Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Debora Lukololo amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limetumia maadhimisho hayo kuwakumbuka wagonjwa kwa kuchangia damu kwa wale wenye uhitaji lakini pia kufanya matembezi ya hiari kwa kushirikiana na Wananchi kwa lengo la kufikisha ujumbe kuhusiana na masuala ya uhalifu.
ACP Lukololo ameendelea kufafanua kuwa kilele cha maadhimisho hayo kitaifa kitakua Septemba 17 mwaka huu huko mkoani Kilimanjaro ambapo kwa mkoa wa Arusha walikutana na makundi mbalimbali ikiwemo wanafunzi, bodaboda, nyumba za ibada na vyombo vya habari kwa ajili ya kutoa elimu juu ya wananchi kujiepusha na vitendo vya uhalifu.
Naye Sajenti Fransis Mlay ambaye alichangia damu leo ametoa wito kwa askari wenzake na jamii kwa ujumla kuwa na utaratibu wa kuchangia damu kwani kwa kufanya hivyo wataenda kuokoa wagonjwa wengi ambao wanauhitaji wa damu katika hospitali.
Maadhimisho hayo yanaenda na kauli mbiu ‘’Huduma Bora za Kipolisi kwa Umma zinapatikana kwa kubadilika kifikra, Usimamizi wa Sheria na Matumizi ya TEHEMA’’.