Picha: Rais Uhuru Kenyatta amzawadia gari Mbunge John Mwirigi

Picha: Rais Uhuru Kenyatta amzawadia gari Mbunge John Mwirigi

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
964418bc2a2053a5e9563693614da3a9.jpg
bf1783de47fe9835bd85ef517e5482d2.jpg
e4af219e784a12918df42b7b3ef71eec.jpg
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amemzawadia gari Mbunge wa Igembe Kusini, John Paul Mwirigi (23) ambalo alikuwa amemuahidi.

John Paul Mwirigi, ndiye mbunge mwenye umri mdogo zaidi nchini Kenya, alichaguliwa akiwa bado Mwanafunzi wa Chuo Kikuu.

Bw. Mwirigi alitumia baiskeli na pikipiki za kusafirisha abiria, maarufu kama bodaboda, kuwafikia watu wakati wa kampeni.

Pesa nyingi alizotumia wakati wa kampeni alizipokea kutoka kwa wahisani.

Wakati wa kuapishwa alitumia magari ya uchukuzi wa umma kufika majengo ya Bunge jijini Nairobi.

Wabunge walipoalikwa Ikulu, alipewa lifti na Mbunge mwenzake.

Hata hivyo wakati wa kuondoka alitumia gari la uchukuzi wa umma maarufu kama matatu.

"Nimetimiza ahadi yangu kwa mbunge kijana wa Igembe Kusini John Paul Mwirigi katika Ikulu ndogo ya Sagana", alisema Rais Kenyatta.
 
mwiringi.jpg
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amemzawadia gari Mbunge wa Igembe Kusini, John Paul Mwirigi (23) ambaye ndiye mbunge mwenye umri mdogo zaidi nchini Kenya

Rais Kenyatta aliahidi kumnunulia mbunge huyo gari ambaye alikuwa ni mgombea binafsi baada ya kutangazwa mshindi katika uchaguzi wa Agosti 8 mwaka huu.

Mbunge huyu mdogo Mwiringi alifanya kampeni zake kwa miguu na baiskel katika jimbo zima.

"Tumeamua kumchagua. Hakuwa na fedha za kufanya kampeni lakini alitoa ahadi nzuri kwetu na ilani yake ni nzuri" wananchi wake walisema.
 
Prado iyo uku bongo no 60mil tsh. ...hongera kwake na Uhuru kwa roho nzuri...
Angeweza kunyamaza tu na asiulizwe na mtu
 
Mpaka atakapogawa kipande kidogo cha ardhi yake kwa watu wa kibera ndipo nitaamini kuwa anajali, laa sivyo ni maigizo tuu.


Hawezi,

Mabepari huwa watamani wachukue hata pichu (boxer) unayovaa ili uwaabudu zaidi.
 
Aisee hivi mbona mimi sikutanagi na vismati kama hivi?
 
Hawezi,

Mabepari huwa watamani wachukue hata pichu (boxer) unayovaa ili uwaabudu zaidi.
Exactly Mkuu. Hasa nchi za Afrika zimezidi kunyonya kila kitu hadi maji mwilini.
 
Back
Top Bottom