Polisi: Gari la kituo cha Gogoni halihusiki na utekaji wa Abdul Nondo

Polisi: Gari la kituo cha Gogoni halihusiki na utekaji wa Abdul Nondo

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Jeshi la Polisi limekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai gari lililoegeshwa Kituo cha Polisi Gogoni limehusika na tukio la utekaji wa Abdul Omary Nondo katika Kituo cha Mabasi cha Magufuli leo alfajiri.

Pia, Soma: Zitto: Tumepata Taarifa Nondo yuko Kituo cha polisi Gogoni, Tumefika tumekuta gari inabadilishwa Plate namba

Kwa mujibu wa Polisi, gari hilo ni la Serikali na limekuwa likiegeshwa kituoni hapo tangu Novemba 29, 2024. Leo mchana, lilichukuliwa na dereva kwenda kuoshwa kwa maandalizi ya kazi za kesho. Aidha, mashuhuda wanasema gari lililotumika katika tukio halikuwa na ngao, tofauti na gari hilo la Gogoni.
IMG_1150.jpeg
 
Kiongozi Mstaafu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema wamejulishwa kuwa Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa ACT, Abdul Nondo amefichwa kituo cha polisi Gogoni, Kibamba Dar es Salaam.

Zitto Kabwe amesema “Tumefika Kituoni, ingawa Polisi wamekataa, tumekuta Landcruiser iliyotumika kumteka Nondo ikiwa inabadilishwa number plates (kutoka zile za IST zilizotangazwa na Msemaji wa polisi na kuwekwa zingine), pichani ndio gari iliyomteka Nondo ikiwa Kituo cha Polisi Gogoni, Kibamba”

“Polisi ni dhahiri mpo na Nondo, tafadhali mwacheni huru akiwa mzima wa afya BILA HATA MCHUBUKO! Tafadhali Tafadhali Tafadhali!”

Itakumbukwa mapema leo Jeshi la Polisi lilisema leo December 01,2024 majira ya saa 11.00 alfajiri katika eneo la stendi ya Magufuli Mbezi Louis Dar es salaam kuna Mtu mmoja Mwanaume amekamatwa kwa nguvu na kuchukuliwa na Watu waliokuwa wakitumia gari lenye usajili wa namba T 249 CMV aina ya Landcruiser rangi nyeupe na kwamba ilielezwa na Mashuhuda kuwa katika purukushani za ukamataji begi dogo lilidondoshwa na baaadhi ya vitu vilivyokuwemo vimetambuliwa ni vya Abdul Omary Nondo “Ufuatiliaji wa tukio hilo ulianza mara tu baada ya kupokelewa kwa taarifa hiyo Polisi, sambamba na kufungua jalada”
#MillardAyoUPDATES
 
Je! km walipoenda kumchukua/kumteka walitoa ngao? Nyie polisi mbona mnatoa majibu mepesi kwenye maswali magumu? Mnasema kwamba lilikuepo tangu tarehe 29 November hapo hapo mnasema lilikuepo hapo Muda mrefu mboni mnajivuruga mara mnasema dereva anakuja kulichukua tarehe 1 December hivi mnatuona sisi mafala si ndio? Gari limepiga tukio likatolewa ngao likatolewa plate number ushaelewa baada ya tukio likapigwa ngao likapigwa plate number mnashindwa kutumia akili ndogo kwenye kufikiri mashahidi wanasema gari ndio hilo maana yake wameremark gari lililohusika na tukio
 
Jeshi la Polisi limekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai gari lililoegeshwa Kituo cha Polisi Gogoni limehusika na tukio la utekaji wa Abdul Omary Nondo katika Kituo cha Mabasi cha Magufuli leo alfajiri.

Pia, Soma: Zitto: Tumepata Taarifa Nondo yuko Kituo cha polisi Gogoni, Tumefika tumekuta gari inabadilishwa Plate namba

Kwa mujibu wa Polisi, gari hilo ni la Serikali na limekuwa likiegeshwa kituoni hapo tangu Novemba 29, 2024. Leo mchana, lilichukuliwa na dereva kwenda kuoshwa kwa maandalizi ya kazi za kesho. Aidha, mashuhuda wanasema gari lililotumika katika tukio halikuwa na ngao, tofauti na gari hilo la Gogoni.
View attachment 3166854
Kwanini plate no.walizotoa kuhusu hilo gari ni za IST na sio Land cruiser
Pia kwanini Hadi sasa mmiliki wa hilo gari ajakamatwa?
Kwanini wao huwa wanakanusha na sio kusimamia Ulinzi na Usalama wa raia na mali zake?
Kwanini walihusika na utekaji wa Ali kibao Soka na hata yule aliyechoma picha ya rais hawajulikani hadi leo?
Kwanini hadi sasa wale walikuwa wanataka kuwateka yule mfanyabiashara (big) pamoja na mmiliki wa online channel hawajakamatwa hadi sasa?
 
Haya siyo "maagizo kutoka juu", bali ni "maelekezo kutoka juu".

Ndugu zangu watanzania inabidi TUCHAPANE ili tuheshimiane.
 
Back
Top Bottom