Picha za Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika zimebeba historia kubwa

Picha za Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika zimebeba historia kubwa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
PICHA HIZI ZA JENGO LA AL JAMIATUL ISLAMIYYA FI TANGANYIKA ZINASEMA MANENO ELFU MOJA

Picha hizo hapo chini za majengo mawili ya Al Islamiyya fi Tanganyika zimekuwa ndani ya Maktaba kwa zaidi ya miaka ishirini lakini zilikuwa picha tu.

Moja katika hizo picha tatu iko kwenye kitabu cha maisha ya Abdul Sykes (1998) lakini ilikuwa picha kama picha nyingine yeyote ile.

Leo picha hizi zikaletwa hapa FB kama, ''Your Memories in Facebook,'' nikawa nazitazama.

Sasa nikawa naangalia picha kwa kuanza na picha moja baada ya nyingine kwa wale ambao mimi niliwafahamu wakati wa utoto wangu hadi nanyanyukia nikiwa kijana na kidogo wengine nikawanao zaidi ya hapo.

Nimeiangalia ofisi ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika iliyokuwa uani nyuma ya jengo lenyewe la taasisi hiyo, jengo lililokuwa Muslim School.

Nyumba hii aliishi Ali Mwinyi Tambwe (akiwa Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya baada ya Kleist kujiuzulu nafasi hiyo mwaka wa 1940), hii nyumba ilikuwa imeungana na ofisi.

Nikamwangalia Maalim Mohamed Matar katika picha wakati ule kijana.

Picha yake ya ujana nimeiweka hapo chini.
Picha hizi imepigwa katika miaka ya 1930s.

Maalim Mohamed Matar alikuwa akisomesha dini hapo shuleni na mwalimu wa Qur'an na ndiye aliyemuanzisha Abdul Sykes, na wadogo zake wawili Ally na Abbas alif kwa kijiti.

Maalim Matar alikuja akawa rafiki mkubwa wa Abdul Sykes ukubwani kwake na Abdul Sykes alipofariki, Maalim Matar ndiye aliyemkosha akisaidiana na Sheikh Kassim Juma.

Naendelea kumwangalia Maalim Matar na mengi katika mambo yaliyomfika ya kukamatwa na kufungwa jela Zanzibar baada ya mapinduzi yananijia.

Yananijia mazungumzo yangu na Kleist Abdulwahid miaka mingi nyuma akinieleza simanzi iliyompata baba yake, Abdul Sykes aliposikia kuwa mwalimu na rafiki yake Maalim Matar kakamatwa na kapelekwa jela Zanzibar.

Ilimshangaza Abdul Sykes ni sababu gani Maalim Matar atakamatwa ilhali Maalim Matar hakupata katika maisha yake kujihusisha na siasa yoyote si Tanganyika wala Zanzibar.

Baadae ikasikika kuwa kulikuwa na watu wanaomba dua serikali ya Karume ianguke.

Katika kamatakamata ya wavutaji nyuradi Maalim Matar akasombwa maana yeye muda wote ana tasbih mkononi anamsabih Mola wake.

Maalim Matar (nyuma wa kwanza kushoto), Kleist Sykes, Ali Mwinyi Tambwe na Abdul Sykes niliowataja mpaka hapa watafute kwenye picha.

Abdul ni huyo mtoto mdogo mwanafunzi wa shule ya msingi hapo Muslim School hapo kwenye picha kavaa koti na kofia ya tarbush.

Baba yake, Kleist Sykes yuko pia kwenye hiyo picha mtafute.

Nakumbuka siku nilipokwenda nyumbani kwa Ali Mwinyi Tambwe wakati natafiti kitabu cha Abdul Sykes.

Ali Mwinyi aliniambia, "Mimi mkubwa sana kwa Abdul na Ally nikiwaona wanakuja sala ya Maghrib Msikiti wa Kitumbini wameshikwa mikono na baba yao."

Mwangalie Ali Mwinyi Tambwe umri wake na mtazame Abdul Sykes uone walivyopishana umri.

