Picha Adimu za Wapigania Uhuru wa Tanganyika: Binti Khalfani wa Bukoba

Picha Adimu za Wapigania Uhuru wa Tanganyika: Binti Khalfani wa Bukoba

Mzee, picha unazoleta ni picha nzuri. Zimesheheni mambo mengi ya historia. Zimejaa mafunzo. nakushukuru.

Ila sasa, shida yako ni kuwa hadithi zake ziko biased. Zinabeba taswira ya udini. Message yake ni kuwa bila ushiriki wa dini yako, tusingepata uhuru.

Siku moja moja sio vibaya kujidanganya nafsi lakini.. 😂 😂 😂 😂 😂
Tangawizi,
Hayo ninayoeleza ndivyo ilivyokuwa na ndiyo ukweli wenyewe.

Ikiwa wewe kusoma historia kama ilivyokuwa na kuona mchango wa Waislam kuwa ni udini hii ni bahati mbaya kwa upande wako.

Ikiwa nitabadili historia hii katika ukweli wake hatutakuwa na historia ya kweli ya TANU.

Chuo Cha CCM Kivukoni wameandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Historia yao imewafuta wazalendo waliounda chama cha TANU kwa hofu kama hiyo uliyonayo wewe hivi sasa.

Kitabu kizima hutomsoma Ally Sykes TANU kadi no. 2 mfadhili wa chama na kadi 1000 za TANU yeye ndiye aliyenunua kutoka mfukoni kwake.

Kitabu kizima hutomkuta kaka yake Abdul Sykes kadi yake no. 3 mfadhili wa chama na ndiye kwa ushauri wa Hamza Mwapachu akamsafishia njia Nyerere kuwa rais wa TAA mwaka 1953.

Haya si mageni hapa nayaeleza kila mara.

Kitabu kizima hutomsoma Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir aliyekuwa akiuza kadi za TANU misikitini.

Wala hutomsoma Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.

Swali langu kwako ni hili: Ungependa historia hii isiwe sehemu ya historia ya Mwalimu Nyerere?
 
Tangawizi,
Hayo ninayoeleza ndivyo ilivyokuwa na ndiyo ukweli wenyewe.

Ikiwa wewe kusoma historia kama ilivyokuwa na kuona mchango wa Waislam kuwa ni udini hii ni bahati mbaya kwa upande wako.

Ikiwa nitabadili historia hii katika ukweli wake hatutakuwa na historia ya kweli ya TANU.

Chuo Cha CCM Kivukoni wameandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Historia yao imewafuta wazalendo waliounda chama cha TANU kwa hofu kama hiyo uliyonayo wewe hivi sasa.

Kitabu kizima hutomsoma Ally Sykes TANU kadi no. 2 mfadhili wa chama na kadi 1000 za TANU yeye ndiye aliyenunua kutoka mfukoni kwake.

Kitabu kizima hutomkuta kaka yake Abdul Sykes kadi yake no. 3 mfadhili wa chama na ndiye kwa ushauri wa Hamza Mwapachu akamsafishia njia Nyerere kuwa rais wa TAA mwaka 1953.

Haya si mageni hapa nayaeleza kila mara.

Kitabu kizima hutomsoma Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir aliyekuwa akiuza kadi za TANU misikitini.

Wala hutomsoma Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.

Swali langu kwako ni hili: Ungependa historia hii isiwe sehemu ya historia ya Mwalimu Nyerere?
Kwa akili hizo za udini walitegemea wakimtoa mkoloni hii nchi ingetawaliwa kidini tena kiislam.
Tanzania ni kubwa zaidi ya walivyokuwa wanafikiri.
 
Kwa akili hizo za udini walitegemea wakimtoa mkoloni hii nchi ingetawaliwa kidini tena kiislam.
Tanzania ni kubwa zaidi ya walivyokuwa wanafikiri.
Kambiko,
Unasema maneno hayo kwa kuwa wewe huijui historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mimi nitakueleza kwa ufupi.

