Picha: Chaneli ya mambo ya Utalii imekuwa chaneli ya Mambo ya Umeme

Picha: Chaneli ya mambo ya Utalii imekuwa chaneli ya Mambo ya Umeme

Pesa ambazo zingefaa kutengeneza maudhui ya hizo channel ya safari zilitumiwa na kigwangala kulala kwenye mahotel na kina stive nyerere na ebitoke, kaeni kwa kutulia mtapewa kanga za chama na chumvi mpige kura tena.
 
Mradi mkubwa Kama huu wa MEGAWATI 2100 Ni kivutio Kikubwa Sana Cha utalii

Hasa hasa kwa nchi zetu hizi za hizi za ukanda wa chini ya jangwa la Sahara.

Hata ingekua inatoa Megawatt 500,000 utalii wa ngono unalipa kuliko huo wa kwenda kuangalia eti maji yakipiga kelele kuchakatwa kua umeme.
 
Wangekuwa wanalink na maafisa habari wa kila sehemu ya kivutio cha utalii nchi nzima, alafu hao maafisa habari wangwezeshwa wanakuwa wanatuma content za sehemu zao
 
Nilikuwa naangalia safari chanel Tanzania, naona matumizi yake yameanza kubadilika, sijui ni kukosa ubunifu au kukosa vipindi

Leo walikuwa wanaongea mambo ya mega watt na kilowatt tu 😂

Sio mambo ya mbuga zetu au Beach zetu

View attachment 1511064
Hakuna Channel mbovu kama hii.
Ni takataka kabisa.
Watayarishaji wa vipindi hawana ubunifu wala uzoefu.
Sasa wameigeuza kuwa CHANNEL YA PROPAGANDA.
Nimeacha kuangalia hii channel muda mrefu sasa.
 
Sijui nini kimevikumba vyombo vya habari Tanzania.Sijui ni ulimbukeni,sijui ni hofu ya kutumbuliwa hasa wakurugenzi wateule,au nini sijui!

Hii Channel ya utalii ilianza vizuri sana. Nilitegemea ijikite kwenye maudhui halisi ya utalii pekee. Cha ajabu kadri siku zinavyosonga inageuka kuwa chanell ya kuonyesha miradi ya Serikali kama Stiglers n.k. Kwani habari kama hizo si ndio kutwa nzima zinaonyeshwa pale TBC1 na Channel Ten? Kwanini mnalazimisha kutupa habari tusizozitaka? Sasa kulikuwa na maana gani ya kuanzisha Safari Channel kama hamna maudhui?

Tanzania ina mambo mengi sana ya kitalii ambayo mtu huwezi kuyamaliza ndani ya miaka 3. Shida ni Management ya TBC kugeuza vyombo vyake vyote kuwa "Praise Team" mpaka mnaharibu. Kusifia kumezidi mpaka wanaotutazama wanatuona washamba. Hebu fikiria mtu wa nje ya nchi ana tune Safari Channel aafu ghafla anakuta kada anahojiwa miradi ya serikali je atarudia tena kutazama?

Primary purpose ya kuanzisha Safari Channel ilikuwa kuwavutia watalii wa nje kuja kufanya utalii nchini na si kuitumia kwa propaganda za kisiasa.Hali ikiendelea hivi baada ya miaka 10 ijayo tutaanza kuona mikutano ya chama ilirushwa live kupitia hii Channel.
 
Ni kweli. Tena hii Channel inatangaza vivutio kwa kuwahabarisha Watanzania waweze kufanya utalii wa ndani na kuongeza kipato kutokana na utalii wa ndani. Matangazo yasiyohusiana na utalii hayafai.

Waache kiherehere chao na kujipendekeza.
 
Usishangae kufungua hii channel kukuta wanaonyesha vituo vipya vya Afya,,SGR,na barabara mpya. Sa sijui lengo lake ni nini? Vyeo hivi!!
 
