Picha za Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika zimebeba historia kubwa

Picha za Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika zimebeba historia kubwa

Hawana ujanja wowote mbali ya kupenda kudhulumu kutokana na kutofuata dini takatifu.
Ukiona upole wa waislamu unaodumisha amani ni sababu ya kufundishwa kuwa na subira.

Siamini katika kudhulumiwa. Naamini katika competence ya mtu. Haya yanayosemwa si kweli. Hakuna anayenyimwa kuabudu Tanzania. Sijafanya kazi serikalini ila najiuliza kwani lazima muwe wakurugenzi na mawaziri kuleta impact?
Dunia ya sasa ni pana na ina mambo mengi. Kusema siasa ndio pekee itamkomboa mtu ni kujidanganya nafsi. One of the unique ways that make some socities, no matter how small there numbers are, continue evolving, is there ability as a society to do self reinvention.
 
Ndahani,
Sehemu katika Waraka wa Shura ya Maimamu Uchaguzi Mkuu 2020:

WAISLAMU TUNATAKA HAKI NA USAWA
Hapo nyuma tumezungumza kama Watanzania. Maelezo yetu yamejadili na kupigania maslahi ya Taifa na Watanzania kwa ujumla. Lakini pia sisi ni Waislamu na kama yalivyo makundi mengine ya kijamii tunao wajibu wa kutafakari, kujitazama na kutazamwa kwa maslahi yetu. Waislamu wanatambua kuwa siasa ni sehemu muhimu ya maisha yao na hawawezi kujitenga na siasa. Kwasababu hiyo wanaelewa mfumo wa siasa usio wa haki na usawa unaweza kuathiri ustawi wa maisha yao ya kila siku kidini, kijamii, kiuchumi, kiusalama, kiutamaduni na kadhalika.

Tunaweza kusema siasa inanafasi kubwa katika mustakbali wa ustawi wao. Waislamu tumeshiriki ipasavyo chaguzi za nyuma ukiwemo uliounda serikali iliopo madarakani. Lengo likiwa ni kushiriki katika ujenzi wa Taifa bora, huru na lenye maendeleo. Taifa la wote linalotenda Haki, Usawa na Uadilifu kwa wote. Tukitaraji tuwe na Uongozi wa nchi unaowatendea haki wananchi wote bila ubaguzi wa Kidini, Kikabila, Jinsia, Rangi au eneo analotoka mtu.

Mpaka sasa Waislamu wameshindwa kuona nafuu yao katika matokeo ya siasa hizo. Hawaoni nafuu katika Uhuru wa kuabudu, Uhuru wa Kujiamulia mambo yao wenyewe (hata yale ya kidini), Usalama wa Viongozi wao, Madrasa zao, Misikiti na Watu wao. Hawaoni usawa wowote katika madaraka na ajira za serikali. Mfumo wa Elimu wa Taifa hautoi fursa sawa wala kutenda haki kwa wote. Orodha ya viashiria vya tatizo hilo ni kubwa mno lakini tunaweza kupitia hivi vichache:

Uadilifu I

Januari 11, 2019, serikali ilifanya uhamisho mkubwa wa kushitukiza kwa wahadhiri na watumishi wandamizi katika Chuo Kikuu cha Serikali cha Dodoma-UDOM. Waliohamishwa walikuwa 11, lakini wote walikuwa Waislamu: Dk. Maryam Khamis (Director of Graduate Studies), Dk. Ibun Kombo (Political Science), Dk. Mwinyikombo Amir (Mwalimu wa Udaktari wa Binadamu), Dk. Yusuf Kambuga (College of Education), Dk. Masoud Masoud (Informatics) , Bw. Subira Sawasawa (Mkurugenzi Mkuu Rasilimali Watu), Bw. Mohamed Mwandege (Bursar/Mhasibu Mkuu), Bi. Aziza Gendo (Seniour Estate Oficer), Bw. Simba Omary (Senior Supplies Oficer), Bw. Wema Mbegu (Legal Oficer), Bw. Khamis Mkanachi (Mwalimu wa Idara ya Historia).

Barua zao za uhamisho hazikuonesha makosa katika utendaji wao wa kazi au uongozi. Pamoja na kutokuwa wakosaji, uhamisho wao uliambatana na udhalilishaji mkubwa, kunyimwa haki stahiki za uhamisho, kuhamishiwa katika nafasi za chini kinyume na hadhi zao.

