Picha:Rais Kikwete afuturisha wasanii ikulu

Picha:Rais Kikwete afuturisha wasanii ikulu

Status
Not open for further replies.
ii. Nini maana halisi ya "Kufuturu" na "Kufuturisha" kwa Mwislamu safi na miiko yake?
/QUOTE]
Mkuu hapa nimepapenda sana....kama alikuwa anataka kufuturisha kwanini asifuturishe yatima na watu wenye mazingira magumu??...hiki kilikuwa kikao ila si rasmi..
 
f41.jpg


hii gauni inayoonyesha ndani inaruhusiwa kwenye mfungo? n.k?

Halafu ni kwa nini asiwaalike wakina Muhidin Gurumo na the like? au wao sio wasanii? au walikuwa na siku yao?
 
Hapa ndipo ninapomsifu Bakhresa, anatukanwa na kukashfiwa
lakini yupo kimya huku akiwafuturisha watu kimyakimya bila
picha wala TV
Huku akiwasaidia anaowasaidia bila kelele wala maneno.
 
Vipi kuhusu watoto wa mtaani ambao hawawezi kuaford hata karanga za shilingi mia nao watafuturishwa? ,na wakina mama wajawazito walioko hospitalini na hawana vitanda vya kulalia,?wazee ambao hawana hata nguo na wengine wako vijijini kwenye baridi? Nasubiri kweli nione na wao wakifuturishwa.
 
sio mbaya kwa rais kuutambua mchango wa wasanii.
asiishie kuwafuturisha ahakikishe pia anawaagiza wahusika
wahakikishe maslahi yao hayaibiwi na hawa kunjubhai......na mapromota au mameneja njaa
190px-Kuchipudi_Mihira_Pathuri_.jpg
 
Sifahamu dhana ya kufuturisha imekaaje!
Je wanaoalikwa ni Bongofleva Waislamu au wote?...
Na je unapomfuturisha mtu mwenye uwezo wa kutosha (kama hao Bongofleva) na kuwaacha wananchi masikini wanaofukuzana kupata muhogo wa kuokota ili kuandaa futari, ni swahihi?

Unatakiwa ufutarishe Maskini sio watu wenye uwezo kama hao Punda wa madawa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom