Tetesi: Polisi Kutopenda Maridhiano: Kuzuia Fujo ni Fursa ya Kipato

Tetesi: Polisi Kutopenda Maridhiano: Kuzuia Fujo ni Fursa ya Kipato

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,455
Reaction score
73,145
Je, ni kweli wadau kuwa maandamano yatokeapo hata yanapokuwa yamefuata sheria polisi huwa wanalianzisha ili kutokee mchanganyiko na wao waingilie kati na kutengeneza fursa ya kipato ndani ya fujo hizo?

Habari hizo baada ya kuzipata na kushangaa nami nikashangawa kuwa ULIKUWA HUJUI CHAKAZA?

Je, nyie wana JF mnalijua hilo? Kwamba mbinu inayotumika ni kujipanga kwanza, kisha amri ya kutawanyika na ghafla mabomu kwenye zile exits zote ambazo ndio zingetumika kutawanyika.

Baada ya hapo ni kipigo, uporaji wa simu na fedha.

Tetesi hizo zinasema baada ya shughuli hiyo sio ajabu kumkuta mtu na simu kumi na fedha ya kutosha.
Jee mnalijua hilo?
 
Jee ni kweli wadau kuwa maandamano yatokeapo hata yanapokuwa yamefuata sheria polisi huwa wanalianzisha ili kutokee mchanganyiko na wao waingilie kati na kutengeneza fursa ya kipato ndani ya fujo hizo?
Habari hizo baada ya kuzipata na kushangaa nami nikashangawa kuwa ULIKUWA HUJUI CHAKAZA?
Jee nyie wana JF mnalijua hilo? Kwamba mbinu inayotumika ni kujipanga kwanza, kisha amri ya kutawanyika na ghafla mabomu kwenye zile exits zote ambazo ndio zingetumika kutawanyika.
Baada ya hapo ni kipigo, uporaji wa simu na fedha.
Tetesi hizo zinasema baada ya shughuli hiyo sio ajabu kumkuta mtu na simu kumi na fedha ya kutosha.
Jee mnalijua hilo?
Wataka liitwe Jeshi la Mardhiano na Polisi?
 
Ulishawahi kuona wapi jeshini kunamaridhiano? Watu wengine wajinga sana hili ni jeshi la polisi siyo polisi jamii maridhiano yanatoka wapi
 
Mtapigwa ile noma na nitaandaa sherehe siku hiyo maana najua ni siku pekee nyumbhu watauawa
 
Jee ni kweli wadau kuwa maandamano yatokeapo hata yanapokuwa yamefuata sheria polisi huwa wanalianzisha ili kutokee mchanganyiko na wao waingilie kati na kutengeneza fursa ya kipato ndani ya fujo hizo?
Habari hizo baada ya kuzipata na kushangaa nami nikashangawa kuwa ULIKUWA HUJUI CHAKAZA?
Jee nyie wana JF mnalijua hilo? Kwamba mbinu inayotumika ni kujipanga kwanza, kisha amri ya kutawanyika na ghafla mabomu kwenye zile exits zote ambazo ndio zingetumika kutawanyika.
Baada ya hapo ni kipigo, uporaji wa simu na fedha.
Tetesi hizo zinasema baada ya shughuli hiyo sio ajabu kumkuta mtu na simu kumi na fedha ya kutosha.
Jee mnalijua hilo?
Kama madai yako yana ukweli basi Kwa nafasi yako na ushawishi ulionao washauri hao waanzisha fujo waache kuchochea fujo ili polisi wasipate fursa unayoizungumzia. Lakini pia inawezekana kwamba waanzisha fujo wanafanya hivyo makusudi Kwa sababu hizo hizo unazowatuhumu polisi Kwa sababu inajulikana wengi wao huanzisha fujo baada ya kupewa viroba!
 
Ulishawahi kuona wapi jeshini kunamaridhiano? Watu wengine wajinga sana hili ni jeshi la polisi siyo polisi jamii maridhiano yanatoka wapi
Maridhiano ni kuona sheria imekiukwa wapi?
Jee hili la kuitwa wao wezi na waporaji na kuwa wanafurahia hilo kwani ni FURSA unalionaje?
 
Mtapigwa ile noma na nitaandaa sherehe siku hiyo maana najua ni siku pekee nyumbhu watauawa
Wote tunafanya siasa ila unakoelekea siko jitafakari, sidhani kama Mwenyekiti wako atafurahia ulichokiandika.

Mtu mwenye akili timamu hawezi kuandaa sherehe kwa kifo cha mtu kwa sababu yeyote ile.
 
