Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
AINA YA KWANZA
Vipimo
1. Siagi - 200g
2. Unga - 2 Vikombe
3. Sukari - 1 Kikombe
4. Vanilla - ½ Kijiko
5. Arki rose ukipenda - 2 matone
6. Mayai - 6
7. Zabibu - ¼ Kikombe
8. Baking powder - 2 Vijiko vya chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Washa oveni 350°c.
- Saga siagi na sukari kwa mashine mpaka mchanganyiko ulainike.
- Ongeza yai moja baada ya moja na huku ukiendelea kusaga mpaka yaishe.
- Tia unga uliochanganwa na baking powder.
- Endelea kuchanganya mpaka ichanganyike vizuri, halafu arki rose, vanilla na zabibu halafu koroga kidogo ilizichanganyike vizuri.
- Mimina mchanganyiko katika chombo cha kuchomea.
- Vumbika (bake) kwa muda wa dakika 20 mpaka 25.
- Ikisha poa kata kata vipande na tayari kuliwa kwa kahawa au chai.
AINA YA PILI
Vipimo
Unga wa ngano - 2 Vikombe
Siagi - 1 Kikombe
Sukari - 1 Kikombe
Mayai - 6
Vanilla - 1 Kijiko
Baking powder - 1 Kijiko cha supu
Zabibu kavu - 1/2 Kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
- Washa oveni moto wa 350°F.
- Kwenye bakuli la kuchanganyia keki la machine, saga sukari na siagi hadi ilainike.
- Kisha tia yai moja moja huku unaendelea kuchanganya.
- Halafu mimina unga uliochungwa pamoja na baking powder na uchanganye vizuri.
- Kisha tia vanilla na mwagia zabibu na ukoroge.
- Kisha umimine katika sufuria ya kiasi ya kupikia keki iliyopakwa siagi.
- Vumbika kwenye oveni kwa muda wa dakika 35 au hadi iwe tayari.
- Iache ipowe na itakuwa tayari kuliwa.