PICHA: Hali ilivyo mjini kuelekea mkutano wa Nishati Dar

PICHA: Hali ilivyo mjini kuelekea mkutano wa Nishati Dar

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Ukienda mjini leo, unaweza kuhisi ni sikukuu au mwisho wa juma (weekend), baada ya barabara kufungwa kutokana na ugeni wa marais na viongozi mbalimbali wanaoshiriki mkutano wa kimataifa wa Nishati unaoanza leo, Januari 27, 2025 jijini Dar es Salaam.
IMG_2780.jpeg

Ilivyozoeleka siku ya Jumatatu katikati ya mji, kuna mishemishe na purukushani za hapa na pale, lakini hali ni tofauti leo, kwani watu si wengi kama ilivyo kawaida, na kimya kimetawala maeneo mbalimbali.

Fuatilia: Mkutano wa Nishati Afrika (Africa Energy Summit) 27-28 Januari, 2025

IMG_2781.jpeg

Baadhi ya maduka yamefungwa, na maeneo kama Kariakoo hakuna msongamano wa magari; hata bajaji ni ngumu kuzipata, ingawa bodaboda wapo wawili watatu.
IMG_2779.jpeg

Hali hii inaweza kudumu kwa siku hizi mbili za mkutano huu, ambao unafanyika Tanzania, ukiwa ni mkutano wa kwanza kuwakutanisha marais zaidi ya 20 kwa mara moja.
IMG_2778.jpeg

Tangazo la Jeshi la Polisi lililotolewa Jumamosi Januari 25, 2025 na Kamanda Kanda Maalumu ya Polisi Dar es Salaam, Jumanne Muliro, lilieleza kuwa kutokana na ugeni wa viongozi watakaokuja kwenye mkutano, barabara zitafungwa.

PICHA: Mwananchi

Soma, Pia

DAR: Barabara 9 kufungwa kwa siku sita kupisha mkutano wa madini chini ya Viongozi kadhaa wa Afrika
 
Siku mbili hizi ambazo serikali ilizuia Bodaboda kuingia Mjini hasa Posta na Kariakoo kupisha Mkutano wa sekta ya Nishati uliohudhuriwa na viongozi wengi wa nchi za Afrika pamoja na World Bank kumesababisha Kariakoo kupumua na kuwa na utulivu sana hasa kwenye Barabara. Kimsingi kumependeza sana , kuanzia juzi kwenye barabara unavuka kwa utulivu na SIO KUVUKA KWA ZIGIZAGA NA BREKI ZA MIGUU KUKWEPA BODABODA .

Kumbe jiji letu ni zuri sana. Natamani serikali iandae utaratibu ambao utalifanya jiji letu liwe na MUONEKANO WA HESHIMA . Bodaboda ziwe na vituo nje ya Kariakoo na biashara yao itakwenda tu sana
 
Hahaha . Niliona eti mkurugenzi wa jiji anafanya nini sijui... .... NI SAWA NA KITU KIPYA HURUHUSIWI KUTUMIA HADI SIKUKUU.
 
Back
Top Bottom