Pinda atimua watumishi Bagamoyo

Mayolela

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2009
Posts
384
Reaction score
7
Habari tulizozipata muda mfupi ni kwamba maofisa sita wa Halmashauri ya wilaya Bagamoyo wametimuliwa kazi na WAZIRI MKUU Mh. Pinda leo hii kwa kosa la ubadhirifu wa mali ya umma, na kutojali kero za wananchi.

Wadau mnasemaje katika hili? Maana huko ndio kwa Mh. RAIS JMK.

Wapo wengi sana wa mfano huu, katika maharmashauri hapa nchni.

 
...kawatimua tu halafu yamekwisha ama ameagiza wafikishwe mahakamani kujibu tuhuma zao?
 
nimeipata sasa hivi kwenye wapo redio ila kama wamefuja pesa wangebanwa kwanza warudishe chenji bana au wakawataifishwe bana au ndo kampeni ya safisha njia ccm ishinde kama jb ni no pls waiziri mkubwa timua na wa epa
 
Nilijua tu vitakuwa vidagaa fulani tu, hivi rahisi sana kuvitimua huku PM akitafuta ujiko.

Ikija kwa mipapa Pinda anakiri kwamba haiwezi, so what's the use?

Wewe umepewa missile unaenda kuua panya, pick a target your size, hao wa wilaya waachie wakuu wa mikoa.

BS tupu, hamna lolote.
 
..amtimue na Prof.Ndulu kwa kufuja 2.5 bilions za BOT.
 

Well said mkubwa.......!

Yaani huko bagamoyo macho yake manne ndo yameona ubnadhilifu serikalini? yaani pale mgogoni penyewe hajauona uozo huo? .....shame on him aiseee.....!

Sitetei wouvu wowote, bali mto huo inatakiwa aureplicate na kwa grand corruptions kama zile za Richmonduli, EPAs etc!...sio kukimbilia hao wasiokuwa na ''kinga'' tu........!
 
Nasikia file lipo dpp pccb wameshamaliza kazi yao....Pinda ametumwa kutokana na feedback ya dpp....kifuatacho ni kamata kamata....wait and see....
 

Na nyie mmezidi bwana, hakuna zuri kwenu? Mlitaka awaache hata kama wamekosea? Ni vizuri pia mjue kwamba Pinda siyo Rais, ni Rais pekee mwenye mamlaka ya kumtimua yeyote katika nafasi yoyote. Lakini si waziri mkuu anayeweza kumfukuza Ndulu. Ya kupongeza tupongeze, na ya kuponda tuponde. sasa nyie yote mnaponda tu, kwani nyie wapinzani?
 

Ayafanyie kazi basi na mapendekezo ya kamati ya Mwakyembe maana amekuwa akiyakimbia kwa muda mrefu sasa.
 


Mkuu si walishatuambia hao wa EPA ni matajiri wakubwa nchini wakikamatwa au kuchukuliwa hatua basi nchi itawaka moto na wao hawataki kuiwasha nchi moto kwa hiyo ni bora hao wa EPA waachiwe wapete tu lakini watalala mbele na hivi vidagaa, lakini mapapa hawataguswa.
 

Mbona hao mafisadi papa hawagusi bana? Kama ana nia ya uongozi afanye kweli kabla ya uchaguzi kuondoa takataka zote za wahujumu uchumi akina Vijisenti, EPA, Dowans, et al. Sio hawa dagaa kutoka Ziwa Tanganyika.
 
Sarakasi kuelekea uchaguzini. Hata hivyo hatudanganyiki!
 
Hawajatimuliwa...ila wamesimamishwa uchunguzi ufanyike,kama watakutwa na hatia wataadhibiwa kama vinginevyo wanarudi kazini na fidia juu..tatizo sio ubadhirifu DC na DED walikuwa hawasalimiani kwa hiyo wakikubali kusalimiana yanaisha
 
Jamani ukifukuzwa kazi serikalini wewe umeshindikana. Maana serikalini watu wanaonywa sana.

Private sector kosa moja nje,hakuna masihara hata kama kosa ni dogo sana. Tatizo serikalini kulundana kwingi sana.
 

Kama mtazamo wako ni huo basi inabidi upewe ushauri nasaha!! Kwa hiyo wewe unataka watu wote wawe na mawazo sawa. Kwani sote tuko kwenye ile 70% ya wafuata upepo kama wewe? Naona uko JF kimakosa au umetumwa. Vinginevyo usingeweza kuandika kitu kama hicho kwenye hili jamvi!
 


Pinda amesema kuwa wametumia report ya CAG ya 2008 ambayo ilionesha kuwa wameshindwa kuthibiti matumizi ya pesa i.e wanatumia vibaya pesa za halmashauri. Kwani CAG aliitaja Bagamoyo peke yake? Nadhani kuna mambo zaidi ya hilo. Haiwezekana ufisadi ufanywe na kila idara ya serikali lakini wawajibishwe Bagamoyo tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…