CECAFA inataka kuwaleta wote hawa pamoja kwa sababu hiyo ndiyo soka! Hiyo ndiyo michezo.

Soon baada ya South Africa kutokomeza ubaguzi wa rangi, michuano mikubwa ikapelekwa SA. Michuano ya kwanza ilikuwa Rugby World Cup! South Africa wakachukua kombe! Michuano ya pili ilikuwa Mataifa huru ya Afrika! Ukweli ni kwamba Afrika Kusini hawajui mpira lakini mwaka ule ( I think 1994) walichukua kombe la mataifa huru!!

I believe ile ilipangwa kwamba SA wachukue kombe. Kombe lile likakutanaisha kizazi cha makaburu wabaguzi na waafrika... wote kwa pamoja wakawa wanashangilia ushindi! Tukawaona akina Mark Fish wenye damu ya kikaburu na vijana wa "Kizulu" wakicheza soka pamoja kitu ambacho hakikuwahi kutokea hapo kabla!!

Hiyo ndiyo soka! Hiyo ndiyo michezo!
 
kwa kuwasaidia tu watanzania wenzengu ni hivi,azam tv sio mdhamini wa mashindano ya cecafa yanayotarajia kuanzia tarehe 3/12/2017 huko kenya bali ni official tournament broadcaster.

azam tv imepewa haki na board ya cecafa kuonyesha mechi zote za cecafa zitakazo chezwa msimu huu.sio mdhamini kama anavyodai mleta mada.

mleta mada ni mpotoshaji na mpiga porojo tu kama wapiga porojo wengine kwenye majukwaa mbalimbali ya jf.hajui akisemacho.tumsamehe bure.
 

Ndiomaana mimi nikasema....jamaa amekuja na chuki zake binafsi na sijaona wa kumuunga mkono humu zaidi ya watu wawili tu nao wamesepa ki aina,,,yeye kama hapendi uislamu na waarabu kwa ujumla asianzishe mada...huu ni uchochezi,,, alafu nashangaa mods wanamuangalia mtu anatukana watu humu na wao wanamtazama tu,,, Hivyo tumsamehe bure,,, yeye angesema tu ukweli kwamba mimi "ninachuki na hii dini na waarabu nawachukia/siwapendi lakini waisrael taifa teule/wazungu nawapenda na ni ndugu zetu"

Angesema wazi ijulikane kuliko kuficha.
 
CECAFA na AZAM Tv waliliona hili ndio maana wamewaita Libya ili wawaonyeshe jinsi tunavyoishi waafrika tu wamoja hivyo wakirudi kwao wawe Mabalozi wazuri kwa nchi yao.kwamba Africa ni moja na Ndio maana tulienda kucheza kwa waafrika wenzetu na si Europe
 
Azam haaliki wewe, CECAFA ndio wanaalika. Yani URA itakuja kucheza Mapinduzi Cup eti kwakua Azam watarusha michuano hiyo ndio wamewaalika URA? Kumbe hata unachoongea hujui
Mtu anapodhamini maana yake ameridhia hiyo timu kuletwa.
 
Shida ni 'inferiority complex', tupaze sauti, Susia Azam, Susia Cecafa challenge cup!
 
Kwakuwa yeye ndio mainbroadcaster, ana nafasi ya kushinikiza Libya iondolewe, Susia Azam, Susia Cacafa challeng cup
 

Maneno kuntu kabisa. Ubarikiwe mkuu!
 
Kwakuwa yeye ndio mainbroadcaster, ana nafasi ya kushinikiza Libya iondolewe, Susia Azam, Susia Cacafa challeng cup

Mkuu sisusii,,, nitaendelea kuwaunga mkono mpaka amani ipatikane...waLibya wapo katika bara letu na wao pia ni waafrika wenzetu tunawapenda sana na tutaendelea kuwapenda....israel inavyowanyanyasa wapalestina na kuwauwa kama wanyama, mali waislamu wanauliwa kila kukicha lakini sijaona mtu akianzisha mada na kukemea.

Ili ipatikate amani Nchini Libya njia rahisi ni hiyo ya "MWALIKO" pia twendelee kununua bidhaa za Azam
 
Kwakuwa yeye ndio mainbroadcaster, ana nafasi ya kushinikiza Libya iondolewe, Susia Azam, Susia Cacafa challeng cup
[emoji116] [emoji116] [emoji116] [emoji116] [emoji122] [emoji122] [emoji122] [emoji122] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…