PICHA: Hili jengo linalojengwa Kariakoo kwa PPP ni balaa ni zaidi ya Mlimani City unaambiwa Serikali itajizolea zaidi ya TZS 2.5bn kila mwaka

Siyo wishful thinkung.

Tuna standards tofauti tu, wewe huijui dunia.
Kama unatumia standard za Nje unakosea, hilo jengo lipo Tanzania, watakaokodi ni Watanzania, kama sio Watanzania waliokodi watauzia Watanzania, kivyovyote Rent zita reflect soko la Kariakoo, ukiweka Rent za Dubai ama London watu wata rent majengo mengine badala ya hilo.

Rent za kariakoo on average ni milioni 2 kwa frame za nje kama ni kubwa sana inafika 3-5M, frame za ndani laki 7 hadi 1.2M, unahitaji maelfu ya frame kugenerate 2.5B kwa mwezi, hakuna jengo la frame 2000 hapo.
 
Wewe upo wapi kwanza unapajua kariakoo lakini..kaa kimya tu..
 
Point nzima ya kuweka watu kama Kafulila na PPP ni kuongeza value, sasa unawekaje project kisomi halafu biashara iendelee kienjeji enyeji tu?

Weka wawekezaji wa kimataifa hapo, weka international mall, weka rents za kubadilisha eneo zima livutie biashara za kimataifa tuondokane kwenye umachinga.

Tatizo hatuna watu daring wenye vision ya kuona kinachoweza kuwa, tuko stuck kuangalia kilichokuwa.

Classic problem of induction scenario.
 
Jambo moja nalipenda kwa Kafulila ni huu uwazi wa mambo yake
 
2.5bn kwa mwaka bado ni pesa dogo kwa Kariakoo naona kama tumepigwa sijui mzalendo Kafulila anasemaje
Kwa akili yako kiasi gani kinapaswa kulipwa? Hata mimi naona ni ndogo ukizingatia jengo litakuwa na wapangaji 900! Kwa K/koo unit ya biashara si chini ya Tshs 1,000,000 kwa mwezi! Hili jengo lingepaswa litengeneze Tshs 900,000,000 kwa mwezi na si chini ya Tasha 10 bln kwa mwaka
 
Hela ndogo sana
 
Kawaida investment inatakiwa irudishe capital na madeni kwa wastani wa miaka saba au chini, sasa return ya 2.5 b kwa investment ya 50b naona itachukua zaidi ya miaka 20, au kuna kitu sielewi?
 
Wawekezaji wa kimataifa DDC? na mali wanatuuzia sisi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ this is too theoretical ...
 
Wawekezaji wa kimataifa DDC? na mali wanatuuzia sisi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ this is too theoretical ...
Kwani kuna chochote kinachowezekana bila kuwa theoretical kwanza?

Hilo jengo kenyewe si kazima ulichore kwanza, ukikichora si ndiyo theoretical yenyewe hiyo?

Mbona mimi nikichora idea unashangaa wakati jengo likichorwa hushangai?

Nyie ndiyo maana mnalialia uchumi mdogo, hamjui hata thamani ya mlichonacho.

Tanzanite ya Tanzania inauzwa Kenya na India, mmeshindwa kudhibiti Tanzanite iuzwe Kariakoo?

Imagine unaweka floor ya kuuza madini ya wachimbaji kutika Tanzania nzima hapo, unawakusanya watu kutoka dunia nzima, utashindwa kupata dola milioni moja kwa mwezi?

Mmeshindwa kufikiria tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…