Polisi barabarani dhidi ya walipa kodi ni hujuma isiyo na afya kwa Taifa

Polisi barabarani dhidi ya walipa kodi ni hujuma isiyo na afya kwa Taifa

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana niko safarini kuelekea pande za Burigi katika kutia shime juhudi za kizalendo zenye mashiko zilizoasisiwa na hayati mzee baba katika kulisukuma gurudumu la utalii wa ndani, mbele.

Niliyoyashudia njiani hasa kuwahusu wale waliozowea kubrashi viatu kwa kutumia pesa za wengine, dhidi ya wale wasiokuwa na ubavu wa kujisimamia wenyewe, yananisukuma kuuleta uzi huu.

Ili kupata takwimu za kutosha kuhusiana na uzi huu kwa maana ya methodology wahanga wote waliachwa kupambana na hali zao (hapana kuingilia), pia uchukuaji picha ulikuwa ni wa kuepukwa kuchelea vipigo vya mbwa koko.

Hiiiiii bagosha. Dhuluma tupu. Mama Samia ana kazi nzito. Yanayotokea si bure!

Kesi mkononi ni 'Nyakanazi' juzi kwenye: "operation rasmi inayosemekana kuendelea ya kukusanya 30,000/= kwa kila gari. Magari lengwa zaidi ni ma Fuso, Mabasi (makubwa kwa madogo) vi probox, Noah, nk na kina yakhe wengine wanaoweza wakajingiza wenyewe kwenye anga zao. Mamwela wameweka foleni ya magari yenye urefu upatao mita 100. Kikosi kazi kimejizatiti - "Kazi inaendelea!"

Binafsi nikisubiria kuhudumiwa kama wanavyodai wenyewe niliyashudia haya:

1. Magari ya abiria kutozwa faini ati kuwa palikuwa na baadhi ya abiria (hata mmoja tu bila kujali alikaa wapi) kuwa hawakufunga mikanda.

2. Magari ya abiria kutozwa faini ati kuwa kuna mafurushi hata ya nguo za wale wanyonge wa mwendazake wasiokuwa na uwezo wa kumudu mabegi na masanduku mazuri mazuri ya kukokota yaliyo maarufu sana kwenye viwanja vya madege.

3. Magari kutozwa faini kwa sababu ya kuwepo crack yenye size yoyote kwenye taa au kioo chochote.

4. Magari kutozwa faini kwa kutokuwa na mikanda au kutokuwa na mkanda mmoja hata kwenye viti visivyokuwa na abiria kwa wakati wa ukaguzi huo.

5. Magari kutozwa faini kwa defect yoyote kwenye bodi hata ya rangi tu.

6. Magari kutozwa faini kwa madai kuwa rangi kwenye kadi za magari siyo 100% perfect kama ilivyo kwenye kadi.

7. Gari kutozwa faini kwa tathmini za macho kuhusu matairi (labda yawe mapya!).

8. Nk, nk.

Alimradi kila gari ya asiyekuwa mkomavu wa type za washupavu za raia wa jamhuri ya Twitter, alirambwa 30,000/=.

Lugha yao rasmi: "Basi acha tukuandikie angalau kosa moja."

Katika safari nzima nimeshuhudia vitimbi vyao vingi achilia mbali vya wale wa kwenye railway crossings za Manyoni na Bahi, wenye kuvizia magari yasiyosimama kwenye vivuko hata kama hamna treni inayokuja kwa wakati huo.

Vitimbi vyao hivi ni vyenye kutia mashaka sana, kama kweli hawa waliopaswa kutulinda wana hata uelewa wa kuwa mishahara yao ni kodi kutoka kwa hao ambao wao ndiyo wamewageuza kuwa wahanga wa dhuluma zao hizi. Na au je, ni mwendelezo ule ule tu wenye mlengo wa kumhujumu kipenzi cha watu Mama Samia rais wa JMT, kwa wananchi?

Hivi abiria asiyefunga mkanda au hata furushi la abiria, kwa nini ziwe ni kesi za dereva ambaye mashimo na mabonde yote barabarani ni yake?

Nikadhani uzi huu hautakamilika bila japo kusimama na kuwasalimia rasmi walinzi wetu hawa pale kituoni kwao, wilayani Biharamuro.

