Polisi jamii auliwa baada ya kuchapwa viboko 70!

Polisi jamii auliwa baada ya kuchapwa viboko 70!

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
askari.jpg

Askari polisi jamii Kata ya Sakina - Arusha ambaye alikuwa pia dereva toyo kwa jina la Goodluck William afariki dunia baada ya kuchapwa viboko 70 kama adhabu aliyopewa na wazee kutokana na mila za Kimasai sababu ikisemekana ni kutelekeza familia yake, ambapo familia yake hiyo aliiacha Monduli, Arusha.

Taarifa ya kifo chake zilisambaa siku ya Jumatatu Tukio Jumatatu tarehe 8/7/2024 baada ya kuchukuliwa na ndugu zake siku ya Jumapili 7/7/2024 kupelekwa Monduli.

Baadhi ya polisi jamii wenzake walimuelezea marehemu kama kijana mpole, ambaye alikuwa hataki kuonewa au kuonea na amefanya kazi kwa miaka 15 na hata ukimtuma mtu kwenda kumchukua mharifu alikuwa anaenda na kumchukua mharifu bila kumjeruhi wala kumnyanyasa.

Na yeye pia alikuwa msaada mkubwa moto ulivyotokea katika hata hivyo, katika kusaidia kuuzima ili usilete madhara makubwa.

Global TV.
 
Inaitwa corporal punishment, tunaitaga 70 ila huwa hazihesabiwi na unapigwa na watu wawili wanapokezana huyu akipiga mwingine anafata hakunaga hata sekunde ya kuskilizia wakichoka kukuchapa ndo wanasema wamekupiga 70 ila kiuhalisia unaweza kuchezea hata fimbo 300 lakini jina lake inabaki kuitwa 70
 
Huyo mwanaume alikubalije kuchapwa viboko 70?
Hiyo adhabu ya Fimbo 70 ipo katika jamii ya Wamasai na Wameru tangu enzi na enzi...kama mzazi wake hasa Baba angeenda kuomba msamaha basi angepaswa kuchinja ng'ombe na kijana wake atachapwa fimbo 35 yaani nusu ya 70

Kufurukuta ni vigumu kwasababu unakamatwa na Wanaume sio chini ya 20 na wanahakikisha huwezi furukuta
 

Askari polisi jamii Kata ya Sakina - Arusha ambaye alikuwa pia dereva toyo kwa jina la Goodluck William afariki dunia baada ya kuchapwa viboko 70 kama adhabu aliyopewa na wazee kutokana na mila za Kimasai sababu ikisemekana ni kutelekeza familia yake, ambapo familia yake hiyo aliiacha Monduli, Arusha.

Taarifa ya kifo chake zilisambaa siku ya Jumatatu Tukio Jumatatu tarehe 8/7/2024 baada ya kuchukuliwa na ndugu zake siku ya Jumapili 7/7/2024 kupelekwa Monduli.

Baadhi ya polisi jamii wenzake walimuelezea marehemu kama kijana mpole, ambaye alikuwa hataki kuonewa au kuonea na amefanya kazi kwa miaka 15 na hata ukimtuma mtu kwenda kumchukua mharifu alikuwa anaenda na kumchukua mharifu bila kumjeruhi wala kumnyanyasa.

Na yeye pia alikuwa msaada mkubwa moto ulivyotokea katika hata hivyo, katika kusaidia kuuzima ili usilete madhara makubwa.

Global TV.
fimbo 70 kwa wala chips, ni kujitafutia tu kesi
 
Basi tu kwa sababu amekufa! Lakini liwe funzo kwa wanaotelekeza familia zao.
Natamani ifanywe kama sheria ya nchi.
 
Janabi Prof alisema chupa moja ya bia kwa saa yaani hii ni standard drinking speed 1bottle/hr
 
Back
Top Bottom