Pole sana Lawrance Mwalusako katibu wa zamani Yanga

Pole sana Lawrance Mwalusako katibu wa zamani Yanga

Pole sana school mate wangu.Mi Iddi tulikuwa wote Milambo.RIP Naomi.
 
R.I.P Naomi jamani bado siamini huyu binti anakua namwona enzi hizo yupo primary mwalusako alikua anatupa lifti toka kwake mpaka pale kona Naomi alikua anasoma filbert bayi daaah soo sad anamwacha kaka yake Duncan alone mean I wamezaliwa wawili tu

Pumzika kwa amani Naomi
Pole familia ya mwalusako
 
Pole kwa kupoteza binti yako kipenzi Naomi kwa ajali.Alikuwa bado binti mdogo akiwa ndio kwanza amehitimu kidato cha sita mwaka huu.

Pole sana brother. Mungu akupe nguvu na familia yako.

Updates;

Leo nimepata taarifa jinsi ajali ilivyotokea kutoka kwa ndugu wa karibu na uzi huu hapa chini ulifunguliwa jana na mwenzetu humu kumbe ndio ajali iliyomuua binti huyu.....


@Ajali haina kinga: Nimeshuhudia watu wakigongwa na daladala

Hii ajari ilikuwa hivi, dreva wa daladala alikwenda kula chakula, akamuachia funguo konda kuwa awe analisogeza gari kwenye foleni, konda alipotaka kulisogeza hilo gari kuliwasha tu kumbe liko kwenye gia namba 2!!!likaondoka kwa kasi ujinga wake ye alikuwa anazidi kukanyanga accelerater!! na kukwepa magari mengini, kwani kwa mida hiyo ya saa, 9 mchana, stendi haikuwa na watu sana kwani ingekuwa balaa kubwa, ndio akawagonga hao watu, conda wa gari lingine na huyo dada yeye alifia hapo hapo, na gari lilipogonga gari jingine na kusimama akashuka na kukimbia, na ukizingatia mida hiyo mfukoni alikuwa kama na laki 2!!pole wafiwa.
 
Back
Top Bottom