Kwa mshangao nikakutana na bango kubwa lenye maandishi haya:

"Karibuni wateja, karibuni sana."

Ama! Kumbe sisi ni wateja!

😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂!

Pana umuhimu wa kuona namna ya kukomesha dhuluma hizi.

Ninaandaa uzi husika wenye muarobaini na sera za wazi zenye uwezekano wa kuhitimisha dhuluma zote binafsi hizi.
 
Unataka tukusaidiaje hapo? Lipa faini

Mmama kusema traffic wasiwabugudhi ilikuwa kisiasa tu. Ni lazima tukusanye kodi

Maneno ya mama Samia yalikuwa ni ya kisiasa tu ni Kama vile alivyosema yeye na Magufuli ni kitu kimoja
 
Unatembeaje gari haina seat belt? Au tairi kipara,waache wale faini.. Safi SANA askari... Pesa ije serikalini...siyo mifukon mwenu..safi SANA..

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
 
Naona yote hayo ni makosa kwa sheria za barabarani na moja kwa moja yanastahili faini, labda machache sana kama vile mafurushi na mengine unaweza kutaka kumtetea dereva japo kiuhalisia analojukumu la kukagua gari lake kabla ya kuanza safari kuhakikisha ni salama kwa safari ikiwemo kukagua belt kwenye seat.
 
Serikali ilipokosea ni pale, walipowapa askari hela ya kiwi kwa kila faini.
Mambo ambayo yalikua ya kummbusha tu Dereva, wao wanakimbilia kupiga faini sababu tu, wanajua kuna sehemu yao, ndani ya faini.
Hivi kwa mfano, uko safarini, kwa bahati kioo, kimepata Crek, ndogo tu, Hivi mtu aipaki gari huko, akisuburi kununua kioo kingine. Jambo ambalo hata huyu askari anakuandikia faini asingefanya hiyo gari lingekua yake
 
Unataka tukusaidiaje hapo? Lipa faini

Mmama kusema traffic wasiwabugudhi ilikuwa kisiasa tu. Ni lazima tukusanye kodi

Maneno ya mama Samia yalikuwa ni ya kisiasa tu ni Kama vile alivyosema yeye na Magufuli ni kitu kimoja

Wapi nilipoomba kusaidiwa? Mtalii wa ndani niko vizuri ninakusanya yanayojiri mitaani nimeanza na hili mengine yanafuata. Wewe unaongelea kusaidiwa? Nyambafu!

Hizi zinazoongelewa hapa ni tozo za dhuluma dhidi ya walipa kodi. Majahili wachache wamekaa mahali kumhujumu mama dhidi ya wananchi.

Mshindwe na mtepete kabisa!

Kama observer nilikaa pale hata zaidi ya muda ambao ilinipasa na kuongea na watu kadhaa wakiwamo wahanga na hata wasafiri wa kawaida kabisa.

Hata gari jipya lililo toka leo kiwandani bado (hasa hasa kama ni bus au fuso) lisingefuzu kupita bila ya hiyo unayoiita kodi ambayo mama Samia kaiita sahihi kabisa:

"Kodi ya dhuluma asiyoitaka!"

Halipo jina sahihi la kuita upuuzi huu zaidi ya kuu qualify kama "Practical Insanity."

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Naona yote hayo ni makosa kwa sheria za barabarani na moja kwa moja yanastahili faini, labda machache sana kama vile mafurushi na mengine unaweza kutaka kumtetea dereva japo kiuhalisia analojukumu la kukagua gari lake kabla ya kuanza safari kuhakikisha ni salama kwa safari ikiwemo kukagua belt kwenye seat.

Theoretically yote ni makosa lakini tatizo ni kuwa mkuluro huo wa blank cheque unatumika tu kuhalalisha kupatikana kwa hilo lengo la 30,000/= kwa kila gari wala si kusimamia sheria wala usalama wa watu.

Nilipata nafasi ya kuyapitia pia magari yao (ya serikali na hata ya binafsi) yaliyokuwapo hapo eneo la tukio). Looh, loooh! Ya kwao yako kwenye hali mbaya zaidi na bado wanakomalia ya wengine hata yenye insignificant issues!

