Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Chagua kutokomeza Ukatili wa Kijinsia.
Akizindua kampeni hiyo leo Disemba 06, 2024 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Bwana Saad Mtambule ameiomba jamii kuendelea kutoa malezi bora kwa jamii huku akiwasihi kushirikiana na Jeshi la Polisi katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia huku akiitaka jamii kukemea vitendo hivyo.
Kwa upande wake kamanda wa Polisi Mkoa wa kipolisi Kinondoni kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Mtatiro Kitinkwi amesema tayari kesi 25 za vitendo vya ukatili zimefikishwa mahakamani huku akisema kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi Kinondoni litaendelea kuwafikisha mahakamani na kutoa elimu kwa makundi mbalimbali katika ili kujenga uwelewa wa pamoja juu ya vitendo vya ukatili vinavyofanywa na baadhi ya watu katika jamii.
Nao baadhi ya wananchi walioshiriki katika kampeni hiyo hiyo licha ya kulishukuru Jeshi la Polisi wamesema kuwa mafunzo na kampeni hiyo iendelee iliitumike kuwakumbusha wananchi juu ya madhara ya vitendo vya ukatili.