Picha: Kashfa nzito "tegeta zoo", simba atafuna mtoto. Mmiliki bwana kusaga anataka kuifunika.

Picha: Kashfa nzito "tegeta zoo", simba atafuna mtoto. Mmiliki bwana kusaga anataka kuifunika.

Sometimes kumbe huwa una point. Sasa ongea basi na hao wenye kijani aka kikundi cha dhaifu wafanyie kazi mawazo yako. Maana wewe ni mshabiki wao mkubwa maybe watakusikiliza!


Hapo wenye zoo wanamakosa na watu wazima waliokwenda na huyo mtoto zoo wana makosa, hiyo hadithi ya kwenda chooni na mwingine kufatwa Inchon haina mshiko wala ukweli ndani yake. Wote (wenye zoo) na waangalizi wa huyo mtoto walikuwa wazembe.

Hapa Serikali lazima iingilie kati, hawa wenye ma zoo wana utaalam wa hizi zoo au wanapewa tu vibali kiushikaji? faida ya hiyo zoo kwa taifa ni nini au kwenda kuwatesa tu wanyama?

Kama ni mimi Tanzania ingeweka zoo ya wale wanyama adimu tu na hiyo zoo iwe inafanyia kazi kuwaongeza idadi yao na sio kwa ajili ya kuwafungia tu kuwacha watu wakatazame. Wange promote hawa watoto wawekewe huduma za kuwapeleka mbuga za wanyama wakajionee live. Faida inayopatikana kutoka kwa watalii wanaokuja kutazama hawa wanyama ingemegwa na kuanzisha idara ambayo itakuwa inawachukuwa mashuleni na kuwapeleka mbuga za wanyama hawa watoto zetu. Inawezekana, ni mipango tu.
 
Kwanza nawapa pole wanafamilia kwa tukio hilo.

Nimesikitishwa tu na hao wazazi kuruhusu watoto wadogo hivyo kwenda eneo hatarishi kama hilo. Hao wenye zoo walipoweka tangazo kuwa usalama ni juu yako mwenyewe walijua tukio kama hilo laweza tokea wakati wowote maana wanyama wa porini si rafiki wa binadamu tena inapotokea wamewekwa kwenye gereza na kuangaliwa na adui zao bila kuwa na uwezo wa kuwakabili. kwa hilo tangazo tayari linawaondoleeni nguvu ya kisheria maana mlitakiwa muwekweli Hapo Mhutumiwa namba moja ni Dada Lucy ambaye aliendanao Tegeta Zoo,Nilivyo sikia yule dada mwanzo alikuwa Mhudumu Tegeta Zoo.cha kushukuru kwenye hiyo familia ni kwamba Mtoto ajapatwa na matatizo makubwa.
 
Kwanza nawapa pole wanafamilia kwa tukio hilo.

Nimesikitishwa tu na hao wazazi kuruhusu watoto wadogo hivyo kwenda eneo hatarishi kama hilo. Hao wenye zoo walipoweka tangazo kuwa usalama ni juu yako mwenyewe walijua tukio kama hilo laweza tokea wakati wowote maana wanyama wa porini si rafiki wa binadamu tena inapotokea wamewekwa kwenye gereza na kuangaliwa na adui zao bila kuwa na uwezo wa kuwakabili. kwa hilo tangazo tayari linawaondoleeni nguvu ya kisheria maana mlitakiwa muwe makini lakini hamkufanya hivyo watoto wakaachwa kisa chooni. Huyo binamu anawezaje kuwaacha watoto wadogo 5yrs kwenye tundu la simba kwa kisingizio cha choo!? kimsingi huyo ndo alitakiwa awe mtuhumiwa namba moja maana yeye angekuwa makini wala ajali hiyo isingetokea na nyie wazazi muwe watuhumiwa namba 2 kwa kuruhusu watoto wasiojua lolote kwenda eneo hatarishi kwa maisha yao.

