Pitso Mosimane apewa $1 million baada ya kufanikiwa kuipandisha daraja(Al Ahly saudi arabia)kama alivyoahidiwa

KENGE 01

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2021
Posts
1,705
Reaction score
4,217
Wakuu

Afrika hii kuna makocha alafu kuna huyu mzee Pitso mosimane ni kocha nusu

Mwamba baada ya kuachana na Al Ahly ya Egypt Alisajiliwa na team ilioshuka daraja huko uarabuni..Rais wa team hiyo alimuahidi Pitso endapo atafanikiwa kuirudisha timu iyo ligi kuu uarabuni..Basi atapewa $1 million kama bonus tu bado kuongezewa mshahara n.k

Sasa majuzi miamba wamefanikiwa kupanda daraja kwahyo ni rasmi Pitso atachuana vikali na Kina Ronaldo.....Pia Messi nauhakika ataenda kuchezea ligi hiyo kwaajili ya pensheni..

Huyu pitso ni jamii ya kina Pep guardiolla yeye mpe team na kibunda tu mengine mwachie yeye kaziimeisha

Nawasilisha
 
Kabisa hiyo team aliyopandisha Saudia ni team kubwa sana tu Al Ahly ya Saudia ilishuka daraja lakini ni team ina fan base kubwa sana huko na huyu mwamba atapewa budget kubwa kuirudisha sehemu yake inayostahili ni club yenye mafanikio makubwa katika soka la huko nadhani imerudi sehemu yake na natabiri makubwa kwa hii club kwani ni kati ya team 4 ma giant huko.
 
Pitso ni prof Nabi mtupu
Usimba na uyanga utawauwa yaani pitso unfananishe na Mhuni Nabi anyway

~Pitso hajawai kufukuzwa klabu yoyote zaidi ya kuondoka mwenyewe kama Nabi alivyotimuliwa Al Hilal

~Kila klabu atakayoinoa pitso anabeba Klabu bingwa,Supercup na makombe yote yanayokatiza

~Ni dhambi kubwa sana kumfananisha Mosimane na robertinho,Nabi,Ibenge,Sven,Kaze n.k
 
Kilichobaki wasajili vizuri tu
 
Huyo kocha wa mechi za kununua ??
Ni masikitiko makubwa sana Rage hapewi Maua yake kwanini lakini na sanamu lake linachelewa kujengwa! Watu wake hawa ni Mali ya Mirembe hospital Huku mtaani wanatumalizia chipsi zetu na mchuzi wa pweza tu, kweli Mbumbumbu kolo fc atabaki Mbumbumbu tu!!

Mpira wa Nabi unauona wazi second half Yanga wakicheza kama Brazil!! Kama wanataka kufia uwanjani!

Hivi tukikuita kolo wewe uje jangwani utasema mbele yetu kuwa Yanga pia imenunua mechi za kuwatoa waarabu na Rivers United shirikisho? Kwa bei Gani?

Unataka kusema mechi pekee ambazo hakununua ni Ihefu na Simba tu Katika ligi Zote?

Hebu rudisha akili kichwani mkuu uweze hata kuvuka Barabara!

Yani Prof Nabi kubeba NBC premier league mara ya pili na kuingia nusu fainali shirikisho umeumia sana jombaa!! Be careful with heart attack!

Nabi ni kocha mkubwa wa makombe itabaki hivyo! Shindeni Leo vs Azam tukutane Tena mtufunge Tena!!
 
Sote tunafahamu isipokuwa wewe kuwa Yanga wananunua mechi.
 
Sote tunafahamu isipokuwa wewe kuwa Yanga wananunua mechi.
Labda ungetaja mechi alizonunua Nabi itapendeza!

Mechi za Ihefu na ya Simba hakununua?

Mechi za shirikisho pia Yanga wananunua?

Humu JF tunatumia logic maana we cannot prove what people with fake ID say.

Akili ikikataa tunatupa kule, Lete more news!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…