Picha ya babu yetu aliyeacha kununua shamba la heka 500 kwa Tsh. 30 akisema hawezi kuishi Kimara porini kwenye fisi!

Enzi hizo baiskel inalipiwa ushauru
 
Huyu jamaa ni Sory Sanlé ilipigwa mwaka 1963 huko Burkina Faso. Mtoa mada kadanganya Hapa.
 
hata kama mimi pia nisingekubali,kila jambo linaenda na wakati,siwezi kununua pori nisilo na kazi nalo.
Uko sahihi kabisa. Hata mitaa ya Sinza kuna wazee wengi tu walisema walikataa kununua kwa bei chee kabisa kwa sababu eneo lilikuwa limejaa maji. Kila kitu na wakati wake. Hata kijana wa leo hebu muuze juzi juzi tu mwaka 2011 bitcoin ilikuwa na thamani ya dola 1 lakini sasa hivi 2024 ina thamani ya dola 68,000. Yaani kama ungekuwa umetumia dola 100 tu kununua bitcoin kipindi hicho cha 2011 sasa hivi ungekuwa na dola 6,800,000.
 
Daa nina picha zangu kama hizo kibao tu
Ila maisha ya zamani raha ingawa tulikuwa hatuna Internet
Siku hizo kuna mitandao na mnashawishiana kuwekeza kupitia forums na simu janja
Sasa sisi zamani kama umezungukwa na wasiojielewa lini utapata ideas
Hata sasa pia kuna fursa zisiwapite vijana
Acheni kula Bata wekezeni sana kama ngumu basi muwe na malengo hata ya miaka 20
 
Tena walikuwa wanakagua stika za ushuru kama pikipiki kwa sasa
 
Ujachelewa hata wewe kwa sasa nenda kakamate mbuga ili miaka 30 usichekwe
 
Nyerere ndie aliyeua Idea za wazee wetu ilikuwa ukiwekeza kwenye mijengo viwanja mashamba unakamatwa ndani kesi ya uhujumu uchumi,ikawalazimu wazee waoe wake wengi walewe na kufungua zipu ili pesa ziishe TU.
Maana ukikutwa nazo kesi.
Ukizingatia usalama wa taifa wa zamani walikuwa viherehere kishenzi wapo mbele ili wakuharibie
 
Huwa nalaani kila leo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…