Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Jamani wacha kuniona kama siko siriasi niko siriasi tena sana nimesema tatizo ni huduma za afya ziko mbali sana kwa wanajua niko bukoba sehemu ya rwanga kijijini usafiri hakuna kabla ya kesho kwenda hosptal kuna njia ya uduma ya kwanza nzuri nichukue kabla ya matibabu na vipimo?
Atakua mnafki uyu ivi kabisa mkee azime ukumbuke nakuingia jf
Jamani wacha kuniona kama siko siriasi niko siriasi tena sana nimesema tatizo ni huduma za afya ziko mbali sana kwa wanajua niko bukoba sehemu ya rwanga kijijini usafiri hakuna kabla ya kesho kwenda hosptal kuna njia ya uduma ya kwanza nzuri nichukue kabla ya matibabu na vipimo?
Mpigie bodaboda aje mwende hospitali hapa jf wenzio wengi wanaokupa ilani wako jijini dar hawafahamu shida ya usafiri na usalama nyakati za usiku huko vijinini
Umepata wapi nguvu za kuingia JF ?
Hebu changamka ufike hospital uokoe hao watu!
Ndg. hukusema ni mjamzito wa miezi mingapi, ila naomba nikusaidie hivi:
Kama ni changa yaani kuanzia mwezi 1 hadi 4, anaweza kupatwa na hali hiyo haswa akisimama saana na haswa kama ni mimba ya kwanza.
Pili kama hujawahi kuona hivyo tena, achana na hayo maneno ya watu kuwa ni kifafa cha mimba. Haiko hivyo. Wamama wengi sana wana dalili za ajab ajab wakiwa na mimba haswa ya kwanza. Kama hana dalili za kuchoka sana, hajavimba miguu, hasikii kichwa kuuma, ngojea tu mpaka asubuhi umpeleke kliniki akapimwe.
Walio kwenye miundo mbinu mizuri ndo hao wanaokutukana na kukuita majina. Usiogope, sema na mkeo maneno mazuri wala usiogope na kufadhaika. Weye mtoto wa kiume, onesha pendo tu kwa mkeo na mwahidi kuwa kesho kukicha weye na yeye ni kiguu na njia mpaka mumwone dakitari.
Pole kwa mipasho ya humu jf. jikaze kiume usipanic kwa maneno ya watu
Kweli niseme Mumgu akujalie hekma na maarifa kwa msaada wako na kunipa mawazo ambayo yamenijenga sana, popote ulipo ulale salama sana.
Wakati tukipata chakula cha jioni ghafla mke wangu niliona anaishiwa nguvu na kunilalia nikajiuliza sina cha kufanya. Kutoka na kuzimia niliamua kuanza kumpepea na baadaye amepata nafuu japo si sana, so kama wajamaa naomba mawazo, ushauri na hatua za kuchukua.
Wewe Doctor Mzima unashindwa kumfanyia huduma ya kwanza mke wako? Au jina hilo la (Dr Shekilango)Doctor ni jina feki? Mkuu Dr Shekilango Muweke sehemu yenye upepo na mpe maji ya uvuguvugu glasi 1na kama unayo Asali weka kijiko 1 ndani ya hayo maji ya uvuguvugu na ikiwezekana asubuhi kukicha salama muwahishe Hospitali haraka iwezekanavyo huenda ana maradhi ya Presha.Wakati tukipata chakula cha jioni ghafla mke wangu niliona anaishiwa nguvu na kunilalia nikajiuliza sina cha kufanya. Kutoka na kuzimia niliamua kuanza kumpepea na baadaye amepata nafuu japo si sana, so kama wajamaa naomba mawazo, ushauri na hatua za kuchukua.
teh teh teh maalim naona unautafuta ugomvi jamvini.Kupoteza fahamu kwa mjamzito kunatokana na sababu zaidi ya moja.
Na wakati mwingine Ukipuuzia Inaweza kumletea madhara makubwa sana mtoto alioko tumboni pamoja na Mama mwenyewe.
Nenda hospitali haraka sana akapimwe.
Na suala km hili unalipeleka kule JF DOCTOR sio humu kwa wahuni wanaojadili Ngono masaa 24.