Msijisumbue na mahakama maana hamtoshinda tuhuma hizi zinawaangukia ninyi wenyewe. mtibieni mtoto apone. Mungu kamsaidia hakufa basi mshukuruni.

Aisee inaelekea sheria imekupiga chenga, imagine kwenye kila swimming pool inayotumika kibiashara kuna muangalizi, ndio ije kuwa zoo, tena ina hadi simba (the most predator animal). kaka usife moyo na michango ya watu hapa JF, huyo mtoto anatakiwa kupewa uangalizi na kama kuna fidia zozote zilipwe, kimbilia tume ya haki za binadamu utapata msaada wa kisheria haraka tu.
 
Na mimi naona hawa simba ni wazembe, simba wawili wanaishia kunyofoa nyama za paja pamoja kuachiwa wote ambapo mdada Lucy alikuwa chooni hata alipotoka akazirai hadi gabachori kaja.
 
Dah! huyo dogo nadhani alifikiri hao ni paka wakubwa kwahiyo akataka kwenda kuwakumbatia. Pamoja na hayo hapo kuna uzembe wa pande zote mbili, wazazi na wenye zoo. Nafikiri busara itumike zaidi kwa wenye zoo kumsaidia huyo mtoto apone kabisa.
 
Hapo wenye zoo wanamakosa na watu wazima waliokwenda na huyo mtoto zoo wana makosa, hiyo hadithi ya kwenda chooni na mwingine kufatwa Inchon haina mshiko wala ukweli ndani yake. Wote (wenye zoo) na waangalizi wa huyo mtoto walikuwa wazembe.

Hapa Serikali lazima iingilie kati, hawa wenye ma zoo wana utaalam wa hizi zoo au wanapewa tu vibali kiushikaji? faida ya hiyo zoo kwa taifa ni nini au kwenda kuwatesa tu wanyama?

Kama ni mimi Tanzania ingeweka zoo ya wale wanyama adimu tu na hiyo zoo iwe inafanyia kazi kuwaongeza idadi yao na sio kwa ajili ya kuwafungia tu kuwacha watu wakatazame. Wange promote hawa watoto wawekewe huduma za kuwapeleka mbuga za wanyama wakajionee live. Faida inayopatikana kutoka kwa watalii wanaokuja kutazama hawa wanyama ingemegwa na kuanzisha idara ambayo itakuwa inawachukuwa mashuleni na kuwapeleka mbuga za wanyama hawa watoto zetu. Inawezekana, ni mipango tu.

wazazi wa mtoto wanaweza kufungua kesi ya madai na wakashinda, sijui watapata faida gani , but wataendelea kuitwa wazembe forever. They are to blame themselves in the first place. Naona kama mtoto alimshambulia simba. Wana JF endeleeni .........................
 
Hii si mara ya kwanza..kuna kipindi mwaka jana Simba alitoroka na kuleta mtafaruku tukawa tunawah kujifungia ndani..Usimamiz hii zoo ni sifuri kabisaa sishangai sababu naifahamu ni jiran na mtaa wetu Tegeta Block F

Isiwe taabu wakati kesi inaendelea tuwarudishe simba mikumi
 
Ikiwa Wizara ya Mali Asili yenyewe imechakachuliwa mara kusafirisha wanyama hai nje hii ya kutoa vibali feki bila kuweka masharti yanayoeleweka itatugharimu Watanzania. Mhe Kagasheki afuatwe Bungeni Dodoma aone mkanda mzima.
 
Je simba wanotafuna watu kwenye mbuga za wanyama serikali uwa ina fidia? au ni uzembe wa marehemu?
 
Negligence in part of Zoo owner kwani kulitakiwa kuwe na Mwangalizi tena mwenye silaa in case chochote kitaenda mrama na aongoze watu wote wanaonda kuangalia ,wanayama huwa wanakumbuka asili once in a while.