Wote tunafanya siasa ila unakoelekea siko jitafakari, hata Mwenyekiti wako akiona post hii sidhani kama atakupongeza.

Mtu mwenye akili timamu hawezi kuandaa sherehe kwa kifo cha mtu kwa sababu yeyote ile.
Watu wengine ni laana tupu, msamehe hajui kuwa hata wazazi wake wanaweza kufa katika hilo afanyialo sherehe
 
Jeshi la police halifanyi siasa. Kama mnataka maridhiano sio kuita jeshi la police . Inaitwa Police Force. Yaani hakuna kubembelezana ni kusimamia sheria.
 
Jeshi la police halifanyi siasa. Kama mnataka maridhiano sio kuita jeshi la police . Inaitwa Police Force. Yaani hakuna kubembelezana ni kusimamia sheria.
Sheria ndio hiyo, mikutano na maandamano yanaruhusiwa wao wanapewa taarifa. Jee hilo wanalisimamia?
Kwenda kinyume ni kuwa nao ni wahalifu wachukuliwe hatua kama IGP wa Uganda aliyeshtakiwa kama mhalifu kwa kupiga watu
 
Ulishawahi kuona wapi jeshini kunamaridhiano? Watu wengine wajinga sana hili ni jeshi la polisi siyo polisi jamii maridhiano yanatoka wapi

Tatizo la Jeshi la Polisi ni kwamba halikupata nafasi ya kuundwa upya kama ilivyotokea kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania - JW. Jeshi lilipoasi, hapo 1964, lilivunjwa na kuundwa upya kwa malengo tofauti kabisa na yale ya enzi ya mkoloni. misingi ya taifa letu imejengwa na mkoloni, kwa hiyo ilihitajika iundwe upya baada ya uhuru. JW ilipoundwa upya, imeendelea vizuri kutekeleza majukumu yake, kuna vitu vichache sana ambavyo vinahitaji marekebisho.

Kwa Polisi haikuwa hivyo. hata hizo sheria zinazowapa Polisi mamlaka ya kuingilia nafasi ya raia kukutana, kubadilishana mawazo, naam, hata kuandamana, ni sheria za mwaka 1954. Inaelekea ziliundwa ili kukabiliana na tishio la kudai uhuru wa nchi, maana kipindi hicho TAA ilianza kuja juu na mwaka huo ndio TANU ilipoundwa. Kwa hiyo Jeshi la Polisi kimuundo ni la kutetea na kuulinda utawala uliopo. Bahati nzuri kwetu, utawala wa awamu ya kwanza ulijishughulisha hasa na kujenga taifa jipya lililo huru. Sheria hizo zilikuja kuhojiwa na Tume ya Jaji Nyalali, kuonekana kwamba hazifai tena kwa mfumo wa Kidemokrasia ya Vyama Vingi. katika mfumo huu, tunahitaji watu wawe huru kutoa maoni yao, na Jeshi la Polisi litoe ulinzi kwa watu na vyama vyao watoe maoni yao kwa uhuru bila bugudha. kazi ya serikali iliyoko madarakani ni kutekeleza sera na ahadi ilizoahidi. kama watu wanaongea, waache waongee, lakini serikali inachapa kazi ili mwisho wa siku, waweze kuwaonesha watanzania ni kwa kiasi gani walitekeleza ahadi zao.

Mimi sioni tatizo lolote hapo, hata kama watu wanaongea, wanafanya mikutano na maandamano, mwisho wa siku anayejijenga zaidi ni yule anayefanya vitu halisi na watu wanaviona. mashaka yanakuja pale huyo ambaye ndio ana fursa ya kufanya hivyo vitu, anaanza kumuogopa huyo ambaye hana fursa hiyo. Anaogopa nini? ana mamlaka ya kukusanya kodi na kupanga ataitumiaje. atatatua kero za watu. hivi kweli watu wataacha kumsikiliza anayetatua kero zao na kuwapa mahitaji yao, kuwatengenezea fursa za maendeleo vijana na wananchi kwa ujumla, fursa za elimu, kuboresha huduma za afya, wamsikilize anayebwabwaja kwenye mikutano? katu! Na kama ndio hivyo, basi kuna tatizo limejificha. na ni jukumu la wanachi wote kwa uzalendo wao, kulitafuta tatizo hilo na kuliweka wazi.

