Polisi Arusha wajitetea uhalali wao wa kuua raia kwa risasi

Polisi Arusha wajitetea uhalali wao wa kuua raia kwa risasi

mwechaga

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2013
Posts
334
Reaction score
57
Wana JF kama mnakumbuka juzi niliandika uzi unao elezea tukio la polis kumuua raia kwa kumpga risasi maeneo ya Sokon one Arusha,jana polisi wamejibu kwa humu JF kwa kutumia jina la mandieta,sasa mimi nataka kuwaeleza ukweli wa mambo maana mimi nakaa jirani na eneo la tukio hilo na nilikuepo na nilishuhudia polisi wakifyatua risasi.

Ilikua ni majira ya kama saa 3 asubuhi marehemu alikua amekaa nje ya nyumba anayoishi alikua anachezea simu yake ya mkononi ndipo wakatokea watu 3 walio vaa nguo za kiraia wawili walikua na bunduki na walipo mfikia marehem karibu waka mwambia leo ndio arubaini yako mwenzio tulisha muua kwa risasi na wewe nilazima ufe,marehem akasimama na kuwauliza kwani vipi wazee? ndipo hapo polisi wakamfyatulia risasi na nyingine wakaendelea kuzipga juu ili raia wasisogee eneo lile.Baada ya hapo nikaona polisi mmoja akimpekua marehem kwenye mifuko ya suruali yake na kutoa wallet na kitambaa na baadae ilikuja gari ya polisi na kuuchukua mwili wa marehem bila na kuingia ndani kupekua bila search warrant wala balozi hakuwepo.
 
Polisi ni janga,ndo maana hata FBI hawakuwaamini mpaka kupekua ofisi ya Kova
 
This is getting very serious and people are just watching and some guys are praising the police for killing citizens. Please please please where is our Government?.
 
Sijui sasa nchi wapi inaelekea kama wanausalama wanaua wanaowalinda napata wasiwasi sana, chuki zikizidi vurugu mitaani.
 
Huyo aliyeuawa huenda ni mmoja wa mashuhuda wa mlipuko wa bomu mkutano wa CHADEMA wanajitahidi kupoteza ushahidi?
 
sasa hivi ni sera, imeshatangazwa wazi kwenye chombo halali cha kutunga sheria na hakuna aliyepinga, kila mtu akae tayari kupigwa kwani polisi wengi wa tanzania wanapokea amri tu na hawaruhusiwi kuhoji.
 
Mwenzio akinyolewa nawewe tia maji. kufa kwaja! lakini wajuwe kuwa tutakufa wote. Just imagine bomu linarushwa katikati ya umati wa watUUUUUU! damu iliyo mwagika bila hatia haitatuacha hivihivi kuna kitu kinakuja hivo tujiandae!
 
Kumbe unaweza kusikiliza maelezo ya pande mbili ukiwa jirani?..kwanini waje kwa huyo badala ya mwingine,huyo mwenzie aliyekwisha uawa alikua nani,how far unajua kuhusu hili jambo...liweke hapa wazi tuchambue mbivu na mbichi!
 
Hakuna aliye salama. Serikali ya kidhalimu ipo madarakani kwa ajili tu ya kulinda maslahi yake. Yeyote anaetishia maslahi yao huyo ni adui, lazima apigwe na kuuwawa. Na tunapokaribia 2015 hali itakuwa ni mbaya zaidi. tujilinde kwa kila hali ili tuweze kufika 2015.
 
Hawa polisi naamin walitumwa kwan hata kama ni jambazi walishindwa kumkamata na kumpeleka kituoni? Akili za kiambiwa changanya na za kwako!!!
 
Wana JF kama mnakumbuka juzi niliandika uzi unao elezea tukio la polis kumuua raia kwa kumpga risasi maeneo ya Sokon one Arusha,jana polisi wamejibu kwa humu JF kwa kutumia jina la mandieta,sasa mimi nataka kuwaeleza ukweli wa mambo maana mimi nakaa jirani na eneo la tukio hilo na nilikuepo na nilishuhudia polisi wakifyatua risasi.

Ilikua ni majira ya kama saa 3 asubuhi marehemu alikua amekaa nje ya nyumba anayoishi alikua anachezea simu yake ya mkononi ndipo wakatokea watu 3 walio vaa nguo za kiraia wawili walikua na bunduki na walipo mfikia marehem karibu waka mwambia leo ndio arubaini yako mwenzio tulisha muua kwa risasi na wewe nilazima ufe,marehem akasimama na kuwauliza kwani vipi wazee? ndipo hapo polisi wakamfyatulia risasi na nyingine wakaendelea kuzipga juu ili raia wasisogee eneo lile.Baada ya hapo nikaona polisi mmoja akimpekua marehem kwenye mifuko ya suruali yake na kutoa wallet na kitambaa na baadae ilikuja gari ya polisi na kuuchukua mwili wa marehem bila na kuingia ndani kupekua bila search warrant wala balozi hakuwepo.

Na ndo maana jamaa wa system kutoka kwa "mnene wa sayari ya 3" waliwatupilia mbali , kwa kuwapa kazi ya kusimamia watu kupanga mistari iliyonyooka wakati wa kumcheki OBAMA 😛lane:, kama wao ( polisi) wanavyokuwaga wana wapanga MGAMBO (CITY MILLITIA :croc: ) au skauti kwenye mikutano au matukio ya "mkulu wa kaya". kwani hawajui kabisa stadi zao za kazi kwani ndo maana saluti yao inamaanisha SINA AKILI ( akiweka mknono kichwani na kushusha) , try kuvuta IMAGARY ya saluti yao (polisi).:bathbaby:
 
Huyu aloandika thread aache uongo. Aliwezaje kushuhudia tukio lote hlo na wakati panafyatuliwa risasi juu hukujaribu kutetea maisha yako? Amakweli ww ni shujaa muongo. Wadanganye wajinga.
 
Back
Top Bottom