Hapa fidia ni muhimu na hata kiubinadamu ilipaswa mwenye zoo ndio achukue jukumu la kuzungumza na familia sio kungoja kwenda mahakamani kama ni mtu mwenye busara maana hata wakienda huku ni Lawyers ndio watafaidi hizo fee tu hamna jingine na hakimu naye kama vipi anakula kidogo hapo. Aaaaaaaaaaaaaah hii nchi !

Kulingana na mtoa mada wenye Zoo walishatoa onyo kuwa unapoingia humu usalama sio Jukumu lao sasa utamwambiaje akulipe fidia na uzembe wako mwenyewe?
 
Kulingana na mtoa mada wenye Zoo walishatoa onyo kuwa unapoingia humu usalama sio Jukumu lao sasa utamwambiaje akulipe fidia na uzembe wako mwenyewe?

Tahadhari za kijinga kabisa hizo wanafikiri wanafuga nyau hapo ,tatizo kuna watu wamepewa leseni za kufanya mambo ambayo hawajui uendeshaji wake ni ubabaishaji mwanzo mwisho.
 
Aisee inaelekea sheria imekupiga chenga, imagine kwenye kila swimming pool inayotumika kibiashara kuna muangalizi, ndio ije kuwa zoo, tena ina hadi simba (the most predator animal). kaka usife moyo na michango ya watu hapa JF, huyo mtoto anatakiwa kupewa uangalizi na kama kuna fidia zozote zilipwe, kimbilia tume ya haki za binadamu utapata msaada wa kisheria haraka tu.

Hawezi kulipwa kitu. Hilo Onyo unapoingia Zoo lina maana kubwa sana kisheria la sivyo lisingewekwa. Hata unapoenda kupaki gari mahala ukakuta bango la park at your own Risk fikiria mara mbili kabla hujapaki ama kuna mlinzi au hakuna; wanapoandika Onyo sigara ni hatari kwa maisha yako... yoote hayo yana maana kisheria kuwa hicho kitu unachotaka kutumia si salama na hakuna atakae wajibika kwa madhara yoyote utakayoyapata kwa namna yoyote ile. Huyo mwenye Zoo hata hiyo 64000 aliotoa ni ubinadamu tosha.

Hao simba wenyewe walikuwa na Huruma vinginevyo wangeweza kumparamia Shingoni kama kinguruwe mwitu wakamchania chania mbali.
 
Shangaa simba?
Mtu alipasuliwa kichwa badala ya mguu we unashangaa simba kujeruhi mtoto?
Daktari bingwa anaamka asubuhi anapiga viroba anaandaa mikasi anamchukua mgonjwa na hayuko peke yake,anamchoma nusu kaputi anamnyoa nywele anaanza upasuaji anakuta hamna kitu anashona na hamna kesi wala mahala al;iposhtakiwa leo mnataka kumshitaki simba?
 
Na mimi naona hawa simba ni wazembe, simba wawili wanaishia kunyofoa nyama za paja pamoja kuachiwa wote ambapo mdada Lucy alikuwa chooni hata alipotoka akazirai hadi gabachori kaja.

hahahahahahahaaaaa... ilitakuwa na huyo Dada Lucy nae atafumwe na huyo Simba hapo palipomfanya aache watoto aende chooni. Kwani huyo simba alikuwa wa kiume au wa kike?

Haikosi kulikuwa na mkono wa ********* hapo.
 