Jeshi la Polisi libakie kuwa na jukumu la kulinda raia na mali zao, na kuzingatia kwamba hii ni nchi ya Demokrasia ya vyama vingi, vilivyoandikishwa na vinatambuliwa kisheria. Jeshi lisijinasibishe na chama kimojawapo, hata kama ni chama tawala. Jeshi lifanye kazi yake kwa weledi wa sayansi ya kipolisi, na siyo kufuata maagizo ya watawala. maana hapo kuna hatari ya kufanya mambo kwa maslahi binafsi ya watawala, hasa kama watawala ndio wanatoa promosheni na maslahi manono kwa wale wanaotekeleza matakwa binafsi ya watawala, na siyo maslahi ya taifa kwa ujumla wake
 
Kama madai yako yana ukweli basi Kwa nafasi yako na ushawishi ulionao washauri hao waanzisha fujo waache kuchochea fujo ili polisi wasipate fursa unayoizungumzia. Lakini pia inawezekana kwamba waanzisha fujo wanafanya hivyo makusudi Kwa sababu hizo hizo unazowatuhumu polisi Kwa sababu inajulikana wengi wao huanzisha fujo baada ya kupewa viroba!
Usikaririshwe nyimbo za majambazi wa kisiasa. Hakuna hata siku moja maandamano au mkutano wa wapinzani ambao haukuingiliwa na polisi kukatokea fujo. Hata siku moja, wao wanautulivu wa ajabu hata huwezi kudhani. Mpaka vibaka wanawadhibiti wenyewe. Hizo hadithi za viroba ni hekaya za matapeli wa siasa
 
Sheria ndio hiyo, mikutano na maandamano yanaruhusiwa wao wanapewa taarifa. Jee hilo wanalisimamia?
Kwenda kinyume ni kuwa nao ni wahalifu wachukuliwe hatua kama IGP wa Uganda aliyeshtakiwa kama mhalifu kwa kupiga watu
Police siyo chama cha siasa. Hiyo ni police force. Mmeenda mahakamani mmeambiwa zuio la mikutano ni halali.

Police kazi yao ni kusimamia sheria zisivunjwe sio kukaa kwenye vikao vya kisiasa.

Tunawasubiri 1 sept. Nyie njooni tu na mtajua ni nani anayevunja sheria.

Police wanasimamia ilani ya CCM. Nyie Chadema ni watoto wa nje ya ndoa. Mkileta jeuri virungu lazima.

Pelekeni vikao vyenu vya kisiasa Ufipa. Sio police. Kama mnataka haki nendeni mahakamani.

Hii ni police force siyo police maridhiano.

Kwikwikwi
 
Mahakama imeshatoa tafsiri yake lakini nyinyi hamtaki kuheshimu utawala wa sheria. Sasa wacha polisi wawatandike na kuwategua viungo. Labda akili itawarudi.
 
Police siyo chama cha siasa. Hiyo ni police force. Mmeenda mahakamani mmeambiwa zuio la mikutano ni halali.

Police kazi yao ni kusimamia sheria zisivunjwe sio kukaa kwenye vikao vya kisiasa.

Tunawasubiri 1 sept. Nyie njooni tu na mtajua ni nani anayevunja sheria.

Police wanasimamia ilani ya CCM. Nyie Chadema ni watoto wa nje ya ndoa. Mkileta jeuri virungu lazima.

Pelekeni vikao vyenu vya kisiasa Ufipa. Sio police. Kama mnataka haki nendeni mahakamani.

Hii ni police force siyo police maridhiano.

Kwikwikwi
Ujeuri haujengi. Kwanza umetoka nje ya mada, jee Polisi kupambana na maandanano ni FURSA ya kupatia mapato?
Nayo mengine ni kuwa kuvunja watu miguu sio ufahari kama madhara mengine yanatokea ambayo yangeepushwa. Hivi unajua madhara yanayoweza kuukumba mji mfano vituo viwili vya mafuta vikiunguzwa? Shughuli za wangapi zitaathirika? Katiba na sheria viheshimiwe na kila mtu ili kukwepa hayo.
 
Mahakama imeshatoa tafsiri yake lakini nyinyi hamtaki kuheshimu utawala wa sheria. Sasa wacha polisi wawatandike na kuwategua viungo. Labda akili itawarudi.
Mkuu mie nasimamia ukweli kwani sitaki hayo yatokee. Na yanaweza yasitokee kama amri ile ya kinyume cha katiba itafutwa .
Hayo ya kutengua viuno msidanganye watu, kwenye fujo hizo wanaoathirika sio waandamanaji zaidi bali wengine. Unapo watawanya wanatawanyika, kisha wezi, majambazi na vibaka ambao hawana itikadi au waweza kuwa na yeyote hata ccm wanachukua nafasi ili watimize makusudio yao.
Maridhiano ya sheria inasemaje hata polisi wa kaburu walifanya maji yalipo zidi unga
 
Back
Top Bottom