Katika uongozi wake Kleist akiwa Katibu na Mzee bin Sudi, Rais ndipo majengo hayo yakajengwa na Muslim School kuanzishwa.

Allah aliwakutanisha hawa watu watatu Maalim Matar, Ali Mwinyi Tambwe na Abdul Sykes miaka mingi baadae katika historia ya kusisimua wakati Tanganyika inadai uhuru wake miaka ya 1950.

Ali Mwinyi Tambwe alikwenda Nansio, Ukerewe na Abdul Sykes mwaka wa 1953 wakati huo Abdul ni Katibu na Kaimu Rais wa TAA kukutana na Hamza Mwapachu kupata kauli yake kuhusu kumtia Julius Nyerere katika uongozi wa juu wa TAA na mwaka unaofuatia, 1954 iundwe TANU na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Ali Mwinyi Tambwe mwaka wa 1964 atahusika katika mapinduzi ya Zanzibar yaliyopelekea baadae Maalim Matar akamatwe Dar es Salaam kusafirishwa Zanzibar na kufungwa jela ambako aliteswa sana.

Jengo la Al Jamiatul Islamiyya lilimaliziwa ujenzi na Aga Khan, Patron wa EAMWS mwaka wa 1936 baada ya kuona juhudi za Waislam kutaka kujenga shule.

Safari ya kwanza ya Julius Nyerere kwenda UNO mwaka wa 1955, hafla ya kumuaga ilifanyika katika jengo hili.

Jengo hili lililobeba historia kubwa ya ukombozi wa Tanganyika limechukuliwa na serikali baada ya kuvunjwa kwa EAMWS na kuundwa BAKWATA mwaka wa 1968 na ingawa jitihada nyingi zimefanyika kutaka lirejeshwe kwa Waislam jitihada hizi hazijafanikiwa.

Maisha ya wazalendo niliowataja yamebeba mengi katika historia ya uhuru wa Tanganyika.




 
1617226372310.png

Hii siyo Lumumba primary school.

Rafiki zangu wengi wamesoma hapa miaka ya ilee..
 
Sheikh Mohammed Said nina suali moja hivi ikiwa sisi waislam tumeweza kuwaondoa wakoloni. Kwanini sasahivi tunashindwa kusimamisha haki na usawa kwa watanzania wote.( Waislam kuwa na haki sawa na Wakristo) nini kimeturejesha nyuma kwenye kupigania harakati zetu za uhuru na usawa?


Mbuzibee 🐐
 
Sheikh Mohammed Said nina suali moja hivi ikiwa sisi waislam tumeweza kuwaondoa wakoloni. Kwanini sasahivi tunashindwa kusimamisha haki na usawa kwa watanzania wote.( Waislam kuwa na haki sawa na Wakristo) nini kimeturejesha nyuma kwenye kupigania harakati zetu za uhuru na usawa?


Mbuzibee 🐐
We jamaa ni sawa na caveman, Neanderthal au Cro magnon.
 
[emoji16]
Underwood,
Historia hii ya wazee wangu katika 1900s imekuudhi?

Kipi kibaya nilichoandika?

Kama kuna lisilopendeza lieleze lifahamike.

Hiyo shule ndiyo aliyosoma baba yangu na babu yangu alishiriki katika kuijenga.

Wewe huna historia kama hii ya wazee wako?

Hayo maneno mengine siyajui ningependa unifahamishe.

Ama roho yako imeungua kusoma kuwa hafla ya safari ya Baba wa Taifa UNO February 1955 ilifanyika ndani ya shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika?

Hii ni historia tu ndugu yangu huwezi kuifuta.
 
Sheikh Mohammed Said nina suali moja hivi ikiwa sisi waislam tumeweza kuwaondoa wakoloni. Kwanini sasahivi tunashindwa kusimamisha haki na usawa kwa watanzania wote.( Waislam kuwa na haki sawa na Wakristo) nini kimeturejesha nyuma kwenye kupigania harakati zetu za uhuru na usawa?


