PICHA: Chukua tahadhari; ukiona hivi usisogelee bahari, ni hatari!

PICHA: Chukua tahadhari; ukiona hivi usisogelee bahari, ni hatari!

Kuwa makini sana kipindi uwapo Beach!

Kabla ya kuingia kwenye maji, angalia vizuri bahari. Ikiwa utaona nafasi iliyojitenga kama uwazi katikati ya mawimbi, usiingie!

Ni mkondo wa chini na utavutwa ndani.

Mkondo huu unaweza kuwa UNDERTOW au RIP CURRENTS (unaweza uka-google kwa maelezo zaidi)

Wajulishe familia, marafiki. Hii inaweza kuokoa maisha.

View attachment 2024928View attachment 2024930View attachment 2024929View attachment 2024937
Sijawahi kutamani kuoga baharini,na sasa hivi nimeshazeeka huwa naiangalia kwa mbaali tu kama picha flani hivi...
 
Ndugu popote pale ulipo Asante sana kwa Elimu yako Kubwa uliyotupa hapa bila Uchoyo. Ubarikiwe!

Nimeamua kurudisha Nguo zangu za Kuogelea na sasa nageuza naenda Kijiweni tu Kucheza zangu Draft na Bao kwani ningeenda Kuogolea bila Kuusoma huu Uzi wako leo huenda KEROZENE ningekuwa no more duniani.

Wale wapenda Kula Uroda Mademu baharini Kazi mnayo nadhani Mawimbi hayo mmeyaona Shauri zenu.
Mimi pia naungana na wewe kama vipi njoo online nikufungee weee mbaka uchoke maana kwenye huo mchezo wa draft naamini nimeshindikana mbaka sasa
 
Wiki hii mwanzoni jirani yetu kapoteza mtoto wa 19 yrs na mjukuu wake wa 5 yrs

Wamezama baharini.. ..

Tahadhari ni muhimu sana!
 
Ndugu popote pale ulipo Asante sana kwa Elimu yako Kubwa uliyotupa hapa bila Uchoyo. Ubarikiwe!

Nimeamua kurudisha Nguo zangu za Kuogelea na sasa nageuza naenda Kijiweni tu Kucheza zangu Draft na Bao kwani ningeenda Kuogolea bila Kuusoma huu Uzi wako leo huenda KEROZENE ningekuwa no more duniani.

Wale wapenda Kula Uroda Mademu baharini Kazi mnayo nadhani Mawimbi hayo mmeyaona Shauri zenu.
Genta una Ids nyingi
 
nakumbuka kipindi cha nyuma bado bwa'mdogo tulikuwa tunaenda kucheza baharini, Unaweza kutembea hata zaidi ya mita 50kwenye maji kuelekea kina kirefu ndio maji yakufike kifuani au mabegani, hapo tunasubiri mawimbi makubwa kama haya unayoyazungumzia linapokuja kwa nguvu unajirusha katikati(mchomo)basi linakubeba kwa kukubingirisha mpaka juu kabisa kusipo na maji halafu yenyewe yanarudi kwa kasi nasisi tunanyanyuka na kuyafuata tena, jambo moja gumu la kuzingati wakati umapojirusha kwenye wimbi la aina hiyo hutakiwi kuvuta pumzi, Mpaka litakapokuacha. Maji ya chumvi ukiyavuta puani au ukiyanywa kwa wingi wakati unapoogelea ni rahisi sana kukuua.
Huu mchezo wako kidogo utoe roho lakini kwa style nyingine, sisi tulikuwa tunatembea hadi maji ya kifua then tunaogelea eneo hilo sasa sielewi baharini kukoje maana huku nyuma tulipotoka maji yanajaa wakati eneo tulipo maji yakawaida tu labda yanafikia shingoni. Mzee wakati wa kurudi ndio ikawa kimbembe maji mengi hadi hatuonekani, ikawa ni mwendo wa kuruka juu unapumua then unazama tena huku unasogea taratibu na siku hiyo nikaiaga bahari mazima
 
Maji nayaogopa kinoma, nilishakoswa na ajari mbili za kwenye maji.

Acha niendelee tu kuwa mtazamaji.
 
Back
Top Bottom