Polisi barabarani dhidi ya walipa kodi ni hujuma isiyo na afya kwa Taifa

Hakuna dhulma yoyote hapo, ni lazima ulipe fine.
Kama hutaki hama nchi
Traffic kwa moyo mkunjufu naomba muongeze speed kwa huyu jamaa
 
Hakuna dhulma yoyote hapo, ni lazima ulipe fine.
Kama hutaki hama nchi
Traffic kwa moyo mkunjufu naomba muongeze speed kwa huyu jamaa

Wapi pasipo na dhuluma? Hivi unajua hata kinachoongelewa wewe?

Au wewe ni yule dada niliyekukuta pale mapokezi ambapo kwa nje mmejitanabaisha vilivyo nyie ni nani kwa kauli mbiu yenu pendwa 'ya kuwa karibu wateja?"
 

Mwenye akili zako unajiuliza, "kama kwa barabara zake serikali ndizo zenye kupelekea damage hizi, na kuwa kwa damage hizo wanapata mapato. Wana motisha ipi ya kuzitengeneza barabara hizo ili damage kama ulizopata zisitokee tena ili wao wa yakose kabisa mapato laini kama hayo?"

Haya ya yanaweza kutokea na kuvumiliwa au kushabikiwa na wananchi wa jamhuri ya Sengerema peke yake.
 
Barabarani kuna mambo mengi lakini nilichokigundua,mambo mengine ni sheria kandamizi,
lakini sehemu nyingine ni uelewa wa askari.Mfano mafunzo ya udereva yanaeleza utasimama kwenye kivuko cha miguu pale ambapo kuna mtu aliyetayari kuvuka,usilazimishe mtu kuvuka au aliyetayari kivukoni usimpigie honi.Lakini polisi wanakutaka ukifika kwenye kivuko usimame hata kama hakuna mtu.Polisi mwingine anaelewa anasimamia kama sheria inavyosema.
Hapa nikajiuliza kwamba labda hawana mafunzo lakini nikagundua,hata tunapoenda kwenye mafunzo kuna wanaofuzu lakini kwa bahati na kuna wanaofuzu hivyo polisi nao kama binadamu kama sisi hili linaweza kuwatokea na ukitaka kupata kashikashi,jifanye kumuelimisha uone moto wake.
Nashauri kwenye paredi zao za asubuhi ni vyema kukumbushana mambo ya msingi.

Haya kuna sheria ya so called LATRA,hawa wakikukuta na kilikuu chako unapigwa faini ya laki mbili na nusu
papo kwa papo au gari inapelekwa yadi ambapo ukienda kuikomboa unalipishwa elfu sita kwa kila siku iliyokaa hapo yadi.
Maelezo yao ni kwamba kila gari za mizigo lazima zilipiwe kila mwaka.Ukiingia kwenye web yao ili kusajili gari unakuta magari yaliyowekwa ni kuanzia tani moja na kuendelea unabaki mdomo wazi.lakini barabarani kilikuu(suzuki carry) tena isiyosajiliwa kufanya biashara,unaambiwa si gari ya kutembea ni ya mizigo lazima isajiliwe ulipe ushuru wa latra,basi unakuta nchi inakuwa kama vile tunatakiwa wote tutembee kwa miguu.
 

Ninakubaliana nawe kwenye hoja zako. Tatizo lililopo sheria zimetengenezwa kuwapa mamlaka kama blank cheque wanayoweza kuandika chochote watakacho.

Kwa maana nyingine wamejimilikisha haki ya kukuona una makosa hata kama huna.

Hii inaweza kutokea kwa watu wa jamhuri ya Sengerema tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…