Baada ya Abdul Sykes na Dr. Vedasto Kyaruzi kuchukua uongozi wa TAA mwaka wa 1950 juhudi za kuunda chama cha siasa zikaanza kwa nguvu sana.

Serikali iliomba mapendekezo ya katiba kutoka kwa wananchi na vyama vyao.

Mapendekezo ya TAA HQ ilikuwa katika moja ya vipingele vyake kutaka wajumbe wa LEGCO wapigiwe kura badala ya kuteuliwa na Gavana na baada ya miaka 13 Waingereza waondoke Tanganyika.

Kipengele hiki kilighadhibisha sana serikali.

Mapendekezo haya yalitengenezwa na TAA Political Subcommitee ambayo wajumbe wake walikuwa: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Hamza Mwapachu, Steven Mhando, Sheikh Said Chaurembo na John Rupia.

Mshauri wa TAA Political Subcommitte alikuwa Earle Seaton.

Dr. Kyaruzi kama adhabu akapewa uhamisho kwenda Kingolwira kisha Nzega kwa nia ya kuidhoofisha TAA na sababu ni hayo mapendekezo ya katiba ambayo TAA HQ waliwasilisha kwa Gavana Edward Twining.

Hamza Mwapachu akahamishiwa Nansio, kisiwani.
TAA HQ akabaki Abdul Sykes akiwa Secretary na Act. President.

Abdul Sykes na Hamza Mwapachu wakaamua katika kikao kilichofanyika Nansio nyumbani kwa Hamza Mwapachu kuwa TAA isisubiri waunde TANU haraka.

Hii ilikuwa 1950/51.

Abdul alikuwa anamtaka Chief David Kidaha Makwaia awe Rais wa TAA kisha waunde TANU mwaka unaofuatia.

Hili halikuwezekana.
Mwaka wa 1952 Nyerere akaja Dar es Salaam na akajuana na Abdul Sykes.

1953 Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe wakaenda Nansio kutaka ushauri wa Mwapachu kuhusu nafasi ya Rais wa TAA katika uchaguzi uliokuwa mbele yao.

Mwapachu alikuwa akimtaka Nyerere atiwe katika uongozi wa TAA.
Mwapachu yeye alikuwa anamtaka Nyerere ashike nafasi ya President.

Abdul Sykes alikwenda kwa Mwapachu kupata kauli yake ya mwisho kuwa yeye (Abdul) ampishe Nyerere nafasi ile na amsaidie ashinde uchaguzi awe Rais na mwaka unaofuatia 1954 waunde TANU na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.

Nyerere bila ya msaada wa Abdul Sykes na viongozi wa TAA HQ asingeweza kiumshinda Abdul Sykes katika uchaguzi katika Dar es Salaam ile ya 1950s.

Mwapachu alisisitiza kuwa nafasi ya Rais wa TAA kwenda TANU na kudai uhuru inahitaji Mkristo ile kuvunja ile dhana kuwa harakati za TAA na TANU itakapoundwa zisichukuliwe kuwa ni harakati za Waislam peke yao.

Waasisi wa harakati hizi walijua kuwa endapo harakati hizi zitapewa sura ya Uislam hii itawaweka Wakristo nje ya ulingo na Waingereza wangepata mwanya ya kuwagawa Watanganyika.

Hili halikutakiwa kabisa.

Nyakati hizo Waislam ndiyo waliokuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukoloni wa Waingereza.

Hawa waasisi wa harakati hizi hawakuwa watu wajinga walijua fitna za wakoloni na walijua faida ya umoja wa wananchi.

Hata siku moja hawakuwaza kuleta ubaguzi.
Historia hii ukiitaka kwa ukamilifu wake nimeandika kitabu hicho hapo chini.

