Pikipiki Boxer ni mbovu kuliko pikipiki zote za kichina

Pikipiki Boxer ni mbovu kuliko pikipiki zote za kichina

devinyo1987

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2021
Posts
268
Reaction score
370
Jamani wana jf nasikia boxa zinakufa sana piston...rings...block

Tena wazoefu wanasema hazirekebishiki zinatoa sana moshi, wengi wao zimewafia na wamezipak ndan.

Pia service yake ni garama sana. Je, wanaJF nini madhaifu ya pikipiki boxer?
 
Jamani wana jf nasikia boxa zinakufa sana piston...rings...block
...tena wazoefu wanasema hazirekebishiki zinatoa sana moshi ....wengi wao zimewafia na wamezipak ndan....pia service yake ni garama sana....je wana jf nini madhaifu ya pikipiki boxa

Sent from my Nokia 1 using JamiiForums mobile app
Ungeleta kama swali wangekujibu Sasa umeleta kama habari kamili tukusaidie nini?

USSR
 
Jamani wana jf nasikia boxa zinakufa sana piston...rings...block
...tena wazoefu wanasema hazirekebishiki zinatoa sana moshi ....wengi wao zimewafia na wamezipak ndan....pia service yake ni garama sana....je wana jf nini madhaifu ya pikipiki boxa

Sent from my Nokia 1 using JamiiForums mobile app
Labda kafanye utafiti Tena huko ulikosikia.
Kwanza ninachofahamu Mimi boxer haitengenezwi China
Pili matatizo mengi tunasababisha sisi watumiaji. Tunatumia bila kufuata taratibu sahihi za kufanya service
 
inategemea umenunua wapi used au mpya? unafanya service kwa wakati? na unaitumia kwa usahihi usije kuwa unaweza mafuta ya elf 2 unafosi ufike mpka kisemvule na service unataka ufanye kila baada ya miez 3
Ongeza na hii.

Mleta mada umejichanganya mwenyewe kwenye andiko. Boxer halisi/original ni ya India. Kama ulinunua ya chapa ya pili, kukwepa bei, hilo sio kosala muuzaji wala mtengenezaji. Issue
ni 'money value'
 
Jamani wana jf nasikia boxa zinakufa sana piston...rings...block

Tena wazoefu wanasema hazirekebishiki zinatoa sana moshi, wengi wao zimewafia na wamezipak ndan.

Pia service yake ni garama sana. Je, wanaJF nini madhaifu ya pikipiki boxer?
Boxer ndiyo pkpk bora kwa pkpk za bei ya chini ni ngumu na himilivu ila si za mizigo ni sport tu.
 
Uza ununue TVs, shida mnanunua pikipiki za laki 7 halafu mnakuja lalamika!

Menya kitu 0 km uone kama itakusumbua na kumwaga oil ni kila week mzee! Usimalize nayo mwezi utaiua hizo rings.
 
Jamani wana jf nasikia boxa zinakufa sana piston...rings...block

Tena wazoefu wanasema hazirekebishiki zinatoa sana moshi, wengi wao zimewafia na wamezipak ndan.

Pia service yake ni garama sana. Je, wanaJF nini madhaifu ya pikipiki boxer?
Naomba ubadilishe heading yako iwe swali ili uelimishwe
1. Nianze tu kukuelimisha kuwa Boxer sio Pikipik ya Kichina, Ile ni Pikikipi kutoka India - Kampuni ya Bajaj
2. Bajaj ipo kwenye kundi la pikipiki zilizotengenezwa kwa tecnologia ya juu zaidi ukilinganisha na hizi za kichina
Ninamaanisha inahitaji vitu OG, Ifanyiwe sevise kwa wakati kwa kutumia Oil sahihi ( sio zile za kupima mtaani ), Iwekwe mafuta safi (sio ya kununua kwenye vichupa nk)

Ukifanya hivyo na ukijua kuiendesha kwa usahihi na maanisha uendeshe kwa gia stahiki kulinganga na speed na mzigo; Sio unaweka gia namba mbili halafu unavuta mafuta hadi mwisho ndio unaua hizo piston. Unaweza kupitwa na pikipiki inangurunga Engine inataka kupasuka, maana yake ameweka gia 1 au mbili na mafuta mengi sana; ni makosa!
Ukweli ni kuwa unaweza kukaa na Boxer bila matengenezo kwa miaka hadi ukasahau kuwa inaharibika

Kuhusu gharama za service, inategemea tu kwani sana sana ni kubadilisha oil filter & Oil yenyewe ambayo hata za kichina zinabadlishwa (Badilisha Oil kila kilometa 1000 hivi) angalia kilometa sio siku kwa kuwa kuna siku unaweza kuwa umepaki au ukatembea kidogo sana, hivyo kuhesabu siku haileti maana kiufundi

Kuhusu kutoa Moshi: Tatizo wengi hununua used (zilizotumika) na aliyetumia mwenyewe alikuwa Sio dereva mzuri, au hafanyi Service kwa wakati au anafanya kwa oil isiyo stahil nk ndio sababu zinatoa moshi
Kwa kuzingatia mahitaji ya Boxer, nafikiri zinafaa zaidi mazingira ya mjini...
 
Pole sana...

Inavyosemekana hakuna Boxer za China... Hua zinatokea India...
 
Back
Top Bottom