Mbuzibee 🐐
Wakristo wajanja sana aisee.
 
Sheikh Mohammed Said nina suali moja hivi ikiwa sisi waislam tumeweza kuwaondoa wakoloni. Kwanini sasahivi tunashindwa kusimamisha haki na usawa kwa watanzania wote.( Waislam kuwa na haki sawa na Wakristo) nini kimeturejesha nyuma kwenye kupigania harakati zetu za uhuru na usawa?


Mbuzibee 🐐
Mbuzi...
Umeuliza swali zuri sana ambalo halijibiki kwa mistari miwili mitatu.

Katika kitabu cha Abdul Sykes mwisho wa kitabu nimeeleza changamoto zilizokuja na uhuru.

Soma kitabu hiki utapata majibu.
 
Sheikh Mohammed Said nina suali moja hivi ikiwa sisi waislam tumeweza kuwaondoa wakoloni. Kwanini sasahivi tunashindwa kusimamisha haki na usawa kwa watanzania wote.( Waislam kuwa na haki sawa na Wakristo) nini kimeturejesha nyuma kwenye kupigania harakati zetu za uhuru na usawa?


Mbuzibee 🐐

Haki gani wanayokosa waislamu wa Tanzania?
 
Haki gani wanayokosa waislamu wa Tanzania?
Ndahani,
Sehemu katika Waraka wa Shura ya Maimamu Uchaguzi Mkuu 2020:

WAISLAMU TUNATAKA HAKI NA USAWA
Hapo nyuma tumezungumza kama Watanzania. Maelezo yetu yamejadili na kupigania maslahi ya Taifa na Watanzania kwa ujumla. Lakini pia sisi ni Waislamu na kama yalivyo makundi mengine ya kijamii tunao wajibu wa kutafakari, kujitazama na kutazamwa kwa maslahi yetu. Waislamu wanatambua kuwa siasa ni sehemu muhimu ya maisha yao na hawawezi kujitenga na siasa. Kwasababu hiyo wanaelewa mfumo wa siasa usio wa haki na usawa unaweza kuathiri ustawi wa maisha yao ya kila siku kidini, kijamii, kiuchumi, kiusalama, kiutamaduni na kadhalika.

Tunaweza kusema siasa inanafasi kubwa katika mustakbali wa ustawi wao. Waislamu tumeshiriki ipasavyo chaguzi za nyuma ukiwemo uliounda serikali iliopo madarakani. Lengo likiwa ni kushiriki katika ujenzi wa Taifa bora, huru na lenye maendeleo. Taifa la wote linalotenda Haki, Usawa na Uadilifu kwa wote. Tukitaraji tuwe na Uongozi wa nchi unaowatendea haki wananchi wote bila ubaguzi wa Kidini, Kikabila, Jinsia, Rangi au eneo analotoka mtu.

Mpaka sasa Waislamu wameshindwa kuona nafuu yao katika matokeo ya siasa hizo. Hawaoni nafuu katika Uhuru wa kuabudu, Uhuru wa Kujiamulia mambo yao wenyewe (hata yale ya kidini), Usalama wa Viongozi wao, Madrasa zao, Misikiti na Watu wao. Hawaoni usawa wowote katika madaraka na ajira za serikali. Mfumo wa Elimu wa Taifa hautoi fursa sawa wala kutenda haki kwa wote. Orodha ya viashiria vya tatizo hilo ni kubwa mno lakini tunaweza kupitia hivi vichache:

Uadilifu I

Januari 11, 2019, serikali ilifanya uhamisho mkubwa wa kushitukiza kwa wahadhiri na watumishi wandamizi katika Chuo Kikuu cha Serikali cha Dodoma-UDOM. Waliohamishwa walikuwa 11, lakini wote walikuwa Waislamu: Dk. Maryam Khamis (Director of Graduate Studies), Dk. Ibun Kombo (Political Science), Dk. Mwinyikombo Amir (Mwalimu wa Udaktari wa Binadamu), Dk. Yusuf Kambuga (College of Education), Dk. Masoud Masoud (Informatics) , Bw. Subira Sawasawa (Mkurugenzi Mkuu Rasilimali Watu), Bw. Mohamed Mwandege (Bursar/Mhasibu Mkuu), Bi. Aziza Gendo (Seniour Estate Oficer), Bw. Simba Omary (Senior Supplies Oficer), Bw. Wema Mbegu (Legal Oficer), Bw. Khamis Mkanachi (Mwalimu wa Idara ya Historia).