Hii stori ilirushwa na ITV wiki kadhaa zilizopita,alipohojiwa huyu dada alokwenda na watoto alisema kwamba yeye alipokua anaendelea na malipo hapo kaunta ya zoo hao watoto waliingia ndan...ndo yakawakuta hayo,,,any way
mwanasheria anapaswa kutoa ushaur,ila najiuliza kwanini hado leo mamlaka husika hazijaifatilia hiyo ZOO,ni muda sasa umeshayoyoma
 
Pole kwa mtoto pole kwa familia, inasikitisha! wao wana pesa nyie simameni upandea wa MUNGU, poleni sana
 
Ni swali tu bandugu: Je na mwenye zoo naye akihitaji fidia
kwa sababu mtoto akuwa chini ya uangalizi wa karibu wa
watu aliokuja nao ambao pia walipaswa kuhakikisha
anakuwa chini ya uhangalizi! Sheria imekaaje hapo?

tarehe09/06/2012 ndugu titus mahanga, aliiruhusu familia yake kwenda tegetazoo kuangalia wanyama. Kwa wale msioifahamu tegeta zoo ipo tegetakibaoni 2km kutoka ilipo barabara kuu. Hii zoo inamilikiwa na bwana wilison kusaga.

mtoto aliyeshambuliwa na simba anaitwa newton titus (5), aliongozana na binamu zake diana (8),
lucy (28).
taratibuza pale zoo unapofika usalama ni juu yako, mtoto newton titus (5)pamoja na binamu zake baada ya kuingia ktk zoo walianza kuzunguka nakuangalia wanyama mbalimbali, walipofika karibu na banda la simba binamu wao (lucy-28) akaenda chooni akawaacha binamu zake (newton na diana) nje wamngoje. mtotonewton (5) akatumia muda huo kwenda banda la simba, chakushangaza banda la simba halikuwa na msimamizi yeyote isitoshe uzio au fensi ya banda lilikuwa halina kufuli bali mlangou mebanwa tu kwa kutumia komeo, mtoto newton (5) akaenda kufungua ulemlango wa banda la simba ndipo akakumbwa na hiyo dhahama, kulikuwa nasimba wawili wakamshambulia vibaya sana mtoto. Wakati tukio hilo likiendelea mtoto mwingine anayeitwa diana (8) akakimbia kwenda kumuita binamu wao aliyekuwa chooni ambaye anaitwa lucy (28) alipotoka choonikwa taharuki akakuta newton (5) akishambuliwa na simba, lucy akaziraipale pale. bahatinzuri alitokea mtalii mwingine mwenye asili ya asia akamwokoa mtoto newton kutoka ktk makucha ya simba na kumkimbiza hospitali kwa gari yake (mico dispensary iliyopo tegeta).

Mtoto newton kajeruhiwavibaya kichwani, pajani na kiunoni. Mtoto baada ya kupewa matibabu pale dispensary mke wa mmiliki wa zoo mrs kusaga akalipia gharama ya tshs. 64,000/=, chakusikitisha hakuwahi kutoa tena msaada wa aina yeyote kwa mtoto newton wala kujulia maendeleo ya mtoto.
baba wa mtoto bwana titus mahanga alipeleka malalamiko police tegeta naakapewa rb, police wakamwita mrs kusaga kwa mahojiano lakini hakuna kitu ambacho kimefanyika mpaka sasa, zaidi ni police kumtisha bwana titus mahanga asijaribu kumshitaki bwana willilson kusaga.

wanajf
bwabatitus mahanga anataka ushauri wenu wa kisheria juu ya bwana willium kusaga mmiliki wa tegeta zoo, ikumbukwe kama banda la simba (uzio)ungefungwa kwa kufuli mtoto newton asingepatwa na dhahama iliyomkutakupelekea kuatarisha maisha yake. Mpaka sasa hivi mtoto bado haliyake sio nzuri. Na kwa mujibu wa daktari anadai mtoto akiri yakeishavurugika, atakuja kuwa katili au mjinga.

namba ya mzazi bwana titus mahanga 0717 / 0767 – 441044
gongola mboto – dar es salaam.
View attachment 57498
mtoto newton akiwa na baba yake.

View attachment 57500
mtoto akipatiwa huduma na daktari

View attachment 57501
nyama ya paja ikiwa imenyofolewa na simba


View attachment 57502
mtoto akiwa na majera ya simba kichwani
 
Back
Top Bottom