Uchaguzi 2020 Polisi, NEC lini walimpa Lissu adhabu ya kutokusafiri?

Uchaguzi 2020 Polisi, NEC lini walimpa Lissu adhabu ya kutokusafiri?

onjwayo

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2020
Posts
1,356
Reaction score
1,309
Hawa polisi sasa ni dhahiri wanaingilia shughuli binafsi za mgombea wa Chadema, Tundu Lissu.

Lissu ni Mwanasiasa na shughuli kubwa kwake ni kufanya siasa. Ili uweze kutekelezwa majukumu yako kisiasa ni lazima utoke point A kwenda B kuhamasisha wanachama wako.

Uhamasishaji siyo kuomba kura bali ni kuongeza idadi ya wanachama.

Jana polisi waliingilia shughuli zake na kumzuia njiani kuendelea kwenda kutekeleza majukumu yake. Polisi walisema walitekeleza majukumu yao kwa Nia ya kumlinda.

Ni kweli Lissu anahitaji ulinzi lakini siyo kumzuia kusafiri. Au tuseme, amezuiwa kusafiri na kuonana na watu wake. Mbona sasa jeshi la polisi hatuwaelewi elewi? . Na je, wanatenda haya kwa amri ya Nani?. Mgombea wa CCM Ni rais anayeendelea lakini tofauti na kugombea {kufanya kampeni} anaendelea na shughuli za urais Kama kawaida.

Lissu ana zuio kutokufanya kampeni kwa muda wa siku 7, Sasa je, asifanye shughuli nyingine za kisiasa au kijamii?

NEC katika katazo lao walisema haruhusiwi kusimama jukwaani akifanya kampeni. Hilo Lissu na timu yake wamelitii tangu Ile trh 3, lakini kule kusafiri pia Yuko jukwaani akipiga kampeni? Unaposafiri Ni kuwa either unakuwa ndani ya gari au chombo chochote, Je, hiyo tuiite Ni kupanda jukwaani kuomba kura?

Polisi na NEC wabanwe na vyama vinavyoshiriki uchaguzi huu watoe tamko kwa nini wanasakama baadhi ya vyama. Vyama vizungumze wazi na kuonya juu ya Tabia ya NEC kuwanyamazia polisi hata pale ambapo wanavunja katiba na kuvuruga mwenendo wa uchaguzi unaoendelea. Polisi na NEC wakae Kando na wasiwe washirika wa kutaka kuona mgombea wa CCM anapita bila kupata upinzani.

Mwaka huu uchaguzi ni tofauti kabisa kwa namna ambavyo Lissu alivyobadili upepo kwahiyo CCM wakubali kushindana na si vinginevyo. Waache Tabia ya kubebwa, mbona wanapowasomba watoto wa shule na kuwssitishia masomo vyama vingine havijalalamika. Wanatumia resources za serikali kwa maana usafiri pamoja na watumishi Ila vyama vingine viko tu kimya. Sasa wameanza kutumia force, polisi na NEC kuwasaidia.

Hii haikubaliki, Lissu afanye Yale aliyoelekezwa na kamwe asiingiliwe. Kwani wasiwasi wa tume na polisi Ni Nini?
 
Huyu kiumbe anawachezesha ngoma CCM na vibaraka wake wakiwemo hao policcm na tumeccm kadiri apendavyo. Lissuuuu!! Endelea kuwanyoosha hawa mchwa.

Walijisahau sana na kudhani kwenye uchaguzi huu basi wangejishukia tu Mlima Kitonga. Sasa mambo yamekua ni tofauti kabisa baada tu ya ujio wako. Hakuna nguvu ya Wasanii 100, hakuna stori za ndege wala sgr kwa sasa!

Habari ya mjini kwa sasa ni ile ya kuitaka ccm na mgombea wake kutuachia nchi yetu. Full stop.
 
Aliwatukana polisi izo wanazompa ni adhabu tosha,polisi wanaweza sema walikua wanamlinda na kwenda kuhakikisha usalama wake,huwezi fundisha kazi polisi ya jinsi ya kumlinda lisu,alitakiwa aseme ili polisi wajue wanajipanga vipi kumlinda sasa akikurypuka tu atalindwa wanavyotaka wao,anajitokea tu ajidhuru alafu aje apate kuwashtumu polisi, mjinga hua anaakili nyingi na anauwezo wa kugundua kitu mjanja asikijue,

Atalindwa hadi akiwa anaenda kunya,mpka pale magufuli atakapo apishwa tena,hatoonana na mabeberu wala kuwasiliana nao,ana uhuru wa kutembea popote ila kwa sasa yupo chini ya uangalizi maalum kwahiyo afuate protokoli na awe na heshima,akijifanya anajua kimbele watu wanajua kinyuma
 
Hawa polisi Sasa Ni dhahiri wanaingilia shughuli binafsi za mgombea wa Chadema Lissu.