Hahaahaaa haa 😂😂😂😂😂! Kweli kazi na iendelee.

Bora tu wangesema inatakiwa 30,000/= kwa gari. Mengine haya hata mtoto mdogo mbona atang'amua?

Ile mbona ni janja ya nyani tu kula mahindi mabichi? Bila shaka ni maslahi binafsi au ni hata dhidi ya mama kwa kujua au kutokujua?

Hakuna lolote!
 
Nasikia hapo Nyakanazi kuna askari wakuda kwelikweli

Kama na hao ni wa Nyakanazi basi sikia yako itakuwa ni sahihi kabisa.

Zingatia kwenye mada wilayani kwao sikulielewa kabisa bango lao la kazi:

"Karibuni wateja, karibuni sana!"

Ebooo 😂😂😂😂😂😂😂!
 
Sijawahi kuamini kama askar wa road wapo kulinda usalama ...nilimpongeza askari mmoja kule geita..yeye akikusimaisha anaomba buku5 moja kwa moja unasepa sio mara washa taa njaa za hawa jamaa sio za nchii hiii
 
Ulipoanza kuandika sijui uzalendo, unaenda burigi sijui kusapoti uzalendo wa mwendazake, Mara sijui bagosha, sijui wazalendo walioachwa na mwendazake nimeachana na Uzi wako wa kijinga kabisa.
 
Unatembeaje gari haina seat belt? Au tairi kipara,waache wale faini.. Safi SANA askari... Pesa ije serikalini...siyo mifukon mwenu..safi SANA..

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app

Umeandika ulichoandika bila kusoma mada. Dalili za wazi za kukupuruka, kama wewe si mnufaika wa moja kwa moja wa hujuma hizi.

Abiria wa bus kufunga mkanda dereva awe anaendesha gari au kuwakagua kila wakati wanaoweza kufungua mikanda yao wakati wowote?

Hivi mikanda kwenye bus haiwezi kuharibiwa hata na abiria kwenye safari hiyo hiyo kwa matumizi yasiyokuwa sahihi?

Hivi barabara zetu ni sahihi kabisa kutosababisha hata defects zozote safarini?

Niliendelee kukuorodheshea niliyoyashudia yaliyonisukuma kuleta uzi huu?

Kweli Tanzania ni kubwa - niliyoyaona labda ni mahsusi pembezoni mwa nchi. Haya hayawezi kujiri kunakotokea jua.

Mbona pangechimbika?
 
Ulipoanza kuandika sijui uzalendo, unaenda burigi sijui kusapoti uzalendo wa mwendazake, Mara sijui bagosha, sijui wazalendo walioachwa na mwendazake nimeachana na Uzi wako wa kijinga kabisa.

Ulipoanza kuandika herufi ya kwanza tu nikajua ni wale wajinga wajinga wenye maslahi na dhuluma hizi. Nikakupuuza moja kwa moja kama ulivyo kuja.

We met perpendicularly on a level ground.

Ni upumbafu usiomithilika kujipa mwenyewe hati miliki ya kumpuuza mtu kana kwamba wewe ni mheshimiwa Mungu.

😂😂😂😂😂😂😂😂!
 
Ulipoanza kuandika herufi ya kwanza tu nikajua ni wale wajinga wajinga wenye maslahi na dhuluma hizi. Nikakupuuza moja kwa moja kama ulivyo kuja.

We met perpendicularly on a level ground.

Ni upumbafu usiomithilika kujipa mwenyewe hati miliki ya kumpuuza mtu kana kwamba wewe ni mheshimiwa Mungu.

😂😂😂😂😂😂😂😂!
Sasa unatukana unaonyesha ulivyo wa hovyo. Anyway endelea kwenda burigi.
 
Sasa unatukana unaonyesha ulivyo wa hovyo. Anyway endelea kwenda burigi.

Mkuu tambua ninaandika kwa tahadhari kubwa kuliko ambavyo unavyoweza kufikiria. Onyesha tusi moja katika nilichoandika. Acheni kuleta siasa uchwara kwenye mambo ya msingi.

Au tusi unaloliona wewe ni hilo hapo kwenye red?

