BilioneaPATIGOO
JF-Expert Member
- Jun 23, 2012
- 12,320
- 11,327
Kanye West alinukuliwa akisema kua tukio la kuvamiwa kwa mkewe lilimfanya awe "helpless" na akasema atafanya kila liwezekanalo kuilinda familia yake(ofkoz pesa anayo)
Hivyo basi kwa kushirikiana na mkewe Kim Kardashian, wameboresha safu yake ya ulinzi(Kim) kujihami na shambulio jipya kufuatia lile la Paris lililohatarisha maisha yake na kuporwa mali zenye thamani ya zaidi ya dola milioni 10.
Sasa atakuwa na ulinzi wenye hadhi ya mkuu wa nchi. Vyanzo vilivyo karibu na Kim vimesema kuwa, sehemu ya timu yake ya ulinzi inaundwa na wafanyakazi wa zamani wa Secret Service, wenye silaha nzito.
Kutakuwepo na walau timu moja ya mapande ya watu kila aendapo. Pia gari yake itakuwa na silaha.
Baada ya shambulio hilo la Paris, Kim alikutana na wanajeshi wa zamani wa jeshi la Israel, CIA pamoja na wafanyakazi wa zamani wa Secret Service. Kanye alikutana na wamiliki wa makampuni makubwa mawili ya ulinzi.
Mlinzi wake, Pascal Duvier amebakizwa. Pia ulinzi umeimarishwa kwa dada zake, Kourtney, Khloe, Kendall na Kylie.
Hivyo basi kwa kushirikiana na mkewe Kim Kardashian, wameboresha safu yake ya ulinzi(Kim) kujihami na shambulio jipya kufuatia lile la Paris lililohatarisha maisha yake na kuporwa mali zenye thamani ya zaidi ya dola milioni 10.
Sasa atakuwa na ulinzi wenye hadhi ya mkuu wa nchi. Vyanzo vilivyo karibu na Kim vimesema kuwa, sehemu ya timu yake ya ulinzi inaundwa na wafanyakazi wa zamani wa Secret Service, wenye silaha nzito.
Kutakuwepo na walau timu moja ya mapande ya watu kila aendapo. Pia gari yake itakuwa na silaha.
Baada ya shambulio hilo la Paris, Kim alikutana na wanajeshi wa zamani wa jeshi la Israel, CIA pamoja na wafanyakazi wa zamani wa Secret Service. Kanye alikutana na wamiliki wa makampuni makubwa mawili ya ulinzi.
Mlinzi wake, Pascal Duvier amebakizwa. Pia ulinzi umeimarishwa kwa dada zake, Kourtney, Khloe, Kendall na Kylie.