Lissu Ni mwanasiasa na shughuli kubwa kwake Ni kufanya siasa. Ili uweze kutekelezwa majukumu yako kisiasa Ni lazima utoke point A kwenda B kuhamasisha wanachama wako...
Waache NEC na Polisi waendeleze ubabe. Tabia hii itachochea wapiga kura na raia wengine kuwachukia.
 
Hawa polisi Sasa Ni dhahiri wanaingilia shughuli binafsi za mgombea wa Chadema Lissu.

Lissu Ni mwanasiasa na shughuli kubwa kwake Ni kufanya siasa. Ili uweze kutekelezwa majukumu yako kisiasa Ni lazima utoke point A kwenda B kuhamasisha wanachama wako...
CCM ni waoga sana,wanatumia vyombo vya dola kubaki madarakani
 
Aliwatukana polisi izo wanazompa ni adhabu tosha,polisi wanaweza sema walikua wanamlinda na kwenda kuhakikisha usalama wake,huwezi fundisha kazi polisi ya jinsi ya kumlinda lisu,alitakiwa aseme ili polisi wajue wanajipanga vipi kumlinda sasa akikurypuka tu atalindwa wanavyotaka wao,anajitokea tu ajidhuru alafu aje apate kuwashtumu polisi,mjinga hua anaakili nyingi na anauwezo wa kugundua kitu mjanja asikijue,

Atalindwa hadi akiwa anaenda kunya,mpka pale magufuli atakapo apishwa tena,hatoonana na mabeberu wala kuwasiliana nao,ana uhuru wa kutembea popote ila kwa sasa yupo chini ya uangalizi maalum kwahiyo afuate protokoli na awe na heshima,akijifanya anajua kimbele watu wanajua kinyuma
Are you drunk? You seem not to be normal. You are portraying your deep hatred against TL. Anyway, there is a day you will wake up.
 
taratibu polisi akili zitawakaa sawa wataacha upendeleo kwa baadhi ya vyama
 
Huyu kiumbe anawachezesha ngoma CCM na vibaraka wake wakiwemo hao policcm na tumeccm kadiri apendavyo. Lissuuuu!! Endelea kuwanyoosha hawa mchwa.

Walijisahau sana na kudhani kwenye uchaguzi huu basi wangejishukia tu Mlima Kitonga. Sasa mambo yamekua ni tofauti kabisa baada tu ya ujio wako. Hakuna nguvu ya Wasanii 100, hakuna stori za ndege wala sgr kwa sasa!

Habari ya mjini kwa sasa ni ile ya kuitaka ccm na mgombea wake kutuachia nchi yetu. Full stop.
Lisu anawafanya maccm, mapolisi, tume na wadhalimu wote wajue hawajui chochote. Ni spana mdomoni, spana zaidi katika matendo. Spana! Spana! Spana. LISSU katupa msamiati mpya pale Kiluvya. Amemaliza hotuba kwa kusema "It's late, but it's okey. Tuko tayari kuingia magogoni.
 
Mie kwa ushauri wangu,nec waongeze kipengele mtu akizuiwa kampeni awekwe house arrest,hamna kutoka ndani zaidi ya kwenda toilet tena under escort,hamna kupost Twitter wala kwenda kufanya ibada hadi adhabu iishe...
 
Aliwatukana polisi izo wanazompa ni adhabu tosha,polisi wanaweza sema walikua wanamlinda na kwenda kuhakikisha usalama wake,huwezi fundisha kazi polisi ya jinsi ya kumlinda lisu,alitakiwa aseme ili polisi wajue wanajipanga vipi kumlinda sasa akikurypuka tu atalindwa wanavyotaka wao,anajitokea tu ajidhuru alafu aje apate kuwashtumu polisi,mjinga hua anaakili nyingi na anauwezo wa kugundua kitu mjanja asikijue...
Lisu anawafanya maccm, mapolisi, tume na wadhalimu wote wajue hawajui chochote. Ni spana mdomoni, spana zaidi katika matendo. Spana! Spana! Spana. LISSU katupa msamiati mpya pale Kiluvya. Amemaliza hotuba kwa kusema "It's late, but it's okey. Tuko tayari kuingia magogoni.
 
Kwa tukio la jana wamejionyesha wazi na dunia imejua ,ni moja ya timu ya CCM iliyojificha kwenye jeshi la police, yani walivyo weupe hara rough walioicheza jana bila ya mafanikio,hata mtoto wa darasa la saba angewazidi kabisa
 
Back
Top Bottom