Picha: Ephrahim Kibonde wa Clouds FM atiwa nguvuni

Nafanya research hapa ....

RESEACH TOPIC: Kupima kukubalika kwa Ephrahim kibonde ktk jamii

SAMPLE SIZE : 295 JF Members waliochangia huu uzi,

STUDY TYPE ; Qualitative study,

RESULTS; 98% Wanampinga huyu mtangazaji na hawakubaliani Na tabia zake mbaya..

CONCLUSION,,

Ni hasara kwa radio station kukumbatia kuwa na mtangazaji wa namna ya kibonde , maana watanzania husikiliza mtangazAji wanayemkubali !! Ni hasara hata kumtumia ktk matangazo ya biashara au kuelimisha jamii! Ni sababu mojawapo ya kuporomoka kwa umaarufu wa radio husika.
 
Kibonde wa Clouds anadaiwa kusababisha ajali asubuhi hii eneo la Makumbusho, amemgonga dereva mwingine kwa nyuma. Trafiki walipofika kupima ajali, Kibonde karudi nyuma kaendesha gari lake kasepa! Trafiki katumia gari lililogongwa kumfukuzia. Walifanikiwa kumkamata eneo la Mwenge. Trafiki aliingia ktk gari lake nakumwomba arudi eneo la ajali ili wakapime na kuchora mchoro wa ajali. Kibonde kagoma na kumtaka trafiki ashuke ktk gari lake, trafiki naye kagoma kushuka. Mchezo ulioendelea Kibonde aliondoa gari na kuanza kupiga misele, akizunguka mitaa akiwa na trafiki huyo! Trafiki aliwasiliana na wenzake ambao walianza kuifuatilia gari hiyo ya Kibonde kila kiunga cha jiji hususani eneo la Mwenge na Ubungo. Hayawi, hayawi yakawa, Kibonde akatokea maeneo ya mataa ya Ubungo, hapo nikashuhudia senema ya Kibonde na trafiki! Trafiki wa kike aliyekua eneo hilo akaipiga mkono gari ya Kibonde iliyokuwa kasi, gari hiyo haikuonesha dalili za kupunguza mwendo. Trafiki alikomaa kusimama mkono wake ukiwa juu kuashiria kumtaka Kibonde asimame huku akipaza sauti ktk radio call akisema ananigonga, afande, ananigonga! Akiwa ktk hali hiyo, kuna gari ilikotokea sikujua ikakatisha kati ya trafiki na gari ya Kibonde ndiyo ikawa kigingi cha gari ya Kibonde na kutiwa mbaroni! Aligoma kuendesha gari ikabidi livutwe hadi polisi Urafiki ambapo kwa sasa amepelekwa Oystabay! Kwa utafiti wangu kidogo nilioufanya nikifukuzana na muda kuwahi kanisani, ni kwamba Kibonde na watu wengine aliokuwanao ndani ya gari lake walikuwa 'TINGASI'!
 

Attachments

  • 1407588812544.jpg
    60.4 KB · Views: 2,879
Mzee wa Mchepuka ni kama anasema : "Aisee Nani amekuruhusu unipige picha..nani?? Unajua niweza kukuchukulia hatua??"..Ninyi askari, hivi mnamfahamu Prof. Anna Tibaijuka ninyii..Mnamfahamu Nehemia Mchechu..Mnanijua mimi ni nani??
 
Tehe tehe tehe..........Kibondeeeeee.......asalam aleikum kaka, kuwa MC kwenye shuhuli za Magamba basi na wewe umejiona unaweza kufanya lolote kama kina Nchemba, Wassira, Lukuvi na usishuhulikiwe.....umeumia kiongozi, kurudisha heshima yako nakushauri jumatatu kwenyue jahazi kiri kosa lako na uombe msamaha kwa askari uliowaonyesha dharau............Sipati picha hilo kosa angefanya Mnyika na wewe kibonde ukaanza kuliongelea.
 
Mzee wa Mchepuka katika hiyo [picha ya "lock up" ni kama anasema : "Aisee Nani amekuruhusu unipige picha..nani?? Unajua niweza kukuchukulia hatua??"..Ninyi askari, hivi mnamfahamu Prof. Anna Tibaijuka ninyii..Mnamfahamu Nehemia Mchechu..Mnanijua mimi ni nani??




Ephraim Kibonde wa Clouds aikiingia na kamera yake baada ya mpiga picha wake kuzuiwa kuingia Ikulu.



Wiki iliyopita Mh. Rais Jakaya Kikwete aliapisha Baraza la Mawaziri katika viwanja vya Ikulu ambapo Wanahabari mbalimbali walialikwa kwa ajili ya kuandika habari na kufanya mahojiano na Mawaziri mbalimbali wa Wizara mara baada ya kuapishwa tayari kwa kuchukua majukumu ya kuongoza Wizara hizo ili kuwakomboa watanzania katika matatizo mbalimbali wanayokabiliana nayo.

