Please jamani, naomba ushauri wa kisheria.

Please jamani, naomba ushauri wa kisheria.

Iselamagazi

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
6,020
Reaction score
6,161
Salaam wana JF.

Tafadhali wataalamu wa mambo ya sheria, naomba msaada wenu wa kisheria. Hivi polisi ngazi ya Wilaya au Mkoa akizuia shtaka la mlalamikaji lisifikishwe mahakamani, ni kitu gani mlalamikaji afanye?

Naomba msaada.
 
Utaratibu upo hivi Mkuu, endapo polisi wilaya na hasa OCD mwenyewe amekataa kesi yako isiende mahakamani, unaweza kuchagua, ama kwenda kumuona/kupeleka malalamiko yako kwa kamanda wa polisi wa mkoa husika(RPC) au Mkuu wa Upelelezi wa jinai wa mkoa husika(RCO) ambao watasikiliza lalamiko lako na kuitisha faili la kesi yako ili waone uhalali wa lalamiko lako, kama ni halali basi shauri lako litafikishwa mahakamani, na kama kuna hatua zilizokwama kiupelelezi msukumo utawekwa na kutendewa haki. Endapo hata ngazi ya mkoa wamekukatalia peleka lalamiko lako kwa ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi au Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi(DCI). Au peleka lalamiko lako kwenye ofisi ya wakili wa serikali mfawidhi wa mkoa uliopo au kwa Mkurugenzi wa mashitaka(DPP) ambaye naye ataliitisha jalada na kulisoma ajiridhishe ukweli wa lalamiko lako pindi atakaporidhika atalipeleka shauri lako mahakamani.
Ni vema ukaelewa kuwa siyo kila kesi inayoripotiwa polisi ni lazima ifikishwe mahakamani, sheria ya Jeshi la Polisi iliyotungwa na Bunge imewapa mamlaka Polisi ya kupeleleza na endapo hawatapata ushahidi wa kutosha wa kosa la jinai wanayo mamlaka ya kukataa kulipeleka shauri mahakamani na kulifunga jalada. Hatua hii ni ya makusudi ili kuzuia kesi za kukomoana kwenda mahakamani na matumizi mabaya ya mahakama, kuifanya mahakama isielemewe na mashauri mengi na kuchelewesha haki za watu wengine wenye kesi halali.
 
Utaratibu upo hivi Mkuu, endapo polisi wilaya na hasa OCD mwenyewe amekataa kesi yako isiende mahakamani, unaweza kuchagua, ama kwenda kumuona/kupeleka malalamiko yako kwa kamanda wa polisi wa mkoa husika(RPC) au Mkuu wa Upelelezi wa jinai wa mkoa husika(RCO) ambao watasikiliza lalamiko lako na kuitisha faili la kesi yako ili waone uhalali wa lalamiko lako, kama ni halali basi shauri lako litafikishwa mahakamani, na kama kuna hatua zilizokwama kiupelelezi msukumo utawekwa na kutendewa haki. Endapo hata ngazi ya mkoa wamekukatalia peleka lalamiko lako kwa ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi au Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi(DCI). Au peleka lalamiko lako kwenye ofisi ya wakili wa serikali mfawidhi wa mkoa uliopo au kwa Mkurugenzi wa mashitaka(DPP) ambaye naye ataliitisha jalada na kulisoma ajiridhishe ukweli wa lalamiko lako pindi atakaporidhika atalipeleka shauri lako mahakamani.
Ni vema ukaelewa kuwa siyo kila kesi inayoripotiwa polisi ni lazima ifikishwe mahakamani, sheria ya Jeshi la Polisi iliyotungwa na Bunge imewapa mamlaka Polisi ya kupeleleza na endapo hawatapata ushahidi wa kutosha wa kosa la jinai wanayo mamlaka ya kukataa kulipeleka shauri mahakamani na kulifunga jalada. Hatua hii ni ya makusudi ili kuzuia kesi za kukomoana kwenda mahakamani na matumizi mabaya ya mahakama, kuifanya mahakama isielemewe na mashauri mengi na kuchelewesha haki za watu wengine wenye kesi halali.

Nashukuru sana Mkuu kwa ushauri.
In fact kuna mtu mmoja kijijini kwa mjomba wangu, anadai ana kinga ya ki-diplomasia hivyo mama yake mzazi kwa kujua hivyo, anatumia nafasi hiyo kunyanyasa watu pale kijijini. Mwanakijiji anaweza kupigwa au kutukanwa na bibi huyo (75yrs) mara anapolewa, na ukijaribu kwenda ktk ngazi zote za serikali ya kijiji kushtaki, Lo! Kila kiongozi anaruka kwamba huyo ni mama yake Balozi wa Tanzania nchini (....) haguswi! Baadhi ya wanakijiji wamefika hadi kwa OCS, OCD na RPC kupeleka mashtaka bila mafanikio!
Kuna tetesi kuwa huyu bwana siyo Balozi, anachofanya ni kupiga simu direct toka nje ya nchi kwa viongozi niliowataja na kujitambuilisha kuwa ni Balozi na kwamba mama yake mzazi apewe ulinzi wa kutosha na asiguswe na mtu yoyote! Anyway kwa ushauri wako mkuu, tumepata sehemu ya kuanzia. Mwenye
kujua jinsi ya kuwatambua mabalozi wanaowakilisha nchi yetu nchi za nje naomba msaada wenu- hata website nikipata sawa tu.










mara pale kilevi kinapokolea (75yrs


ni mkorofi sana pale kijijini
 
Nashukuru sana Mkuu kwa ushauri.
In fact kuna mtu mmoja kijijini kwa mjomba wangu, anadai ana kinga ya ki-diplomasia hivyo mama yake mzazi kwa kujua hivyo, anatumia nafasi hiyo kunyanyasa watu pale kijijini. Mwanakijiji anaweza kupigwa au kutukanwa na bibi huyo (75yrs) mara anapolewa, na ukijaribu kwenda ktk ngazi zote za serikali ya kijiji kushtaki, Lo! Kila kiongozi anaruka kwamba huyo ni mama yake Balozi wa Tanzania nchini (....) haguswi! Baadhi ya wanakijiji wamefika hadi kwa OCS, OCD na RPC kupeleka mashtaka bila mafanikio!
Kuna tetesi kuwa huyu bwana siyo Balozi, anachofanya ni kupiga simu direct toka nje ya nchi kwa viongozi niliowataja na kujitambuilisha kuwa ni Balozi na kwamba mama yake mzazi apewe ulinzi wa kutosha na asiguswe na mtu yoyote! Anyway kwa ushauri wako mkuu, tumepata sehemu ya kuanzia. Mwenye
kujua jinsi ya kuwatambua mabalozi wanaowakilisha nchi yetu nchi za nje naomba msaada wenu- hata website nikipata sawa tu.










mara pale kilevi kinapokolea (75yrs


ni mkorofi sana pale kijijini

Huyo bwana mweke wazi, je ni nchi gani aliko halafu watu watamwaga kila kitu
 
Back
Top Bottom