Philip Mangula ang'atuka nafasi ya Umakamu Mwenyekiti CCM Taifa. Abdulrahman Kinana apendekezwa na Halmashauri Kuu kuchukua nafasi yake

Kikao Cha Halmashauri Kuu ya CCM kimependekeza jina la Katibu Mkuu wa zamani Abdulrahman Kinana kuteuliwa kupigiwa kura za kuwa Makamu Mwenyekiti CCM Bara ambapo atachukua nafasi ya Philip Mangula. Kikao hicho kimefanyika leo 31 Machi 2022 Jijini Dodoma.
 
Naye Bernad Membe amerudi kundini. WITHER SUKUMA GANG.

Mungu Ibariki Tanzania, siasa za chuki zimeshindwa
Huyu mzee mangula hamtamfuata tena arudi? Maana si Mara ya kwanza hii kumuondoa
 
Timu Msoga wanarudia ya 2005 kumuondoa Mzee Mangula,Maji yalipozidi unga JK ikabidi amtafute Mzee Mangula.Mama naona kama amezidiwa kete na Msoga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…