Hata mie siku za mwanzoni nilikuwa naifuatilia sana, ila siku maramoja moja sana, wanashindwa kuelewa kama kuna wana nchi ambao hawana mlengo wa vyama, matangazo mengine hutuchefua tu bora hata kutizama Al Jazeera
 
Kosa kubwa tunalofanya watanzania ni kukubali udikteta. Tutajuta sana awamu ya pili.
Sijui nini kimevikumba vyombo vya habari Tanzania.Sijui ni ulimbukeni,sijui ni hofu ya kutumbuliwa hasa wakurugenzi wateule,au nini sijui!

Hii Channel ya utalii ilianza vizuri sana. Nilitegemea ijikite kwenye maudhui halisi ya utalii pekee. Cha ajabu kadri siku zinavyosonga inageuka kuwa chanell ya kuonyesha miradi ya Serikali kama Stiglers n.k. Kwani habari kama hizo si ndio kutwa nzima zinaonyeshwa pale TBC1 na Channel Ten? Kwanini mnalazimisha kutupa habari tusizozitaka? Sasa kulikuwa na maana gani ya kuanzisha Safari Channel kama hamna maudhui?

Tanzania ina mambo mengi sana ya kitalii ambayo mtu huwezi kuyamaliza ndani ya miaka 3. Shida ni Management ya TBC kugeuza vyombo vyake vyote kuwa "Praise Team" mpaka mnaharibu. Kusifia kumezidi mpaka wanaotutazama wanatuona washamba. Hebu fikiria mtu wa nje ya nchi ana tune Safari Channel aafu ghafla anakuta kada anahojiwa miradi ya serikali je atarudia tena kutazama?

Primary purpose ya kuanzisha Safari Channel ilikuwa kuwavutia watalii wa nje kuja kufanya utalii nchini na si kuitumia kwa propaganda za kisiasa.Hali ikiendelea hivi baada ya miaka 10 ijayo tutaanza kuona mikutano ya chama ilirushwa live kupitia hii Channel.
Uoga wa kutumbuliwa tu...

Au labda wanataka na watalii waipigie kura CCM..
Ni kweli. Tena hii Channel inatangaza vivutio kwa kuwahabarisha Watanzania waweze kufanya utalii wa ndani na kuongeza kipato kutokana na utalii wa ndani. Matangazo yasiyohusiana na utalii hayafai.

Waache kiherehere chao na kujipendekeza.
Usishangae kufungua hii channel kukuta wanaonyesha vituo vipya vya Afya,,SGR,na barabara mpya. Sa sijui lengo lake ni nini? Vyeo hivi!!
 
Wameona chaneli inapata traffic kuzidi TBC na Channel 10 wakaona isiwe kesi. Ngoja propaganda tuwapelekee huko huko🤣🤣🤣
 
Kama wanazungumzia ule mradi wa JNHEP sioni tatizo.

Miradi hiyo ya HEP imekuwa vivutio vya utalii pia na si bongo tu na wala si lazima wawe wanalengwa foreigners.
 
Kama hawana content waseme kama wananunua content vijana waanze kuzama porini watengeneze documentaries za ukweli.
 
Ubunifu nalo ni tatizo. Wasitegemee kutumia watumishi wao ambao mwisho wa siku wanakosa fedha kuwagharamia. Nashauri, katika kila Halmashauri kuna vivutio vya utalii na vitengo vya habari, ikiwa ni pamoja na Maafisa habari wa mikoa. kwa nini wasiwatake wawe wanaandaa vivutio kutoka katika maeneo yao na kutuma hizo footage TBC ambako watafanya uhariri wa mwisho na kuvitumia katika vipindi? Lakini pia kuna nafasi ya kuwasiliana na wenye mahoteli pamoja na Tour operators waweze kujitangaza, hii itawafanya watalii wa ndani na wa nje kuvutika kwa kuona kumbe na facilities zipo?
 
Back
Top Bottom