Chukua muda ukisome ndiyo utawajua Waislam na ukweli wa historia yao.
Laiti wangelikuwa wabaguzi Nyerere asingefika hapo alipofika.

Lakini kubwa utajua kwa nini wewe hukusomeshwaa historia hii mahali popote.

1685709351385.png

Baraza la Wazee wa TANU 1957

1685708480478.png
 
Yoda,
Picha hiyo kama nilivyoandika kaniletea ndugu yangu.

Nitakuwekea picha nyingine uangalie labda tunaweza kuona mwelekeo ulikuwaje.
Acha udini we Mzee,sijui ungekuwa kiongozi kama wagalatia ungewaacha salama,Acha udini
 
Kambiko,
Unasema maneno hayo kwa kuwa wewe huijui historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mimi nitakueleza kwa ufupi.

Baada ya Abdul Sykes na Dr. Vedasto Kyaruzi kuchukua uongozi wa TAA mwaka wa 1950 juhudi za kuunda chama cha siasa zikaanza kwa nguvu sana.

Serikali iliomba mapendekezo ya katiba kutoka kwa wananchi na vyama vyao.

Mapendekezo ya TAA HQ ilikuwa katika moja ya vipingele vyake kutaka wajumbe wa LEGCO wapigiwe kura badala ya kuteuliwa na Gavana na baada ya miaka 13 Waingereza waondoke Tanganyika.

Kipengele hiki kilighadhibisha sana serikali.

Mapendekezo haya yalitengenezwa na TAA Political Subcommitee ambayo wajumbe wake walikuwa: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Hamza Mwapachu, Steven Mhando, Sheikh Said Chaurembo na John Rupia.

Mshauri wa TAA Political Subcommitte alikuwa Earle Seaton.

Dr. Kyaruzi kama adhabu akapewa uhamisho kwenda Kingolwira kisha Nzega kwa nia ya kuidhoofisha TAA na sababu ni hayo mapendekezo ya katiba ambayo TAA HQ waliwasilisha kwa Gavana Edward Twining.

Hamza Mwapachu akahamishiwa Nansio, kisiwani.
TAA HQ akabaki Abdul Sykes akiwa Secretary na Act. President.

Abdul Sykes na Hamza Mwapachu wakaamua katika kikao kilichofanyika Nansio nyumbani kwa Hamza Mwapachu kuwa TAA isisubiri waunde TANU haraka.

Hii ilikuwa 1950/51.

Abdul alikuwa anamtaka Chief David Kidaha Makwaia awe Rais wa TAA kisha waunde TANU mwaka unaofuatia.

Hili halikuwezekana.
Mwaka wa 1952 Nyerere akaja Dar es Salaam na akajuana na Abdul Sykes.

1953 Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe wakaenda Nansio kutaka ushauri wa Mwapachu kuhusu nafasi ya Rais wa TAA katika uchaguzi uliokuwa mbele yao.

Mwapachu alikuwa akimtaka Nyerere atiwe katika uongozi wa TAA.
Mwapachu yeye alikuwa anamtaka Nyerere ashike nafasi ya President.

Abdul Sykes alikwenda kwa Mwapachu kupata kauli yake ya mwisho kuwa yeye (Abdul) ampishe Nyerere nafasi ile na amsaidie ashinde uchaguzi awe Rais na mwaka unaofuatia 1954 waunde TANU na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.

Nyerere bila ya msaada wa Abdul Sykes na viongozi wa TAA HQ asingeweza kiumshinda Abdul Sykes katika uchaguzi katika Dar es Salaam ile ya 1950s.

Mwapachu alisisitiza kuwa nafasi ya Rais wa TAA kwenda TANU na kudai uhuru inahitaji Mkristo ile kuvunja ile dhana kuwa harakati za TAA na TANU itakapoundwa zisichukuliwe kuwa ni harakati za Waislam peke yao.

