Uchaguzi 2020 Polepole: Kama watu wamefungana kura hatutarudia zoezi kwa sababu hatutafuti mshindi katika kura za maoni

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Polepole
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mh. Polepole ameeleza kuwa hakutakuwa na zoezi la kurudia upigaji wa kura hata kama kuna baadhi ya watia nia wamefungana kwa idadi ya kura walizopata kwa sababu mchakato huu ulikuwa hautafuti washindi.

Katika kueleza jambo hili Polepole amesema "Kama watu wamefungana kura hatutarudia zoezi kwa sababu hatutafuti mshindi katika kura za maoni, tumetoa tu nafasi kwa wana CCM kuweka maoni yao ya awali ambayo yatasaidia vikao vya mbele kufanya uamuzi."

Kauli hii ya Polepole imekuja mapema baada ya kutokea kwa sintofahamu katika matokeo ya kura za maoni za baadhi ya Wagombea kufungana kwa idadi.

Mathalani, idadi ya kura za maoni za Wagombea zimegongana katika majimbo yafuatayo:

Jimbo la Mlimba
- Godwin Kunambi - 193

- Rose Rwakatare - 193

Jimbo la Mwibara
- Kangi Lugola - 173

- Charles Kajege - 173

Jimbo la Buchosa
- Dkt. Charles Tizeba - 354

- Erick Shigongo - 354
 
Safi Sana. Ndo dhana ya Conditional Party loyalty.
 
Nadhani kura zinatoa muongozo tu kuwa Nani anafaa na nani hafai. Ila mwisho siku wao ndo wanachagua mgombea.
 
Ila kangi hapa anahusika inabidi apigwe chini Mana alifika mbali Sana mpaka kuitana Yesu
 

' Intellectual ' huwa akitoa Maelekezo / akielezea Changamoto anatoa pia na ' Solution ' sasa hapa Polepole ametuachia Jibu gani la jumla Kwetu?
 
Hapo nadhani ni Turufu ya Mwenyekiti Taifa itakayoamua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…