Pogba hastahili thamani ya pound million 100,ni mchezaji wa kawaida tu
Kumbuka Man City walikuwa na viungo wengi wanaocheza karibu karibu.
Wakati Man U walikuwa na viungo wachache wanaocheza mbali mbali. Angalia Space iliyokuwepo kati ya Fellaini, Pogba, Micki, Lingard na Rooney utaelewa.
Wenzake walim isolate peke yake kati ya dimba, ikawa inabidi alazimike ku drible ili kuwafikia. Hiyo ilimfanya kuchoka mapema.
Mpira ni ushirikiano, ndicho walichotuonyesha City leo. Huwezi kufanikiwa kwa kutumia mchezaji mmoja mmoja.
At least Herrera aliongeza balance pale katikati kabla ya Pep kuua game kwa kumuongeza Fernando.
Mou anapaswa aanze kumuamini Herrera ili kumsaidia Pogba, Fellaini ni mrefu, ana maguvu, lakini hawezi ku cover space kubwa kusaidia wenzake.
Pia, ni muda muafaka kumchezesha Smalling kwa sababu Blind ameanza kurudia makosa ya last season, si mzuri kukaba (timu ikiwa under pressure).
Pogba "The Slow but Sure man"
Still nina Imani, ndo game zinaanza.