Waasisi wa harakati hizi walijua kuwa endapo harakati hizi zitapewa sura ya Uislam hii itawaweka Wakristo nje ya ulingo na Waingereza wangepata mwanya ya kuwagawa Watanganyika.

Hili halikutakiwa kabisa.

Nyakati hizo Waislam ndiyo waliokuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukoloni wa Waingereza.

Hawa waasisi wa harakati hizi hawakuwa watu wajinga walijua fitna za wakoloni na walijua faida ya umoja wa wananchi.

Hata siku moja hawakuwaza kuleta ubaguzi.
Historia hii ukiitaka kwa ukamilifu wake nimeandika kitabu hicho hapo chini.

Chukua muda ukisome ndiyo utawajua Waislam na ukweli wa historia yao.
Laiti wangelikuwa wabaguzi Nyerere asingefika hapo alipofika.

Lakini kubwa utajua kwa nini wewe hukusomeshwaa historia hii mahali popote.

View attachment 2643528
Baraza la Wazee wa TANU 1957

View attachment 2643518
SO what?
 
Acha udini we Mzee,sijui ungekuwa kiongozi kama wagalatia ungewaacha salama,Acha udini
Mdukuzi,
Niache udini gani ndugu yangu?

Una maana kwa kuandika historia ya kweli ya TANU ambayo haikuwa inafahamika ndiyo nimekuwa mdini?

Wale walioelezwa kuwa hiyo waliokuwa wanaandika si historia ya kweli ya TANU wala historia ya kweli ya Julius Nyerere na wakakataa kupokea historia ya kweli kwa kuwa ilikuwa imejaa Waislam wewe unawaitaje?

Udini ni kueleza mchango wa Waislam uliokataliwa kwa hiyo kufutwa?

Ndiyo tusema historia ya uhuru wa Kenya ukiwataja Wakikuyu na Mau Mau na majina ya akina Dedan Kimathi utakuwa mkabila?

Kipi kinachokughadhibisha kiasi unaniita ''We Mzee?''
Hakika mimi si kijana tena ni mzee na uzee unastahili heshima.

Miaka 71 si midogo hudhani unawajibika kunitaja kwa adabu?
Ungeweza ukasema, ''Mzee Mohamed acha udini.''

Nakuwekea picha hapo chini katika miaka yangu ya ujana labda itakufanya utafakari:

1685722123407.png

 
Mdukuzi,
''So what.''

Unasema.
Kwa Kiswahili ni kama kusema, ''Sasa ndiyo nini?''

Inaelekea unaghadhibishwa na historia ya kweli.

Nitakueleza kwa kifupi nini kilitokea baada ya kitabu cha Abdul Sykes kuchapwa London 1998 na kufika Tanzania.

Prof. Haroub Othman alipokisoma alipata mshtuko mkubwa.
Haya kanieleza kwa mdomo wake mwenyewe.

Akaomba miadi kukutana na Mwalimu.

Alimweleza Mwalimu kuwa kitabu hiki cha Abdul Sykes kimebadili historia yote ya TANU, uhuru wa Tanganyika na historia yake Nyerere.

Prof. Haroub alimwomba Mwalimu aridhie kuandikwa kwa kitabu cha maisha yake.

Mwalimu aliridhia lakini kitabu hakikuandikwa kwa muda uliokusudiwa kwani Pro. Haroub Othman alifariki dunia na Nyerere akafariki pia.

Kitabu kikaja kuandikwa na jopo lililoongozwa na Prof. Issa Shivji baada ya miaka kusogea kidogo.

Nilikuwa mmoja wa watu waliohojiwa kuhusu kitabu cha maisha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ''Nyerere Biography'' (2020) na kitabu kilipochapwa nilitunukiwa kitabu hicho kwa mchango wangu.

1685727392479.png

Kulia Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Othman Yahya na Dr. Ng'wanzi Kamata
wakinihoji nyumbani kwangu 2013
1685723572011.png
 
Back
Top Bottom