Pitia hapa huenda utanikumbuka

Pitia hapa huenda utanikumbuka

ni kweli lakini pia utajiri ni siri ya mtu mbona hakuna rais wa darasa la saba? pia hii hali ya kutokusoma na kufanikiwa inafanya kazi zaidi kwa nchi zilizoendelea
 
tanzania matajiri wengi ni viongozi pamoja na watoto wao mnaosema hawakusoma sana pia na watu wanaofanya biashara haramu vinginevyo utapotosha watu wasisiome
 
MAFANIKIO YA MAISHA SIO ELIMU TU, UTHUBUTU, KUJIAMINI NA UJASIRI WA MAAMUZI

✍Ukichunguza katika jamii, utabaini kuwa sehemu kubwa ya matajiri ni wale ambao wana elimu ndogo ama hawakusoma kabisa.

[emoji117]Katika miji na maeneo yote; wenye majengo ya maana, wenye makampuni makubwa, wenye utitiri wa malori na mabasi, wenye maduka makubwa ni wale wa "darasa la saba” au wale ambao hawakuingia darasani kabisa

[emoji144][emoji432] Wasomi wengi wana maisha ya kawaida yaani yale ya kiwango cha kubadilisha mboga, wakijitahidi sana wanaishia kujenga nyumba za kuishi [emoji537] na [emoji594] [emoji592]magari mawili ya kutembelea (tena kwa mikopo!)

[emoji117]Wapo [emoji144][emoji432]wasomi wengi tu wanaoishi kimasikini, kwa lugha ya kistaarabu tunasema wana maisha ya kuungaunga. Kiukweli idadi ya wasomi walio matajiri ni ndogo sana

[emoji117]Lakini Umasikini wa wasomi wengi umeanzia huko shuleni na vyuoni wanakopatia usomi wao. Madarasani kuna mambo mawili wanafundishwa wasomi ambayo ndio yanayowaroga

Hii inachangiwa na mambo mawili:-
[emoji116]
I. Wameelimishwa na kuaminishwa kwamba yule anaepata maswali yote kwa usahihi ndio anaonekana amefaulu. Ukikosea unahesabika kuwa u mjinga na wenyewe wanaita umefeli

[emoji117]Hata hivyo katika maisha ya kawaida hasa kwenye mchakato wa kutafuta hela, kujaribu na kukosea ni sehemu ya mafanikio

[emoji117]Kadiri unavyojaribu na kukosea mara nyingi ndivyo unavyojifunza na ndivyo nafasi ya kutajirika kwako inakuwa kubwa!

[emoji144][emoji432]Wasomi wengi kwa sababu ya "mentality" ya kuogopa kukosea huwa hawapendi kujaribu biashara kwa hofu ya kushindwa kuiendesha, na huamua kufa kimasikini wakitegemea mishahara pekee kwa sababu mishahara ndio pato lao la uhakika
[emoji116]
II. Madarasani kunahimizwa ubinafsi badala ya umoja. Angalia namna mitihani inavyofanyika. Kila mwanafunzi anafanya mtihani peke yake, na ukikutwa unaangalizia ama mnasaidiana na mwenzio ndani ya chumba cha mtihani mtapata adhabu kali ikiwemo kufutiwa mtihani!

[emoji117]Katika maisha ya kawaida hasa ya kusaka fedha, unahitajika ushirikiano mkubwa sana, baina yako na wadau, wateja, wafanyakazi wenzio, marafiki n.k. Kwa kifupi unatakiwa kuwa na Networking ya kutosha.

[emoji113]Huwezi kufika mbali kiuchumi kama utakuwa na "mentality" ya ubinafsi unaosisitizwa madarasani!

Simaanishi kusoma hakuna maana, isipokuwa ninakwambia: Kama ukipata nafasi ya kusoma, soma kwa bidii; lakini usibebe kila wanachokulisha madarasani; ukakileta huku mtaani

Mtaani panahitaji akili ambayo ni tofauti na hiyo iliyopimwa kupitia kukariri ya vitabuni, mwishoni wanakuzawadia makaratasi yaitwayo vyeti

[emoji41]Ukitaka kufanikiwa ungana na waliofanikiwa wakuelekeze

[emoji3][emoji120] Hii habari haitaki hasira, vumilia tu na jiongeze
....hata mimi sijawa tajiri bado[emoji12][emoji3][emoji3][emoji3][emoji115]
Ni kweli na pia watu wanapaswa kufahamu kuwa kuna AKILI inayotokana na elimu na kuna akili inayotokana na KIPAWA yaani TALENT sasa katika uhalisia mara nyingi mafanikio na hata utajiri huwaendea watu wenye Vipawa,na kipawa ni namna ya karama "GIFT" na mtu huzaliwa nacho kama majaaliwa . Sasa hata kama mtu ana elimu ya kiwango gani ikiwa hana kipawa ni vigumu kwake kufanikisha majukumu kwa ufanisi ili kuleta maendeleo. Mtu anaweza akawa na shahada (elimu) ya business administration lakini akawa hana hata uwezo wa kubuni au kuendesha biashara ya kiosk cha kuuza voucher za simu tu, lakini mwingine akawa hana elimu yoyote ya shule na bado akaweza kufanya biashara kubwa kupitia kipawa. Mafanikio ya hali ya juu huja pale mtu anapokua na vyote viwili mfano unakuta katika kundi la madaktari wasomi wa ngazi inayofanana kati yao mwenye kipawa atakuwa daktari bingwa au katikati ya majaji miongoni mwao mwenye kipawa lazima atakuwa kiongozi nk. Katika msahafu (Bible) kuna nukuu inayosema "...kipawa alichonacho mtu kitamfanyia nafasi" hii ikiwa na maana kuwa kipawa alichonacho mtu kitamtengenezea fursa, na pia nukuu nyingine inasema " kipawa cha mtu kitamketisha na wakuu" ndio maana unakuta Mrisho Mpoto ameishaonja MEALS za ikulu ukilinganisha na maelfu ya maprofesa ambao hata mlango wa Ikulu hawaujui rangi.
 
Back
Top Bottom