Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwaua majambazi watatu

Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwaua majambazi watatu

Polisi wasio na weledi ndio wanakimbilia kutumia silaha, Polisi majambazi ndio wanaua watu na kuwabatiza ujambazi, Polisi wa mambosasa mwenye fremu za maduka 100 mabwepande ndio deal likibuma wanakuondosha usijewataja.

Kumbuka mnaowaua wana wategemezi wao ambao wataathirika maisha bila hatia, kumbuka laana mnayoitengeneza mpaka kizazi chenu cha tatu itawatafuna hata mkiwa kaburini.

Mh. Samiah badilisha uongozi wa polisi makao makuu, mpe mtu ambaye ni kweli analipenda jeshi na amefanya utafiti mpaka amepata PhD ya kazi za Polisi zinavyotakiwa kuendeshwa atarudisha heshima ya taasisi hii ambayo wananchi wanaichekea mdomoni moyoni wanalia, wanaiogopa hawaipendi, wanahofu nayo na wala hawaiheshimu.

Wapo polisi wamewekeza kwenye uhalifu wanafanya uhalifu ndio kitega uchumi wanashiriki moja kwa moja ujambazi nakisha rais ukiwalaumu hawafanyi kazi wanatafuta wa kuwatoa kafara wakuridhishe. Inauma sana.
Hotel mpya nayo inajengwa fasta, ghorofa jipya nalo linaota kwa ufadhili wa wahalifu
 
Tulitoa tahadhari kwa majambazi baada ya kauli ya Mh SSH ,watakula vyuma sana wasipoacha ujambazi ,dawa ya jambazi hakuna kujadiliana nae ni kumlisha chuma tu na mtandao wao wote.
Pia tujiulize kwanini wauawe baada ya kauli ya SSH?
Kabla ya kauli walikuwa wanawaogopa au walikuwa na mgawo?
 
Pia tujiulize kwanini wauawe baada ya kauli ya SSH?
Kabla ya kauli walikuwa wanawaogopa au walikuwa na mgawo?

Nahisi vyombo vya dola walijisahau wakadhani tayari washamaliza kazi,mama SSH kama kawakumbusha majukumu yao,ujambazi ulipungua kwa sababu wengi walikula vyuma....Dawa ya jambazi ni kula chuma tu.
 
Back
Top Bottom