Pre GE2025 Picha: CCM hawa Wachina ni wapiga kura wenu? Kwanini mmewavalisha Tshirt za Rais Samia?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Baada ya wasanii na mashirika mbalimbali kuunga mkono juhudi sasa CCM wameanza kwenda hadi kwa raia wa kigeni.

Kuna muda CCM wanapenda tu watu tuongee mseme watu wanakosoa kila kitu.

Hapa ilikuwa ni kwenye ufunguzi wa Kiwanda cha Chokaa na Saruji cha Maweni huko mkoani Tanga.

Kulikuwa na haja gani ya kuwavalisha hawa Wachina Tshirt za Rais Samia? Au ni wapiga kura wenu hawa?


 
Baadanya Kuona Uchaguzi ulijaa mabalozi Dunja nzima wao wamejaza wafungwa wa uchina😀😀😀
 
Wadau
 
Nimevaa Tshirt ya MAGA na picha la Trump kwani na mimi ni Mmarekani,

Sio kila jambo u alichukulia serious

USSR
 
5R
1. Recolonization
2.Resource privatization
3. Retention of poverty
4.Reverse econimization
5. Rights deprivation
 
Nimevaa Tshirt ya MAGA na picha la Trump kwani na mimi ni Mmarekani,

Sio kila jambo u alichukulia serious

USSR

Hata Trump akikusikia unaishi in a third world country and unavaa Tshirt iliyoandikwa Make AMERICA great again atakushangaa.

Akili yako inapaswa ipigwe window upya na ifanyiwe factory setting
 
Kwani wewe ukienda China ukavaa mavazi yenye picha ya rais wa China kuna shida gani?

China sio multiparty state kama sisi. Wao Rais ni wao wa maisha na ni a partisan state.

Ngoja na wewe nikuulize.

Kwanini hao wachina wasingevaa nguo za kawaida, kwanini wavae Tshirt zenye picha ya Rais? Walikuwa wanataka wafikishe ujumbe gani?

Kwanini wasingevaa Tshirt zenye picha ya Lissu?
 
Daah 😔 Namuona Zhang Xung pamoja na Lui Meng hapo sijui Mheshimiwa Xi Jing Ping anajua kuna wachina wamekuwa Chawa!??
 
Sawa ni namba one ndo hadi wachina?
 
Wao walipenda kuvaa hivyo usiwapangie... Mbona mimi nimevaa tisheti ya kiduku hapa
 
Mbona watanzania wengi wanavaa nguo zimeqndikwa Jordan, mara Ronald mara Messi kwani hao ni watanzania , na kwani wamekuambia wamevalishwa au wamevaa kwa mapenzi yao.
 
Kwani hii desperation ya kuonesha mama anapendwa inatokana na nini?
Kwanini inatumika nguvu kubwa sana?

Mama wakati anashika hatamu moja kati ya mambo aliyonikosha nayo ni aliposema hatoruhusu kuabudiwa (machawa)
Ila mambo yamekuwa tofauti.

Ningekuwa mimi ndio yeye ningepiga marufuku haya mapichapicha yote hadharani, kazi tu ndio zingeongea.

Huwa nikiona yeyote kavaa chochote chenye picha yake nasikia aibu sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…