Mtangazaji wa Kipindi cha Jahazi na Kibonde Show vyote vya Clouds Radio Fm na Clouds Televishen alikuwa ni mmoja wa wanahabari walioalikwa akiwa na lengo la kuja na mpiga picha wake wa Video kwa ajili ya kurekodi kipindi chake cha Kibonde Show.

Kibonde hivi karibuni alisikika katika kipindi cha Jahazi akiponda na kushutumu waandishi waliovaa suluali za (Jeans) wakati Mh. Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akitangaza Baraza la Mawaziri Ikulu ambapo pia wanahabari walialikwa katika mkutano huo, Kiukweli hata mimi nilimwelewa kwamba alikuwa akizungumzia suala ambalo ni la muhimu juu ya uvaaji wa nguo wakati wanahabari tunapokuwa tumealikwa Ikulu kwa ajili ya kazi za kiuandishi kwani ikulu ni mahali panapotakiwa kuheshimiwa kwa uvaaji wa mavazi yetu.

Ila naona katika hili kwa upande mwingine Ephraim Kibonde aliona Kibanzi cha Wenzake lakini akashindwa kuondoa boriti katika jicho lake, kwani Ephraim Kibonde amesikika jana jioni kwenye kipindi cha Jahazi akizungumzia tena juu ya kuzuiwa kwa mpiga picha wake ambaye ilikuwa afanye naye kazi wakati baraza la Mawaziri lililpoapishwa jumamosi ya wiki iliyopita, hii imetokana na kutomtahadharisha mpiga picha wake huyo juu ya uvaaji wa nguo atakapokwenda kufanya kazi katika shughuli za kuapisha baraza la mawaziri Ikulu katika siku hiyo.

Hii ilipelekea Watu wa Usalama kumzuia mpiga picha huyo kwa kuwa alikuwa amevaa (Jeans) na Kibonde alipojaribu kuwabembeleza watu wa usalama aliambiwa kwamba "wewe ndiye uliyekuwa ukipigia kelele juu ya uvaaji wa nguo hapa Ikulu sasa leo unataka kuvunja utaratibu huo tena haiwezekani Mwambie aende tu nyumbani akabadilishe nguo" walimwambia wanausalama.

Jambo hili lilimfanya Ephraim Kibonde kuchukua Kamera na kupiga picha Mwenyewe ili kazi yake iweze kwenda ilivyopangwa kama utakavyomuona kwenye viwanja vya Ikulu akiwajibika ipasavyo hata hivyo inaonekana kazi ilikuwa ni ngumu sana.

Hapa akionyesha kamera yake.

Hapa Kazi ya kupiga picha imeanza kama unavyomuona akiwa ameganda kama akkari analenga Shabaha ili aweze kupata picha Nzuri.


Hapa akifanya mahojiano na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernald Membe huku Afisa Habari wa Wizara hiyo Assh Mwambene akisaidia kushika kipaza sauti
 

Attachments

  • KIBONDE-1.jpg
    45.9 KB · Views: 283
  • KIBONDE-2.jpg
    49.4 KB · Views: 232
  • KIBONDE-3.jpg
    20.1 KB · Views: 238
Jina husadifu Matendo. í-½íº¶í-½íº¶í-½íº¶í-½íº¶
 


Mkuu hapo nilipotia red naunganga na wewe kwa 100% jamaa ilibidi akitoka hapo selo akutane na barua ya kufukuzwa kazi na mikataba yote ya matangazo ikatishwa maana anaelimisha nini katika jamii kama anaweza kulewa na kutenda makosa kama hayo nini kitamzuia akilewa asichepuke kupingana na tangazo lake.........
 
Nobody is above the law, sifa mbaya sana.
 
Inasemekana ishu ya kibonde ni tangazo walikua wanafanya la utii wa sheria bila shuruti kupitia Clouds TV na Radio
 
Kuna jamaa amemfuatilia kinoma. Kibonde tayari yuko nyuma ya nondo za polisi. Mods unganesheni thread yenye picha ya kibonde akiwa selo.
 
I hope clouds itajifunza kuchagua watangazaji wake, na huyu akirudi hewani jumatatu basi hapo ndio itaonyesha kuwa nchi yetu imejaa majanga haswa. Naona hapo anachungulia kusubiria kutokewa. eeehh ningekuwa na muda na mie ningepita.

haya tutaona kama polisi wetu wanapenda rushwa au la kama atafikishwa mahakamani. au hata kulala hapo kwa masiku.

Kosa lake ni mfano mbaya kwa vijana wanaokua nchini kwetu as wanaweza kuigiza na kudhani ni gemu na sio kosa. so lazima wafate sheria hapa au ndio tutulie tuangalie movie ikiendelea
 
Duh JF ni noma hadi picha mmeipata..... Si mchezo.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…