Pogba atuhumiwa kumroga Mbappe, kutumia uchawi ili kuzuia majeraha

Pogba atuhumiwa kumroga Mbappe, kutumia uchawi ili kuzuia majeraha

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mathias Pogba kaka wa Mchezaji Paul Pogba amefichua madai mengine ya kushtua dhidi ya mdogo wake ambaye ni kiungo wa kati wa Juventus, huku mgogoro kati ya ndugu hao ukiendelea.

Lakini katika kuongezea chumvi kwenye kidonda, kaka mkubwa wa Pogba alifichua kuwa mshindi huyo wa Kombe la Dunia mwaka wa 2018, amekuwa akitumia mamilioni ya pesa katika uchawi ili kujilinda dhidi ya kupata jeraha.

“Kutokana na hayo, njia pekee ya kujinusuru ambayo mimi [Mathias] ninayo ni kufichua uwongo wake [Paul] na udanganyifu wake," alisema kama alivyonukuliwa na Get French Football News.

“Ndiyo maana nilithibitisha uchawi wake kwa sababu cha muhimu hapa si kwamba iwapo inafanya kazi au uniamini au usiniamini, ni kwamba ina nia mbaya kwa sababu uchawi huu unategemea kufanya mambo mabaya kwa matambiko yao kwa nia ya kudhuru."

“Pia, ninauliza, je, hivi Paul hakukataa kukimbilia kwa waganga? Sasa kwa nini alifichua hilo kwa mpelelezi? Pogba alikiri kwa polisi kuwa alimlipa mganga katika msafara wake kujikinga na majeraha."

"Je, kujikinga na majeraha kunahitaji kulipa mamilioni ya euro kwa mchawi huyu kwa miaka? (hasa kwa vile haikufanya kazi)," alimaka.

Hata hivyo, Paul Pogba amekanusha vikali tuhuma za kaka yake kwamba anajihusisha na uchawi.

Jina la Kylian Mbappe pia limekuwa likitajwa mara kwa mara katika sakata hilo kati ya Paul Pogba na kaka yake Mathias alifichua kwamba Pogba amekuwa akitumia uchawi kumvuruga Mbappe.

Paul kwa majibu yake ya haraka kupitia kwa mawakili wake alidai kuwa kaka yake anashirikiana na magenge ya uhalifu yaliyopangwa kumlaghai kitita cha Pauni milioni 13.
 
Jamaa kaona ishu yakumpiga mdogo Ake imefeli anazingizia uchawi inaonekana Mathias ndio mchawi anashindwa kujib tuhuma zinazomkabili anawaza uchawi tu
 
Hawa watu naona kazi ipo, tena si kazi ndogo
 
Miafrica bana ..Yani yapo Ulaya halafu yanawaza ndumba tu..apo utakuta Ni wivu tu kisa Pogba labda kamnyima ela au attention. Pumbavu kabisa hii ngozi nyeusi bado hijafika hatua ya kuwa binadamu kamili.
 
Mbape and pogba playing in different club and position even in national how can someone bewitch a player who doesn't have any impact in pogba career in national team and club that is nonsense allegations from the so called elder brother of paul pogba African ancestral will not allow their generation and siblings to shine after rejecting their huge number amount of money demands it's real interesting to see.
 
Africa bado n tatzo akifanikwa mmoja kwenye familia bas ujue ww ndo unatumikishwa
Mizigo yote
 
watu weusi kwenye ubora wao, hata akina Drogba na Etoo walitesa sana wazungu kwa ndumba. Shevchenko, Kezman, Torrez, Pazzini, Milito, Pandev walikua ni baadhi ya wahanga.

siku wazungu wakija kuyaelewa vizuri haya watatimua watu weusi ulaya.
 
watu weusi kwenye ubora wao, hata akina Drogba na Etoo walitesa sana wazungu kwa ndumba. Shevchenko, Kezman, Torrez, Pazzini, Milito, Pandev walikua ni baadhi ya wahanga.

siku wazungu wakija kuyaelewa vizuri haya watatimua watu weusi ulaya.
kama unaona wazungu wanarogeka jaribu kufanya kama utafanikiwa awa jamaa ni nextelever kwenye ayo masuhala
 
Back
Top Bottom