Barua zao za uhamisho hazikuonesha makosa katika utendaji wao wa kazi au uongozi. Pamoja na kutokuwa wakosaji, uhamisho wao uliambatana na udhalilishaji mkubwa, kunyimwa haki stahiki za uhamisho, kuhamishiwa katika nafasi za chini kinyume na hadhi zao.

Baada ya uhamisho huo, Serikali ilifanya uteuzi mwingine katika chuo hicho hicho cha Serikali. Katika uteuzi huo walioteuliwa walikuwa 11, wote Wakristo: Prof. Leonard James Mselle, Prof. Adam B. Swebe Mwakalobo, Prof. Julius William Nyahongo, Prof. Justin Ntalikwa, Prof. Frowing Paul Nyoni, Prof. Odass Bilame, Prof. Ainory Piter Gasese, Dkt. Victor George Mareale, Dkt. Alex Shayo, Dkt. Calvin Swai, Dkt. Augustine Mwakipesile.

Kuhamisha wahadhiri 11, katika Chuo Kikuu si jambo dogo. Vilevile kuhamisha Wahadhiri 11, wa dini moja (Waislamu) katika Chuo Kikuu ukaingiza wahadhiri 11 wa dini moja (Wakristo), na hao Waislamu 11, baadhi yao ukawatoa kabisa katika mfumo wa elimu kwa kuwapeleka sekta nyingine na zisizo lingana na hadhi zao si jambo dogo. Wala si hatua ya kitaalamu ya kuboresha mfumo wa Elimu wa Taifa. Na wala si hatua ya kijinga bali ya werevu uliofurutu ada dhidi ya maslahi ya Taifa. Hatuwa hiyo ni salamu nzito kwa jamii yao na Taifa kwa ujumla. (Ndio maana katika maoni yetu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tulipendekeza Katiba Mpya imtambuwa Mwenyezi Mungu na Dini liwe suala rasmi na la wazi katika uendeshaji wa nchi).

Uadilifu II

Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:

Mawaziri na Manaibu: 30.

Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.

Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.

Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.

Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.

Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.

Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.

Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.

Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.

Wakurugenzi mbalimbali: 249.

Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.

Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.

Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.

Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.

Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33

Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.

Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.

Jumla Kuu ya Uteuzi:

Waislamu asilimia 20%.

Wakristo asilimia 80%.
 
Waarabu ni Watakatifu, hawaujui uovu na wala hawajahi kuutenda, ndio maana kwao hamna Pombe, kitimoto, mademu, ufisadi nk
Sio kweli kwa mtazamo huo.Ukikuta waarabu wako kama hivyo basi ni imani yao ya dini basi. Binadamu na shetani daima wako vitani na ushindi wa binadamu upo pale ambapo anafuata imani thabiti ya dini nayo ni uislamu.

Yapo maovu yaliyofanywa na waarabu ambayo yanatisha kabla hawakumbushwa imani ya Kiislamu.
 
Mmeanza chokochoko baada ya kuona bwana mkubwa ni mwenzetu
 
Kaka Mohamed hujachoka na propaganda zako za kutaka tusione maovu ya waarabu wenzako kaka? Du!
Hahaha.. huna ulijualo..umelishwa tango pori!

FYI, mshukuru Mungu umetumia lugha ya kiarabu kujieleza humu na kuwa Civilized... Ustaarabu na elimu na lugha yako umefundishwa na waarabu!! Hebu rudi huko Pangoni, porini unauliza.

Umezaliwa na chuki, hasira na ukatili.
 
Back
Top Bottom