mzeewapori
Member
- Jul 15, 2010
- 9
- 0
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda, amesema Tanzania imefanya vizuri katika elimu, kupunguza umasikini na kukabiliana na magonjwa ya Malaria na Ukimwi.
Alisema juhudi hizo zinafanyika, ikiwa ni katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) na itajitahidi kukamilisha malengo yaliyobaki katika kipindi kilichobakia cha miaka mitano.
Alikuwa akitoa taarifa ya Tanzania kwenye mkutano mkuu wa utekelezaji wa malengo hayo mjini New York, Marekani juzi jioni ambako anamwakilisha Rais Kikwete.
Pinda alisema kwenye malengo ya elimu, uandikishaji wa watoto katika shule za msingi umefikia asilimia 95.4 Tanzania Bara na asilimia 81.5 Zanzibar na uwiano wa wanafunzi wa kiume na wa kike katika shule hizo uko sawa kwa sawa.
Alisema ukuaji wa uchumi ni wastani wa asilimia saba kwa muongo mmoja uliopita na umasikini kwa wanaoishi chini ya dola moja kwa siku, umepungua kutoka asilimia 38.6 mwaka 1991/92 hadi asilimia 33.6 mwaka 2006/07.
Kwa mujibu wa Pinda, kwa vile asilimia 80 ya Watanzania milioni 40 wanajishughulisha na kilimo, uwekezaji katika kilimo ndiyo utakaowaondoa katika umasikini na ndiyo maana Serikali imeanzisha azma ya Kilimo Kwanza ili kuendeleza kilimo cha kisasa na cha umwagiliaji.
Kuhusu Ukimwi, alisema maambukizi mapya yamepungua kutoka asilimia saba 2003 hadi asilimia 5.7 mwaka huu kwa Tanznia Bara na Zanzibar imebaki asilimia 0.6 tu.
Alisema malaria karibu imekwisha kabisa Zanzibar na kwa Bara mbinu mpya za kukabiliana na ugonjwa huo zinatekelezwa, alisema.
Hata hivyo, alisema bado hatua kubwa haijapigwa nchini katika kupunguza vifo vya kinamama vinavyotokana na uzazi na vifo vya watoto wachanga.
Mkutano wa New York unaohudhuriwa na wakuu wa Nchi na wa Serikali, wakiungana na viongozi wa taasisi za kijamii na sekta binafsi, unapima utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia tangu mwaka 2000 mpaka sasa kabla ya mwaka 2015 ambapo utekelezaji unatakiwa ufikie asilimia 100.
Hiyo niliyo bold siielewi...naomba ufafanuzi
Alisema juhudi hizo zinafanyika, ikiwa ni katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) na itajitahidi kukamilisha malengo yaliyobaki katika kipindi kilichobakia cha miaka mitano.
Alikuwa akitoa taarifa ya Tanzania kwenye mkutano mkuu wa utekelezaji wa malengo hayo mjini New York, Marekani juzi jioni ambako anamwakilisha Rais Kikwete.
Pinda alisema kwenye malengo ya elimu, uandikishaji wa watoto katika shule za msingi umefikia asilimia 95.4 Tanzania Bara na asilimia 81.5 Zanzibar na uwiano wa wanafunzi wa kiume na wa kike katika shule hizo uko sawa kwa sawa.
Alisema ukuaji wa uchumi ni wastani wa asilimia saba kwa muongo mmoja uliopita na umasikini kwa wanaoishi chini ya dola moja kwa siku, umepungua kutoka asilimia 38.6 mwaka 1991/92 hadi asilimia 33.6 mwaka 2006/07.
Kwa mujibu wa Pinda, kwa vile asilimia 80 ya Watanzania milioni 40 wanajishughulisha na kilimo, uwekezaji katika kilimo ndiyo utakaowaondoa katika umasikini na ndiyo maana Serikali imeanzisha azma ya Kilimo Kwanza ili kuendeleza kilimo cha kisasa na cha umwagiliaji.
Kuhusu Ukimwi, alisema maambukizi mapya yamepungua kutoka asilimia saba 2003 hadi asilimia 5.7 mwaka huu kwa Tanznia Bara na Zanzibar imebaki asilimia 0.6 tu.
Alisema malaria karibu imekwisha kabisa Zanzibar na kwa Bara mbinu mpya za kukabiliana na ugonjwa huo zinatekelezwa, alisema.
Hata hivyo, alisema bado hatua kubwa haijapigwa nchini katika kupunguza vifo vya kinamama vinavyotokana na uzazi na vifo vya watoto wachanga.
Mkutano wa New York unaohudhuriwa na wakuu wa Nchi na wa Serikali, wakiungana na viongozi wa taasisi za kijamii na sekta binafsi, unapima utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia tangu mwaka 2000 mpaka sasa kabla ya mwaka 2015 ambapo utekelezaji unatakiwa ufikie asilimia 100.
Hiyo niliyo bold siielewi...naomba ufafanuzi