Baada ya uhamisho huo, Serikali ilifanya uteuzi mwingine katika chuo hicho hicho cha Serikali. Katika uteuzi huo walioteuliwa walikuwa 11, wote Wakristo: Prof. Leonard James Mselle, Prof. Adam B. Swebe Mwakalobo, Prof. Julius William Nyahongo, Prof. Justin Ntalikwa, Prof. Frowing Paul Nyoni, Prof. Odass Bilame, Prof. Ainory Piter Gasese, Dkt. Victor George Mareale, Dkt. Alex Shayo, Dkt. Calvin Swai, Dkt. Augustine Mwakipesile.

Kuhamisha wahadhiri 11, katika Chuo Kikuu si jambo dogo. Vilevile kuhamisha Wahadhiri 11, wa dini moja (Waislamu) katika Chuo Kikuu ukaingiza wahadhiri 11 wa dini moja (Wakristo), na hao Waislamu 11, baadhi yao ukawatoa kabisa katika mfumo wa elimu kwa kuwapeleka sekta nyingine na zisizo lingana na hadhi zao si jambo dogo. Wala si hatua ya kitaalamu ya kuboresha mfumo wa Elimu wa Taifa. Na wala si hatua ya kijinga bali ya werevu uliofurutu ada dhidi ya maslahi ya Taifa. Hatuwa hiyo ni salamu nzito kwa jamii yao na Taifa kwa ujumla. (Ndio maana katika maoni yetu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tulipendekeza Katiba Mpya imtambuwa Mwenyezi Mungu na Dini liwe suala rasmi na la wazi katika uendeshaji wa nchi).

Uadilifu II

Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:

Mawaziri na Manaibu: 30.

Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.

Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.

Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.

Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.

Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.

Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.

Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.

Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.

Wakurugenzi mbalimbali: 249.

Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.

Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.

Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.

Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.

Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33

Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.

Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.

Jumla Kuu ya Uteuzi:

Waislamu asilimia 20%.

Wakristo asilimia 80%.

Kwahiyo Shekhe Mohammed, leo kwa mfano serikalini waislam wakawa asilimia 80, mambo yenu yatakuwa sawa?
Naogopa sana mtu anayeidanganya nafsi yake mwenyewe.
Sifanyi kazi serikalini na kusema kweli sio lazima. Hata watoto wangu nawafundisha ukweli kuwa Dunia hii ni pana sana. Watafute maarifa. If they opt to narrow their minds, they should not blamed anybody.
Kama society haijaweza kujitambua na kutambua nini malengo ya maisha yao hapa duniani, hata tuwape nafasi gani bado watalalamika wanaonewa.
Sikubaliani na wewe kabisa unaposema waislamu wanazuiwa kuabudu. Wapi? Na kwanini?
Kuna sehemu wamejenga msikiti wakakatazwa kuabudu? Au wamechukua jengo ambalo hawana mahesabu nalo wakakatazwa.
 
Kwahiyo Shekhe Mohammed, leo kwa mfano serikalini waislam wakawa asilimia 80, mambo yenu yatakuwa sawa?
Naogopa sana mtu anayeidanganya nafsi yake mwenyewe.
Sifanyi kazi serikalini na kusema kweli sio lazima. Hata watoto wangu nawafundisha ukweli kuwa Dunia hii ni pana sana. Watafute maarifa. If they opt to narrow their minds, they should not blamed anybody.
Kama society haijaweza kujitambua na kutambua nini malengo ya maisha yao hapa duniani, hata tuwape nafasi gani bado watalalamika wanaonewa.
Sikubaliani na wewe kabisa unaposema waislamu wanazuiwa kuabudu. Wapi? Na kwanini?
Kuna sehemu wamejenga msikiti wakakatazwa kuabudu? Au wamechukua jengo ambalo hawana mahesabu nalo wakakatazwa.
Ndahani,
Nadhani umeingia katika mjadala huu ukiwa umeshasonga mbele sana kwa hiyo huelewi maudhui yake.
Ikiwa una haja ya kufanya mjadala na mimi sasa itakubidi uanze mwanzo usome nini mimi na wengine tumeandika.

Hakuna popote nimezungumzia suala la kuabudu.

Lakini kwa haraka na wepesi unaweza kuanza na hizo takwimu za mgawao wa nafasi kama zilivyoandikwa na Shura ya Maimamu.
 