IMG_20210529_190634_458.jpg



Siyo tu baada ya Burigi nina nyuzi zaidi kuhusu safari hii zikiwamo:

1. Muarobaini kwa wanufaika nyie na kadhia hizi.
2. Biashara haramu za wizi zilizohalalishwa na polisi ambako mnachukua kodi haramu zikiwa Mo kwa mwezi kwa mwezi.

Habari ndiyo hiyo.
 
Mkuu tambua ninaandika kwa tahadhari kubwa kuliko ambavyo unavyoweza kufikiria. Onyesha tusi moja katika nilichoandika. Acheni kuleta siasa uchwara kwenye mambo ya msingi.

Au tusi unaloliona wewe ni hilo hapo kwenye red?

View attachment 1801582
Boss achana na mabishano mie nipo kwenye starehe Mambo ya kubishana mitandaoni huwa yanapoteza muda tu. Unabishana ili upate nini sasa??? Mtu humjui, hakuna prize inatolewa , relax mzee. Just relax🤷
 
Boss achana na mabishano mie nipo kwenye starehe Mambo ya kubishana mitandaoni huwa yanapoteza muda tu. Unabishana ili upate nini sasa??? Mtu humjui, hakuna prize inatolewa , relax mzee. Just relax🤷

Yale yale ya hati miliki.

Hata miye niko kwenye starehe na ndiyo maana naelekea Burigi.

Kwani wewe unanijua? Relax mzee, hakuna prize. Just relax 😂😂😂😂.
 
Hivi kwa mfano, uko safarini, kwa bahati kioo, kimepata Crek, ndogo tu, Hivi mtu aipaki gari huko, akisuburi kununua kioo kingine. Jambo ambalo hata huyu askari anakuandikia faini asingefanya hiyo gari lingekua yake
Hii ilinikuta mimi Iringa, wakati huo barabara inakarabatiwa nilipishana na roli likiwa mwendo kasi sana maeneo ya kona za Iyovyi, kokoto zikaruka na kupasua kioo cha mbele, kufika maeneo ya Ruaha Mbuyuni darajani nikakutana na traffic police akanisimamisha, nikamwomba kujua utaratibu nafanyaje iwapo nimepata damage ile njiani, akaniambia niende kwa RTO Iringa ili aniandikie karatasi ya kipindi cha grace kubadili kioo kwakuwa nilikuwa ugenini na sina fedha ya kubadilishia kioo, cha kushangaza nilipokuwa nakwenda ofisini kwa RTO, nikakutana na traffic police mwingine (namkumbuka kwa jina walimtaja wenzake Hamza) maeneo ya Tanesco Iringa akaniandikia fine 30K, nikafika kwa RTO hata hakunisikiliza akasema kalipe tu.
 
Sijawahi kuamini kama askar wa road wapo kulinda usalama ...nilimpongeza askari mmoja kule geita..yeye akikusimaisha anaomba buku5 moja kwa moja unasepa sio mara washa taa njaa za hawa jamaa sio za nchii hiii

Nakubaliana nawe mkuu. Ila kwa hili kama ingekuwa futi boli kipyenga kikali sana cha offside kiliwahusu sana wahusika wote.
 
Hii ilinikuta mimi Iringa, wakati huo barabara inakarabatiwa nilipishana na roli likiwa mwendo kasi sana maeneo ya kona za Iyovyi, kokoto zikaruka na kupasua kioo cha mbele, kufika maeneo ya Ruaha Mbuyuni darajani nikakutana na traffic police akanisimamisha, nikamwomba kujua utaratibu nafanyaje iwapo nimepata damage ile njiani, akaniambia Niende kwa RTO Iringa ili aniandikie karatasi ya kipindi cha grace kubadili kioo kwakuwa nilikuwa ugenini na sina fedha ya kubadilishia kioo, cha kushangaza nilipokuwa nakwenda ofisini kwa RTO, nikakutana na traffic police mwingine (namkumbuka kwa jina walimtaja wenzake Hamza) maeneo ya Tanesco Iringa akaniandikia fine 30K, nikafika kwa RTO hata hakunisikiliza akasema kalipe tu.

Pole sana mkuu. Tozo za dhuluma kama hizi tokea kwa magenge rasmi yaliyo mithili ya wanyang'anyi ndiyo ambazo mama hazitaki.
 
Back
Top Bottom