Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Picha za hivi karibuni zilizotolewa na kampuni ya ujasusi ya teknolojia ya anga ya Marekani Maxar zinaonyesha kwamba shuguli za kijeshi za jeshi la urusi zimeendelea kuwepo karibu na mipaka yake na Ukraine, licha ya madai ya hivi karibuni ya Urusi ya kuondoa vikosi vyake kwenye mipaka hiyo.
Picha hizo ambazo zilichukuliwa kati kati ya mwezi wa Februali, zinaonyesha kuwa Ukraine bado imeendelea kuzingirwa katika maeneo matatu- kwenye mipaka yake na Urusi na Belarus - na zana za kijeshi za Urusi pamoja na vikosi viko kwenye mipaka hiyo kwa wingi.