Kwahiyo Shekhe Mohammed, leo kwa mfano serikalini waislam wakawa asilimia 80, mambo yenu yatakuwa sawa?
Naogopa sana mtu anayeidanganya nafsi yake mwenyewe.
Sifanyi kazi serikalini na kusema kweli sio lazima. Hata watoto wangu nawafundisha ukweli kuwa Dunia hii ni pana sana. Watafute maarifa. If they opt to narrow their minds, they should not blamed anybody.
Kama society haijaweza kujitambua na kutambua nini malengo ya maisha yao hapa duniani, hata tuwape nafasi gani bado watalalamika wanaonewa.
Sikubaliani na wewe kabisa unaposema waislamu wanazuiwa kuabudu. Wapi? Na kwanini?
Kuna sehemu wamejenga msikiti wakakatazwa kuabudu? Au wamechukua jengo ambalo hawana mahesabu nalo wakakatazwa.
Wewe inaonekana ni mtu wa kuropoka na kweli hauko serikalini na jengine umezoea kuwatukana waislamu na huwajui waislamu ni nani katika hii Tanzania angalau kabala mtazamo mpana wa dunia,
Mfano wa matusi yako kwa waislamu unapatikana hata kwenye hiki kipande kifupi ulichoandika.Unaposema mkiwa asilimia 80 ndio mambo yenu yatakuwa sawa?.Mambo yetu sisi kama nani kwako.Wewe kwa mtazamo wako huna sifa ya kuwaambia waislamu ni narrow minded na waislamu upana wa mawazo haufundihiwi na wewe na wala mtu mwengine yoyote.Upana wa mawazo ya waislamlu unapatikana katika Qur'an na sunna za Mtume Muhammad s.a.w.
Ukija upande mwengine uliogusia hapo kwa ujinga wako ni kuwa unadhani maendeleo ya waislamu yamekosekana si kwa sababu ya uchache wao serikalini na kubaguliwa isipokuwa ni asili ya maumbile yao.Hili halikubaliki.Iwapo Mwenyezi Mungu kwa uadilifu wake anawapa nyinyi mnaomkufuru atashindwaje kutupa sisi tunaomuabudu kisawasawa.Na kwa maneno yake anapotupa tukamshukuru basi hutuongezea zaidi na zaidi.
Kwa mtazamo wako usiozingatia elimu ya kiislamu unadhani ibada kwa waislamu iko misikitini tu na ukiona misikiti imeongezeka unataka waislamu wasilalamike kwa jengine ambalo wanazuiwa kulitekeleza katika ibada.Huelewi kuwa kuwajengea watu wa jamii fulani uwezo wa kiuchumi na kuwaajiri kwa wingi serikalini kuna uhusiano mkubwa na ukandamizwaji wa kiimani.Kwani watakaokuwa wakifaidi jasho la wenzao zao ndio watakaokuwa na jeuri ya kuwakandamiza na kuwafanya wengine wadharaulike mitaani.
 
Wewe inaonekana ni mtu wa kuropoka na kweli hauko serikalini na jengine umezoea kuwatukana waislamu na huwajui waislamu ni nani katika hii Tanzania angalau kabala mtazamo mpana wa dunia,
Mfano wa matusi yako kwa waislamu unapatikana hata kwenye hiki kipande kifupi ulichoandika.Unaposema mkiwa asilimia 80 ndio mambo yenu yatakuwa sawa?.Mambo yetu sisi kama nani kwako.Wewe kwa mtazamo wako huna sifa ya kuwaambia waislamu ni narrow minded na waislamu upana wa mawazo haufundihiwi na wewe na wala mtu mwengine yoyote.Upana wa mawazo ya waislamlu unapatikana katika Qur'an na sunna za Mtume Muhammad s.a.w.
Ukija upande mwengine uliogusia hapo kwa ujinga wako ni kuwa unadhani maendeleo ya waislamu yamekosekana si kwa sababu ya uchache wao serikalini na kubaguliwa isipokuwa ni asili ya maumbile yao.Hili halikubaliki.Iwapo Mwenyezi Mungu kwa uadilifu wake anawapa nyinyi mnaomkufuru atashindwaje kutupa sisi tunaomuabudu kisawasawa.Na kwa maneno yake anapotupa tukamshukuru basi hutuongezea zaidi na zaidi.
Kwa mtazamo wako usiozingatia elimu ya kiislamu unadhani ibada kwa waislamu iko misikitini tu na ukiona misikiti imeongezeka unataka waislamu wasilalamike kwa jengine ambalo wanazuiwa kulitekeleza katika ibada.Huelewi kuwa kuwajengea watu wa jamii fulani uwezo wa kiuchumi na kuwaajiri kwa wingi serikalini kuna uhusiano mkubwa na ukandamizwaji wa kiimani.Kwani watakaokuwa wakifaidi jasho la wenzao zao ndio watakaokuwa na jeuri ya kuwakandamiza na kuwafanya wengine wadharaulike mitaani.

