Uncle Jei Jei
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,684
- 2,156
Habari wana JF, Nimelazimika kuwapa pole hawa vijana kwa kazi ngumu wanayoifanya na huyu Kibonde ambaye ki ukweli si kwamba ni kada tu wa MAGAMBA,bali hata kichwani hana kitu!!!!!! yaani ni empty kabisaaaa!! Leo wanaongelea matokeo ya kidato cha nne ambayo kila mtu anajua kuwa ni mabaya na kwa kiasi kikubwa matokeo haya yamechangiwa na uzembe mkubwa wa serikali na watendaji wa wizara ya elimu kwa ujumla HASA KWA DHARAU WANAYOONYESHA KWA WALIMU AMBAO NDIO WADAU WAKUBWA WA ELIMU. Huyu jamaa; KIBONDE, yaaani kila kitu anatetea serikali. Anachoongea kinatia kichefuchefu. Hawa vijana; WASIWASI NA MUSSA, kila wakijaribu kwenda kinyume nae yeye anapinga na anakuwa mkali. yaani anawadrive na lawama kibao kwa kila anayesema kuwa haya ni matokeo ya uzembe na umburula wa serikali wa kutoijali ELIMU na wadau wa Elimu hasa WALIMU kwa kutowaheshimu. HILI NI FUNDISHO KWA SERIKALI NA JAMII KWA UJUMLA KUIPA KIPAUMBELE SEKTA YA ELIMU KWA KUANZA NA KUSHINIKIZA WAZIRI KAWAMBWA AJIUZULUUUU!!!! nataman sana huyu jamaa aondoke kabisa kwenye media kwani ana boa