Pole FL1...

Pole FL1...

Pole sana FL1, Mungu akupe nguvu na akulinde katika kipindi hiki kigumu wewe na familia ya marehemu.
 
Habari zimenifikia kuwa dada yetu FL1 amempoteza rafiki yake wa karibu mapema leo. Naomba kutoa pole zangu kwake na kwa familia ya rafiki yake huyo kwa msiba huu. Tunamwomba Mungu awafariji familia ya Marehemu, ndugu, jamaa na marafiki na ailaze pema peponi, roho ya marehemu, Amina


Pole sana mama wa kwanza.
 
Nilikuwa kwenye mikakati ya mazishi ajali ya jana ile we acha tu.

pole sana shem...lile basi nilishalipanda nalijua...kwa kweli kunahitajika jicho lingine maana naona TBS wameresign wote....haiwezekani kila siku mabasi yanapata ajali kwa kupasuka matairi...iko namna
 
Dah pole sana FL1 tupo pamoja katika hiki kipindi kigumu mwenyewe nimepoteza rafiki wa mchumba angu humo humo. Lihimidiwe jina la bwana. Amina.
what do you mean? kwani hii ndio ajali nilosikia jana imetokea mwanza?
 
Pole sana FL1 na wafiwa wote. BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA. JINA LAKE LIHIMIDIWE.
 
what do you mean? kwani hii ndio ajali nilosikia jana imetokea mwanza?

Yaani wifi yenu kapoteza rafiki yake alikuwa anaenda MZ kwenye hilo basi la jana jioni linaitwa A.M coach.
 
pole sana FL, jamani mcba uckie kwa mwenzio, ukikufika ni balaa.
 
Pole sana FL1 kwa kuondokewa na rafiki mpendwa. Mungu Ailaze pema peponi roho yake.
 
poleni sana..FL1 na familia ya rafikiyo.... njia yetu sote. kila nafsi itaonja mauti. stay strong
 
jamani nawe...kasema wifi yetu kapoteza rafiki yake...kwa nini hutaki kumuelewa shem langu lakini?
Ahaa! Ngoja nimpigie anambie ni wifi yetu yupi aliyempoteza rafiki yake. Usisahau anao sita anaowafanyia mchakato kwa ajili ya projekti ya 2012.
 
poleni sana..FL1 na familia ya rafikiyo.... njia yetu sote. kila nafsi itaonja mauti. stay strong
Sasa mkwe mbona hujamwaga dua kama ile ya siku ile? Nakumbuka neno moja tu rajjun! Mtoto inaelekea madrassa ilipata gradueti wa first class. BTW Unaendeleaje na ile projekti yetu?
 
Ahaa! Ngoja nimpigie anambie ni wifi yetu yupi aliyempoteza rafiki yake. Usisahau anao sita anaowafanyia mchakato kwa ajili ya projekti ya 2012.

mi namjua nkashilingi....labda kuwe na mwingine
 
Nashukuru sana Mwanakijiji kwa bandiko lako lakini sijui hizi habari umezipata wapi ...Ni kweli nimeondokewa na mpendwa wangu wa moyo alikuwa ni rafiki yangu wa karibu,alikuwa ni ndugu yangu alikuwa ni kila kitu kwangu lakini mwenyezi mungu kampenda sana na kumuita kwa muda aliomuhitaji yeye..Najua wote hapa duniani tu wapitaji ..ni vyema tuwe tayari kila saa na kila siku kwani hatujui siku wala saa
naona ni jinsi gani mnanipenda na kunijali..kwa sasa sitaongea kitu chochote msiba utakuwa mwanza ..sina uhakika kama itakuwa kesho ..lakini nitawafahamisha itakavyokuwa
Nawapenda wote
Bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake libarikiwe zaidi

"......Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. Yeye huchanua kama vile ua, kasha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe… ……" (Ayubu 14:1-2,14)……………mimi ndimi huo ufufuo na uzima. Waniaminio mimi wajapokufa wataishi. …" (Yohana 11:25-26).
Pole sana FL1, pole kwa wasifiwa....

MUNGU MWENYE ENZI YOTE ALIYEPENDEZWA NA JAMBO HILI NA KULIFANYA KWA MAPENZI YAKE, NA AZIDI KUWAPA FARAJA!.


Marehemu apumzike kwa Amani.
 
Nakupa pole sana mdogo wangu FL1 pamoja na familia ya marehemu.Huyo amemaliza ngwe yake tumebakia sisi, tujiandae.
 
Pole my bestlady kwa kumpoteza bestlady wako!!
Stay strong my dear!!
Yote mapenzi yake Mungu.
 
pole wafiwa na dada yetu FL1, Allah awatie nguvu.
 
Back
Top Bottom