Chonde chonde. Msilazimishe mambo ambayo hayapo.
Tanzania ni yetu sote. Mnapotaka nyinyi mpewe special preference mnatumia kigezo gani? 😂😂😂😂
 
Ndahani,
Nadhani umeingia katika mjadala huu ukiwa umeshasonga mbele sana kwa hiyo huelewi maudhui yake.
Ikiwa una haja ya kufanya mjadala na mimi sasa itakubidi uanze mwanzo usome nini mimi na wengine tumeandika.

Hakuna popote nimezungumzia suala la kuabudu.

Lakini kwa haraka na wepesi unaweza kuanza na hizo takwimu za mgawao wa nafasi kama zilivyoandikwa na Shura ya Maimamu.

Kuna siku Mama alisema mwanga mpe mwanao akulelee. JK angelijaribu kujenga msikiti wa Bakwata kama ushawishi au ufuatiliaji kama JPM angeitwa mdini.
Tunapoongea haya mambo tuwe na kiasi. Sio rahisi kufanyika kama mnavyotaka.
Nashauri kama nia ni kuongoza kwa wingi, wekezeni kwenye elimu bora na uadilifu. Tanzania inahitaji watu waadilifu wenye elimu bora na si vinginevyo.
 
Chonde chonde. Msilazimishe mambo ambayo hayapo.
Tanzania ni yetu sote. Mnapotaka nyinyi mpewe special preference mnatumia kigezo gani? 😂😂😂😂
Kauli nzuri ya chonde chonde Tanzania ni yetu sote.Lakini hii huwa kiuhalisia inahusu pale waislamu wanapokandamizwa wakae kimya .Inapokuja kutoa fursa sawa basi waislamu haiwahusu. Inakuwaje unachagua baraza la mawaziri wote wakristo isipokuwa watatu na wabunge wote wakristo isipokuwa wachache halafu useme chonde chonde.
 
Kuna siku Mama alisema mwanga mpe mwanao akulelee. JK angelijaribu kujenga msikiti wa Bakwata kama ushawishi au ufuatiliaji kama JPM angeitwa mdini.
Tunapoongea haya mambo tuwe na kiasi. Sio rahisi kufanyika kama mnavyotaka.
Nashauri kama nia ni kuongoza kwa wingi, wekezeni kwenye elimu bora na uadilifu. Tanzania inahitaji watu waadilifu wenye elimu bora na si vinginevyo.
Kwani viongozi Tanzania ni wangapi wote.Na jee waislamu wenye elimu kuliko yako ni wangapi.Hii ni kabla hata ya uwekezaji wowote mwengine.
 
Kuna siku Mama alisema mwanga mpe mwanao akulelee. JK angelijaribu kujenga msikiti wa Bakwata kama ushawishi au ufuatiliaji kama JPM angeitwa mdini.
Tunapoongea haya mambo tuwe na kiasi. Sio rahisi kufanyika kama mnavyotaka.
Nashauri kama nia ni kuongoza kwa wingi, wekezeni kwenye elimu bora na uadilifu. Tanzania inahitaji watu waadilifu wenye elimu bora na si vinginevyo.
Ndahani,
Miradi mitatu ya elimu imehujumiwa Tanzania na laiti serikali ingeruhusu miradi hiyo leo tusingekuwa hapa wewe unahimiza Waislam wathamini elimu.

Unazungumza hapa mambo usiyoyajua.

1968 mradi wa ujenzi wa Chuo Kikuu kilichokuwa kinajengwa na EAMWS ulihujumiwa kwa EAMWS kupigwa marufuku na kuundwa BAKWATA.

1970s serikali iliwakatalia IOC kujenga Chuo Kikuu Tanzania chuo hicho kikajengwa Mbale, Uganda.

1980s Darul Imaan ilihujumiwa isijenge Shule ya Ufundi Kibaha.

Haya nimeyarudia kukukumbusha.
 
Back
Top Bottom